Wiki hii nilikuwa busy sana baada ya kufiwa na Jirani yangu ambaye tulikuwa na ukaribu sana.
Ilinibidi kwenda mpaka kijiji cha MBASA Ifakara kumzika jirani huyu.
Msiba huu umenifunza mengi..
Tuna familia za Kipumbavu sana sisi waafrika.
Nimethibitisha hili👇
Jirani yangu alifanikiwa kujenga mjini nyumba ya kawaida tu.
Lakini kwenye familia yao ndiye alikuwa mtu pekee aliyethubutu kufanya hivyo Mjini Dar
Jamaa ameacha watoto wawili wadogo na mkewe akiwa mjauzito.
Shida ilianza tangu Hospitalini Muhimbili
Wakati mkewe akidamka na ujauzito wake na kushinda hospitali, Familia ya mume ikawa inamsema kuwa hana msaada wowote kwa ndugu yao.
Mjane wa watu akaamua kuwaita wazazi wake wamsaidie kuuguza wajinga wakasema kajaza watu kwenye nyumba ya kaka yao.
Siku aliyofariki mmewe, jambo la kwanza ndugu wakampokonya simu ya marehemu mjane. Pia wakampokonya mjane simu aliyokuwa amenunuliwa na marehemu mumewe.
Bila soni mdogo wa marehemu ndiyo anatumia simu hiyo kwa amani kabisa.
Sasa tuendelee
• • •
Missing some Tweet in this thread? You can try to
force a refresh
Wakili Fatuma Karume alisafiri kutoka Dar kwenda mkoani Kilimanjaro.
Wakili huyu alikuwa amesafiri akiwa amebeba nyaraka furani ya muhimu.
Nyaraka ile alikuwa anaenda kumsomea na kumkabidhi mzee fulani aliyefahamika kwa jina la Juma
Actually, Mzee Juma naye alikuwa ni wakili ambaye sasa amestaafu akiwa amefanikiwa kurithisha taaluma hiyo pia kwa mwanae ambaye alikuja kuwa ni wakili maarufu sana mkoni Arusha.
Fatma hakujua kama nyaraka aliyobeba ingeleta taflani kubwa ndani ya familia ya Mzee Juma.
Fatma aliwasili nyumbani kwa ambako alikuta waombolezaji ambao walikusanyika baada ya kusambaa taarifa za msiba za mmoja wa watoto wa Mzee Juma.
Fatma alitegemea kuikuta hali hii nyumbani pale na hata safari yake ilitokana na yeye kupata taarifa hizi.
Nimesikiliza hotuba ya leo ya mheshimiwa rais, na hii ndio analysis yangu.
1. Hotuba hii imekuja siku chache baada ya rais kuviagiza vyombo vyake vya ilinzi vimpelekee taarifa ya nini kilicho nyuma ya matukio ya utekaji na mauaji hasa baada ya kifo cha Ali Kibao
2. Inaonekana rais alipokea ripoti hii mapema kama alivyoagiza na yafuatayo ndiyo yalikuwa ndani ya ripoti hiyo:
(a)Kuwa haya yote anayoyasikia juu ya mauaji na utekaji, ni zao ya kikao cha siri kililichofanyikia Ngurero mkoani Arusha mnamo Sept 11, 2024
(b) Maazimio ya kikao kile yaliamua kutumia vibaya 4R alizoziasisi mheshimiwa rais ili kuzua ghasia nchini, kufitini jeshi la polisi na kufanya fujo misibani.
Kama ripoti hii ni sahii, kuna mambo yanayohitaji ufafanuzi..
Satiiva ammedai kumtambua Mafwele kama mtu aliyeenda usiku kwa Land Cruiser kwenye karakana ya polisi Oysterbay alipotekwa
Kuwa ndiye mtu mwembamba, mkakamavu, aliyekuwa kavaa Jezi ya Simba na pensi
Amemtambua baada ya kuona picha ya Mafwele ikisambaa mtandaoni.
