Fortunatus Buyobe Profile picture
Pool of thoughts. A commander of the hand to mouth battalion. Environmental Pioneer. Social Engineer. #CertifiedMchapaUzi . Telegram: https://t.co/aEEOOryJWO
Hangi ๐Ÿ“ฟ Profile picture Mjukuu Profile picture peter August Profile picture Kendrick Profile picture Mc_Carl Profile picture 15 subscribed
Jan 24 โ€ข 48 tweets โ€ข 17 min read
Before writing this masterpiece to this X street, I gave myself ample opportunity to scrutinize and verify the facts.

The matter beforehand today is fragile as it can defame someone's business and reputation.

But why should I lie when I can speak the Truth?

Tariq M. Machibya Image Bwana Tariq Machibya alipofikishwa mahakamani kwa kuendesha biashara ya upatu, watu wengi tulimuhurumia kwa kuhisi Serikali inamuonea kijana mdogo mjasiliamali.

Kijana ambaye alibeba ndoto na maono ya wenye mitaji wasiojua pa kuwekeza.

Some sort of financial intermediary

Alas! Image
Nov 30, 2023 โ€ข 31 tweets โ€ข 11 min read
Bado nipo kwenye coma nikijiuliza kama kulikuwa na ulazima wowote kwa askari huyu kuingia na mtutu wa bunduki kwenye eneo la starehe.

Bado najiuliza,

Kulikuwa na ulazima wa kumuelekezea bunduki namna hii yeyote awaye(hata kama ni kahaba) ambaye hajainua silaha yoyote

Najiuliza Image Kuna mambo mengi yamekuwa yakifanywa na polisi kiholela sana.

Moja ya mambo haya ni kazi ya kukamata walevi au wenye bar wakipitisha muda wa kufunga bar.

Polisi hapaswi kukamata kosa hili bila kuwepo kwa mlalamikaji ambaye ni afisa biashara wa manispaa aliyetoa leseni ya kileo Image
Nov 16, 2023 โ€ข 23 tweets โ€ข 10 min read
KUWENI MAKINI NA MCHANGA WA KABURINI:

#X-Ushirikina

Kuna watu wamepata nuksi, mikosi na mabalaa makubwa katika maisha yao kwa sababu ya matumizi ya mchanga wa makaburini bila kuzingatia au kufuata maelekezo. Image Unapokuwa unafanya kitu chochote kile kinacho yahusisha makaburi, iwe ni kutumia mchanga, kuzika vitu, kuoga, kuchoma ama kutambika, unatakiwa kuwa makini sana na kufuata na kuzingatia kanuni na taratibu zake kwa sababu usipo zingatia hayo yatakupata makubwa. Image
Nov 7, 2023 โ€ข 55 tweets โ€ข 17 min read
Miaka minne iliyopita, Jimmy Kizota alishitakiwa kwa kosa la kumuua mchumba wake aliyekuwa akiishi naye jijini Dar es salaam.

Ni baada ya kumfumania akifanya mapenzi na mwanaume mwingine sebuleni kwao aliporudi nyumbani ghafla akitokea kazini majira ya saa tano asubuhi. Image Mwanaume aliyefumaniwa alifanikia kumzidi nguvu Jimmy na kukimbia

Wivu na hasira kaishia kwa kumpiga mchumba wake hadi akapoteza fahamu.

Baadae mwanamke huyu akafariki akipatiwa matibabu hospitali.

Jimmy akashitakiwa kwa mauaji ya kukusudia

Kesi ilimkalia vibaya sana Image
Nov 6, 2023 โ€ข 11 tweets โ€ข 4 min read
Ndani ya behewa moja, kulikuwa na abiria aliyekuwa ametulia kimya kwenye kiti akiwaangalia abiria wenzake waliokuwa kwenye harakati za kushuka.

