Discover and read the best of Twitter Threads about #HabariTech

Most recents (16)

🎁T O R R E N T S, Zinafanya vipi kazi?

Naweka dau langu kwamba ukisikia torrents, kitu kinakuja kichwani mwako ni software, video au audio za wizi (Pirated Files).

Uko sahihi lakini, torrent protocol haihusiana na hivyo tu.

#HabariTech
🎁Torrents ni nini?

Kwanini pirates wanatumia torrents kusambaza na kupakua files zao?

Huduma nyingine za internet zinazoendana na torrents kwanini hazitumiki katika sharing ya pirated files?

Haya maswali yote yanapatiwa majibu kupitia Bittorrent protocol.
🎁Unapofungua browser ili kuperuzi mtandao, browser inatuma request kwenda kwenye server yenye IP address ya website unayotaka kuifikia.

Request hii inaenda kuiomba server ikupe HTML za hiyo website ili uweze kuiona na kufanya kitu unataka.
Read 28 tweets
👽Russia hawataweza kuvuka vikwazo vya Teknolojia

24 February 2022, baada ya Russia kuvamia Ukraine, serikali ya Marekani ilitangaza vikwazo vya kwanza Russia.

Katika vikwazo hivyo vilikuwemo vinavyogusia teknolojia.

#HabariTech
👽Moja ya kikwazo kilisema, "Kuzuia zaidi ya nusu ya uagizaji wa Russia kuingiza teknolojia ya juu nchini mwao, Kuzuia Russia kupata pembejeo muhimu za kiteknolojia, Kudhoofisha msingi wao wa viwanda...
👽...na kudhoofisha matarajio ya kimkakati ya Russia ya kuwa na Ushawishi katika jukwaa la ulimwengu." -mwisho wa nukuu.

Inawezekana ilionekana ni kikwazo kikubwa kwa muda huo. Ila ni kidogo sana ukilinganisha na yaliyofata baada ya hapo.
Read 33 tweets
🍿Nini Kiliwakuta Founders wa Pirates Bay

Pirates bay ni kati ya website bora za kufanya piracy ya Games, Softwares, Movies, Music na aina nyingi ya files zinazokuwepo online.

Ni website ambayo iko kinyume na sheria za hakimiliki na haikutakiwa kuwepo.

#HabariTech
🍿Kampuni nyingi na wanasheria duniani wamejaribu sana kuhakikisha website hii haipatikani mtandaoni bila mafanikio.

Kwa kuwa content zinazokuwepo huko hazikutakiwa kuwepo na mara nyingi zinawakosesha mauzo kwa kuwa ni usambazaji wa content usio sahihi.
🍿Kuna miaka ya nyuma waliwahi fanikiwa kuiondoa online. Bahati mbaya mafanikio yao hayakudumu kwa muda mrefu.

Saa chache baada ya kuondolewa online website ya Pirates bay ilirudi online. Hivyo wakaona wabadili namna ya mashambulizi yao.
Read 41 tweets
⚡Namna ya (ku)bypass restrictions za Channels na bots telegram

Kila mara whatsapp isipopatikana watu wengi hutumia telegram kwa muda.

Ukiacha hivyo telegram imekuwa sehemu nzuri ya kuendesha biashara kama anavyofanya @itzjacton na group la Soko Letu

#HabariTech
Au wanavyofanya @CipherdotM na channel yao ya movies. Kwa wengine telegram ni sehemu ya kupakua miziki ya Spotify, YouTube au Apple Music bila kuwa na account katika platform hizo.

Na wengine wanatumia kupakua movies za Netflix ama Amazon Prime
Bahati mbaya channel & bots nyingi zinazotumia majina na content za kampuni kubwa huwa zinafungiwa na telegram kwa sababu ya ukiukaji wa hakimiliki (copyright infringement).

Telegram wapo kulinda maslahi yao na ya kampuni nyingine, hivyo ni lazima wafanye hivi.
Read 7 tweets
📡Camera Iliyofichwa

Kila siku inayoanza na kuisha kuna watu wanalala Hotelini, lodge, nyumba za wageni na wengine wanakuwa wageni majumbani mwa watu.

