Discover and read the best of Twitter Threads about #watunistory

Most recents (24)

"Harakati za shule na kusoma nikajikuta nimepangiwa shule moja huko Mtwara inaitwa Ndanda.

Kiukweli nilikuwa sijawahi kufika na sijui kabisa tamaduni za watu wa kule. Nikasema Tanzania ni moja hakuna sehemu nitashindwa kuishi,
hivyo mwanaume nikajipanga tayari kwenda kuanza safari ya masomo huko.

Kumbuka ile likizo ya kusubiri matokeo ya kwenda kidato cha tano, nilikuwa mtu shamba. Yaani nilipiga sana jembe na kazi nzito kusaidia mishe za home. Hivyo nilikuwa nakula saaana.
Sasa kufika shule, nakuta dishi la msosi yaani ugali ambao ningeweza kumaliza mimi na dada yangu, tunakula wanaume kama saba.

Hili lilinitesa sana aisee kipindi cha kwanza. Nakumbuka ilipita miezi kama mitatu mwanaume sijawahi kushiba.
Read 5 tweets
"Ipo hivi, mimi ni kijana wa miaka 25, nilikuwa na mpenzi wangu ana mtoto sio wangu. Kipindi nipo nae nilikuwa sina kazi na tulikuwa tumepanga tunaishi pamoja lakini yeye alikuwa na kazi. Sasa hakutaka kubeba mimba yangu akihofia hali ngumu ya maisha ambayo ninapitia.
Kile kitendo kikaniumiza sana, nikaja Dar kutafuta maisha, ikawa kila baada ya miezi mitatu narudi nyumbani kumtembelea.

Sasa mwezi wa tisa nikashindwa kwenda kwa wakati, lakini tulikubaliana kwakuwa mkataba ulikuwa karibu kuisha, nimalizie mkataba ndio niende nyumbani.
Kweli, nikaenda mwezi wa 12 ila cha ajabu namkuta na mimba ya mwezi na ananieleza kuwa aliempa mimba hakuwa na mahusiano nae na hamtaki tena.

Kwa hasira nikaondoka, nikamwacha. Ety katoa mimba ananiomba msamahe na turudiane.
Read 4 tweets
"Ilikuwa Jumapili weekend moja nimekaa ghetto kwangu nimefulia mbaya. Simu yangu inaita, kucheck alikuwa mwanangu.

Kupokea ananiambia ana msala inabidi nimsaidie kuu-solve. Inakuaje? nikauliza. Image
Ndio ananiambia amempa mimba binti wa kidato cha nne hivyo anaomba aje kwangu kufanya harakati za kuitoa. Ashaongea na dokta, na dogo yupo tayari bado eneo la tukio tu sababu hawawezi kufanyia hospital.

Daah!nikicheck ni mwanangu sana. Na kwao ana mke na mtoto.
Nikaona sio mbaya nilibebe hili nimsaidie mshkaji. Nikamwabia njoo haina noma.

Walipofika ikabidi niwapishe wafanye yao. Nikakaa zangu nje.

Nikiwa na mawazo mengi na dakika nyingi kupita, mshkaji anakuja kunishtua dogo amezima. Haelewi anayeingia wala anayetoka.
Read 10 tweets
"Ipo hivi mimi ni kijana wa miaka 28 sasa.

Nilipokua chuo mwaka 2018 nikisomea course ya IT nilibahatika kupata mdada ambaye niliishi nae kama mchumba na kumpa mahitaji yote na tulikubaliana tuzae. Image
Basi nikampa kweli ujauzito huku nikimhudumia kwa kila kitu bila wazazi wangu kujua na hakuwahi kukosa kitu alichohitaji kwangu japo sikuwahi kuomba msaada kwa mtu, ila niliendeleza life langu kwa mishe zangu za kitaani(kwa wanaoelewa IT huwa hatukosi mishe za hapa na pale).
Ilipofika mwezi mmoja na nusu kabla ya binti kujifungua alisema anaenda jifungulia nyumbani.