Mtu huyo aliyeonekana kutokuwa na haraka, alikuwa amekaa kwa kuuegemeza mguu mmoja juu ya mwenzake kama bado akiendelea na safari. Image Mtu huyo ambaye safari yake ilianzia kituo cha treni cha Kingorwila Morogoro, alipanda akiwa hana mzigo wowote aliobeba mkononi

Tangu anaingia hadi kupata siti kwenye behewa aliloingia, hakuzungumza na abiria yeyote, hakuinuka kwenda kokote, hakutikisika wala kumwangalia yeyote. Image
Nov 5, 2023 โ€ข 49 tweets โ€ข 16 min read
Kitendo cha mtu huyu kuingia bila kupiga hodi kwenye ofisi yake ya mapokezi,kilimshitua binti huyu.

Mwonekano wa mtu huyo ulimfanya binti huyo aamini huyu si mgeni wa ofisi yake bali amekosea njia kwani ilikiwa ni mara ya kwanza kumuona mtu yule

Binti akagundua jambo lingine Image Sura ya mgeni yule haikuwa ya kiungwana.

Alionekana kutoyafurahia maisha kwa ujumla

Binti akabaki akimtazama mgeni huyu akisubiri kuombwa msamaha wa kukosea ofisi

Haikuwa vile!

"Jimmy yupo?" Aliuliza mgeni yule bila ya salamu

Ikawa zamu ya binti kushangaa Image
Oct 27, 2023 โ€ข 28 tweets โ€ข 10 min read
Taarifa alizozipata rais Kabila baada ya kushikiliwa kwa wale wamarekani zilimshtua sana,

Hakuchukua muda wakati akitafakari taarifa ile ili kujua cha kumfanya, zikaja habari za kuvushwa mzigo mwingine wa tani 2.5

Akatanguliza timu yake ya mawaziri wakamuone raisi Kibaki Image Rais Kibaki akaunda timu chini ya mamlaka ya mapato Kenya kufatilia swala lile

Timu ile ikaongozwa na Kamishina msaidizi wa KRA bwana Joseph Cheprarus

Tarehe 24 February 2011 kamishina huyu, akaongoza timu yake kuvamia na kukagua kwenye Godown linalomilikiwa na Paul Kobia. Image
Oct 16, 2023 โ€ข 36 tweets โ€ข 17 min read
Tumerudi tena darasani kwa hali mpya na nguvu mpya

Darasa letu la mwisho, tulisoma kuhusu njia ya kumtambua mhalifu/wahalifu halisi kutoka kwenye utitiri wa washukiwa. Image Nilifafanua kuwa njia hii hujaribu kufanya linkage kati ya tabia alizozionesha mhalifu kwenye eneo la tukio na tabia za suspects nje ya eneo la tukio. Image
Oct 9, 2023 โ€ข 5 tweets โ€ข 3 min read
"Hatukupata ishara ya aina yoyote bali shambulio hili asubuhi hii lilikuwa ni total suprise.

"Haikuwa kabisa kwenye fikra zetu na hatukujua kama wana makombora ya aina hii na hatukujua kama yangetumika kwa ufanisi kiasi hiki leo hii".

"Tunashuku makombora haya yaliingizwa Gaza kwa njia ya magendo kupitia baharini, yakafanyiwa mazoezi ya kutosha na Hamas kwa usiri mkubwa, kiasi ambacho idara ya ujasusi Israel ilishindwa kuwa na fununu"

Hivi ndivyo alivyonukuliwa mkuu wa zamani wa Idara ya ujasusi Israel (MOSSAD) Bwana Efraim Halรฉvy akiongea na shirika la habari CNN

Maneno haya yanayodhihirisha udhaifu wa MOSSAD shirika linaloheshimika duniani kwa intelijensia, yanakuja wakati MOSSAD ikiwa inajivunia teknolojia yake ya PEGASUS inayoitumia kukusanya taarifa za kiintelejensia katika ukanda wa Gaza

Teknolojia hii ambayo hudukua simu za watu na message kwa kutumia artificial intelligence iliweza kuwavutia FBI ambao nao walikuwa mbioni kuomba leseni yake kutoka Israel.

Haya yote hayakufua dafu mbele ya wanamgambo wa Hamas na Islamic Jihad ambao walikuwa wamechoshwa na manyanyaso ya waisrael huko West Bank.

Wakajipenyeza (infiltrate) hadi kwenye jamii za waisrael na kuchanganana nao

Wakiwa na kazi moja tu!

