Paul Bonaventure Profile picture
|| PEACE MAKER ✌🏿 || Author | - Medicines are my tools!💊 | Pharmacist | A human. Being. | Meditation Instructor 🧘‍♀️| HipHop🎶 |
May 16 21 tweets 3 min read
Ukilisoma andiko hili kwa jicho la kawaida, unaweza kuona ni hoja ndefu ya kujitetea.

Lakini ukiliangalia kwa jicho la kiintelijensia, unaanza kuona layers nyingi zinazogongana.

Kuanzia urvival narrative, perception management, operational distancing, controlled disclosure,..👇🏾 psychological positioning, na selective transparency.

Hapa ndipo andiko linakuwa interesting sana.

Kwanza kabisa, Buyobe ameandika kwa style ambayo intelligence analysts huiita pre emptive framing.

Yaani kabla hata hajaanza kujibu tuhuma, anaanza kwa kujitengenezea identity..
Dec 21, 2025 6 tweets 8 min read
Kuyeyuka kwa ndoto ya Marekani kumiliki kbi ya Jeshi ukanda wa Bahari ya Hindi nchini Tanzania tangu mwaka 1947

Ndoto ya Marekani kumiliki kambi ya jeshi eneo la ukanda wa bahari ya Hindi nchini Tanzania ilianza zamani tangu mwaka 1947.

Kipindi cha msuguano wa vita baridi kati ya Marekani na washirika wake wenye itikadi na falsafa za kibepari dhidi ya Umoja wa Nchi za Kisovieti, yaani USSR na washirika wake wenye itikadi na falsafa za Kikomonisti.

Lengo la Marekani kutaka kumiliki kambi ya jeshi Tanzania alitaka kudhibiti biashara na nguvu za Umoja wa Nchi za Kisovieti Kwa sababu Marekani aliona nguvu ya Ureno ni ndogo katika koloni la Msumbiji.

Mwaka 2002-2003 Mkuu wa majeshi ya Tanzania Generali George Waitara alipokea ujumbe kutoka kwa maafisa wa juu wa serikali ya Marekani.

Baada ya maongezi marefu na Hayati Benjamin William Mkapa, ikabidi Mkapa awaambie wakaonane na mkuu wa majeshi.

Generali George Waitara akawasikiliza na kuwaambia wataje masharti yao.

Ndipo maafisa hao wakachomoa makaratasi kwenye mkoba na kuanza kusoma mambo ambayo yangefanyika endapo serikali ya Tanzania ingekubali Marekani apate eneo la kujenga kambi ya jeshi.

Mkataba huo ulikuwa na vipengere kumi kwa mujibu wa Brigedia Generali mstaafu jina X.

Kwanza, Wanajeshi wa Marekani wakifanya uhalifu kwenye ardhi ya Tanzania hata kama ni kuua watapaswa kushtakiwa kwao Marekani.

Pili, Serikali ya Tanzania haipaswi kuingilia mambo yanayofanyika katika kambi ya jeshi ya Marekani.

Tatu, Eneo pendekezwa la kambi ya jeshi ya Marekani litakuwa na uwanja wa ndege ambao utajitegemea mawasiliano yake bila kuingiliwa wala kuwa chini ya mfumo wa Mawasiliano na intelijensia ya serikali ya Tanzania.

Nne, Marekani itawashambulia maadui zake ukanda wa bahari ya Hindi kupitia kambi yake ya jeshi itakayojengwa Tanzania.

Tano, Marekani itatoa msaada mkubwa wa silaha na mafunzo kwa Wanajeshi wa Tanzania na Tanzania atakuwa mshirika mwaminifu.Image Sita, Marekani itafanya uwekezaji mkubwa wa huduma za kijamii kama shule, hospitali na maji kwa maeneo ya karibu na kambi ya jeshi ya Marekani nchini Tanzania.

Saba, Meli za kijeshi za Marekani zinapaswa kupewa uhuru wa kufanya doria eneo la ukanda wa bahari ya Hindi bila masharti.

Nane, Marekani itatoa ajira kwa vijana Wakitanzania kujiunga na Jeshi la Marekani.

Tisa, Marekani na washirika wake watatumia eneo la Bahari ya Hindi ukanda wa Tanzania kufanya mazoezi ya kijeshi na washirika wake.

Kumi, Makubaliano haya yana nafasi ya majadiliano.

