Fortunatus Buyobe Profile picture
Jan 31, 2022 42 tweets 8 min read Read on X
ASKARI MSTAAFU ALIYEKUWA ANANYONGA WATU GEREZA LA ISANGA -DODOMA.

Kifo kinatisha; kifo hakina huruma; kifo hutenganisha wapendanao, lakini kwa bahati mbaya, siku ikifika hakuna anayeweza kukikwepa. Image
Akionyesha hofu ya kifo alipokuwa na bendi ya Orchestra Makassy, Remmy Ongala aliimba kibao kinachoitwa “Siku ya Kufa”. Maudhui ya kibao hicho yalirejewa na Remmy mwenyewe japo kwa mahadhi tofauti alipojiunga na bendi ya Super Matimila. Huko alitunga kibao kiitwacho “Kifo” Image
Kana kwamba ana uwezo wa kufanya majadiliano na kifo aliimba: “Kifo, kifo, siku yangu ikifika eeh, kifo niarifu mapema, niage wanangu, niage familia yangu yote, pesa zangu nizigawanye, zimebaki nizile mwenyewe, kifo nakusubiri kwa hamu.”
Mwanamuziki huyo, aliyefahamika zaidi kwa jina la Dk Remmy, alifariki dunia akiacha kifo kikiendelea kuchukua uhai wa mamilioni ya watu duniani katika mazingira tofauti.
Baadhi hufa ghafla ajalini, wapo wanaofariki dunia baada ya kuugua, wengine huuawa na wenzao kwa hasira au kisasi au kwa bahati mbaya au bila kujua, lakini kuna wanaouawa kwa hukumu inayotolewa na vyombo vya haki; huhukumiwa kunyongwa hadi kufa. Image
Wanaopatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia huhukumiwa kifo. Japokuwa kila nafsi itaonja mauti, wanaohukumiwa kifo ndio huweza kujua siku na aina ya kifo.
Hivi mtu akihukumiwa kifo na mahakama, je, wanaofanya kazi hiyo ni nani? Kitanzi kikoje? Hali inakuwaje kabla? Je, hupata fursa ya kuaga ndugu na jamaa? Wanaotekeleza hukumu ya kunyonga wenzao hadi kufa pia wanakuwa wametenda kosa la kuua, je, huchukuliwa hatua gani kisheria? Image
Je, wanaoajiriwa kufanya kazi hiyo wanapatikanaje? Wanajisikiaje kukatisha uhai wa wenzao?

Lakini pia katika utumishi wao, ufanisi wao unapimwaje? Je, hupata utulivu wa moyo na amani kiroho? Image
Kwa kawaida kazi nyingi hutangazwa wazi magazetini na wale wanaojiona wana sifa zinazohitajika, huandika barua za kuomba na kusubiri kuitwa kwa mahojiano. Lakini, ni vigumu kukutana na tangazo la kazi hii ngumu kuliko zote.
Pia, najua kwamba baadhi ya kazi huhitaji wasomi wa kiwango cha juu, nyingine watu wenye ujuzi fulani lakini zipo zinazohitaji wenye nguvu.

Binafsi nadhani kazi hii inahitaji watu wenye moyo wa ujasiri ambao hawawezi kukosa utulivu wa moyo wala amani kiroho.
Maswali hayo na mengine mengi nimekuwa nikijiuliza kwa siku nyingi na katika kufuatilia nililazimika kufunga safari hadi mkoani Dodoma ambako nilifanikiwa kumshawishi mtekelezaji wa hukumu hizo afanye mahojiano nami. Image
Saa 12.00 jioni, nikiwa na mwenyeji wangu wa Dodoma tulifika nyumbani kwa mtu tuliyekuwa tukimtafuta, Anangisye (siyo jina lake halisi).
Huyu ni askari mstaafu aliyefanya kazi Jeshi la Magereza miaka 32 huku akitumia miaka 22 kufanya kazi hiyo maalumu ya kutekeleza hukumu za kifo
Tulipokewa na mjukuu wake, ambaye alituambia kuwa babu yake aliondoka nyumbani tangu asubuhi. “Shuuuuu,” tulishusha pumzi ikiwa ni ishara ya kukata tamaa, lakini kijana yule alitusihi tuvute subira.
Kijana yule alitukaribisha ndani na wakati tunaingia mama mwenye nyumba, Matilda (pia siyo jina lake halisi) alitupokea na kutukaribisha sebuleni.
Tunaingia katika nyumba hii, ya matofali, ina vyumba vitano na sebule. Vyumba vitatu vimepangishwa na vingine vinatumiwa na Anangisye na familia yake.
Mimi na mwenyeji wangu tukaendelea kukaa sebuleni tukimsubiri Anangisye huku mama mwenye nyumba akituelezea jinsi jino linavyomsumbua.