Kazi ya kusubiri waisrael wakiwa off-guard

Naam!

Wakiwa kwenye mapumziko ya kuazimisha mwaka mtakatifu wa Kiyahudi

Yes!

The Days of Awe
Image Kwa tamaduni za Kiyahudi, Kila mwaka hutenga siku 10 za toba(teshuvah), Sala(tefilah) na Matendo mema(tzedakah/sadakka)

Siku hizi kumi (Days of Awe) huanzia kwa siku ya mwaka mpya wa kiyahudi huitwao Rosh Hashanah na kuishia siku Yom Kipur

Wayahudi huamini kuwa Mungu huwa anaandika jina la kila mtu kwenye kitabu cha huai au kifo siku ya Rosh Hashanah kwa ajili ya mwaka ujao.

Mungu atandelea kuandika majina ya watu hao hadi siku ya Yom Kippur ambayo hufunga vitabu vyake.

Hivyo wayahudi hutumia siku za Rosh Hashanah kusameheana magomvi na madeni baina yao ili kuwa safi mbele za Mungu kama njia ya kumshawishi Mungu acute majina yao kwenye kitabu cha kifo.

Katika Siku hizi wayahudi hula ma apple kama kuomba matunda mema kwa mwaka ujao na hunywa asali kama kuomba mwaka mtamu usio na mabalaa

Pia humpigia mungu Kinubi (shofar)

Hapa wayahudi hufanya hivi kutekeleza maandiko ya kwenye biblia katika kitabu cha Kutoka 23:24-25
Image
Oct 4, 2023 โ€ข 69 tweets โ€ข 40 min read
Umuofia kwenu!

Kuna wasomaji wangu wanapenda kunitania kwa kuniita BEN KAMANYOLA

Jina hili limetokana na story yangu ya Kwanza katika mtandao huu.

In fact hii ni kazi ya mtunzi mahili Mzee BEKA MFAUME katika kitabu alichoamua kukipa jina lake la MZEE BEKA

Kutokana na maombi ya wasomaji wengi walioomba nirudie mkasa huu, nimeona si vibaya nikiurudia mkasa huu huku mwishoni nikitoa namba ya mwandishi ili mumuunge mkono kwa kujinunulia nakala ya kitabu hiki na mwendelezo wake alioupa jina la THE ASSASSIN

Naam!

Ukisoma mkasa huu, hakika utakuwa mateka wa THE ASSASSIN

Twende kazi๐Ÿ‘‡
Image Kitabu kinaongelea marafiki wawili ambao ni Bernard na Bakari.

Bakari aliingia jijini Dar es salaam akiwa ni mlughalugha akitokea mkoani Kigoma.

Dar Es Salaam ndipo anafanikiwa kujuana na Bernard aishiye kinondoni kwenye nyumba ya familia iliyoachwa na marehemu baba yake.

In fact, Ben anaishi kwenye nyumba ile na Mama yake, dada yake aitwaye Maria na kaka yake aitwaye Lucas.

Ben ndio muhimili wa familia hiyo kwani ndiye anayechukua jukumu la kuziba pengo la marehemu baba yao la kuwatunza mama na ndugu zake.

Ben anatimiza majukumu hayo huku mara kadhaa akifika pale nyumbani kwao kwa ajili ya chakula cha mchana.

Familia ya Ben haijui kazi ya Ben!

Lakini kwa kuwa mkono unakwenda kinywani,haikuhoji hilo
Image
Sep 27, 2023 โ€ข 4 tweets โ€ข 4 min read
rubani Captain Reinhard Knoth akiwa anaruka katika anga la kati ya Frankfurt na jiji la New York, alibadilisha mawimbi ya radio ya ndege yake na kuyapeleka kwenye mfumo wa โ€œUnicomโ€

Mawimbi ya mfumo huu huruhusu mawasiliano baina ya marubani wa ndege zilizo angani kupashana habari za hali ya hewa katika viwanja mbalimbali vya ndege.