Generali George Waitara alikataa ombi la Marekani kutaka eneo la ukanda wa bahari ya Hindi nchini Tanzania hasa pwani ya Kimbiji na kisiju na alinukuliwa kwa kusema yafuatayo.

"Kumkaribisha Marekani ni kukaribisha kifo mlangoni, Tanzania ni nchi huru, hatuwezi kujenga nyumba halafu funguo tukamkabidhi mtu wa mbali ambaye tunamjua historia yake na vituko vyake."

Wamarekani hawakukata tamaa wakarudi kwa Mheshimiwa Benjamin William Mkapa naye akawajibu Kwamba msimamo wa jeshi ndio msimamo wake.

Baada ya serikali ya Tanzania kukataa kuuza eneo kwa Marekani Ili ajenge kambi ya jeshi kulinda maslahi yake eneo la ukanda wa bahari ya Hindi.

Ikabidi ndugu zetu kutoka Kenya kukubali kuuza eneo la Jubaland mpaka wa Kenya na Somalia ambapo mpaka sasa kuna kambi ya jeshi ya Marekani.

TURUDI KWENYE HISTORIA KIDOGO

Baada ya Ujerumani na washirika wake kupoteza kwenye vita ya kwanza ya dunia mwaka 1918, mwaka 1919 January wababe watatu wa dunia walikutana Paris Ufaransa kujadili hatma ya ulinzi na usalama wa dunia (Versailles Peace Treaty).

Raisi wa 28 wa Marekani Wilson Woodrow, Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Lyold David George na waziri mkuu wa zamani wa Ufaransa George Clemenceau walikuja na maazimio kadhaa.

Ambayo yalimminya Ujerumani na kumdogosha kiuchumi, kisiasa na kijeshi ambapo Ujerumani alipoteza makoloni yake Afrika ikiwemo Tanganyika, Rwanda, Burundi,Togo, Cameroon na Namibia.

Tanganyika ilichukuliwa na Uingereza kwa uangalizi wa muda wa Umoja wa Mataifa wa kipindi hicho League Of Nations.Image
Feb 3, 2025 6 tweets 5 min read
Katika dunia ya sasa, pesa si tu kipimo cha mafanikio, bali ni chombo cha utawala.

Mtu au kikundi kinachoshikilia pesa, ndicho kinachoshikilia dunia.

Hii ni dhana ambayo Freemason waliielewa mapema zaidi kuliko mtu mwingine yeyote, na wakajenga mfumo wa kifedha ambao unawapa mamlaka ya kuamua hatima ya kila mtu.

Walijua kwamba ili kudhibiti dunia, hawakuhitaji mabavu wala vita.

Walihitaji tu kushikilia mzunguko wa pesa kuamua zinakotoka, zinakokwenda, na nani anazimiliki. Walifanikiwa.

Njia ya kwanza waliyoitumia ni benki. Walizianzisha na kuzifanya kuwa sehemu ya lazima katika maisha ya binadamu wa sasa.

Leo, unaweza kuishi bila nyumba, lakini huwezi kuishi bila akaunti ya benki.

Kwa nini? Kwa sababu:

Kila mshahara lazima upitie benki.
Kila biashara kubwa lazima ipitie benki.
Kila mkopo lazima utolewe na benki.

Kwa njia hii, wanajua unaingiza kiasi gani, unapoteza kiasi gani, unatumia kwa vitu gani, na hata ukiwa unaelekea kufilisika, wanajua hilo kabla yako.

Ndiyo maana matajiri wakubwa wa dunia, wale walioanzisha benki hizi, si watu wa kawaida. Wanatoka katika familia ambazo zimeshikilia pesa kwa vizazi vingi.Image Walipoona benki pekee haitoshi, wakaanzisha soko la hisa. Wakahakikisha hakuna mtu anayeweza kufanya biashara kubwa bila kupitia mifumo yao.

Hii ni sababu kubwa kwa nini watu wengi wanaogopa mfumo wa benki lakini hawawezi kuuacha. Kwa sababu mfumo huu umewafanya watumwa wa kifedha.

Freemason walipoona wanashikilia mzunguko wa pesa, wakagundua kitu kingine muhimu, Taarifa za Binadamu.

Hivi leo, hakuna mtu anayemiliki maisha yake kikamilifu. Taarifa zako zote zipo mikononi mwao, iwe unajua au hujui.