Sikumkataza kwa vile na mimi niliona sitaweza ghaili masomo nisaidie malezi. Hivyo nikamruhusu aende na kumpatia vitu vyote muhimu alivyohitaji kwa ajili ya safari na mambo mengine.
Read 7 tweets
"Kuna demu mmoja nina urafiki nae kiasi kwamba binafsi nikiwa na shida yoyote ananisaidia. Mara nyingi huwa anakuja home hata nguo zangu huwa anafua na usafi anafanya. Chochote nitakachomwambia anafanya.
Alishaniweka wazi kuwa ana ngoma na mambo yake yote huwa hanifichi hata awe na mahusiano basi ataniweka wazi kwa kila kitu hata akalale na huyo mwanaume.

Tatizo linakuja sehemu moja, hatujawahi kuongelea swala la kuwa na mahusiano. Mimi na yeye huwa ni stori za kawaida tu.
Mimi nina mahusiano na demu mwingine na anamfahamu hata nikikosana na demu wangu anakuwa wa kwanza kutusuluhisha. Alishawahi kuolewa wakaachana na mume wake kisa huyo mwanaume alimwambia aache mazoea na mimi akakataa.
Read 10 tweets
"Miaka kadhaa iliyopita Vijana mtaani kwetu waligundua kuwa Kuna mama huwa anaacha wazi madirisha ya nyumba yake pindi akiwa anabadilisha nguo. Ni mama mgeni ambae alikua kahamia miezi michache tu iliyopita.
Alikua akifanya hivyo kila siku mida ya saa moja na nusu usiku akitoka kuoga.

Yule mama MashaAllah alijaliwa shape. Yani alikua na shape moja ya ukorofi sana. Alienda hewani.. huko nyuma ni kama pembe la ng'ombe tuu.. halifichiki.. hatari sana.
Basi Vijana ndo ukawa mchezo wao.. Taarifa ziliponifikia nikawa natamani nikamwambie yule mama kuna raia wanamla chabo maana alikua ni jirani yangu na ananifahamu vizuri tunaheshimiana halafu alikua mwalimu wa shule ya msingi.
Read 9 tweets
"Tangu naanza Shule Ya Msingi, O level na A level Mungu alinijalia Uwezo Mkubwa Darasani. Nikafanikiwa kumaliza kidato cha Sita Vizuri na kuweza kuchaguliwa kujiunga na Chuo kikuu Cha Afya Muhimbili.
Ndipo nilipo anza kuonja joto la kufeli masomo semester ya kwanza nikakamatwa kwenye moja ya somo gumu (Anatomy), second semester Nikapita vizuri, nikarudi October kuja kusapua.

Kutoka na maandalizi duni nikafeli tena nika carry.
Nikaingia mwaka wa pili semester ya Kwanza nikanasa tena kwenye somo moja konk (Micro 1 and 2).
Presha ikanianza kwamba semester inayofuata nikishikwa tena ndo disco.

Semester ya pili nikanasa tena kwenye somo konk (Pharmacology 1 and 2) Ila siku Disco.
Read 9 tweets
"Katika harakati za kutafuta maisha,wanaume huwa tunapitia mambo mengi kweli. Mengine yanabaki mioyoni na kuwa siri zetu.

Nakumbuka baada ya kukosa mishe na harakati za kuingiza hela, nilijikuta naingia kwenye kuuza bangi. Naweza kusema tabia yangu ilisanifu kazi yangu.
Maana nilikuwa mbabe sana na mtu mwenye matukio mengi sana mtaani.

Ilikuwa ni ngumu sana kwangu kupitisha wiki na sijafanya tukio lolote la kibabe au kuogopwa. Hayo ndio yalikuwa maisha yangu.
Kama unavojua hii kazi huwezi kwepa kufuatiliwa na jeshi la polisi, yaani kila muda wanakutamani.