Pia waliweza kupashana taarifa juu ya ndege zilizochelewa kuruka au kutua katika viwanja mbalimbali

Rubani huyu ayekuwa anaendesha ndege ya Boing 747 alikuwa akatembea kwa Speed 600 Miles kwa kwa saa (Roughly 521 Knots)

Kwenye topic ya hesabu ya โ€œThe Earth as a Sphereโ€, watu wa anga na majini hupima umbali kwa kuzingatia kuwa dunia ni duara (Angular Distance)

Kwa hiyo umbali huwekwa kwa units za Neutical Mile na sio Mile
Neutical Mile per hour ndio inaitwa โ€œKnotsโ€ na ndio unit ya speed ya ndege au meli.

Tuendelee,

Usinichoshe, Nisikuchoshe, Tusichoshane

Captain huyu akiwa mtulivu kabisa huku akiwasikiliza marubani wenzake redioni akasikia taarifa ya kushangaza katika rekodi yake ya urubani ambao alikuwa anaelekea kuzeekea kwenye kazi hiyo.

Ni taarifa aliyosikia kupitia radio kutoka kwa rubani wa ndege ya KLM!

Captain wa KLM alisema redioni kwa mshtuko mkubwa....

โ€œKuna kitu kinatokea New York.. Ajaliโ€

Captain Knoth akaamua kuitoa redio yake kwenye Unicom frequency na
kurudisha kwenye commercial Frequency akatafuta mawimbi ya BBC

Akakuta station ya redio ile ikirusha matangazo mubashara kutokea New York!

Mtangazaji akidai umetokea mlipuko mkubwa katika jengo la kaskazini la kituo cha biashara WTC uliosambabishwa na ajali ya ndege.

Captain Knoth akawa ametatizika.
Akawatazama Co-pilot na injia wake wa ndege kuona kama wamesikia alichosikia.

Swali likawa hii inawezekanaje?
Kwa taaluma yake ya urubani aliona haiwezekani!

Co-pilot wake akamjibu labda ndege hiyo ni ndogo, ya binafsi na rubani wake alipata heart attack na kupoteza fahamu.

Lakini swali likawa rubani alitembeaje kimo kifupi hadi kugonga jengo la ardhini?

Taaluma yao haikukubaliana na ukweli.

Wakiwa bado wanaulizana maswali, wakakatizwa tena na sauti ya mtangazaji wa BBC

โ€œMlipuko mwingine... ndege nyingine imegonga jengo la World Trade Centerโ€
Image Hii ilikuwa ni saa tatu na dakika 3 Asubuhi

Captain Knoth akihama kutoka redio moja kwenda nyingine kutafuta uhakika wa asikiacho!

Ndege mbili zinagonga jengo?

Hapana!

Hizi sio ajali! Captain aliwaza!

Kwa taaluma yake ya urubani hata angewekewa bastola kichwani alazimishwe kusema ni marubani ndio wamegonga ndege zile angekataa katakata.

Aliamini ndege zile hazikuwa zikiendeshwa na marubani labda watu wengine!

Captain Knoth hakuwa rubani pekee kati ya marubani waliokuwa angani aliyeshitukia hili.

Kila rubani angani sasa alikuwa makini kuwa ndege yake inaweza ikawa target ya โ€œHijackersโ€

Kila dakika iliyosogea, sauti za marubani redioni kwa njia ya Unicom, zilithibitisha kupagawa.

Maswali yalikuwa;

โ€œKuna rubani yeyote maefanikiwa kufahamu ndege zilizopata ajali?

โ€œJe, ni ndege za mashirika gani? American Airlines? United Airlines ? Au Delta?โ€

โ€œKuna ajuaye namba za ndege zilizopata ajali?โ€

โ€œMpaka muda huu ndege ngapi zimeshapata tena ajali?โ€

9:15 AM

Muda huu shirika la anga Jijini New York likatangaza kuvifunga viwanja vyake vyote vya ndege.

Captain Knoth akiwa hana la kufanya baada ya tangazo hili, akaamua kuwasiliana kwa dharula na uwanja wa ndege wa Lufthansa jijini Frankfurt Ujerumani kuomba muongozo.

Alikuwa bado umbali wa masaa manne kabla ya kufika New York.

Akawa anajiuliza aendelee kwenda New York na kutua kokote au ageuze kurudi Ujerumani?