Walifanya hivi kwa kutumia simu na intaneti.

Wakaanzisha kampuni kubwa za simu kama Apple, Samsung, Huawei na zinginezo.

Wakaweka kamera kwenye simu ili waweze kukuona muda wote.

Wakakuletea Facebook, Instagram, WhatsApp na mitandao mingine ili wakufuatilie zaidi.

Wakakuhamasisha kutumia GPS ili wajue unakoenda.

Hivi leo, hakuna kitu unachofanya bila wao kujua.

Ndiyo maana magaidi wa kimataifa wamekatazwa kutumia simu zenye kamera au hata kutumia kompyuta zilizounganishwa kwenye mtandao.

Kwa sababu pale tu wanapofungua simu zao, wanakuwa wamejifunua kwa dola kubwa za dunia.Image
Jan 27, 2025 5 tweets 4 min read
Kabla ya Captain Ibrahim Traoré, Alikuwepo Captain Thomas Sankara, Shujaa Aliyegeuka Alama ya Mapinduzi Afrika.

Thomas Sankara, mwanamapinduzi na rais wa Burkina Faso kati ya mwaka 1983 na 1987, alikuwa zaidi ya kiongozi wa kawaida.

Alikuwa sauti ya matumaini kwa Waafrika waliokuwa wakihangaika na mizigo ya ukoloni mamboleo na ubeberu wa mataifa ya Magharibi.

Sankara, ambaye mara nyingi huitwa "Che Guevara wa Afrika," aliongoza nchi yake kwa miaka minne tu, lakini athari zake zimeendelea kuishi kwa vizazi hadi leo.

Katika kipindi kifupi cha uongozi wake, Sankara aliwapa watu wa Burkina Faso maono ya nchi huru, inayojitegemea, na yenye ustawi.

Sankara aliamini kuwa elimu ni ufunguo wa maendeleo. Katika kipindi chake, aliweka juhudi kubwa kuhakikisha kuwa watoto wa Burkina Faso wanapata elimu bora.

Alifanikiwa kuongeza kiwango cha wanafunzi mashuleni kwa asilimia 6, juhudi ambazo zilikuwa ngumu kwa nchi masikini yenye rasilimali chache.Image Hili ni moja ya mafanikio makubwa ya uongozi wake.

Sankara alizindua kampeni kubwa ya chanjo, na kufanikisha kuwapatia watoto milioni 2.6 chanjo za kupambana na magonjwa kama pepopunda, surua, na homa ya ini. Kampeni hiyo iliwasaidia maelfu ya watoto kuepuka vifo vya mapema.

Kutokana na hali ya kijiografia ya Burkina Faso, ambayo iko katika ukanda wa Sahel na mara nyingi hukumbwa na ukame, Sankara alizindua kampeni ya upandaji miti.

Alifanikiwa kupanda miti milioni 10, juhudi zilizolenga kupambana na jangwa na kuhifadhi mazingira.

Sankara aliongoza harakati za kuikomboa Burkina Faso kutoka kwenye utegemezi wa Kifaransa.

Alikataa misaada ya kifedha kutoka kwa nchi za Magharibi, akisisitiza kuwa misaada hiyo ilikuwa njia ya kudumisha utegemezi.

Alihamasisha wananchi kufanya kazi kwa bidii na kujitegemea.Image
Jan 24, 2025 6 tweets 4 min read
Hakuna Zaidi ya Milioni Moja kwa Talaka.

Sauti ya Rais wa Marekani, Donald Trump, siku zote imekuwa na uzito wake.

Lakini safari hii, hotuba yake imezua mjadala mzito si tu nchini Marekani, bali duniani kote.

Katika kikao kilichokuwa kimejaa viongozi wa kisheria, Trump alitangaza mapendekezo mapya ya mabadiliko makubwa katika sheria za ndoa, akidai kuwa mfumo wa sasa unamnyonya mwanaume na kugeuza ndoa kuwa "biashara."

Trump alisisitiza kuwa sheria mpya zitalinda wanaume, haswa wale waliofanikiwa kifedha, dhidi ya wanawake wanaoingia kwenye ndoa kwa malengo ya kifedha pekee.

“Haiwezekani mwanaume awe ametumia miaka mingi kujenga utajiri wake, kisha mwanamke aingie kwenye ndoa, afanye madudu, na mwisho wa siku atoke na nusu ya mali za mwanaume huyo,” alisema kwa ukali.

