Discover and read the best of Twitter Threads about #mymindspeak

Most recents (12)

THOUGH IT WAS SHORT BUT I'LL NEVER FORGET πŸ’”

Kuna wakati naona kama nilikua character wa hadithi nzuri ya mapenzi iliyoishia njiani, nawaza pengine Mwandishi wa ile hadithi yangu aliishiwa wino na hakuona haja ya kununua kalamu nyingine kumalizia story
#Thread
Kwa kawaida ikifika mwisho wa wiki hasa nyakati za jioni ni mida ya watu kutoka kwenda kuupa mwili pole baada ya heka heka za week ndio maana wengine huita FurahiDay japo kama hauna pesa unaweza kuamua tuu kubaki ndani kama Bulb, inaruhusiwa pia.
Ilikua Ijumaa moja jioni nikiwa home nimechill nikaona nikiendelea kukaa peke yangu naweza nikajikuta nawaaibisha ancestors kwa kutext maEx ovyo. So nikaona nipige mahesabu miguu inipeleke wapi jioni ile na karata ikaangukia kiunga kimoja wanaita IpoIpo.
Read 22 tweets
AN OPEN LETTER TO YOU BROTHER πŸ“œ

Habari za siku kaka , imekua muda mrefu sana bila mawasiliano nadhani ni vile changamoto za maisha zinatuweka mbali lakini kwa kuwa tupo chini ya anga moja natumai ni suala la muda mimi na wewe kukutana
#Thread
Matumaini yangu umzima sana hasa kiafya na harakati zako za kila siku ,ningeweza kukutumia ujumbe mfupi wa maandishi ( sms) au kukupigia simu lakini nikaona kama barua kidogo ingebeba ujumbe na hisia zote zaidi ingekupa muda wa kuitafakari tofauti na ilivo meseji ambapo ingefutwa
Dear brother, nia na dhumuni la barua hii ni kukuuliza kwamba " vipi bado una ari ile ile ya utafutaji? Vipi malengo yako bado yako vile vile? bado una sababu ya kutafuta maisha?
itakua vema kama bado upo yule yule wa zamani aliyekua na malengo mengi sana na molari
Read 18 tweets
HAKUSTAHILI KUPITA NJIA NGUMU KIASI KILE
Wakati mwingine dunia inatuweka darasani kujifunza masomo ambayo hatukuwahi kuwaza kujifunza. Pengine hata mitihani ya hayo masomo hatujui itakuja lini
Tabasamu na uchangamfu wake vilificha mengi lakini hakustahili yale #Thread
Unaweza kuchagua marafiki lakini sio jirani maana wewe utajenga hapa ila atakaekuja kujenga pembeni yako hauwezi kumjua ,hivohivo kwenye kupanga chumba. Nilijikuta nimepanga chumba ambapo nyumba ya jirani waliishi familia nzuri na sisiti kusema nilivutiwa nayo kiukweli
Walikua na furaha muda mwingi .Wazazi walikua wa makamo ya miaka 34 na mtoto mdogo wa miaka 10, kutokana na uchangamfu wangu nikajikuta nimekua rafiki na baba wa hiyo familia ambaye alikua ameajiriwa kwenye kampuni moja hapa Mjini . Aliitwa Mr Beda , nilipenda sana kuwa nae hasa
Read 25 tweets
LET MY MIND SPEAK
So, hakuna kizazi bora kama kizazi chenye wingi wa maarifa na vijana wenye kuchangamkia fursa kila inapotokea.
SHORT THREADπŸ‘‡
My brother @veggiesfarmer once said " We are in knowledge economy,what you know is what will differentiate you and accelerate your growth, your growth will highlight your value and your value will elevate your worth.
Imekua muda mrefu nikitafuta platform ya kuweka kila kitu nlichokua nacho kichwani coz i've a lot man!! My head is about to burst!!
Nimekua nikiandika sana humu twitter but naona haitoshi
Read 9 tweets
WE CAN'T BE THE SAME!!

Yawezakua nyuma yako ikawa mbele yangu, au mbele yako ikawa nyuma yangu. Hii haipingiki na ni ngumu kuikataa.
Safari ni moja ya wote tunapotaka kufika ijapokua tunatofautiana maana ya mafanikio na njia ya kuyafikia
T H R E A D πŸ‘‡πŸΌ
Tusichukuliane poa kabla hatujaijua kesho yako na yangu pia.

