Fortunatus Buyobe Profile picture
Pool of thoughts. A commander of the hand to mouth battalion. Environmental Pioneer. Social Engineer. #CertifiedMchapaUzi . Telegram: https://t.co/aEEOOryJWO
Hangi ๐Ÿ“ฟ Profile picture Mjukuu Profile picture peter August Profile picture Kendrick Profile picture Mc_Carl Profile picture 16 subscribed
Sep 17 โ€ข 12 tweets โ€ข 2 min read
Nimesikiliza hotuba ya leo ya mheshimiwa rais, na hii ndio analysis yangu.

1. Hotuba hii imekuja siku chache baada ya rais kuviagiza vyombo vyake vya ilinzi vimpelekee taarifa ya nini kilicho nyuma ya matukio ya utekaji na mauaji hasa baada ya kifo cha Ali Kibao 2. Inaonekana rais alipokea ripoti hii mapema kama alivyoagiza na yafuatayo ndiyo yalikuwa ndani ya ripoti hiyo:

(a)Kuwa haya yote anayoyasikia juu ya mauaji na utekaji, ni zao ya kikao cha siri kililichofanyikia Ngurero mkoani Arusha mnamo Sept 11, 2024
Sep 10 โ€ข 7 tweets โ€ข 3 min read
Satiiva ammedai kumtambua Mafwele kama mtu aliyeenda usiku kwa Land Cruiser kwenye karakana ya polisi Oysterbay alipotekwa

Kuwa ndiye mtu mwembamba, mkakamavu, aliyekuwa kavaa Jezi ya Simba na pensi

Amemtambua baada ya kuona picha ya Mafwele ikisambaa mtandaoni. Image Pia Sativa ameshaujulisha uongozi wa Jeshi la polisi juu ya utayari wake wa kuhojiwa na jeshi hilo ili kuwashirikisha anachokifahamu nyuma ya kutekwa kwake.

Jeshi limemjibu likipata nafasi litamuita kumuhoji Image
Sep 10 โ€ข 41 tweets โ€ข 14 min read
Kifo cha Ali Kibao kimekuwa ni kama sauti ya wote waliokuwa wanabeza kuwa hakuna matendo ya utekaji na summary executions nchini.

Ni sauti iliyowasemea victims wote wa matendo haya.

Lakini pia kinaweza kuleta mwanga kwa kuwa sasa watu wameanza kugusia jambo fulani muhimu. Image Jambo la kwanza kugusiwa ni dai la kuundwa kwa chombo huru kinachotakiwa kuufatilia utendaji wa jeshi la polisi.

Majirani zetu nchini Kenya wanacho chombo hiki kwa jina la IPOA

Independent Policing Oversight Authority

Nini umuhimu wa kuwa na chombo hiki? Image
Sep 8 โ€ข 11 tweets โ€ข 2 min read
SECURITY TIPS TO HOOFMEN

Imeshathibitika kuwa, watu wanaojitambulisha kuwa ni askari wanaweza kumkamata mtu mbele ya watu, kuondoka naye na baadaye unakuja kupatikana mwili wake usio na uhai au asionekane kabisa.

Pia kwa kuwa @tanpol wameishia kutoa matamko bila suluhisho.. Yafuatayo ndiyo mambo tutakiwayo kufanya wote kwa pamoja ili kuokoa maisha ya wengine.

Kwani wakimaliza kwa huyo, wewe ndie utakayefata

1. Kataa kabisa kukamatwa kwa sasa hata kama utatolewa kitambulisho. Piga kelele zote uwezavyo, fanya fujo kwani upole wako hautakusaidia.
Jul 31 โ€ข 21 tweets โ€ข 8 min read
Kuna kitu fulani wataalamu wa siasa hukiita "Political Paranoia"

Paranoia ni ugonjwa wa akili ambapo mgonjwa huwa na wasiwasi mkubwa kuwa kuna watu wanamfatilia mambo yake, wanapanga kibaya juu yake, wanamdanganya etc

UZI๐Ÿ‘‡

CHOCHORO ZA MADARAKA -2 Image Mgonjwa wa Paranoia mara nyingi hutuhumu watu fulani wana njama fulani dhidi yake.