Baada ya robo saa hivi, sauti ya mwanamume ilisikika nje huku mama mwenye nyumba na yule kijana wakisema, “huyoo”.
Alipokuwa anaingia sebuleni, sote tulisimama na kusalimiana naye huku tukikumbatiana kana kwamba tulifahamiana siku nyingi. Punde alimwita mjukuu wake na kumtuma dukani akatununulie soda.

“Mnasema mnataka kujua kuhusu kazi maalumu?” aliuliza Anangisye nami nikajibu, “ndiyo baba”
“Mnanitafutia kazi nini maana nimestaafu tangu mwaka 2006,” alisema katika hali ya masihara.

Mara alibadilika na kusema kwa utani. “Lakini endapo itatokea kazi ya kunyonga niko tayari kufanya kwa sababu hakuna mtu yeyote anayeiweza kazi hiyo zaidi yangu,” alisema.
Anangisye ni mcheshi na mkarimu na wajihi wake ni mrefu, mnene, mwenye sauti nzito na anayependa masihara.

Baada ya masihara ya hapa na pale, Anangisye alianza kusimulia historia yake, alivyosoma, alivyopata kazi na jinsi alivyokuwa akitekeleza wajibu wake huo bila hofu.
Na hii ndiyo simulizi yake:👇

Mimi bwana ni mzaliwa wa Mbozi, sasa iko mkoani Songwe. Nilisoma hadi darasa la nane katika Shule ya Kati wilayani Mbozi. Mwaka 1974 niliomba kazi ya uaskari magereza. Nilipopata ajira nilipangwa gereza la Sengerema, Mwanza.
Huko nilifanya kazi kwa muda mrefu tu nikiwa askari wa kawaida wa magereza.

Mwaka 1984, yaani baada ya kufanya kazi kwa miaka 10 lilitolewa tangazo na Wizara ya Mambo ya Ndani kwamba anahitajika mtu kwa ajili ya kazi ya maalumu. Niliposikia tangazo lile niliomba nafasi
Basi, baada ya muda nikaitwa na Kamishna Mkuu wa makao makuu ya Magereza, Dar es Salaam. Nilipofika Kamishna akaniuliza: “Wewe ndiye Anangisye?”

“Nikamjibu, “ndiyo”.

Akaniuliza tena kama niliomba kazi maalumu na nikamjibu “ndiyo”.

“Basi umekubaliwa,” akasema.
Baada ya kuambiwa hayo nilielezwa zaidi kuwa Jeshi la Magereza limechagua watu wawili, yaani mimi na mwenzangu mmoja ambaye niliambiwa tutakutana Gereza la Isanga, Dodoma ambako kutakuwa kituo kikuu cha kazi yetu.
Niliambiwa kuwa kuanzia siku hiyo nitapelekwa Isanga na nitaripoti kwa RPO. Kwa hiyo nikawa nimeondolewa Sengerema Image
Nilipofika Isanga nilitambulishwa kwa mwenzangu na nikaambiwa kuwa tupo wawili tu nchi nzima na tutafanya kazi hii maalumu pale inapotokea na maelekezo mengine tutaendelea kuyapata.

Tuliambiwa kuwa tutakuwa tunafanya hiyo kazi nchi nzima, tutakuwa tunazunguka mikoani pale kazini Image
Kozi ya kunyonga.