Swala la kugeuza ndenge angani nalo pia lilihitaji maneuver magumu kutoka kwa rubani aliyebobea.

Kwani hili lingezivuruga tena ndege nyingine angani kwa kuwa kila rubani angani anakuwa na taarifa za awali pekee za kila ndege iliyo angani (ripple effect)

Kwa hiyo kugeuza kunatakiwa kufanyika kwa umakini mkubwa (Choreographed)

Captain Knoth alipaswa kufanya maamuzi ya haraka!

Alikuwa anakaribia nusu ya bahari ya Atlantic kwenye nyuzi 30 ya mstari wa longitudo.

Rubani akishavuka mstari huu haruhusiwi tena kugeuza.
Image
Sep 20, 2023 โ€ข 17 tweets โ€ข 6 min read
Watu wa kusini wana msemo wa โ€œMbwanda kala mbwandaโ€ wakimaanisha mbwa kala mbwa.

Ndivyo ambavyo ninaweza kuliita tukio hili.
ย 
Baada ya mauaji ya Kimbari nchini Rwanda, wengi wa waliohusika kupanga na kutekeleza mauaji yale walikamatwa na kufikishwa kwenye mahakama ya mauji ya Kimbari mkoani Arusha.
ย 
Serikali ya Kagame iliyochukua madaraka ilihakikisha hakuna hata mmoja aliyekuwa na mkono wake katika unyama ule anabaki uraiani bila kufikishwa kwenye vyombo vya sheria ili haki itendeke.
ย 
Lengo hili halikutimia kwa 100%
Image Ni kwa sababu baadhi ya wahusika walikimbilia nchi jirani kama vile Kongo RDC,Kenya na kwingine kokote.
ย 
Mmoja ya waliofanikiwa kukimbia alikuwa ni mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa Felicien Kabuga.

Alikuwa ni mtu wa karibu na rais Habyarimana na mabinti wake wawili waliolewa na watoto wa rais Habyalimana.
ย 
Bintiye Bernadette Uwamaliya aliolewa na Jean-Pierre Habyarimana.

Pia bintiye Francoise Mukazinza aliolewa na Leon Habyarimana.

Uzi๐Ÿ‘‡

KIFO MBELE YA FBI
Image
Sep 19, 2023 โ€ข 18 tweets โ€ข 9 min read
Mwezi march 1974, jamaa wetu akaitwa na bosi wake aindoke Misri na kurudi Urusi kisha akatakiwa kuripoti kwa mwenyekiti wa KGB Yuri Andropov

Hakujua kabisa sababu ya kuitwa kwake Image Jamaa alipofika Moscow akakutana na Yuri Andropov katika hospitali ya Kuntsevo

Hospitalini hapa, ndipo sehemu ambayo bosi huyu wa KGB alipapenda kukutana na watu aliotaka kujadili nao mambo nyeti.

Walipokutana hapa, Jamaa akatakiwa atoe ripoti jinsi anavyoona uelekeo wa siasa za Misri na athari zake kwenye mahusiano yake na Urusi.

Jamaa akaeleza kila kitu kwa ufasaha na mazungumzo yakahitimishwa rasmi.

Jamaa akaenda nyumbani kwake kusalimia familia yake ili kujiandaa na maandalizi ya safari kurudi kazini kwake Egypt.

Baada ya siku mbili akapokea tena taarifa akutane na Yuri Andropov.

Jamaa kidogo akatatizika!

Akawa anajiuliza kutakuwa na shida gani?

Mbona alishaonana na bosi huyu siku mbili tu zilizopita?

Pamoja na maswali yote aliyojiuliza, hakuwa na jinsi yoyote ya kutoitikia wito huo.
Image
Sep 11, 2023 โ€ข 10 tweets โ€ข 6 min read
Kuna watu wawili huwa mara nyingi tunashindwa kuwatofautisha, kati ya Shushushu(spy) na Kachero(detective)

Ingawa watu hawa wawili wanaweza kuwa wanafanya kazi zinazokaribia kurandana, lakini ni watu wawili tofauti sana.

Shushushu hufanya kazi ya kukusanya taarifa za intelejensia kwa matumizi yoyote ya sasa au baadae.