Watu wanaofatilia sana movies na conspiracies huwa na wasiwasi wa kuwa recorded na camera zilizofichwa.

#HabariTech
📡Mara nyingi camera zilizofichwa huwa na lengo zuri la kudaka wezi au matukio ambayo yanaweza hatarisha usalama.

Na wakati mwingine camera hizi hufungwa kwa lengo la kutumika kudaka matukio ya faragha ili kusambaza kwa lengo la kumtia mtu aibu au kufanya blackmail.
📡Itakuwa vyema leo nikikujuza kuwa unaweza tumia smartphone yako kujua kama kuna camera zimefichwa katika chumba ulichopo.

MUHIMU: Njia hizi hazihusiana na kutambua camera ya Smartphone iliyofichwa.
Read 16 tweets
🚀Thetan Arena MOBA

Leo tuzungumze kuhusiana na Game moja wapo unayoweza kulipwa kwa kuicheza. Game hii inaitwa Thetan Arena MOBA.

MOBA (Multiplayer Online Battle Arena). Hii ni gam ambayo unacheza kwa kupigana battles na watu wengine Online.

#HabariTech Image
🚀Kumekuwa na P2E games nyingi zilizoundwa hivi karibuni. Nyingi zikiwa na mfumo wa card based na nyingine trading based.

Thetan Arena inatumia mfumo wa battles (yaani kupiganisha characters ndani ya game).

Battles hizi zinapigwa mtandaoni kati ya character wako na wa adui yako Image
🚀Characters wa Thetan Arena tunawaita Heroes. Heroes hawa utawapiganisha katika teams.

Na kwa ushindi unaopata utazawadiwa tokens za game hii ambazo kwa sasa token moja ina thamani ya $4.
Read 26 tweets
✨Kwa sasa simu nyingine zinatumia sim card ile ya card ya kutoa na kuweka.

Ili mtu uwe na namba zaidi ya moja unalazimika kuwa na sim card zaidi ya moja.

eSim itakuja kuondoa hii tabu.

#HabariTech 🧵
✨eSim (Electronic Sim Card au Embedded Sim Card)

Hii ni sim card ambayo unaweza download ya mtandao wowote na kuitumia ndani ya simu yako. Nasema unaweza download kwa maana ya kwamba.

Ndani ya simu yako unakuwa na chip ambayo inafanya kazi kama hizi sim card za kawaida.
✨ili uweze kupata mtandao itakubidi uijaze na taarifa za mtandao husika unaotaka kutumia.

Kwa sasa ukiwa na namba moja ya Voda au Tigo kwenye sim card yako, huwezi ibadili hiyo namba bila kubadili sim card.
Read 7 tweets
📡iOS ni Bora kuzidi Android mbali sana 👀

Hii vita tungewapa silaha nani atashinda? Tuachana na hayo tusifike huko.

Hii mada kila ikiwekwa mezani mashabaki wa hizo OS huongelea sana kwamba wanayotumia wao ni bora.

Je, Ni kweli?

#HabariTech
📡Najua kwamba kuna mtu tayari anajizuia sana mpaka amalize kusoma ndipo ajibu.

Kuwa mpole bro/sis maisha sio vita 😁.

Binafsi mimi ni shabiki mkubwa wa Android na huwezi nibadilisha kwa lolote, ila pale ambapo utaalamu utatumika ukweli lazima usemwe.
📡Kwa sababu hiyo kwa kujiamini kabisa naweza kusema kwamba iOS ni bora kuzidi Android kwa mtumiaji wa kawaida wa simu.

Swali tukiacha liwe na mjadala kwamba ipi bora kuna vitu lazima utasikia kutoka pande zote mbili.
Read 22 tweets
📡Tabia zinazo haribu PC yako kwa haraka.

Sisi sote tunapenda kuona vifaa vyetu kama PC zikidumu kwa muda mrefu, lakini mara nyingi huwa zinaharibika mapema tofauti na mategemeo yetu.