Mimi nimekamatwa na kushtakiwa mara tatu kwa kuuza bangi.
Read 10 tweets
"Kuna story ambayo baba yangu Mzazi (Mzee Eugeni) alinisimulia kuwa kipindi cha nyuma akiwa kijana alikuwa anaishi mwanza kufanya kazi ndogo ndogo katika harakati zake alioa Mwanamke ambaye anaitwa Maria na alipata naye watoto wawili. Image
Mtoto wa kwanza wa kike alikuwa anaitwa Agnes (Eugeni)alizaliwa 1979 na mtoto wa Pili alikuwa anaitwa Ana(Eugeni) alizaliwa 1983.

Mwaka 1984 baba alisafiri kusalimia Nyumbani kwake alipozaliwa ambapo ni Kilimanjaro.
Kutokana na maisha ya kipindi kile alishindwa kurudi Mwanza ilimlazimu yeye kubaki Kilimanjaro ambapo alioa mwanamke mwingine ambaye ni mama yangu mzazi.
Read 6 tweets
"Nimetokea kwenye familia maskini sana na kibaya zaidi ilidharaulika sana, tena kwa pande zote mbili yaani upande wa baba na mama.

Nimekuwa huku kauli za kejeri zinasikika na kuishi masikioni mwangu.
Hilo kwangu ndio lilikuwa tatizo kubwa. Niliwachukia sana jamaa zangu mpaka nimekua mkubwa sikuwahi kuomba msaada wa aina yoyote kwao.

Hadi wazazi wangu niliwahi kuwakataza, niliwaambia shida zote na huduma wanibebeshe mimi.
Kuwaeleza shida zetu, ilikuwa kama kuwalilia njaa kwao.

Leo Mungu amesaidia tunakula kwa muda sahihi na tunalala pazuri. Kiukweli sitamani hata kuwapigia simu. Sasa hivi wamenibadilisha jina wanasema mimi ni jeuri.
Read 4 tweets
"Mwaka 2016 nilipoteza kazi niliyokuwa nimeajiriwa kwa makosa ambayo sikuhusika, lakini upepelezi ulipokuja kufanyika nilionekana ni kama na mimi nilihusika kwenye huo wizi ingawa ukweli sikuhusika.

Sikujua chochote na wala sikula hata sh 100.
Wanasema siku ya kusurubiwa kwako manabii wa uongo watakuja ili kukutolea ushahidi wa uongo lengo uangamie, ndio kilichonitokea mimi.
Baadae ya kupoteza kazi Mungu alinipa ujasiri sana maana sikuwahi kujutia kupoteza kazi bali nilianza kuwaza naishije kwa sasa na nafanya nini ili maisha yaende?.
Read 7 tweets
"Tulikuwa kwenye mahusiano miaka saba. Katika uhusiano wetu nilibahatika kupata mimba yake.

Aliikataa kabisa sio mimba yake. Niliumia sana. Ikabidi nilee mimba mwenyewe, hadi najifungua sikujua alipo na sikuwahi kumuona. Image
Mtoto alipokuwa na mwaka na nusu nilipost picha yake Facebook. Alimuona na akaanza kunifuatilia.

Badae alinitafuta akaja hadi nyumbani na kwa ndugu zangu, akaomba msamaha. Hatukuwa na hiyana nae, tulimsamehe.
Tukalea mtoto mpaka akanunua uwanja. Alianza kujenga na nyumba ilipoisha akanimbia nijiandae tufunge ndoa tumlee mtoto pamoja.

Gafla akaanza kubadilika na mwaka huu akaanza kuniambia kwao ndugu zake hawanitaki hivyo nitafute bwana na anioe na mtoto anamchukua.
Read 6 tweets
“Wakati naanza mwaka wa kwanza pale IFM nilimpa mimba mpenzi wangu. Nilikua naye toka mimi nikiwa Form 5. Bahati mbaya alifeli Form 4 akaishia hapo hapo.