Hata jambo fulani ambalo linaweza kutokea kwa bahati mbaya (just coincidence) ambavyo hata watu wengine huamini hivyo, lakini mgonjwa wa paranoia huamini si bahati mbaya bali makusudi. Image
Jul 17 โ€ข 7 tweets โ€ข 2 min read
Kwako mpedwa Mama,

Naamini u mzima wa afya ukiendelea na majukumu yako.

Mimi mwanao, naandika barua hii nikiwa ndani ya simanzi kubwa kama mwakilishi wa tabaka la vijana tunajipatia ridhiki zetu kwa jasho na damu.

Sio siri Mama, maisha yetu ni magumu sana

Hata hivyo... Mama, kuna kitu kinasikitisha sana jinsi pesa yetu ya urithi aliyotuachia baba inavyofujwa na kina dada na kaka, wajomba na majirani.

Mama unafahamu kuwa juzi dada alitupunguzia baadhi ya huduma kwenye kitita cha bima yetu ya afya.

Alitueleza unafanya vile kutokana na ukata.
Jul 12 โ€ข 5 tweets โ€ข 1 min read
Fanya haya
1. Amini Mungu yupo
2.Mpende jirani yako
3.Fanya kazi kwa bidii
4.Saidia wenye uhitaji

Acha haya
1.Usitegemee miujiza (Haipo) kwani chochote kinachokutokea kiwe kizuri au kibaya ni reality of life na hakuna mwanadamu aliyekifanya kiwe

2.Usiabudu sanamu(mafuta, maji) Image Uzi wa jana nimejaribu kutumia maneno makali na reasoning ya ajabu.

Sikufanya hivi kwa malengo mabaya au labda useme mimi ni mpagani

Nikifanya vile kwa lengo la kutaka tuamke.

Hizi dini mpya mpya ni scam

Why not Mwakasege, Moslems, RC, Anglican, and Lutheran?
May 16 โ€ข 29 tweets โ€ข 10 min read
"๐Š๐š๐š๐š๐š! ๐Š๐š๐ค๐š ๐ฒ๐š๐ง๐ ๐ฎ..๐ƒ๐š๐ฆ๐ฎ ๐ฒ๐š๐ง๐ ๐ฎ ๐ฎ๐ฆ๐ž๐ž๐ง๐๐š ๐ค๐ฎ๐Ÿ๐ข๐š ๐ง๐ฒ๐ฎ๐ฆ๐›๐š๐ง๐ข....

"๐“๐ฎ๐ง๐ ๐ž๐ค๐ฎ๐ฐ๐ž๐ฉ๐จ ๐ญ๐ฎ๐ง๐ ๐ž๐ฐ๐ž๐ณ๐š ๐ค๐ฎ๐ค๐ฎ๐ฅ๐ข๐ง๐๐š. ๐’๐ข๐ฃ๐ฎ๐ข ๐ง๐ข๐ญ๐š๐ข๐ฌ๐ก๐ข๐ฃ๐ž ๐›๐ข๐ฅ๐š ๐ฐ๐ž๐ฐ๐ž..๐’๐š๐ฌ๐š ๐ง๐š๐ž๐ฅ๐ž๐ฐ๐š ๐ค๐ฐ๐š ๐ง๐ข๐ง๐ข ๐ฎ๐ฅ๐ข๐ค๐š๐ฌ๐ข๐ซ๐ข๐ค๐š ๐ง๐ข๐ฅ๐ข๐ฉ๐จ๐ฌ๐ก๐ข๐ง๐๐ฐ๐š ๐ค๐ฎ๐ญ๐จ๐ค๐ž๐š ๐ค๐ฐ๐ž๐ง๐ฒ๐ž ๐ฆ๐ข๐š๐๐ข ๐ฒ๐ž๐ญ๐ฎ ๐ฒ๐š ๐ฆ๐ฐ๐ข๐ฌ๐ก๐จ..๐Š๐ฎ๐ฆ๐›๐ž ๐ฎ๐ฅ๐ข๐ญ๐š๐ค๐š ๐ญ๐ฎ๐š๐ ๐š๐ง๐ž..๐๐ข๐ค๐จ ๐ง๐ฃ๐ข๐š๐ง๐ข ๐ค๐ฐ๐ž๐ง๐๐š ๐ค๐ฎ๐ฆ๐Ÿ๐š๐ซ๐ข๐ฃ๐ข ๐ฆ๐š๐ฆ๐š"

