ASKARI MSTAAFU ALIYEKUWA ANANYONGA WATU GEREZA LA ISANGA -DODOMA.
Kifo kinatisha; kifo hakina huruma; kifo hutenganisha wapendanao, lakini kwa bahati mbaya, siku ikifika hakuna anayeweza kukikwepa.
Akionyesha hofu ya kifo alipokuwa na bendi ya Orchestra Makassy, Remmy Ongala aliimba kibao kinachoitwa “Siku ya Kufa”. Maudhui ya kibao hicho yalirejewa na Remmy mwenyewe japo kwa mahadhi tofauti alipojiunga na bendi ya Super Matimila. Huko alitunga kibao kiitwacho “Kifo”
Kana kwamba ana uwezo wa kufanya majadiliano na kifo aliimba: “Kifo, kifo, siku yangu ikifika eeh, kifo niarifu mapema, niage wanangu, niage familia yangu yote, pesa zangu nizigawanye, zimebaki nizile mwenyewe, kifo nakusubiri kwa hamu.”
Mwanamuziki huyo, aliyefahamika zaidi kwa jina la Dk Remmy, alifariki dunia akiacha kifo kikiendelea kuchukua uhai wa mamilioni ya watu duniani katika mazingira tofauti.
Baadhi hufa ghafla ajalini, wapo wanaofariki dunia baada ya kuugua, wengine huuawa na wenzao kwa hasira au kisasi au kwa bahati mbaya au bila kujua, lakini kuna wanaouawa kwa hukumu inayotolewa na vyombo vya haki; huhukumiwa kunyongwa hadi kufa.
Wanaopatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia huhukumiwa kifo. Japokuwa kila nafsi itaonja mauti, wanaohukumiwa kifo ndio huweza kujua siku na aina ya kifo.
Hivi mtu akihukumiwa kifo na mahakama, je, wanaofanya kazi hiyo ni nani? Kitanzi kikoje? Hali inakuwaje kabla? Je, hupata fursa ya kuaga ndugu na jamaa? Wanaotekeleza hukumu ya kunyonga wenzao hadi kufa pia wanakuwa wametenda kosa la kuua, je, huchukuliwa hatua gani kisheria?
Je, wanaoajiriwa kufanya kazi hiyo wanapatikanaje? Wanajisikiaje kukatisha uhai wa wenzao?
Lakini pia katika utumishi wao, ufanisi wao unapimwaje? Je, hupata utulivu wa moyo na amani kiroho?
Kwa kawaida kazi nyingi hutangazwa wazi magazetini na wale wanaojiona wana sifa zinazohitajika, huandika barua za kuomba na kusubiri kuitwa kwa mahojiano. Lakini, ni vigumu kukutana na tangazo la kazi hii ngumu kuliko zote.
Pia, najua kwamba baadhi ya kazi huhitaji wasomi wa kiwango cha juu, nyingine watu wenye ujuzi fulani lakini zipo zinazohitaji wenye nguvu.
Binafsi nadhani kazi hii inahitaji watu wenye moyo wa ujasiri ambao hawawezi kukosa utulivu wa moyo wala amani kiroho.
Maswali hayo na mengine mengi nimekuwa nikijiuliza kwa siku nyingi na katika kufuatilia nililazimika kufunga safari hadi mkoani Dodoma ambako nilifanikiwa kumshawishi mtekelezaji wa hukumu hizo afanye mahojiano nami.
Saa 12.00 jioni, nikiwa na mwenyeji wangu wa Dodoma tulifika nyumbani kwa mtu tuliyekuwa tukimtafuta, Anangisye (siyo jina lake halisi).
Huyu ni askari mstaafu aliyefanya kazi Jeshi la Magereza miaka 32 huku akitumia miaka 22 kufanya kazi hiyo maalumu ya kutekeleza hukumu za kifo
Tulipokewa na mjukuu wake, ambaye alituambia kuwa babu yake aliondoka nyumbani tangu asubuhi. “Shuuuuu,” tulishusha pumzi ikiwa ni ishara ya kukata tamaa, lakini kijana yule alitusihi tuvute subira.
Kijana yule alitukaribisha ndani na wakati tunaingia mama mwenye nyumba, Matilda (pia siyo jina lake halisi) alitupokea na kutukaribisha sebuleni.
Tunaingia katika nyumba hii, ya matofali, ina vyumba vitano na sebule. Vyumba vitatu vimepangishwa na vingine vinatumiwa na Anangisye na familia yake.
Mimi na mwenyeji wangu tukaendelea kukaa sebuleni tukimsubiri Anangisye huku mama mwenye nyumba akituelezea jinsi jino linavyomsumbua.