Aliniambia mimba ni yangu na nilikubali nikaanza kuilea ile mimba. Japo tulisumbuana sana kwenye pesa za matumizi kwa sababu
sikua na pesa za kutosha kila kitu kwa wakati huo.

Chuki kwangu ikazidi balaa. Sikuiweka moyoni niliamini ni mimba inamsumbua.

Alienda kwao kujifungua mkoa mwingine. Na akajifungua mtoto wa kiume. Baada ya siku tatu akaniambia mtoto amefariki na baada ya hapo hakupokea simu
zangu tena wala za mama yangu. Mama yangu alilia sana.

Tayari tulishanunua vitu kibao vya kwake na vya mtoto. Kuna namna niliamini huu ni mchezo nimechezewa ila nilikaza maisha yakaendelea. Nikasonga na maisha mapya.

Baadae nikapata mwanamke mwingine na tulipendana sana japo
Read 7 tweets
“Nakumbuka nikiwa shule ya msingi maisha hayakua mazuri. Biashara ya mama yangu ya bagia ikawa ndio inaendesha maisha yetu. Mimi ndio mkubwa na ndiye mtoto wa kiume kwetu. Kwa kipindi hicho mdogo wangu wa kike alikua bado mdogo sana.

Ilinibidi nisaidiane na mama kuuza bagia. Image
Nikitoka shule nakuta zimeshatayarishwa nabeba sufuria natembeza mpaka vijiji vya jirani. Nahakikisha zimeisha ndipo narudi nyumbani.

Utaratibu ulikua ni huo huo tangu darasa la tatu hadi form three. Nakumbuka wenzangu walikua wananicheka. Nilikosa marafiki.
Kila mtu alikua ananitenga na kunidhihaki kwamba mtoto wa kiume nabebaje sufuria na kwenda kuuza bagia. Walisema ni kazi za kike.

Ilifika muda nikikuta wenzangubwanapiga stori nikifika tu wote wanatawanyika. Nabaki mnyonge.
Read 4 tweets
“Hii siri nitaitunza mpaka lini? Nibaki nayo au nijisalimishe?

Nilikuja Dar kutokea kijijini kupambania ugali. Mungu mwema mitikasi ilikubali. Kama unavyojua tena jiji la Dar wanawake warembo kila kona. Ni kama nilikua na ngekewa kila nilipotupa ndoano ilinasa. Nilijichanganya
nilitembea na kila aina ya mwanamke niliyemtamani.

Katika haya mahangaiko nilikutana na dada mmoja wa Songea. Huyu dada alikuja kunieleza amepata mjamzito. Ila akawa ameenda kwao Songea. Nilikua nikituma matumizi ila ilifika mahali mawasiliano yalikufa. Sikumpata tena. Ni miaka
mitano sasa sina mawasiliano yoyote sijui alipoteleaga wapi.

Maisha yaliendelea huku Dar nikakutana tena na mwanamke kutoka Kahama. Na yeye akapata ujauzito. Alirudi kwao Kahama pia ila mawasiliano yaliendelea kuwepo.

Ulifika muda nikaona hii njia sio sahihi. Nikabadilika
Read 5 tweets
"Wakati nakutana na mpenzi wangu ambaye kwa sasa ni mchumba wangu na tutaoana sio mda mrefu, nilimwambia kabisa mimi sina mapenzi ya maonyesho.

Sinaga habari za mitoko wala kupostiana kuandikiana caption za makopakopa. Wewe ukitaka kutoka, toka na rafiki zako. Wala sitajalii. Image
Me nifanyie vitu vya kawaida tu kabsa nitafurahi sana.

Nina amini katika mahusiano ya siri na yenye staha. Kupostiana watu huleta chuki na maneno ambayo hayapo.
Wengine wana vijicho, wanataka mazuri unayopata wewe na yeye ayapate. Mpenzi wako anakupost kwa mapenzi tu ila unakuta mtu wivu unamshika anaanza kujipendekeza kwake.