Haya si maneno yangu!Image Haya ni maneno ya Joe akiomboleza kifo cha utata cha kaka yake katika ukurasa wake wa Instagram.

Mazingira nyuma ya kifo cha kaka yake yamemuachia Joe kitendawili Kigumu. Image
Mar 7 โ€ข 39 tweets โ€ข 12 min read
Miriam Mirita akiwa makwaya akipambana na kesi yake, mama mkwe wake akafungua kesi mahakama ya Arusha kuomba Miriam atolewe kama msimamizi wa mirathi na badala yake awe yeye.

Sababu ikiwa ni kushindwa kuorodhesha mali za marehemu na kufunga mirathi. Image Ni katika wakati huu, mtoto wa kwanza wa Bilionea Msuya alisikika akilalamika kuwa wameondolewa nyumbani na ndugu wa upande wa baba yake nyumba zote kutiwa kufuli. Image
Jan 24 โ€ข 48 tweets โ€ข 17 min read
Before writing this masterpiece to this X street, I gave myself ample opportunity to scrutinize and verify the facts.

The matter beforehand today is fragile as it can defame someone's business and reputation.

But why should I lie when I can speak the Truth?

Tariq M. Machibya Image Bwana Tariq Machibya alipofikishwa mahakamani kwa kuendesha biashara ya upatu, watu wengi tulimuhurumia kwa kuhisi Serikali inamuonea kijana mdogo mjasiliamali.

Kijana ambaye alibeba ndoto na maono ya wenye mitaji wasiojua pa kuwekeza.

Some sort of financial intermediary

Alas! Image
Dec 13, 2023 โ€ข 43 tweets โ€ข 15 min read
Naam!

Aliyekuwa mke wa marehemu bilionea Msuya anayeshitakiwa kwa mauaji ya wifi yake Aneth Msuya inakaribia ukingoni.

Dalili za "kutema ngeze" ziko wazi baada ya wazee wa baraza kutoa maoni haioni hatia dhidi yake.

Uzi huu ni mtiririko wa matukio A-Z

Image
Image
Image
Usiku wa manane kuamkia 26 july 2013,ndugu WILLY MUSHI ONESMO anapigwa risasi na kufariki akiwa kazini

WILLY MUSHI ONESMO alikuwa ni mfanyakazi wa mgodi wa madini TANZANITE ONE huko MIRERANI Simanjiro. Image
Nov 30, 2023 โ€ข 31 tweets โ€ข 11 min read
Bado nipo kwenye coma nikijiuliza kama kulikuwa na ulazima wowote kwa askari huyu kuingia na mtutu wa bunduki kwenye eneo la starehe.

Bado najiuliza,

Kulikuwa na ulazima wa kumuelekezea bunduki namna hii yeyote awaye(hata kama ni kahaba) ambaye hajainua silaha yoyote

Najiuliza Image Kuna mambo mengi yamekuwa yakifanywa na polisi kiholela sana.

Moja ya mambo haya ni kazi ya kukamata walevi au wenye bar wakipitisha muda wa kufunga bar.