*Sheria Mpya Inasemaje?
Kwa mujibu wa mabadiliko yaliyopendekezwa.

Mwanamke atakayetalakiana na mume tajiri hataruhusiwa kuchukua nusu ya mali zake. Badala yake, atapewa kiwango cha dola milioni moja ($1,000,000) pekee, bila kujali kiwango cha utajiri wa mume huyo.Image Watoto wa ndoa watakuwa chini ya malezi ya baba yao, hasa ikiwa mama atajitetea kuwa hana uwezo wa kifedha wa kuwalea.

Sheria hizi zinalenga kuzima tabia za baadhi ya wanawake masikini wanaoingia kwenye ndoa na matajiri kwa lengo la kupata mali kupitia talaka.

Trump alisema wazi, “Hii si sawa! Haiwezekani ndoa iwe biashara ya haraka ya kutajirika. Mwanamke anaingia masikini, lakini kwa talaka tu anageuka mamilionea. Hilo halitokuwepo tena.”

Trump alieleza kuwa mfumo wa sasa wa talaka Marekani unakandamiza wanaume, hasa wale waliofanikiwa kifedha.

Wengi wamejikuta wakipoteza nusu ya utajiri wao kwa talaka ambazo zinakuja kwa sababu zisizo za msingi.

Mfano mmoja uliojadiliwa sana ni wa Jeff Bezos, mwanzilishi wa Amazon, ambaye alitoa dola bilioni 38 ($38 billion) kwa aliyekuwa mke wake, MacKenzie Scott, kama sehemu ya makubaliano ya talaka.

Ingawa Bezos aliendelea kuwa tajiri zaidi duniani, mfano huu umeibua maswali mengi kuhusu uwiano wa haki katika ndoa na talaka.Image
Jan 2, 2025 4 tweets 2 min read
Wanaume tukiwaangalia wake zetu, tunajua ni lipi sahihi kwako kufanya na lipi si sahihi japokuwa sometimes wanawake wanajifanya kujua kila kitu.

Wakati Kanye West amemuoa Kardashian na kuishi pamoja, kuna siku mwanamke huyo alimwambia mumewe kwamba amepata dili la kupiga picha za bidahaa fulani na ameahidiwa kulipwa dola milioni moja.

Kanye alipoambiwa, alimkatalia na kumwambia haiwezekani.

Hiyo si kampuni nzuri, wamekupa pesa nyingi lakini gharama zake ni kubwa sana mbeleni.Image Na watu wanasema kampuni hiyo inaweza kuwa ni Ciroc ambayo ilikuwa inatangazwa sana na Diddy na kuwa na asilimia kadhaa za umiliki mpaka alipotolewa kutokana na skendo zake.

Kardashian anasema alikasirika sana, yaani siku hiyo alimlaani sana mumewe kwa kuwa alimkosesha dili la pesa nyingi.

Muda huo walikuwa wakiwasiliana tu kwenye simu, kesho yake, akapokea cheki ya dola milioni moja kutoka kwa mumewe na zawadi nyingine kibao.

Hii ilimaanisha kwamba pesa si tatizo, ila utu wako ndiyo kitu cha muhimu sana.

Ukiachana na hilo la mkewe, hata Kanye West aliwahi kukutana na kisanga kutoka kwa Ulluminate.Image
Dec 27, 2024 4 tweets 2 min read
50 Cent anasema kwamba Eminem ndiye aliyemfanya kuwa na mafanikio makubwa aliyokuwanayo mpaka sasa hivi.

Albamu yake ya kwanza iliuza kopi milioni 13 huku albamu ya eminem ya Marshall Mathers ikiuza kopi milioni 23.

50 Cent anasema Eminem alikuwa na uwezo wa kutoa albamu na kuuza sana zaidi ya hiyo lakini hakufanya hivyo kwa sababu ya mtoto wake.

Ikumbukwe kwamba Eminem hakupata malezi mazuri kutoka kwa mama yake na hivyo naye hakutaka kutoa malezi yaleyale kwa mtoto wake, Hailie.Image Mama yake Haile aitwaye Kim alikuwa amekubuhu kwenye matumizi ya madawa ya kulevya.