#HabariTech Image
📡Huenda tabia zetu na namna tunatumia hivi vifaa ikawa ni sababu ya hizi mashine kuharibika haraka Image
📡Hakuna kitu kinachodumu milele na hasa vifaa vya elektroniki. Watengenezaji wa vifaa hutengeneza vifaa wakiwa na malengo kwamba kwa matumizi sahihi hicho kifaa kitadumu kwa miaka kadhaa.

Muda huo huwa sahihi ukitumia ipasavyo kwa usahihi.

Nini kinaua PC yako mapema?
Read 23 tweets
📡Part 2: Sim Cards zinaiwezesha vipi simu kufanya kazi?

Simu yako haina maana kama utashindwa kupiga/kupokea simu za kawaida au kutuma SMS.

Unapokuwa na simu utahitaji kuunganishwa na mtandao flani ili kupata huduma ya za simu.

#HabariTech
📡Unapochagua kusajili sim card ya mtandao uupendao unakuwa umesajili akaunti ambayo utakuwa unailipia bando ili kuweza pata huduma zao.

Huwa tunasema SIM Card bila kujua maana yake ni nini.
📡SIM ni kifupi cha Subscriber Identity Module. Ni card ambayo inatunza IMSI (International Mobile Subscriber Identity) na funguo za kumtambulisha na kumthibitisha mtumiaji katika mfumo wa mawasiliano.
Read 18 tweets
📡A.I inajifunza kujitengeneza Yenyewe

Hofu kubwa ya watu duniani ni kuona AI ikiiteka dunia na binadamu tukawa ni watumwa wa AI.

Wenye hofu wengi ni watazamaji wa filamu kama Terminator, iRobot, Transcendence na Matrix.

#HabariTech
📡Lakini wengine ni wale wenye hofu ya kupoteza kazi zao, hasa madereva.

Hakuna wa kumlaumu mtu anayeiogopa AI kwa sababu ni kitu ambacho hata baadhi ya watu wa teknolojia wanashindwa kuelewa vizuri.
📡Miaka 2 iliyopita ungeniuliza iwapo kuna siku AI itaiteka dunia, ningejibu hiv, “Inawezekana iwapo tu tutafikia uwezo wa watu kama Tony Stark wa Iron Man.

Leo baada ya kuelewa AI kidogo nitajibu hivi, “Chochote kinawezekana na haina maana tuache kuboresha kwa sababu ya uoga.”
Read 17 tweets
📡Mass Surveillance Afrika na Duniani kote.

Huu ni uchunguzi ambao unajikita kufatilia umati mkubwa wa watu na mara nyingi huwa kwa kigezo cha kupunguza uharifu na kuzuia ugaidi.

Mass surveillance inasemakana kuanza miaka ya 3800 kabla ya kristo huko Babylon.

#HabariTech Image
📡Kwa vizazi vya sasa Mass Surveillance haikuonekana mpaka miaka ya mwisho ya 1940s baada ya UK na USA walikubaliana kubadilishana taarifa za intelejensia.

Baadae katika makubaliano haya ziliongezeka Canada, Australia na New Zealand na kufanya muunganiko huu kuitwa “Five Eyes”. Image
📡Muungano huu baadae mwaka 1971 ulileta kitu kilichoitwa “Global Surveillance Network” ambayo ilipewa jina la “ECHELON”.

ECHELON ni mtandao maalum wa uliofuatilia mawasiliano ya kijeshi na kidiplomati ya Soviet Union na washirika wake wa Mashariki kipindi cha Vita Baridi. Image
Read 19 tweets
📡Hakuna Tesla iliyotengenezwa China kuingia nchini India.

Hivi karibuni waziri wa usafiri wa barabara nchini India amesem, aliongea na Elon Musk na kumuomba kwamba Tesla kwa za india zitengenezwe nchini India.

Maalumu kabisa hakutaka Tesla za China kuwepo India.

#HabariTech
📡Akongea katika "India Today Conclave 2021", waziri huyo alisema kwamba, Gari za umeme zilizoundwa na Tata Mottors zina ubora unaokaribiana na zile za Tesla.