Polisi hapaswi kukamata kosa hili bila kuwepo kwa mlalamikaji ambaye ni afisa biashara wa manispaa aliyetoa leseni ya kileo Image
Nov 16, 2023 โ€ข 23 tweets โ€ข 10 min read
KUWENI MAKINI NA MCHANGA WA KABURINI:

#X-Ushirikina

Kuna watu wamepata nuksi, mikosi na mabalaa makubwa katika maisha yao kwa sababu ya matumizi ya mchanga wa makaburini bila kuzingatia au kufuata maelekezo. Image Unapokuwa unafanya kitu chochote kile kinacho yahusisha makaburi, iwe ni kutumia mchanga, kuzika vitu, kuoga, kuchoma ama kutambika, unatakiwa kuwa makini sana na kufuata na kuzingatia kanuni na taratibu zake kwa sababu usipo zingatia hayo yatakupata makubwa. Image
Nov 7, 2023 โ€ข 55 tweets โ€ข 17 min read
Miaka minne iliyopita, Jimmy Kizota alishitakiwa kwa kosa la kumuua mchumba wake aliyekuwa akiishi naye jijini Dar es salaam.

Ni baada ya kumfumania akifanya mapenzi na mwanaume mwingine sebuleni kwao aliporudi nyumbani ghafla akitokea kazini majira ya saa tano asubuhi. Image Mwanaume aliyefumaniwa alifanikia kumzidi nguvu Jimmy na kukimbia

Wivu na hasira kaishia kwa kumpiga mchumba wake hadi akapoteza fahamu.

Baadae mwanamke huyu akafariki akipatiwa matibabu hospitali.

Jimmy akashitakiwa kwa mauaji ya kukusudia

Kesi ilimkalia vibaya sana Image
Nov 6, 2023 โ€ข 11 tweets โ€ข 4 min read
Ndani ya behewa moja, kulikuwa na abiria aliyekuwa ametulia kimya kwenye kiti akiwaangalia abiria wenzake waliokuwa kwenye harakati za kushuka.

Mtu huyo aliyeonekana kutokuwa na haraka, alikuwa amekaa kwa kuuegemeza mguu mmoja juu ya mwenzake kama bado akiendelea na safari. Image Mtu huyo ambaye safari yake ilianzia kituo cha treni cha Kingorwila Morogoro, alipanda akiwa hana mzigo wowote aliobeba mkononi

Tangu anaingia hadi kupata siti kwenye behewa aliloingia, hakuzungumza na abiria yeyote, hakuinuka kwenda kokote, hakutikisika wala kumwangalia yeyote. Image
Nov 5, 2023 โ€ข 49 tweets โ€ข 16 min read
Kitendo cha mtu huyu kuingia bila kupiga hodi kwenye ofisi yake ya mapokezi,kilimshitua binti huyu.

Mwonekano wa mtu huyo ulimfanya binti huyo aamini huyu si mgeni wa ofisi yake bali amekosea njia kwani ilikiwa ni mara ya kwanza kumuona mtu yule

Binti akagundua jambo lingine Image Sura ya mgeni yule haikuwa ya kiungwana.

Alionekana kutoyafurahia maisha kwa ujumla

Binti akabaki akimtazama mgeni huyu akisubiri kuombwa msamaha wa kukosea ofisi

Haikuwa vile!