Kitu cha kwanza baada ya kukubaliwa kupata kazi hii mimi na mwenzangu tulipewa mafunzo maalumu kwa muda wa mwezi mmoja palepale Isanga, tukafuzu, sisi wawili tu.
Mafunzo yetu yalihusisha namna ya kufanya kazi hiyo, namna ya kutumia kamba, mikanda ya kumshikilia mtu anayenyongwa pamoja na maandalizi yake.
Kuna namna ya kufunga kile kitanzi, ni lazima kiwe imara na salama ili yasitokee makosa. Lakini pia mikanda na eneo lenyewe na tulielekezwa jinsi ya kumweka mhalifu katika kitanzi chenyewe.
Katika ufanyaji kazi tulikuwa tunalindwa na askari magereza. Kwa mfano, siku ya kufanya kazi, tulikuwa tunasindikizwa na askari wakati wa kwenda na kurudi. Ilikuwa lazima tulindwe na ulinzi mkali wa askari ili isije kutokea tukapata madhara na kushindwa kutimiza wajibu wetu
Kwa mfano, tulipotakiwa kufanya kazi Mbeya tulikuwa tunapewa ulinzi wa askari kutoka Dodoma hadi Mbeya na tulikuwa tunapewa huduma za hali ya juu za malazi na chakula ili tuwe na nguvu.
Kitu kingine ni kwamba ule usiku wa kuamkia siku ya kazi, tulikuwa tunapewa pombe. Mimi nilikuwa nakunywa bia aina ya Safari; basi unawekewa hata kreti zima, tunakunywa, tunakunywa hadi asubuhi.
Hadi ninapoamka asubuhi bado nakuwa na pombe kichwani; kabla ya kazi kuanza bado nakuwa na mning’inio wa pombe kichwani. Jambo hili lilikuwa linatusaidia sana kufanya kazi yetu vizuri na kwa ujasiri.
Mwisho wa mwezi tulikuwa tunalipwa mshahara mzuri tu na pia tulikuwa tunalipwa posho. Kwa wakati ule, kila tukitekeleza kazi tulikuwa tunapewa Sh700 kwa kichwa, baadaye katika miaka ya 1990 posho hii iliongezeka hadi Sh5,000 na baadaye miaka ya mwanzoni mwa 2000 tulipewa Sh50,000
Matanga kabla ya kifo

Unajua vifo vingine vyote hutokea ghafla, lakini kifo cha kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa kinajulikana. Mhalifu anajua kifo chake tangu siku anaposomewa hukumu yake ila anachosubiri ni kutekelezwa kwa hukumu hiyo basi.
Kwa utaratibu wa magereza, mhalifu aliyehukumiwa kifo, hutayarishiwa matanga siku moja kabla ya kunyongwa. Wanamweka katika chumba maalumu; kila mmoja kwenye chumba chake. Wanamfungia humo na wanampa chakula na huduma yoyote anayoitaka, hayo ndiyo matanga yake.
Wakati waliohukumiwa kifo wakiwa kwenye matanga, wafungwa wengine huimba nyimbo za maombolezo kama sehemu ya kuwaombea wenzao kabla kifo hakijawameza. Matanga hayo ni ya siku moja tu.
Kabla ya kumweka kitanzini, mfungwa yeyote huwa na maandalizi yake. Viongozi wa dini zote mbili za Kiislamu na Kikristo huitwa, wanafika magereza na kuwaongoza wahalifu sala ya toba.
Huo ndio utaratibu. Wakishafanyiwa sala ya toba au kuongozwa sala yoyote ile inayofaa kabla ya kifo, huwekwa tayari kwa ajili ya kunyongwa.