Hivyo Eminem akaona kabisa kama angeruhusu mwanamke huyo amlee mtoto wake basi asingekuwa kama vile anavyotakiwa kuwa na ndiyo maana akamchukua na kuishi naye.

Eminem akawa bize na kumlea mtoto wake, hata ugawaji wa tuzo za Grammy aliposhinda, hakutaka kwenda ukumbini, alibaki nyumbani akiangalia katuni na mtoto wake.

Kama jamaa angeamua tu niendelee kufanya muziki kama kawaida, nikapige show basi angekuwa anauza sana kwenye show zake na hata albamu zake nyingine zingefanya mauzo makubwa mno.Image
Dec 13, 2024 6 tweets 4 min read
Bob Makani Muasisi wa CHADEMA akiwa na Edwin Mtei 1966

Hayati Bob Nyanga Makani alizaliwa mwaka 1936 katika Hospitali ya Kolandoto, Shinyanga.

Alikuwa ni mmoja wa watoto wengi katika familia ya Mzee Makani.

Alipokuwa na umri wa miaka sita alianza masomo yake katika Shule ya msingi Ibadakuli huko huko Shinyanga.

Kama ilivyokuwa kawaida ya Serikali ya Mkoloni Muingereza hapa Tanzania wakati huo, watoto wa Machifu walipelekwa kusoma Shule ya Sekondari Tabora, ndivyo ilivyokuwa kwa Hayati Bob pia.

Kutokana na uhodari wake katika masomo, Mheshimiwa Bob Makani alifaulu na kupelekwa katika Chuo Kikuu cha Makerere kilichopo Nchini Uganda.

Wakati huo kikiwa Chuo Kikuu cha pekee Afrika Mashariki, ambako alifuzu na kupata Shahada ya kwanza ya uchumi (BA Economics).Image Mwaka 1961 alikwenda Chuo Kikuu cha Liverpool kilichopo Nchini Uingereza na mwaka 1965 alitunukiwa Shahada ya Sheria (LLB).

Kwa mujibu wa Sheria za Uingereza, anayehitimu Shahada ya Sheria, ni lazima vile vile afaulu mitihani ya Sheria kwenye Middle Temple, London, Uingereza.

Hivyo Mheshimiwa Bob Makani alifanikisha hilo mwaka huo huo na kurejea nyumbani Tanzania.

Aliporudi Tanzania, aliajiriwa na Serikali kama Mwanasheria wa Serikali kwa muda mfupi kabla hajapandishwa Cheo na kuwa Exchange Control Manager wa Benki Kuu.

Hapo ndipo alipokutana na kuwa karibu na Mzee Edwin Mtei aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu wakati huo.

Ndiyo maana haikuwa ajabu lilipoanza vuguvugu la Siasa za mabadiliko Nchini mwaka 1966, Mheshimiwa Makani na Mzee Edwin Mtei walikuwa pamoja.

Mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi vya siasa ulipokubaliwa rasmi Nchini, Mhe.Bob Makani na Mzee Edwin Mtei walikuwa mstari wa mbele katika kuunda Chama cha Siasa.Image
Dec 9, 2024 7 tweets 5 min read
Ilikuwa ni mwaka 1995 wakati huo Bill Clintoni akiwa katika kipindi chake cha kwanza cha uongozi mareka akiwa na umri wa miaka 46.

Monica yeye alianza kufanya kazi Ikulu katika ofisi ya katibu mkuu kiongozi (Chief of Staff) Leon Paneth tangu June, 1995 kam mfanya kazi mwanafunzi (Intern) akiwa ametok kuhitimu chuo cha Lewis & Clark college.

Ni hapo Bill Clinton alipomuona na kuvutiwa na binti huyo aliekuwa bado mchanga na mbichi wa miaka 21 tu na kwa mujibu wa Monica walianza mahusiano na Rais November mwaka huohuo.

Baada ya Rais kuwa na mahaba na Monica na hivyo kunogewa nayo msaidizi wa katibu mkuu kiongozi Evelyn Liberman alishtukia mchezo na April 19 aliamua kumwamisha Monica katika ofisi ya msema msaidizi wa wizara ya Ulinzi (Pentagon) bwana Ke Bacon.

Bi Evelyn alitoa sababu kuwa amemwamishi kutokana na Monica kuonyesha tabia zisizofaa na kitoto “Inappropriate and immature behavior".Image Lakini pia watendaji wengine walikuwa wakitilia shaka ukaribu uliopitiliza kati ya Monica na Rais.