Kachero mara nyingi huusika na kufumbua mafumbo ya mikasa ya kijinai ili kuwapata wahusika halisi wa tukio la kijinai.

Mbinu zitumikazo na wote kufikia malengo yao, zinaweza kufanana lakini tofauti kati yao ni muda.

Yaani Shushushu anakusanya taarifa kabla hata ya tukio wakati kachero anaanza kukusanya taarifa baada ya tukio.

Watu hawa wote lazima wawe na taaluma ya โ€œEspionageโ€

Espionage ni nini?
Image Espionage ni kitendo cha kukusanya taarifa za siri ziitwazo โ€œIntelligenceโ€

Kwa hiyo kwa ufupi, Espionage ni โ€œIntelligence gatheringโ€

Watu wa espionage wanaweza kutumiwa na serikali, makampuni hasimu ya kibiashara (Industrial espionage) na hata wachunguzi wa matukio ya jinai.

Nchi zote hufanya espionage kwa lengo la kujua uwezo wa majeshi ya adui, teknolojia anayotumia etc

Haya hufanyika kwa kuingia kwenye ngome ya adui (Infiltration) na kuweza hata kupata cheo ndani ya majeshi yake.

Pia kuwatafuta watu ndani ya jeshi la adui na kuwashawishi wakuuzie taarifa (recruiting dissidents and defectors)

Lengo la kufanya yote haya, ni kujua nguvu ya adui na hata kumuhujumu (sabotage) na pia kuandaa mapema budget kamili ya kumshughurikia
endapo vita itaibuka baina naye wakati wowote.

Hata adui anaponunua vifaa vingi vya kivita, ni lazima ifanyike espionage kubaini ni kwa nini kanunua wakati huu. (Hapa ndipo umuhimu wa bandari yetu unapokuja ingawa sio mada ya leo)
Image
Aug 16, 2023 โ€ข 15 tweets โ€ข 12 min read
UHAINI

Kuna jambo linaendelea ambalo limenikumbusha kesi ya uhaini ya mwaka 1982

Ndugu msomaji, kazi yako itakuwa ni kusoma na kuoanisha kati ya Uhaini kanyaboya na uhaini original

MPANGO WA MAPINDUZI 1982

Aliyekuwa kinara wa Kuratibu mpango huu alikuwa ni Hatibu
Gandhi maarufu kama McGhee
Huyu alikuwa ni rubani wa ndenge ndogo za abiria

Alikuwa ni โ€œshombeshombeโ€ au โ€œmmangaโ€ mwenye asili ya mkoani Tanga na kabila lake alikuwa ni mbondei.

Wakati wazo la mipango hii inaanza alikuwa akiishi nchini Kenya na alikuja nchini pale tu mpango huu ulipokuwa umeiva.

Alipofika nchini kwa mara ya kwanza alifikia kwenye nyumba namba 65/32P mtaa wa Livingstone Kindondoni Mkwajuni ya mke wa baba yake mdogo aliyeitwa Hadija Omari

McGhee alimwambia Hadija kuwa alikuwa ni mwajiriwa wa shirika la ndege ATC kama rubani na alikuwa akitafuta nyumba ya kuishi kwani alikuwa akikaa hotelini.

Hadija ndipo akampatia nyumba yake kwa moyo Mkunjufu kama mwanae.

Baada ya Kupata nyumba, McGhee akafanikisha kumleta nchini Komandoo Tamimu (Captain Musa Tamimu) ambaye naye alikuwa akiishi nchini Kenya.

Ni Komandoo Tamimu ndiye aliyekuja kuishi kwenye nyumba hii iliyotafutwa na McGhee. Hadi wakati huu Komandoo Tamimu alikuwa akitafutwa na Jeshi la wananchi kwa kosa la utoro baada ya vita vya Uganda.

Tamimu baada ya kuingia nchini akamuuganisha McGhee na Captain Metusela Suleman Kamando ambaye alikuwa ni rubani wa ndege za jeshi akitokea Air Wing Ukonga.

Huyu Captain Metusela Kamando akawa ndiye anaambatana na McGhee sehemu mbalimbali katika kufanikisha mipango yao.

