MAWAZO YA BIASHARA Ambayo unaweza kuyatumia kulingana na Mazingira yako. THREAD👇
Wananzengo Mnaendeleaje na majukumu ya kujenga Taifa? Poleni na nipende kuwapongeza kila mmoja kwa nafasi yake.
Wengi wamekua wakiulizia mawazo ya Biashara ambayo wanaweza kuyatumia ili kuingiza chochote. Kama kijana na mtafutaji nakutana na mengi na wewe pia una mengi ya kushare na wadau na kwa namna moja au nyingine ukawasaidia kujikwamua kimaisha.
Huenda wengine Mitaji kwao si tatizo sana ila Management ndo kikwazo, haswa kwa wale ambao ndo wanaanza Biashara. Hizi ni Ideas (Mawazo ya Biashara) kadhaa ambayo unaweza yatumia naamini unaweza ongeza ubunifu zaidi na ukafanya Biashara yako kuonekana Bora zaidi.
Kumbuka Biashara nyingi bado zinafanyika local na zinakosa vitu kama Marketing, Branding n.k na nyingi zinazingatia uhitaji wa eneo husika. Leo Sitachambua sana Naweka mawazo tu (Ideas). Pitia na washirikishe wengine.
Twende zetu..... ✍️
1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha. 2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha. 3. Kutengeneza na kuuza tofali 4. Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na Makampuni mbalimbali.
5. Kuanzisha kituo cha redio na televisheni 6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa vya compyuta na mawasiliano. 7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k 8. Kushona na kuuza nguo.
9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suits, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali, n.k 10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine. 11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.
12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu (Consultancy) 13. Kutengeneza bidhaa mbalimbali za vyakula mfano viazi, karanga & ndizi (Crips) 14. Kusambaza vyakula site. (Catering) 15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta (Bodaboda & Maguta)
16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika. 17. Kuuza Mitumba (Grades na Ubora lazima Uhusike) 18. Kurepea (Fundi) simu & computers. 19. Kufungua duka la kuuza pembejeo. 20. Kufungua banda la chakula na chips (Ubunifu na ubora lazima vizingatiwe)
21. Kukodisha turubai viti na meza 22. Kufungua Supermarket 23. Kufungua Saluni 24. Kufungua Bucha 25. Video Shooting & Editing. 26. Kufungua Internet cafe 27. Duka la kuuza matunda
28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline. 29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi. 30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT 31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k
32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor) 33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k 34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja. 35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.
36. Kukodisha Music 37. Kuanzisha Mradi wa Taxi 38. Kuanzisha mradi wa Daladala 39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, flash, simu, Cases mbalimbali za simu & computers.
40. Kununua magenerator na kukodisha 41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu 42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP) 43. Kutengeneza urembo. 44. Kujenga apartments 45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote (Sheli)
46. Kufungua Duka la samaki 47. Kusambaza Nafaka, wakati wengine wanalima Tafuta soko. 48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo. 49. Kujenga hostel 50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.
51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda vidogo na wananchi. (Sites na mashambani) 52. Ufundi simu 53. Kufungua Hospitali, Zahanati. 54. Maabara ya Macho, Meno 55. Kuchimba/Kuuza Madini
56. Kuuza second hand Electronics materials. 57. Kuuza miti na mbao 58. Kufungua Grocery, bar 59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha 60. Kucharge simu/battery 61. Duka la TV , Redio na vifaa vingine
62. Biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na matamasha mbalimbali (catering). 63. Huduma ya choo na Kuoga (kwenye mikusanyiko) 64. Kuuza na kushona Uniform za shule 65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla. 66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari
67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe 68. Kuuza fanicha 69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi
ya magari na mitambo. 70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel, Lodge, Guest House) 71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium. 72. Kuuza vioo
73. Kushona na kukodisha nguo za harusi 74. Kufungua car wash kwa ajili ya kuosha na kulaza magari 75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine). 76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc) 77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi
78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni 79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games) 80. Kufuga na Kuprocess samaki. 81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga 82. Kuuza vifaa vya ulinzi Fencing, CCTV Camera, n.k
83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali 84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane) (Mitambo) 85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu. 86. Kuanzisha Bakery ya kutengeneza vitafunwa na cakes. Inaweza kutengeneza vitafunwa vya asili pia kwa bei poa.
87. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao 88. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo. 89. Biashara ya kuagiza magari. 90. Kufungua duka la vifaa vya kufugia nyuki, Kuuza na kununua asali.
91. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha 92. Kufungua Duka la vinyago. 93. Kuanzisha huduma za kiwakala (Agenct) wa Huduma za Fedha 94. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym). 95. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi. 96. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).
97. Kufungua Kampuni ya Ulinzi 98. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding" 99. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki 100. Kuuza baiskeli na toys (Haswa za watoto )
Wadau mnaendeleaje? Leo tuendelee na List kidogo na nitakua naiupdate kila nitakapokua napata muda.
NOTE: Kama kuna Idea Umeipenda na unatamani kuandika MPANGO BIASHARA (Business Plan) Utanicheck nikupe Direction kwa wanaoandika kwa Ubora na Bei Rafiki......✍️
101. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe, vijiko n.k 102. Kuuza marumaru. 103. Kuuza kokoto. 104. Kuuza mchanga.
105. Kufundisha Masomo ya ziada / mafunzo mbalimbali , mapishi, muziki, mazoezi n.k 106. Biashara za bima. 107. Kusafirisha abiria. 108. Biashara za kitalii. 109. Biashara za meli na Boti, kukodisha kwa ajili ya uvuvi, usafirishaji. 110. Kampuni ya kuchimba visima.
111. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea. 112. Kuuza mkaa. 113. Kutengeneza mashine Mbalimbali , za kutengeneza tofali, za kupukuchua / kusindika mazao mbalimbali. 114. Kampuni ya Matangazo. 115. Kutengenezea Vifungashio.
116. Kutengeneza vitanda vya chuma 117. Kununua nyumba (Apartments) na kuzikodisha. 118. Kukarabati Fenicha. 119. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe. 120. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka. 121. Kazi ya ususi na kusafisha kucha.
122. Kuchimba, kusupply na kuuza Gypsum. 123. Malori ya kusafirishia Mizigo 124. Duka la kuuza mboga za majani fresh. 125. Duka la kuuza maua. 126. Kampuni ya kuzoa takataka na kuzitengenezea bidhaa mbadala kama mkaa n.k 127. Gereji inayotembea. 128. Kuuza viwanja. 129. Uvuvi
130. Uchoraji wa mabango. 131. Ukumbi wa kuonesha soka, filamu n.k 132. Yadi kwa ajili ya kupaki magari 133. Mradi wa trekta za kukodisha. 134. Kutengeneza ghala / storage Facilities za kisasa.
135. Biashara ya kufuga mbwa wa kisasa kwa ajili ya Ulinzi, Petties. Species / Breeds pendwa. 137. Uandishi wa Ripoti na Miradi mbalimbali (Proposals) Hizi zinafanyika sana mavyuoni, wale wanafunzi wavivu lazima wasaidiwe.
138. Kutengeneza kampuni ya umwagiliaji. 139. Kutengeneza / kuunda vipuri (Spares). 140. Kutengeneza na kuuza Vipodozi. 141. Anzisha Coffee shop 142. Anzisha salon / Babershop & Spa.
143. Shoe shine ya kisasa. 144. Kutengeneza Barafu (Ice Creams) na kuziuza kwa wahitaji wakubwa kama Bucha za samaki n.k 145. Packegers (Kampuni ya kufungasha Bidhaa) 146. T-Shirts Printing.
• • •
Missing some Tweet in this thread? You can try to
force a refresh
Aliwahi kuwa Raisi wa awamu ya Tatu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi. Na aliongoza kuanzia Mwaka 1995-2005, Mwanasiasa aliyeiva na mbobezi wa mambo mengi hasa ya kidiplomasia na Uandishi.
Historia ya Mzee Mkapa inaanzia huko Ndanda, Masasi Mkoani Mtwara ambapo alizaliwa huko Tarehe 12.11.1938 Safari yake ya elimu ilianza mwaka 1945 ambapo alipata Elimu.
Katika historia yake ya maisha ya Shule mzee Mkapa alieleza magumu kadhaa aliyoyapata ikiwemo kwenda shule bila kuwa na viatu kwa umbali mrefu sana ili kupata elimu katika shule za wamishenari.
Aliishi kuanzia 14.10.1930 mpaka 07.09 1997. Alikua mwanasiasa, aliwahi kua Afisa wa juu wa jeshi pia aliwahi kuwa Raisi wa Taifa la Zaire enzi hizo ambalo kwa sasa linaitwa Congo mwaka 1965- 1997.
Mobutu alipata elimu yake katika shule ya kimishenari na alianza rasmi kazi kama mwanajeshi katika jeshi lenye mchanganyiko wa wabelgiji na wa Congo (The Force Publique) na alipata vyeo kadhaa ikiwemo Sergent major cheo kilichokua kikubwa kwa jamii ya kiafrika.
Alichangia na kuandika makala kadhaa katika gazeti la Léopoldville na baadaye alikua ripota katika gazeti la daily L’Avenir na baadaye alikua Mhariri wa Actualités Africaines.
VIGEZO MUHIMU VYA KUZINGATIA KABLA HUJAANZA BIASHARA YOYOTE.
Biashara ni shughuli ya kuuza bidhaa au huduma kwa lengo la kupata faida. Biashara hii inaweza kuwa katika mfumo rasmi au mfumo usio rasmi. Biashara ni kupata na kukosa na si kupata tu kama wengi wanavyodhani.
Ni kweli zipo changamoto za hapa na pale. Ila Wengi wamekua wakiweweseka wanaposikia mtu anaanzisha biashara, bila kujua ni vigezo gani haswa amezingatia.
Si hivyo tu wapo wanaoanzisha biashara kimakosa na mwisho wanapogundua yapi yalikua makosa yao wanakua wamepoteza muda na mitaji yao na mwisho huzichukia biashara.
U hali gani mpenzi msomaji wa Nyuzi mbalimbali? Naamini unaendelea vema na unapambana kuhakikisha unatimiza yaliyo majukumu yako ya kila siku. Kutimiza ndoto zako yahitaji muda na malengo muhimu na thabiti. Japo vikwazo havikosi, Usife moyo siku zote mambo mazuri yanahitaji muda.
Niendelee kukusihi kuchukua tahadhari madhubuti juu ya Ugonjwa mbaya wa Corona. Fuatilia Taarifa sahihi kutoka kwa wataalamu na matabibu.
Tujikumbushe kidogo tu kwamba Covid_19 ilianza mwishoni mwa mwaka 2019, ambapo visa kadhaa vilianza kuibuka maeneo ya Uchina , Hasa katika jiji la Wuhan.
Pamoja na jitihada kadhaa ambazo zilichukuliwa tangu kipindi kile mpaka sasa ninapoandika uzi huu Bado Corona imebaki kua ni janga ambalo linausumbua ulimwengu, kama ni ndoto basi bado ni usiku wa manane.