Ni katika ofisi hi za pentagon ndipo Monica akakutana na Linda Trip binti aliyekuwa mfanyakazi wa idara ya Ulinzi katika wizara hiyo wakaunda urafiki.

Kutokana na ukaribu wa kiutendaji kati ya Pentagoni na Ikulu bado Monica alikuwa na nafasi kubwa ya kuwa anafika Ikulu mara kwa mara na mara nyingi alitumia muda mwingi sana katika ofisi ya Rais.

Kitu ambacho bado hakikuwa kikiwafurahisha wafanyaka wa Ikulu na hivyo October 1997 Ikulu iliandaa mpango wa kumwamisha tena bi Monica na kumtaka ahamie ofisi za umoja wa mataifa UN.

Ni balozi Bill Richardso aliyeombwa ampangie kazi Monica lakini baada ya usaili wa kazi bi Monica aliikata nafasi hiyo na hivyo kubakishwa Pentagon.Image
Dec 7, 2024 8 tweets 6 min read
Wanajeshi wengi wa Kijerumani walikuwa wanampenda sana Adolf Hitler kwa sababu alionekana kuwa mkombozi wa kweli.

NB: Turudi darasani kidogo

Wakati wa vita vya dunia vya kwanza vinamalizika mwaka 1918, kulikuwa na wanajeshi wengi sana waliouawa lakini mataifa makubwa Ulaya yalimwambia Ujerumani kwamba wao ndiyo walioua watu wengi, hivyo ilikuwa ni lazima kulipishwa.

Wakawa wanakatwa pesa nyingi, hawakutakiwa kutengeneza silaha yoyote ile na muda wote walikuwa kwenye uangalizi.

Tazama hata sasa hivi, Ujerumani huwa hapendi vita kwa sababu anajijua yeye ni nani.

Ana nguvu kubwa mno ya kupambana, mfano cheki hata uimara wa vifaa vyake anavyotengenezea, ubora wake, kuna picha fulani itakujia kichwani.

Sasa Ujerumani haikutakiwa kufanya chochote kile kitu kilichowaumiza hata wao wenyewe Baadaye kuna mkombozi akatokea, huyu alikuwa dogo mchoraji aliyelelewa na mzee mmoja wa Kiyahudi.Image Sasa baadaye akaona mbona kama mambo yanakuwa ya kijinga sana, inakuwaje tumezuiwa kuproduce kitu chochote kile halafu hapohapo tunatakiwa kulipia mapesa mengi kwa maafa tuliyosababisha? Mbona wao pia waliua? Haiwezekani, ni lazima lifanyike jambo.

Hapo ndipo kwa siri akawakusanya Wajerumani wenzake na kuanza kuwapanga kwamba walitakiwa kufanya jambo na si kukaa kifala kama walivyokaa, wakakubaliana na hatua ya kwanza kabisa ilikuwa ni kutengeneza silaha.

Huwezi kupambana na mtu kama huna silaha, walizitengeneza kwa siri na walipoona wapo tayari, wakagoma kutoa pesa, wakagoma kuendeshwa, waligomea kila kitu.

Sasa Muingereza, Mfaransa na washiriki wenzake wakaona haiwezekani, hawa watu mbona wamekuwa jeuri? Kuna nani nyuma yake.

Unajua mtu akiwa chini yako ni lazima umuendeshe, sasa ikitokea siku moja ameanza ujeuri, lazima ujue kuna mtu anampa nguvu.

Watu waliowahi kuoa na kuachana na wake zao watakuwa wanalijua hili.Image
Oct 26, 2024 7 tweets 5 min read
LEO NAKUJUZA USIYO YAJUA KUHUSU KITABU CHA ENOKO

NB: Uzi ni mrefu sana

Kwa Mujibu wa simulizi za kiebrania, Enoko ndiye Mtu pekee aliyeweza kukutana na Malaika tofauti tofauti yaani zaidi ya mmoja.

Binadamu Wengine waliowahi kukutana na Malaika walikutana aidha na Gabriel au Mikael au Rafael

Enoko ndiye Mhusika pekee aliyeweza kuwataja Malaika wengi zaidi Kwa majina na Sifa zao za kimaumbile.

Enoko ndiye Mhusika pekee kwenye Biblia aliyeweza kuelezea Mianga kama Jua na Mwezi na mizunguko yake.