Baada ya robo saa hivi, sauti ya mwanamume ilisikika nje huku mama mwenye nyumba na yule kijana wakisema, “huyoo”.
Alipokuwa anaingia sebuleni, sote tulisimama na kusalimiana naye huku tukikumbatiana kana kwamba tulifahamiana siku nyingi. Punde alimwita mjukuu wake na kumtuma dukani akatununulie soda.
“Mnasema mnataka kujua kuhusu kazi maalumu?” aliuliza Anangisye nami nikajibu, “ndiyo baba”
“Mnanitafutia kazi nini maana nimestaafu tangu mwaka 2006,” alisema katika hali ya masihara.
Mara alibadilika na kusema kwa utani. “Lakini endapo itatokea kazi ya kunyonga niko tayari kufanya kwa sababu hakuna mtu yeyote anayeiweza kazi hiyo zaidi yangu,” alisema.
Anangisye ni mcheshi na mkarimu na wajihi wake ni mrefu, mnene, mwenye sauti nzito na anayependa masihara.
Baada ya masihara ya hapa na pale, Anangisye alianza kusimulia historia yake, alivyosoma, alivyopata kazi na jinsi alivyokuwa akitekeleza wajibu wake huo bila hofu.
Na hii ndiyo simulizi yake:👇
Mimi bwana ni mzaliwa wa Mbozi, sasa iko mkoani Songwe. Nilisoma hadi darasa la nane katika Shule ya Kati wilayani Mbozi. Mwaka 1974 niliomba kazi ya uaskari magereza. Nilipopata ajira nilipangwa gereza la Sengerema, Mwanza.
Huko nilifanya kazi kwa muda mrefu tu nikiwa askari wa kawaida wa magereza.
Mwaka 1984, yaani baada ya kufanya kazi kwa miaka 10 lilitolewa tangazo na Wizara ya Mambo ya Ndani kwamba anahitajika mtu kwa ajili ya kazi ya maalumu. Niliposikia tangazo lile niliomba nafasi
Basi, baada ya muda nikaitwa na Kamishna Mkuu wa makao makuu ya Magereza, Dar es Salaam. Nilipofika Kamishna akaniuliza: “Wewe ndiye Anangisye?”
“Nikamjibu, “ndiyo”.
Akaniuliza tena kama niliomba kazi maalumu na nikamjibu “ndiyo”.
“Basi umekubaliwa,” akasema.
Baada ya kuambiwa hayo nilielezwa zaidi kuwa Jeshi la Magereza limechagua watu wawili, yaani mimi na mwenzangu mmoja ambaye niliambiwa tutakutana Gereza la Isanga, Dodoma ambako kutakuwa kituo kikuu cha kazi yetu.
Niliambiwa kuwa kuanzia siku hiyo nitapelekwa Isanga na nitaripoti kwa RPO. Kwa hiyo nikawa nimeondolewa Sengerema
Nilipofika Isanga nilitambulishwa kwa mwenzangu na nikaambiwa kuwa tupo wawili tu nchi nzima na tutafanya kazi hii maalumu pale inapotokea na maelekezo mengine tutaendelea kuyapata.
Tuliambiwa kuwa tutakuwa tunafanya hiyo kazi nchi nzima, tutakuwa tunazunguka mikoani pale kazini
Kozi ya kunyonga.
Kitu cha kwanza baada ya kukubaliwa kupata kazi hii mimi na mwenzangu tulipewa mafunzo maalumu kwa muda wa mwezi mmoja palepale Isanga, tukafuzu, sisi wawili tu.
Mafunzo yetu yalihusisha namna ya kufanya kazi hiyo, namna ya kutumia kamba, mikanda ya kumshikilia mtu anayenyongwa pamoja na maandalizi yake.
Kuna namna ya kufunga kile kitanzi, ni lazima kiwe imara na salama ili yasitokee makosa. Lakini pia mikanda na eneo lenyewe na tulielekezwa jinsi ya kumweka mhalifu katika kitanzi chenyewe.
Katika ufanyaji kazi tulikuwa tunalindwa na askari magereza. Kwa mfano, siku ya kufanya kazi, tulikuwa tunasindikizwa na askari wakati wa kwenda na kurudi. Ilikuwa lazima tulindwe na ulinzi mkali wa askari ili isije kutokea tukapata madhara na kushindwa kutimiza wajibu wetu
Kwa mfano, tulipotakiwa kufanya kazi Mbeya tulikuwa tunapewa ulinzi wa askari kutoka Dodoma hadi Mbeya na tulikuwa tunapewa huduma za hali ya juu za malazi na chakula ili tuwe na nguvu.