KAZI YAANZIA UDSM CHUONI

Mwaka 1982, pale chuo kikuu cha mlimani kulikuwa na mwanajeshi wa cheo cha Luteni aliyekuwa akimalizia mwaka wake wa mwisho wa shahada yake ya Sayansi ya siasa.

Huyu hakuwa mwingine bali ni Luteni Eugene Maganga aliyekuwa anatokea kikosi cha vifaru (Artillery)

McGhee na Kamando walimfata mwanajeshi huyu baada ya kuelezwa na Tamimu kuwa alikuwa ni mtu muhimu kushawishiwa kujiunga na mpango wao.

Walipompata walitumia mbinu nyingi sana kumshawishi kuwa mwelekeo wa nchi ulikuwa unaelekea kubaya na wao wanahitajika kuwakomboa watanzania.

Luteni Eugene aliposhawishika, akawashauri kuwa ili kufanikiwa kuna mwanajeshi mmoja wa muhimu sana anatakiwa kushawishiwa ili naye awepo mpangoni.

Aliwaeleza anamjua mwanajeshi huyu kwa kuwa alisoma naye mwaka wa kwanza pale Mlimani lakini alirudishwa kazini baada ya kufeli masomo yake.

Huyu hakuwa mwingine bali ni Komandoo wa cheo cha Captain Eugene Ballati ambaye alikuwa amehamishiwa Zanzibar baada ya kumuua kwa bahati mbaya mwanajeshi mwenzake walipokuwa mazoezini kikosi 41 KJ Nachingwea.
Aug 7, 2023 โ€ข 15 tweets โ€ข 8 min read
Jioni ya jumatano, tarehe 15 September 2010 ilimkuta mfanyabiashara wa mafuta na gesi
ndugu Gregory Joseph Fleniken akiwa amejipumzisha katika chumba namba 348 cha hoteli ya MCM Elegante Hotel kitongoji cha Beamont, Texas.

Alikuwa kajilaza kitandani akivuta sigara hukuโ€ฆ https://t.co/gcZYObVqYktwitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
Image Mfanyabiashara huyu alijiwekea utamaduni wa kuianza week yake ya kazi kwa kuendesha gari kila jumatatu asubuhi kutoka nyumbani kwake Lafayette Illinois mpaka Beamont, Texas ilipo kampuni ya OGM Land Company

Kampuni hii aliimiliki kwa ubia na kaka yake aitwaye Michael
Jul 20, 2023 โ€ข 19 tweets โ€ข 10 min read
โ€œ๐ˆ๐ญ ๐ข๐ฌ ๐Ÿ๐ฎ๐ง๐ง๐ฒ ๐ก๐จ๐ฐ ๐ฌ๐จ๐ฆ๐ž๐ญ๐ข๐ฆ๐ž๐ฌ ๐ญ๐ก๐ž ๐ฉ๐ž๐จ๐ฉ๐ฅ๐ž ๐ฒ๐จ๐ฎ ๐ฐ๐จ๐ฎ๐ฅ๐ ๐ญ๐š๐ค๐ž ๐š ๐›๐ฎ๐ฅ๐ฅ๐ž๐ญ ๐Ÿ๐จ๐ซ, ๐š๐ซ๐ž ๐ญ๐ก๐ž ๐จ๐ง๐ž๐ฌ ๐›๐ž๐ก๐ข๐ง๐ ๐ญ๐ก๐ž ๐ญ๐ซ๐ข๐ ๐ ๐ž๐ซโ€

Anaonekana mtu wa miraba minne akitembea chini ya ulinzi wa askari polisi wa Pakistan akiongozwaโ€ฆ https://t.co/NX2D9uM2bptwitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
Image ๐Ž๐ง๐ž ๐‡๐จ๐ฎ๐ซ ๐›๐ž๐Ÿ๐จ๐ซ๐ž