Anakuwepo pia mwanasheria wa magereza. Haiwezekani wakanyongwa bila ya kuwepo viongozi wa dini.
Hanyongwi mtu mmoja, inawezekana kwa siku moja wakawa watu wanane au kumi, inategemea na waliohukumiwa mwezi huo. Baada ya kutekeleza hukumu hiyo kwa mtu mmoja, nilikuwa naenda kupumzika kwa dakika 45 kabla ya kuendelea na kazi hiyo kwa mtu mwingine.
Kwa kawaida kazi huanza saa 2.00 asubuhi, baada ya kumaliza kazi tunakwenda kupumzika ofisini, tunakunywa kinywaji pale, baada ya dakika 45 tunarudi tena kuendelea na kazi.
Baada ya mapumziko ya dakika 45, tunakwenda kuangalia kama ameshafariki dunia, tukimaliza kuhakiki tunaendelea na wengine hadi waliopangwa siku hiyo wameisha. Kwa siku walikuwa watu wanane kutegemeana na idadi ya waliohukumiwa na kitanzi kinaweza kutumiwa na watu watatu kwa mpigo
“Kwa hiyo, tukimaliza watatu, tunasubiri na kuendelea na kazi.”

Follow account yangu @fbuyobe kisha weka notifications nitaendelea baadae.

Usisite kunifata telegram kwa

t.me/fbuyobe

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Fortunatus Buyobe

Fortunatus Buyobe Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @fbuyobe

Sep 6, 2025
Huko Harare, Zimbabwe katika barabara ya Borrowdale, kuna eneo la maduka makubwa maarufu kwa jina la Ballantyne Park Shopping Centre

Mwaka 2008, ilikuwa ukienda katika duka No. 19 kwenye maduka haya, ungekutana na mgahawa maarufu wa Millers Cafe

Mgahawa huu umebeba simulizi Image
Siku moja mchana mwaka 2008, nikiwa nimeboreka, niliingia kwenye mgahawa wa Millers

Niliongoza kwenye kiti kimojawapo ndipo nikasikia sauti ya mtu aliyekuwa ameketi nyuma yangu ikiniita

Nilipogeuka nikashtuka kubaini anayeniita ni mchungaji Uebert Angel Mudzanire Image
"Kijana, tangu ulipokuwa unaingia ndani ya mgahawa nimekuwa naona namba 33 kwenye paji la uso wako"

Aliniambia Mchungaji Angel

Sikumuelewa hivyo ikabidi nimuulize mchungaji:-

"Unataka kumaanisha nini?"

Jibu alilonipa lilikuwa mbali na uhalisia Image
Read 24 tweets
Sep 5, 2025
𝐒𝐨𝐦𝐞𝐭𝐢𝐦𝐞𝐬 𝟐𝟎𝟐𝟑

𝐋𝐨𝐠𝐢𝐬𝐭𝐢𝐜𝐬 𝐂𝐚𝐦𝐩
𝟖𝟑𝟏 𝐊𝐉
𝐌𝐆𝐔𝐑𝐀𝐍𝐈

𝟎𝟓𝟒𝟐 𝐇𝐑𝐒

Lutueni Kanali E.A Sambila ambaye ndiye Commanding Officer wa 831 KJ anapokea taarifa nyeti ofisini kwake kutoka kwa askari wake wawili wahusikao na ulinzi amani kikosini (MPs) Image
Askari hawa wawili ambao ni P.12925 Captain Theresia Cylil Massawe na MT. 88710 Sergeant Mohammed Faki Haji walifika ofisini kwa Lt.Gen Msambila wakieleza kuwa wana taarifa ya dharula

Kuwa kuna uwezekano wa muda wowote amani kutoweka mle kikosini

Wakaruhusiwa kuingia Image
Taarifa inayotolewa mbele ya CO, inalazimu muda mfupi unaofuata, askari wale wawili, kwa maelekezo ya CO wavamie ofisini kwa serviceman MT. 85115 Sergeant Sahani

Askari yule anawekwa chini ya ulinzi, na kwenye upekuzi, wanachukua simu mbili anazomiliki

Upekuzi ukahamia nyumbani Image
Read 13 tweets
Aug 30, 2025
Tarehe 28 August 2025, chama tawala, CCM kilizindua kampeni zake za uchaguzi mkuu wa urais na wabunge katika viwanja vya Tanganyika packers