Pia Sativa ameshaujulisha uongozi wa Jeshi la polisi juu ya utayari wake wa kuhojiwa na jeshi hilo ili kuwashirikisha anachokifahamu nyuma ya kutekwa kwake.
Jeshi limemjibu likipata nafasi litamuita kumuhoji
Lakini ni jeshi hilihili, lilipata nafasi ya kunitumia timu ya makachero watatu, mmoja akiwa wa cheo kikubwa cha SACP, Mwingine akiwa ni katibu wa DCI, kusafiri kutoka makao makuu ya polisi Dodoma hadi Central DarEsSalaam kunihoji habari za ASP Fatuma Kigondo.
Kifo cha Ali Kibao kimekuwa ni kama sauti ya wote waliokuwa wanabeza kuwa hakuna matendo ya utekaji na summary executions nchini.
Ni sauti iliyowasemea victims wote wa matendo haya.
Lakini pia kinaweza kuleta mwanga kwa kuwa sasa watu wameanza kugusia jambo fulani muhimu.
Jambo la kwanza kugusiwa ni dai la kuundwa kwa chombo huru kinachotakiwa kuufatilia utendaji wa jeshi la polisi.
Majirani zetu nchini Kenya wanacho chombo hiki kwa jina la IPOA
Independent Policing Oversight Authority
Nini umuhimu wa kuwa na chombo hiki?
Ni kwa sababu si rahisi kujichunguza kwa uhuru dhidi ya tuhuma unazotuhumiwa wewe mwenyewe.
Watu wanaojitambulisha kama askari polisi, ndio wanaotuhumiwa kwa utekaji na mauji hivyo haiwezekani hata kidogo chombo hiki kikaachwa kijichunguze chenyewe kisha tutarajie majibu chanya.
Imeshathibitika kuwa, watu wanaojitambulisha kuwa ni askari wanaweza kumkamata mtu mbele ya watu, kuondoka naye na baadaye unakuja kupatikana mwili wake usio na uhai au asionekane kabisa.
Pia kwa kuwa @tanpol wameishia kutoa matamko bila suluhisho..
Yafuatayo ndiyo mambo tutakiwayo kufanya wote kwa pamoja ili kuokoa maisha ya wengine.
Kwani wakimaliza kwa huyo, wewe ndie utakayefata
1. Kataa kabisa kukamatwa kwa sasa hata kama utatolewa kitambulisho. Piga kelele zote uwezavyo, fanya fujo kwani upole wako hautakusaidia.
2. Kama mtu anakamatwa eneo la watu wengi, wengine saidieni kwa kuongeza fujo, kuhoji makosa yake na kuwarekodi kwa simu zenu wakamataji.
MSIOGOPE: Ni wao ndio wametufikisha kwenye ujeuri kwa ajili ya maisha yetu.
Kuna kitu fulani wataalamu wa siasa hukiita "Political Paranoia"
Paranoia ni ugonjwa wa akili ambapo mgonjwa huwa na wasiwasi mkubwa kuwa kuna watu wanamfatilia mambo yake, wanapanga kibaya juu yake, wanamdanganya etc
UZI👇
CHOCHORO ZA MADARAKA -2
Mgonjwa wa Paranoia mara nyingi hutuhumu watu fulani wana njama fulani dhidi yake.
Hata jambo fulani ambalo linaweza kutokea kwa bahati mbaya (just coincidence) ambavyo hata watu wengine huamini hivyo, lakini mgonjwa wa paranoia huamini si bahati mbaya bali makusudi.
Viongozi wengi barani Afrika, ni Paranoid.
Muda wote hutembea na hisia kuwa kundi fulani linakula njama za kuwatoa madarakani
Hii ndio maana unaona wengi wa viongozi hawa hupanga na kupangua safu za wasaidizi wao.