Na wanaume sio wa kustahimili vishawishi na hapo ndoa ndio inaanza kuwa ngumu.
Read 4 tweets
Baada ya kumaliza shule nilimpata binti niliyeamini atakuwa wa maisha yangu alikuwa anaitwa Mwajuma, hapo ndio kwanza nilikuwa ninaanza kuingia katika ulimwengu wa mapenzi.
Sikuwa ninaelewa kabisa kuhusu maana ya neno penzi, watu waliotabiri mwisho wangu na Mwajuma niliamini kuwa ni wanafiki na walikuwa na malengo mabaya dhidi yetu.
Siku zilivyozidi kusonga penzi letu lilizidi kustawi kama bustani iliyokuwa inasimamiwa vizuri, tulipanga hadi kutambulishana kwa wazazi.
Read 7 tweets
"Tulifanya interview kutafuta mtu wa finance katika kampuni yetu. Tulipokea maombi mengi, watu tano ndio walifanikiwa kupigiwa simu na kuitwa kwa ajili ya usahili.

Wote walifika. Kila mtu alipangiwa muda wake. Image
Nakumbuka kuna kijana alikuja amependeza, yuko smart na alikuwa na vigezo vyote vya kupata ajira.

Alikuwa na madaha na majivuno ya hapa na pale wakati tunafanya nae interview. Alitaka mshahara wake usishuke si chini ya milioni moja na laki tano.
Alisema bila mshahara huo hawezi kutoka kwenye kampuni anayoifanyia kazi.

Hatukuwa na hiyo hela. Hivyo tulimchagua mtu mwingine ambaye tulielewana nae.
Read 5 tweets
1/10 “Naitwa William Adam Lukoo ,mzaliwa wa mkoa wa Morogoro. Mwaka 2003 familia yetu ilihamia jijini Tanga kwa ajili ya harakati za kimaisha. Haikua rahis kwa sababu ya ugeni lakini wazazi walipambana kuhakikisha napata elimu bora. Licha ya kutoka kwenye familia ya kimaskini...
2/10 ..nilihakikisha nafanya vizuri kwenye masomo kiasi cha kuwavutia walimu na kujizolea umaarufu shuleni. Nilifanikiwa kuhitimu mwaka 2010 shule ya msingi Majani Mapana wilayani Tanga mjini. Mwaka 2011 nilianza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Usagara..
3/10 ..lakini kutokana na ugumu wa maisha, wazazi wangu wote hawakuwa na kazi. Ikawalazimu kufikia hatua ya kuuza vitu vya ndani ili kuweza kunilipia ada. Maisha yalikuwa magumu mno nyumbani kiasi cha kufikia hatua ya kushindwa kupata chakula na kodi.
Read 8 tweets
"Kipindi nipo nyumbani Mwanza, nilikuwa napigiwa simu na Kaka mmoja ambaye nilikuwa nafahamiana nae sana. Alikuwa ananiomba nije sana Kahama akiwa na ahadi ya kunipa kazi, kunipangishia nyumba na ahadi nyingine nyingi nzuri.
Siku niliyofika kahama, nilifikia guest house. Yule kaka ndiye aliyenipokea, hivyo nililala nae na mambo mengine ya chumbani yalifanyika.

Alivyoondoka asubuhi ndio ilikuwa mwisho kunipigia simu. Nikawa kila nikimtafuta naambulia matusi tu. Hakunipa chochote kama alivyoniahidi.
Kwa bahati nzuri nilivyotoka nyumbani Mwanza nilikuwa na akiba ya kama elfu 60.