Imagine unafanya kazi kujinufaisha wewe peke ako lakini mimi napambana natafuta maisha kwa ajili yangu ya familia yangu pia kwahiyo ukiona sipigi hatua ya maendeleo usishangae HATUWEZI KUWA SAWA.
Wote tunaishi dunia moja chini ya anga moja.
Japo wewe unavaa kupendeza na kuwa mtu anaekwenda na wakati lakini mimi mwenzako navaa kujistiri tuu..Sikulaumu wala sikuonei wivu lakini priorities zetu zinatofautiana sana kuna vingi vya msingi kwangu kuliko kuvaa.Hatuwezi kuwa sawa
Read 12 tweets
AN OPEN LETTER TO MY CRUSH πŸ’Œ

Dear crush,
Nimetuma meseji lakini nachoambulia ni Bluetick lakini najipa moyo pengine unakuaga bize, nikipiga simu mara kadhaa nikikuta inatumika basi najipa moyo utakua unaongea na ndugu yako
Nimeona ni bora leo nikuandikie barua
T H R E A D πŸ‘‡ Image
I hope uko salama
Umekua furaha yangu kila nikikuona ukipita mwenyewe au na wenzio, umekua my mood changer maana nawezakua naskiliza reggae lakini ukipita tuu nahisi nachosikiliza ni blues.
Unaniweza sana dear crush maana simu yangu imejaa screenshots nyingi za picha zako
Wananicheka marafiki jinsi navyokosa kujiamini pale napokuona,
Huwezi amini umetawala kichwa changu nakumbuka ile siku tumekutana ulivonambia nimependeza ilibidi nipite dukani kwa Mangi ninywe soda kwa kujipongeza 😁
My dear, msonyo wako kwangu naona kama busu
Read 14 tweets
I ONCE EXPERIENCED THE POWER OF LOVE ❀

Nilidhani nguvu ya treni kuvuta behewa ndio nguvu kubwa kuwahi kutokea nikapingana na fikra hizo pale nilipowaza nguvu ya maji kunyanyua meli
Nlipingana na hayo pale nilipokumbana na nguvu iliyopo katika fikra za walopendana
T H R E A DπŸ‘‡
Binafsi sijizuii kupenda inapobidi japo haimaanishi siwezi kuishi bila mpenzi, naamanisha kisu changu kina kata vyoote lakini hakikati tamaa tuu
Nikimuhitaji mtu akaona siendani nae, naachana nae najiandaa kwa "come back " kubwa πŸ˜„
Ndio kilichotokea bana enzi hizo nasoma
High school nliwahi kumpenda mtu akahitaji mpaka niwe na funguo tatu " three keys" ya gari, ya nyumba na ya ofisi nkaona nisonge mbele kama injili maana local man ntavitoa wapi vitu ambavyo wengine wanapata wakistaafu πŸ˜‚

So baada ya mission hiyo kufeli nkapenda tena.Story began
Read 30 tweets
AN OPEN LETTER TO MY FUTURE DAUGHTER πŸ’Œ

Dear daughter,
Angekuepo bibi yako ambae pia ni mama yangu leo hii siku ya MAMA duniani basi ingemuhusu yeye zaidi, lakini binafsi nimeona niitumie siku hii kukuandikia barua ili siku ukizaliwa uikute
T H R E A D πŸ‘‡
Nuru ya asubuhi haitofaa kitu bila kuona uso wako. Kifungua kinywa hakitakua na maana bila kupata kumbatio lako pindi unapoamka.

Lile tabasamu lako ukinikaribia ni ishara halisi ya binti shupavu aliyebeba urithi wa asili ya mtu mkarimu wa Afrika.
My daughter wewe ni MAMA AFRICA
Dear daughter, sidhani kama ntachelewa sana au labda ntawahi sana kukuleta duniani, lakini naamini wakati ukifika basi utakuja kuungana nasi.
Sina haraka sana ya kukupata maana nakutafutia mama ambae kwa urembo wake atakutoa binti mzuri ili usije ukamaliza pesa zako kwa make upπŸ˜„
Read 14 tweets
AN OPEN LETTER πŸ’Œ TO MY LOVE