"Jimmy yupo?" Aliuliza mgeni yule bila ya salamu

Ikawa zamu ya binti kushangaa Image
Oct 27, 2023 โ€ข 28 tweets โ€ข 10 min read
Taarifa alizozipata rais Kabila baada ya kushikiliwa kwa wale wamarekani zilimshtua sana,

Hakuchukua muda wakati akitafakari taarifa ile ili kujua cha kumfanya, zikaja habari za kuvushwa mzigo mwingine wa tani 2.5

Akatanguliza timu yake ya mawaziri wakamuone raisi Kibaki Image Rais Kibaki akaunda timu chini ya mamlaka ya mapato Kenya kufatilia swala lile

Timu ile ikaongozwa na Kamishina msaidizi wa KRA bwana Joseph Cheprarus

Tarehe 24 February 2011 kamishina huyu, akaongoza timu yake kuvamia na kukagua kwenye Godown linalomilikiwa na Paul Kobia. Image
Oct 16, 2023 โ€ข 36 tweets โ€ข 17 min read
Tumerudi tena darasani kwa hali mpya na nguvu mpya

Darasa letu la mwisho, tulisoma kuhusu njia ya kumtambua mhalifu/wahalifu halisi kutoka kwenye utitiri wa washukiwa. Image Nilifafanua kuwa njia hii hujaribu kufanya linkage kati ya tabia alizozionesha mhalifu kwenye eneo la tukio na tabia za suspects nje ya eneo la tukio. Image
Oct 9, 2023 โ€ข 5 tweets โ€ข 3 min read
"Hatukupata ishara ya aina yoyote bali shambulio hili asubuhi hii lilikuwa ni total suprise.

"Haikuwa kabisa kwenye fikra zetu na hatukujua kama wana makombora ya aina hii na hatukujua kama yangetumika kwa ufanisi kiasi hiki leo hii".

"Tunashuku makombora haya yaliingizwa Gaza kwa njia ya magendo kupitia baharini, yakafanyiwa mazoezi ya kutosha na Hamas kwa usiri mkubwa, kiasi ambacho idara ya ujasusi Israel ilishindwa kuwa na fununu"

Hivi ndivyo alivyonukuliwa mkuu wa zamani wa Idara ya ujasusi Israel (MOSSAD) Bwana Efraim Halรฉvy akiongea na shirika la habari CNN

Maneno haya yanayodhihirisha udhaifu wa MOSSAD shirika linaloheshimika duniani kwa intelijensia, yanakuja wakati MOSSAD ikiwa inajivunia teknolojia yake ya PEGASUS inayoitumia kukusanya taarifa za kiintelejensia katika ukanda wa Gaza

Teknolojia hii ambayo hudukua simu za watu na message kwa kutumia artificial intelligence iliweza kuwavutia FBI ambao nao walikuwa mbioni kuomba leseni yake kutoka Israel.

Haya yote hayakufua dafu mbele ya wanamgambo wa Hamas na Islamic Jihad ambao walikuwa wamechoshwa na manyanyaso ya waisrael huko West Bank.

Wakajipenyeza (infiltrate) hadi kwenye jamii za waisrael na kuchanganana nao

Wakiwa na kazi moja tu!

Kazi ya kusubiri waisrael wakiwa off-guard

Naam!

Wakiwa kwenye mapumziko ya kuazimisha mwaka mtakatifu wa Kiyahudi

Yes!

The Days of Awe
Image Kwa tamaduni za Kiyahudi, Kila mwaka hutenga siku 10 za toba(teshuvah), Sala(tefilah) na Matendo mema(tzedakah/sadakka)

Siku hizi kumi (Days of Awe) huanzia kwa siku ya mwaka mpya wa kiyahudi huitwao Rosh Hashanah na kuishia siku Yom Kipur

Wayahudi huamini kuwa Mungu huwa anaandika jina la kila mtu kwenye kitabu cha huai au kifo siku ya Rosh Hashanah kwa ajili ya mwaka ujao.

Mungu atandelea kuandika majina ya watu hao hadi siku ya Yom Kippur ambayo hufunga vitabu vyake.

Hivyo wayahudi hutumia siku za Rosh Hashanah kusameheana magomvi na madeni baina yao ili kuwa safi mbele za Mungu kama njia ya kumshawishi Mungu acute majina yao kwenye kitabu cha kifo.