Kitu kingine ni kwamba ule usiku wa kuamkia siku ya kazi, tulikuwa tunapewa pombe. Mimi nilikuwa nakunywa bia aina ya Safari; basi unawekewa hata kreti zima, tunakunywa, tunakunywa hadi asubuhi.
Hadi ninapoamka asubuhi bado nakuwa na pombe kichwani; kabla ya kazi kuanza bado nakuwa na mning’inio wa pombe kichwani. Jambo hili lilikuwa linatusaidia sana kufanya kazi yetu vizuri na kwa ujasiri.
Mwisho wa mwezi tulikuwa tunalipwa mshahara mzuri tu na pia tulikuwa tunalipwa posho. Kwa wakati ule, kila tukitekeleza kazi tulikuwa tunapewa Sh700 kwa kichwa, baadaye katika miaka ya 1990 posho hii iliongezeka hadi Sh5,000 na baadaye miaka ya mwanzoni mwa 2000 tulipewa Sh50,000
Matanga kabla ya kifo
Unajua vifo vingine vyote hutokea ghafla, lakini kifo cha kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa kinajulikana. Mhalifu anajua kifo chake tangu siku anaposomewa hukumu yake ila anachosubiri ni kutekelezwa kwa hukumu hiyo basi.
Kwa utaratibu wa magereza, mhalifu aliyehukumiwa kifo, hutayarishiwa matanga siku moja kabla ya kunyongwa. Wanamweka katika chumba maalumu; kila mmoja kwenye chumba chake. Wanamfungia humo na wanampa chakula na huduma yoyote anayoitaka, hayo ndiyo matanga yake.
Wakati waliohukumiwa kifo wakiwa kwenye matanga, wafungwa wengine huimba nyimbo za maombolezo kama sehemu ya kuwaombea wenzao kabla kifo hakijawameza. Matanga hayo ni ya siku moja tu.
Kabla ya kumweka kitanzini, mfungwa yeyote huwa na maandalizi yake. Viongozi wa dini zote mbili za Kiislamu na Kikristo huitwa, wanafika magereza na kuwaongoza wahalifu sala ya toba.
Huo ndio utaratibu. Wakishafanyiwa sala ya toba au kuongozwa sala yoyote ile inayofaa kabla ya kifo, huwekwa tayari kwa ajili ya kunyongwa.
Anakuwepo pia mwanasheria wa magereza. Haiwezekani wakanyongwa bila ya kuwepo viongozi wa dini.
Hanyongwi mtu mmoja, inawezekana kwa siku moja wakawa watu wanane au kumi, inategemea na waliohukumiwa mwezi huo. Baada ya kutekeleza hukumu hiyo kwa mtu mmoja, nilikuwa naenda kupumzika kwa dakika 45 kabla ya kuendelea na kazi hiyo kwa mtu mwingine.
Kwa kawaida kazi huanza saa 2.00 asubuhi, baada ya kumaliza kazi tunakwenda kupumzika ofisini, tunakunywa kinywaji pale, baada ya dakika 45 tunarudi tena kuendelea na kazi.
Baada ya mapumziko ya dakika 45, tunakwenda kuangalia kama ameshafariki dunia, tukimaliza kuhakiki tunaendelea na wengine hadi waliopangwa siku hiyo wameisha. Kwa siku walikuwa watu wanane kutegemeana na idadi ya waliohukumiwa na kitanzi kinaweza kutumiwa na watu watatu kwa mpigo
“Kwa hiyo, tukimaliza watatu, tunasubiri na kuendelea na kazi.”
Mwaka 2012, Blandine Nyoni akiwa katibu mkuu wizara ya afya, alinukuliwa akitoa kauli tata ya kuwabeza madaktari kuwa "wanajiona bora wakati ni wachafu na hawajui kiingeleza"
Katibu huyu akaendelea kusema kuwa hata yeye alisoma mchepuo wa PCB na kufaulu vizuri tu lakini kwa kutambua ubovu wa Medicine mzazi wake akamsomesha Accounts so hajui madaktari wanalalamikia nini.
Kauli hii ikang'oa kilaka kwenye jeans ya bishoo!
Ni kwamba mwaka huo, madaktari walikuwa katikati ya mgomo wa kihistoria
Kauli hii ikawatibua madaktari wakalianzisha upyaaaaa
Wiki hii tumeshuudia waliokuwa wanachama wa Chadema wakitangaza kuachana na chama hicho huku wakiahidi kuelezea hatima zao za kisiasa siku za mbeleni
Kati ya waliohama ni waliowahi kuwa viongozi waandamizi wa chama hicho
Hii inamaanisha nini?