Ilibidi niingie mtaani kutafuta kazi mimi mwenyewe, kwa maana nisingeweza kurudi tena Mwanza, Ningeambia nini watu maana nilikuwa nimeshaaga.
Read 4 tweets
Nimeona bora niongee na kuomba ushauri wenu kwani nimekaa kimya siku nyingi. Hali inazidi kuwa mbaya. Nazidi kudhoofika kisaikolojia na imefikia hatua Kuna mawazo mabaya yananijia kichwani.
Ni hivi, nilikua na biashara zangu kama tatu hivi nilizokua naziendesha zikiwa eneo moja. Kwa kuwa mimi ni mwalimu wa shule binafsi (private school) muda mwingi nashinda kazini, Hivyo msimamizi mkuu wa biashara zangu alikuwa mke wangu.
Mwezi wa 7 wakati wa likizo ya Corona mke wangu alisafiri kwenda nyumbani kusalimia.

Nikawa nasimamia mimi mwenyewe.

Shule zikafunguliwa huku mke wangu akiwa bado hajarudi.
Read 9 tweets
1/3 Mimi ni kijana wa kiume natokea Geita. Mwaka 2011 baada ya kumaliza O-level. Kipindi nangoja matokeo nilipata rafiki wa kike kwa njia ya redio. Sikumbuki ilikua redio gani ila ni kipindi cha kutafuta marafiki. Tulizoeana sana, nae alikua mwanafunzi. Alinitafuta kila alipotoka Image
2/3 ..shule na kabla ya kwenda pia, alinitumia pesa nilipokua na shida. Tuliishi kama marafiki maana niliogopa kumtongoza. Hata sura yake sikua naifahamu, alinijali sana, alikua ndio faraja yangu. Siku ya mwisho kuwasiliana nae ilikua mida ya saa tano asubuhi alinitumia please..
3/3 ..call me kama mara 3 na haikua kawaida yake. Usiku nilipoweka salio nilimtafuta ila sikumpata mpaka leo takribani miaka 9 sasa. Sitamsahau maana alionyesha kunijali sana wakati hanijui hata nafanana vipi.” #WatuNiStory
Read 3 tweets
"Niliwahi kuanzisha kundi la wasanii watatu ambao kwa pamoja tulikubaliana kuwa mimi ndio nitakuwa nasimamia kazi zao.

Baada ya kutoa wimbo na kuanza kukubalika kila sehemu, uliweza kumfikia hadi Marehemu Ruge na aliupenda, Image
aliwapa ahadi wasanii wale kwenda Dar kufanya kazi nyingine zaidi.

Baada ya hapo wakaanza kunizimia simu na hata salamu walikuwa hawatoi nikikutana nao kitaa.
Kwa bahati mbaya lile dili lao halikuweza kufanikiwa, hivyo wakabaki wanazurura tu mtaani na kurudi kwangu walikuwa wanaona noma". Producer Crash Designer, Kahama.
#MchongoLive
#WatuNiStory
Read 3 tweets
1/5 “Nilisoma chuo UDSM hadi mwaka wa tatu lakini sikuhitimu. Sikuhitimu kwa sababu ukweli ni kwamba, sikuzingatia masomo ipasavyo, nilipata ajira nikashindwa ku-balance kati ya shule na kazi. Nikaishia kufeli mitihani kadhaa. Ilikua nihitimu mwaka 2015. Miaka yote nimeendelea.. Image
2/5 ...kufanya kazi mbalimbali kwa kutegemea kipaji changu tu. Japo kuna nyakati nilikosa kazi zilizohitaji mtu mwenye degree na sikua na hizo sifa. Ni jambo ambalo limekua likiniumiza na kunifanya nijiskie vibaya. Familia yangu pia iliumizwa na hilo sababu walilipa ada miaka..
3/5 ..yote mitatu ya chuo. Na niliumia sana kuiumiza familia yangu. Namshukuru Mungu mwaka huu baba yangu amenipa nafasi tena ya kurudi chuo na kunilipia ada. Nime-apply tayari nangoja majibu. Japo naona kama miaka mingi imeshapita, nina miaka 28 sasa..
Read 5 tweets

Related hashtags

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!