Katika Siku hizi wayahudi hula ma apple kama kuomba matunda mema kwa mwaka ujao na hunywa asali kama kuomba mwaka mtamu usio na mabalaa

Pia humpigia mungu Kinubi (shofar)

Hapa wayahudi hufanya hivi kutekeleza maandiko ya kwenye biblia katika kitabu cha Kutoka 23:24-25
Image
Oct 4, 2023 โ€ข 69 tweets โ€ข 40 min read
Umuofia kwenu!

Kuna wasomaji wangu wanapenda kunitania kwa kuniita BEN KAMANYOLA

Jina hili limetokana na story yangu ya Kwanza katika mtandao huu.

In fact hii ni kazi ya mtunzi mahili Mzee BEKA MFAUME katika kitabu alichoamua kukipa jina lake la MZEE BEKA

Kutokana na maombi ya wasomaji wengi walioomba nirudie mkasa huu, nimeona si vibaya nikiurudia mkasa huu huku mwishoni nikitoa namba ya mwandishi ili mumuunge mkono kwa kujinunulia nakala ya kitabu hiki na mwendelezo wake alioupa jina la THE ASSASSIN

Naam!

Ukisoma mkasa huu, hakika utakuwa mateka wa THE ASSASSIN

Twende kazi๐Ÿ‘‡
Image Kitabu kinaongelea marafiki wawili ambao ni Bernard na Bakari.

Bakari aliingia jijini Dar es salaam akiwa ni mlughalugha akitokea mkoani Kigoma.

Dar Es Salaam ndipo anafanikiwa kujuana na Bernard aishiye kinondoni kwenye nyumba ya familia iliyoachwa na marehemu baba yake.

In fact, Ben anaishi kwenye nyumba ile na Mama yake, dada yake aitwaye Maria na kaka yake aitwaye Lucas.

Ben ndio muhimili wa familia hiyo kwani ndiye anayechukua jukumu la kuziba pengo la marehemu baba yao la kuwatunza mama na ndugu zake.

Ben anatimiza majukumu hayo huku mara kadhaa akifika pale nyumbani kwao kwa ajili ya chakula cha mchana.

Familia ya Ben haijui kazi ya Ben!

Lakini kwa kuwa mkono unakwenda kinywani,haikuhoji hilo
Image
Sep 27, 2023 โ€ข 4 tweets โ€ข 4 min read
rubani Captain Reinhard Knoth akiwa anaruka katika anga la kati ya Frankfurt na jiji la New York, alibadilisha mawimbi ya radio ya ndege yake na kuyapeleka kwenye mfumo wa โ€œUnicomโ€

Mawimbi ya mfumo huu huruhusu mawasiliano baina ya marubani wa ndege zilizo angani kupashana habari za hali ya hewa katika viwanja mbalimbali vya ndege.

Pia waliweza kupashana taarifa juu ya ndege zilizochelewa kuruka au kutua katika viwanja mbalimbali

Rubani huyu ayekuwa anaendesha ndege ya Boing 747 alikuwa akatembea kwa Speed 600 Miles kwa kwa saa (Roughly 521 Knots)

Kwenye topic ya hesabu ya โ€œThe Earth as a Sphereโ€, watu wa anga na majini hupima umbali kwa kuzingatia kuwa dunia ni duara (Angular Distance)

Kwa hiyo umbali huwekwa kwa units za Neutical Mile na sio Mile
Neutical Mile per hour ndio inaitwa โ€œKnotsโ€ na ndio unit ya speed ya ndege au meli.

Tuendelee,

Usinichoshe, Nisikuchoshe, Tusichoshane

Captain huyu akiwa mtulivu kabisa huku akiwasikiliza marubani wenzake redioni akasikia taarifa ya kushangaza katika rekodi yake ya urubani ambao alikuwa anaelekea kuzeekea kwenye kazi hiyo.

Ni taarifa aliyosikia kupitia radio kutoka kwa rubani wa ndege ya KLM!