Sweetheart ,
Natumai uko salama, kuandika barua ni utaratibu wa zamani maana ningeweza kukupigia simu au kutuma meseji lakini nimeona vyote hivo visingebeba hisia zangu zote kama ambavyo barua imeweza

T H R E A D πŸ‘‡
Dear love, we ni binadamu wa maana sana kwangu maana umefanyika nuru katika ulimwengu wangu wangu wa huba.
Nilifikiri mwangaza wa jua la asubuhi unaumiza sana macho mpaka nilivokutana na tabasamu lako kutoka kwenye kinywa chenye meno yalopangika vizuri naam ulinivutia❀
Nilidhani apple 🍏 ndio tunda lenye thamani sana mpaka nilivokutana na rangi yako ya chungwa kwenye ngozi inayong'aa
Wanavosema Monalisa ndio mchoro wa thanani sana nadhani hawajaona ile picha yako japo umegeuka mgongo tuu lakini thamani yake ni zaidi ya Pyramids za Misri
Read 17 tweets
AN OPEN LETTER πŸ’Œ TO MY FUTURE SON.

Dear son,
Najua bado upo umening'inia katikati ya mapaja yangu na ndani ya nyonga ya mama yako mtarajiwa. Sijui ntakuleta lini duniani lakini natamani siku utakapokuja basi uikute hii barua yako.
T H R E A D πŸ‘‡
Dear son, natamani nikupate kama mtoto wangu wa kwanza kwenye familia ili ukomavu wako kama mwanaume uwe nuru kwa wadogo zako.
Natamani pia uwe wa pili kuzaliwa baada ya dada yako ili kutokana na yeye kuwa mkubwa wako basi utajifunza kumheshimu kila mwanamke utakae kutana naye
Mpendwa kijana wangu, changamoto ni nyingi sana hapa duniani. Umri wa kukuleta unawezakua umefika lakini wakati wa kukuleta ukawa bado haujafika.

Tizama siwezi kuruhusu kukuleta mapema ndani ya dunia hii chungu kwa mtu ambae bado maisha yake hayana uelekeo endelea kusubiri
Read 14 tweets
THEY BOTH FELL IN LOVE WITH A VET β€πŸ’Š
So
kila mtu hujikuta katika mahusiano kwa namna ya tofauti.Usishangae sana ukiona mtu anatoka jela na mpenzi wa maisha yake. Au hata muharifu akatoka rumande na mpenzi wa maisha yake ambae mwanzo alikua askari wa hiko kituo

T H R E A D πŸ‘‡
Ni katika pirika za kila siku ambapo mioyo miwili iliyoshibana huungana na kutengeneza kitu kimoja cha thamani sana (upendo).
Pirika za kila siku huleta watu pamoja na ule muingiliano wa baina ya watu ndio huongeza ukaribu na mwisho katika hayo mazingira watapatikana wapenzi ❀
Pirika na harakati za kila siku ziliniletea mtu wangu wa muhimu.

Story yangu inaanza wakati ule,nimetoka chuo nimechoka sana halafu jioni maana kile chuo wale wazee kukutoa saa moja jioni hawaoni sooπŸ˜”
So ile nafika home hata kabla sijaamua nakula nin au naanza na kipi
Read 29 tweets
SHE DESERVED LOVE BUT I DECIDED TO RESPECT HER,I WAS WRONG πŸ’”

So guys,heshima na upendo ni vitu viwili ambavyo vinashabihiana.Kuna wakati utadhani unapendwa kumbe una heshimiwa na kuna wakati utaheshimiwa we ukadhani unapedwa
Nilishindwa kujua tofauti yake

T H R E A D πŸ‘‡
This might be my first love story tangia nazaliwa, nilikua na umri mdogo sana lakini ilitosha kunifunza jinsi mapenzi yanavotawala kila rika. Ni zamani sana miaka ile shule ya msingi, shule zetu izi za kawaida so wale wa kupanda school bus inabidi mtuvumilie kidogo kuna vitu
nawezakua nataja humu mkahisi ni ushirikina πŸ˜‚ but we enjoyed that life by the way.
Back in the days primary school nilikua na rafiki yangu wa kike ambae pia alikua ni jirani yangu pale nyumbani.Wote tulikua tunaishi Tabora na elimu yetu ya msingi tulisomea pale. Aliitwa Alice
Read 31 tweets

Related hashtags

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!