Enoko alikuwa Mtu wa kusafirishwa na Malaika kutoka anga Moja kuelekea nyingine. Ilikuwa kawaida Kwa Enoko kupotea hata miaka 50 bila kujulikana alipo.

Enoko ndiye Mhusika pekee aliyeelezea Kwa majina Malaika 200 Walioasi na kuzaliana na Wanadamu.

Kwa jinsi nilivyoielewa simulizi ya Enoko ni Kwamba, binadamu ni kama mnyama, tofauti yake ni utashi tuu.

Stori ya Kitabu cha Enoko Kwa kifupi Ipo hivi.

Kuna mbingu 12 na kila mbingu kuna Malaika wake Mkuu anayoiongoza.

Malaika 200 waliasi wakiongozwa na Kiongozi wao aitwaye Samzaiya. Viongozi Wengine ni Azazel

Katika hao Malaika kila Malaika alikuwa na sifa, uwezo na nguvu zake. Wapo waliokuwa na mbawa Mbili, wapo mbawa nne (Serafi) wapo wa mbawa sita (Makerubi) na yupo Malaika mmoja aitwaye Samael mwenye mbawa Kumi na Mbili (Huyu role yake ipo kitofauti)

Malaika hawa walikuja kuzaa na Wanawake wa wanadamu. Wakazaa majitu, Nephili au miunguwatu (Demigods)

Azazel Moja ya Malaika alioasi aliwafundisha Wanadamu Teknolojia za silaha, uchawi, unajimu, urembo kama kupaka makeup. Kitabu kinaeleza kuwa Malaika walioasi wakawafundisha mambo mengi sana àmbayo Kwa Sasa ndîo tunaita Teknolojia na utandawazi.

Jambo lililonishangaza ni kuona mpaka masuala ya Teknolojia ya kutumia Dawa Fulani ili Wanawake wasibebe mimba ili kutoharibu urembo wao. Hii ilifanya Baadhi ya Wanawake waliotumia Teknolojia ya Kuzuia mimba baadaye kushindwa kupata watoto.

Enock anaeleza hayo.Image Demigods yaani wale machotara wa Malaika na binadamu ambao Kwa uelewa wangu ndio nahisi wanaitwa Majini.

Wakawa wanakula kupita kiasi Jambo ambalo mama zao (Wanawake wa kibinadamu) walishindwa kuwalisha, wale Demigods wakaanza Kunywa damu za watu, kisha nyama zao, kisha wakawa wanakula ndege, wanyama na samaki wa baharini.

Kipindi hicho nafikiri wanyama kama Godzilla waliishia kuliwa na hawa Demigods.

Urefu wao (Demigods) ulikuwa Mita thelasini kwenda juu na walikuwa na uwezo mchangayiko yaani uwezo wa kibinadamu na kimalaika.

Wanadamu wakawa wanalia kutokana na kuuawa na hawa Watoto chotara (Demigods au wanefili).

Kilio chao kilitokana na dhulma ya uhai, kuchukuliwa Wake zao, kuteswa n.k.

Kilio kikafika mbingu ya Tano huko alikuwepo Malaika Mikael, Gabriel, Rafael na Uriel.

Malaika hao nao cheo chao ni kikuu, Wakaweka kikao huku wakilalamika wao Kwa wao Kwa matendo yanayofanywa na kina Samzaiya na Azazel na wenzao.
Mar 7, 2024 14 tweets 5 min read
HATUA ZA KUFANYA MEDITATION (TAHAJUDI):

Kinachotakiwa wakati unajiandaa
Kufanya meditation ni kama ifuatavyo:

• Tafuta sehemu iliyotulia, isiyo na makelele, Kaa kwenye kiti au chini, au lala kitandani. Hakikisha huumii mahali popote, Legeza mwili wako pamoja na misuli yote..
. Image ya mwili wako kwa kadri utakavyoweza.

• Sahau matatizo yako yaliyopita, yaliyopo na yajayo. Sahau matatizo yako ya kazini au nyumbani. Jitahidi usifikirie chochote.

• Ni muhimu sana kujali hisia zako wakati unafanya meditation.

• Pumua kwa kuingiza pumzi ya kutosha..
.
. Image
Dec 17, 2023 21 tweets 5 min read
UKWELI KUHUSU DUA YA ALBADIRI KATIKA DINI YA UISLAMU:

Albadiri ni neno linalotumika kurejea kwa Ahlul-Badr (Waliopigana Vita vya Badr).