CCM walilazimika kutumia jukwaa hilo la uzinduzi wa kampeni kujibu mashambulizi kutoka kwa mwanachama wake mwandamizi Humphrey Polepole Image
Image
Tangu kujiuzuru kwake July 13, mwaka huu kwa kile alichoeleza kama "kutoridhishwa na mienendo" ya serikali yake, balozi huyo wa zamani wa Tanzania nchini Cuba, amekuwa akitoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi waandamizi wa chama chake na serikali Image
Image
Polepole ameeleza juu ya uwepo wa kikundi anachokiita "CCM mtandao" ambacho huakikisha wanaohodhi madaraka ya rais

Kuwa mtandao huo nchini tangu mwaka 1995 zilipoanza siasa za vyama vingi na mtandao huu una agenda ya kuhakikisha kila rais anakuwa chini ya himaya yao Image
Read 45 tweets
Aug 2, 2025
Una uhakika kuwa wewe binafsi ulionana na IGP Sirro?

Unaweza kunieleza kwa ushaidi ni mara ngapi na wapi ulionana naye?

Unajua kuwa tuhuma unazotoa ni nzito ukihusisha watu wakubwa sana nchini?

Ilikuwa zamu yangu kuanza kumhoji mwanamama Jeannie Pollaert raia wa Netherlands Image
Nililazimika kumuuliza mama huyu maswali haya usiku wa manane baada ya kumaliza kusoma makabrasha mengi aliyonitumia kwa njia ya barua pepe.

Nilichokikuta ndani ya makabrasha yale kilifanya usingizi uliokwishaanza kunitongoza utoweke

Infact niliogopa sana

Nilihitaji ushaidi Image
Itakuwaje endapo Simon Sirro atakana kuwahi kukutana na wewe na kufanya na wewe kikao chochote?

Lilikuwa swali langu la kwanza.

Jeannie: Itakuwa vigumu sana kwa Sirro kukataa kuwa hajakutana nami

Akanipa ushaidi wa mawasiliano yao na jinsi Sirro alivyomjibu Image
Image
Read 25 tweets
Jun 27, 2025
Mwaka 2012, Blandine Nyoni akiwa katibu mkuu wizara ya afya, alinukuliwa akitoa kauli tata ya kuwabeza madaktari kuwa "wanajiona bora wakati ni wachafu na hawajui kiingeleza" Image
Katibu huyu akaendelea kusema kuwa hata yeye alisoma mchepuo wa PCB na kufaulu vizuri tu lakini kwa kutambua ubovu wa Medicine mzazi wake akamsomesha Accounts so hajui madaktari wanalalamikia nini.

Kauli hii ikang'oa kilaka kwenye jeans ya bishoo! Image
Ni kwamba mwaka huo, madaktari walikuwa katikati ya mgomo wa kihistoria

Kauli hii ikawatibua madaktari wakalianzisha upyaaaaa

Uzi👇

Dr. Ulimboka and total tools down

Nisome Image
Read 76 tweets
May 9, 2025
Wiki hii tumeshuudia waliokuwa wanachama wa Chadema wakitangaza kuachana na chama hicho huku wakiahidi kuelezea hatima zao za kisiasa siku za mbeleni

Kati ya waliohama ni waliowahi kuwa viongozi waandamizi wa chama hicho

Hii inamaanisha nini? Image
Kabla sijajibu swali hilo ni vyema tukipitia kwa ufupi mtiririko wa matukio (A quick refresher)

1. Dec 12,2024, Tundu Lissu anatangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA taifa

Nia hii ya Lissu ilikuja baada ya kuwa uchokozi wa wazi dhidi yake ndani ya chama Image
Kabla ya uamuzi huu, Lissu aliyekuwa ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA, alishamwandikia barua katibu mkuu wake kumjuza nia yake ya kuendelea kugombea kubaki kwenye nafasi hiyo.

Ulikuwa ni utaratibu wa CHADEMA kwa viongozi wa juu kutoshindania nafasi moja endapo mmoja ataonesha nia Image
Read 34 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(