๐“๐ก๐ฎ๐ซ๐ฌ๐๐š๐ฒ

๐Ÿ๐Ÿ•, ๐‰๐š๐ง ๐Ÿ๐ŸŽ๐Ÿ๐Ÿ

๐๐ฎ๐ซ๐ญ๐š๐›๐š ๐‚๐ก๐จ๐ฐ๐ค ๐“๐ซ๐š๐Ÿ๐Ÿ๐ข๐œ ๐‹๐ข๐ ๐ก๐ญ๐ฌ,

๐‹๐š๐ก๐จ๐ซ๐ž, ๐๐š๐ค๐ข๐ฌ๐ญ๐š๐ง

Afisa huyu alijikuta akiwa kwenye foleni kubwa ya magari na akijaribu njia mbalimbali โ€œto negotiate his way out ofโ€ฆ https://t.co/IOlMAsfHk4twitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
Image
Jul 9, 2023 โ€ข 6 tweets โ€ข 3 min read
RWANDAโ€™s UNTOLD

Sehemu ya 2

Tuliishia kikosi cha intelejensia cha ROA kimeanza kufanya Survey kuangalia njia ambayo ndege ya rais Habyarimana inaweza kupita wakati inashuka kwenye uwanja wa ndege wa Kanombe jijini Kigali.

Ili kazi hii ingekuwa ngumu kufanyika bila msaada waโ€ฆ https://t.co/lWKusJrcEdtwitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
Hapa waliweza kuona vizuri taa za uwanja wa ndege wa Kanombe

Pale mlimani walitengeneza hema lililokuwa na maandishi ya UNHCR ambalo walipewa na mfanyakazi wa UN

Pale ikafanyika assembling ya makombora na launchers zake

Ilishatimia saa moja na nusu usiku muda huu

Baada yaโ€ฆ twitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
Jul 8, 2023 โ€ข 8 tweets โ€ข 5 min read
โ€œUsipoteze muda wako kusikiliza habari kuwa huyu kanyongwa kwa kamba kwenye ghorofa ya nane kwenye nchi yoyote. Ukichagua kuwa mbwa, utakufa kama mbwa, na watu wa usafi wataondoa mzoga wako ili usiwatolee harufu yako mbayaโ€

Haya si maneno yangu.

Ni maneno ya waziri wa ulinzi waโ€ฆ https://t.co/KXJt2arAFEtwitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
โ€œBei hiyo sio tatizo kabisaโ€ฆ Naamini utaona shukrani yetu kwako kama kazi itafanywa vizuri โ€ฆ Lazima utalipwa vizuriโ€.

Haya maneno yanatamkwa na mtu mmoja kwenye mazungumzo kwa njia ya simu.

Ndugu msomaji,

Katika simu hii, bei ambayo inayotajwa kuwa si tatizo, tenaโ€ฆ https://t.co/UlUVSX76JBtwitter.com/i/web/status/1โ€ฆ
Jun 23, 2023 โ€ข 22 tweets โ€ข 6 min read
Niliamua kujipa muda wa kutosha kabla ya kukiingilia kisa hiki ninachotaka kukichambua leo hii.

Sina shaka hata kidogo kuwa wewe ndugu msomaji, umeshakisoma mitandaoni au kukisikia kisa cha binti mwanafunzi aliyepotea tangu tarehe 18 May mwaka huu. Binti huyu anaitwa ESTER NOAH MWANYILU

Alikuwa ni mwanafunzi wa kidato cha tano mchepuo wa PCB katika shule ya sekondari Panda Hill mali ya kanisa katoliki jimbo la Mbeya

Mazingira yanayozunguka kupotea kwa mwanafunzi huyu yanaacha โ€œred flagsโ€ na โ€œblack holesโ€ nyingi
Jun 22, 2023 โ€ข 11 tweets โ€ข 4 min read
Msafiri ni mkazi wa Banana.

Tarehe 8 Nov 2013, majira ya saa tatu usiku, alikuwa njiani akitoka kibaruani kiwanda cha MUZA OIL

Akashangaa polisi wanamuweka chini ya ulinzi akiambiwa ni mwizi.

Aliweza kumtambua mmoja ya askari waliomkamata kwa jina la Mselemu Naam!

Aliweza hata kutambua force number ya askari huyu

Kuwa ni E 755 Detective Corporal Mselemu

Akapelekwa kituo cha polisi Stakishari.

Kesho yake afande Mselemu akamtoa mahabusu na kumwambia kuna karatasi za ku โ€œsignโ€ ili apate dhamana.