Kabla sijajibu swali hilo ni vyema tukipitia kwa ufupi mtiririko wa matukio (A quick refresher)
1. Dec 12,2024, Tundu Lissu anatangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA taifa
Nia hii ya Lissu ilikuja baada ya kuwa uchokozi wa wazi dhidi yake ndani ya chama
Kabla ya uamuzi huu, Lissu aliyekuwa ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA, alishamwandikia barua katibu mkuu wake kumjuza nia yake ya kuendelea kugombea kubaki kwenye nafasi hiyo.
Ulikuwa ni utaratibu wa CHADEMA kwa viongozi wa juu kutoshindania nafasi moja endapo mmoja ataonesha nia
Polisi katika upelelezi wao wakatajiwa kuwa gari ile imeonekana akiwa nayo jambazi mmoja sugu sana ambaye alikuwa kwenye radar za polisi kwa muda mrefu.
Jambazi huyu si mwingine bali ni Ernest Joseph Sambua Mushi maarufu kwa jina la White
Taarifa zikadokeza jambazi lile lipo mkoni Kilimanjaro kwa wakati ule
Yule mfanyabiashara akajulishwa juu ya hili na akatoa gari lake na dereva ili kwenda Kilimanjaro
Jan 22, 2024 kwenye kikao cha baina ya CDF na makamanda kwa upande mmoja, na Amiri Jeshi mkuu kwa upande mwingine,Mkuu wa majeshi alitoa kauli iliyoibua udadisi
"Kuna wakimbizi wameteuliwa serikalini kwenye nafasi za maamuzi"
Kauli hii ilikuwa ni nzito kutoka kwa mtu mzito.
Nasema mtu mzito kwa kuwa, mtu aliyetoa kauli hii ni mwenye nafasi ya kupata taarifa zote za intelejensia za nchi hii
Kwanza kama mwenyekiti wa kamati ya majeshi ya ulinzi
Pili akiwa kama kiongozi kwenye taasisi yenye chombo kinachofanya "military intelligence" siku zote.
Kwa hiyo CDF Mkunda alikuwa anajua anachokizungumza ni sahii kutoka vyanzo sahii
Undisputed and not farfetched facts
Kauli hii kwa mtu asiyeutumia ubongo wake vizuri, ataisoma tu kwenye magazeti na kuachana nayo bila kuusumbua ubongo kuona yale yasiyoonekana.
Kumekuwepo na taarifa za kukamatwa kwa wahusika wa kampuni ya LEO BENEATH LONDON (LBL) inayoendesha biashara ya upatu, kukusanya amana, na kutoa riba kwa wanachama wake.
Victims wengi wa kampuni hii wakiwa ni watumishi wa kada ya ualimu
Pia Benki kuu imetoa taarifa ya kutoitambua wala kuipatia leseni kampuni hiyo.
Hapa ndipo napata maswali kuhusu umakini wa taasisi zetu zinazohusika na ukusanyaji wa taarifa za kiitelejensia
Taasisi hizi huwa hazipati fununu ya uwepo wa kampuni hizi kabla watu hawajatepeliwa?
Sasa hivi kuna kampuni nyingine inayojiita FIC
Kampuni hii inajinadi kuwa imesajiliwa BRELA na kupata cheti No. 177461385
Imepata TIN ya TRA No. 177-461-385 na kupewa cheti cha Tax Clearance
Sometimes March 2013 Wakili Fatuma Karume alisafiri kutoka Dar kwenda mkoani Kilimanjaro. Wakili huyu alikuwa amesafiri akiwa amebeba nyaraka furani ya muhimu. Nyaraka ile alikuwa anaenda kumsomea na kumkabidhi mzee fulani aliyefahamika kwa jina la Juma
Actually, Mzee Juma naye alikuwa ni wakili ambaye sasa amestaafu akiwa amefanikiwa kurithisha taaluma hiyo pia kwa mwanae ambaye alikuja kuwa ni wakili maarufu sana mkoni Arusha. Fatma hakujua kama nyaraka aliyobeba ingeleta taflani kubwa ndani ya familia ya Mzee Juma.
Fatma aliwasili nyumbani kwa ambako alikuta waombolezaji ambao walikusanyika baada ya kusambaa taarifa za msiba za mmoja wa watoto wa Mzee Juma. Fatma alitegemea kuikuta hali hii nyumbani pale na hata safari yake ilitokana na yeye kupata taarifa hizi.