Captain wa KLM alisema redioni kwa mshtuko mkubwa....

โ€œKuna kitu kinatokea New York.. Ajaliโ€

Captain Knoth akaamua kuitoa redio yake kwenye Unicom frequency na
kurudisha kwenye commercial Frequency akatafuta mawimbi ya BBC

Akakuta station ya redio ile ikirusha matangazo mubashara kutokea New York!

Mtangazaji akidai umetokea mlipuko mkubwa katika jengo la kaskazini la kituo cha biashara WTC uliosambabishwa na ajali ya ndege.

Captain Knoth akawa ametatizika.
Akawatazama Co-pilot na injia wake wa ndege kuona kama wamesikia alichosikia.

Swali likawa hii inawezekanaje?
Kwa taaluma yake ya urubani aliona haiwezekani!

Co-pilot wake akamjibu labda ndege hiyo ni ndogo, ya binafsi na rubani wake alipata heart attack na kupoteza fahamu.

Lakini swali likawa rubani alitembeaje kimo kifupi hadi kugonga jengo la ardhini?

Taaluma yao haikukubaliana na ukweli.

Wakiwa bado wanaulizana maswali, wakakatizwa tena na sauti ya mtangazaji wa BBC

โ€œMlipuko mwingine... ndege nyingine imegonga jengo la World Trade Centerโ€
Image Hii ilikuwa ni saa tatu na dakika 3 Asubuhi

Captain Knoth akihama kutoka redio moja kwenda nyingine kutafuta uhakika wa asikiacho!

Ndege mbili zinagonga jengo?

Hapana!

Hizi sio ajali! Captain aliwaza!

Kwa taaluma yake ya urubani hata angewekewa bastola kichwani alazimishwe kusema ni marubani ndio wamegonga ndege zile angekataa katakata.

Aliamini ndege zile hazikuwa zikiendeshwa na marubani labda watu wengine!

Captain Knoth hakuwa rubani pekee kati ya marubani waliokuwa angani aliyeshitukia hili.

Kila rubani angani sasa alikuwa makini kuwa ndege yake inaweza ikawa target ya โ€œHijackersโ€

Kila dakika iliyosogea, sauti za marubani redioni kwa njia ya Unicom, zilithibitisha kupagawa.

Maswali yalikuwa;

โ€œKuna rubani yeyote maefanikiwa kufahamu ndege zilizopata ajali?

โ€œJe, ni ndege za mashirika gani? American Airlines? United Airlines ? Au Delta?โ€

โ€œKuna ajuaye namba za ndege zilizopata ajali?โ€

โ€œMpaka muda huu ndege ngapi zimeshapata tena ajali?โ€

9:15 AM

Muda huu shirika la anga Jijini New York likatangaza kuvifunga viwanja vyake vyote vya ndege.

Captain Knoth akiwa hana la kufanya baada ya tangazo hili, akaamua kuwasiliana kwa dharula na uwanja wa ndege wa Lufthansa jijini Frankfurt Ujerumani kuomba muongozo.

Alikuwa bado umbali wa masaa manne kabla ya kufika New York.

Akawa anajiuliza aendelee kwenda New York na kutua kokote au ageuze kurudi Ujerumani?

Swala la kugeuza ndenge angani nalo pia lilihitaji maneuver magumu kutoka kwa rubani aliyebobea.

Kwani hili lingezivuruga tena ndege nyingine angani kwa kuwa kila rubani angani anakuwa na taarifa za awali pekee za kila ndege iliyo angani (ripple effect)

Kwa hiyo kugeuza kunatakiwa kufanyika kwa umakini mkubwa (Choreographed)

Captain Knoth alipaswa kufanya maamuzi ya haraka!

Alikuwa anakaribia nusu ya bahari ya Atlantic kwenye nyuzi 30 ya mstari wa longitudo.

Rubani akishavuka mstari huu haruhusiwi tena kugeuza.
Image