Hivyo Tesla za kuuzwa India inabidi zitengenezwa ndani ya India na sio China na kuuzwa kutoka India kwenda nchi jirani.
📡Sambamba na hilo alisisitiza kuwa, Tesla watapata sapoti yoyote wanayohitaji kutoka serikali ya India.

Tesla waliomba kupata punguzo la ushuru wa kuingiza gari za umeme India. Mpaka sasa hawajafikia muafaka na serikali ya India kuhusiana na maombi haya yote.
Read 5 tweets
📡Zima hizi settings za windows 10 haraka sana

5 Oct Microsoft waliachia windows 11, lakini hatutegemei watumiaji wake watakuwa wengi kwa sababu ya vigezo vinavyohitajika kuweza tumia Windows 11.

Kuna zaidi ya PC 1 billion zinazotumia windows 10 mpaka sasa duniani.

#HabariTech Image
📡Kati ya watumiaji hawa kuna wengi wasiofahamu baadhi ya settings ambazo zinakusanya taarufa zao, zinawafanya waone matangazo mengi au kufanya PC zao ziwe pole pole.

Ukiacha madhaifu ubora wa Win10 ukilinganisha na zile za nyuma, bado ina madhaifu mengi unakutana nayo kila siku Image
📡Kati ya hayo ni pamoja na kutokuwa na uhuru wa usiri (Privacy) wako, spidi ya OS na urahisi wa kutumia.

Leo tuchambue baadhi ya settings ambazo ni vyema ukaziweka off ili uendelee kutumia Win10 yako kwa raha.
Read 21 tweets
Unaijua simu isiyo na tundu la chaji wa earphone?

Ni kama uhalifu vile namna kampuni za simu zinaleta mabadiliko mapya kila kukicha.

Apple alianza kwa ondoa headphone jack kwenye iPhone 7 na matoleo yaliyofuata na baadae Samsung akafuata.

Kuna cha zaidi? Ndiyo 🧵

#HabariTech
📡Watazamaji wa Sci-Fi movies mtakuwa mmewahi kutana na zile simu ambazo ni kioo tu lakini zinafanya kila kitu.

Huenda huko ni mbali sana kufika labda 2050 huko. Twende mpaka 2030 ambapo nadhani huenda tutakuwa na simu zisizo na button yoyote, headphone jack wala tundu la chaji.
📡Unakumbuka iPhone X ilikuja na notch 2017? ikawa mwanzo wa kubadili muundo wa display za simu. Hapo tayari iPhone hazikuwa na port ya earphone

Oppo F9 ikawa simu ya kwanza kuja na teardrop screen na kumpa mtumiaji nafasi ya kutumia screen nzima.

Na sasa kuna Hole Punch.
Read 17 tweets
Njia rahisi kutunza UZI za twitter uweze zisoma kwa muda wako.

Twitter ni social media pendwa ambayo uhusiano wa watu unaendeshwa kwa mazungumzo ya tweets. Tweets zimekaa kwenye muundo rahisi mtu kusoma.

Bahati mbaya ni rahisi pia tweet kukupotea kama hukuitunza.

🧵#HabariTech
Ushakutana na uzi za @JemsiMunisi au @TOTTechs ?

Unakuta ni uzi flani hivi zina flow matata. Unajiuliza sasa zikipotea hizi nazipata vipi tena?

Usipate tabu tena. Leo nitakupa njia 5 ambazo zinaweza kukusaidia kutunza tweets/uzi unazokutana nazo hapa twitter.

Kana flow eeh!
1. Twitter Bookmark

Hii feature watumiaji wengi wa twitter huwa hawazingatii au hawaijui. Kwa wanaoijua ukifungua bookmark zao utakuta madini ya kutosha huko.

Kuiweka tweet kwenye Bookmark

Gusa "Share" kwenye hiyo tweet unataka save kisha chagua "Add tweet to Bookmark".
Read 11 tweets

Related hashtags

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!