Badr ni sehemu iliyo karibu na mji wa Madina nchini Saudia Arabia na ndio iliyokuwa sehemu ambayo Waislamu wakiongozwa na Mtume...
.
. Image (Swalla Allahu ‘alayhi wa aalihi wa Sallam) walipambana na Makureishi waliokua wakiwapiga vita Waislamu.

Wasiokuwa Waislamu na hata Waislamu wamekuwa wakisikia kisomo cha "Albadiri" au wengine huiita "Alalbadiri" na kwamba hutumika kumsomea mtu au watu waovu kama vile wezi,..
.
Dec 13, 2023 15 tweets 4 min read
WATU WALIOPOTEA NA KUTOONEKANA TENA DUNIANI:

• D.B.Cooper

Ni jina linalotumika kumrejelea mwanaume mmoja wa makamo ambaye jioni ya November 24, mwaka 1971 alichukua kiasi cha Dola za Kimarekani 200,000 kama malipo mara baada ya kuiteka ndege huko portland nchini Marekani.
.
. Image Licha ya msako mkali wa zaidi ya miaka 45 uliofanywa na FBI kwa kushirikiana na idara nyingine za kiusalama nchini Marekani, bado D.B Cooper hafahamiki ni wapi alipo wala pesa alizopewa hazikuwahi kuingia kwenye mzunguko wala kupatikana.
.
.
Oct 6, 2023 11 tweets 3 min read
"I LOOK JESUS AS SON OF JOSEPH NOT AS THE MESSIAH":

Siku mbili kabla ya sikukuu ya Krismas yaani 23, December 2011 nchini Kenya ilifunguliwa kesi maarufu na bwana Dola Indidis mwanasheria maarufu nchini Kenya aliyeishtaki nchi ya Israel kwa kumuua Yesu.
.
. Image Kesi hiyo namba FOJ/001/D10/11 Wakili msomi Indidis alidai hakuipeleka kesi mahakamani kwa misingi ya kidini bali kwa misingi ya Kisheria.

Alisema "Its academic thing not a theological thing", Yeye alichoangalia si unabii bali legal procedure.

Pia alisisitiza ameamua kumtetea..
May 27, 2023 4 tweets 2 min read
BOB MARLEY NA WATU WASIOJULIKANA:

Tarehe 3 December Mwaka 1976 muasisi wa Reggae Bob Marley alishambuliwa kwa risasi nyumbani kwake.

Jaribio hilo lililofanywa na "Wasiojulikana"lilifeli na badala yake kumjeruhi kidogo mkononi.
.
. Image Baada ya tukio hilo Bob Marley aliondoka nchini Jamaica na kuelekea Ulaya kwa usalama wake.

Akaitumia nafasi hiyo ya miezi 18 nje ya Jamaica akifanya matamasha mbalimbali ya muziki.

Katika mahojiano na mwandishi flan Bob Marley aliulizwa kwanini ameamua kukimbia nchini Jamaica Image
May 24, 2023 11 tweets 4 min read
TUJIKUMBUSHE KIDOGO KUHUSU DONALD TRUMP NA CHUKI YAKE DHIDI YA WATU WEUSI KWENYE HOTUBA YAKE YA MWAKA 2018:

Alisema

Hatulazimiki hata kwa sekunde moja kuthibitisha kwa yeyote yule kuwa sisi ni wenye nguvu (superior) kuliko wao. Tuna njia zaidi ya 1001 za kuthibitisha hilo kwao. Image Marekani tunayoiona leo haikuundwa kwa matamanio ya kifikra, Iliundwa kwa gharama kubwa ya akili, jasho na damu.

Hatuwezi kufanya unafiki kama wafanyavyo wazungu wengine kwa kujifanya tunawapenda waafrika.

Lazima tukiri bila hofu yoyote kwamba HATUWAPENDI na tuna sababu nyingi Image
Apr 26, 2023 11 tweets 4 min read
JAILI CHINJA CHINJA ALIYEVUMA MBEYA NA MAMA YAKE ALIYEKUFA NA KUFUFUKA MARA TATU:

Ukifika Mbeya Mjini kuna eneo linaitwa Forest Mpya.

Siku za nyuma eneo hilo lilijulikana tu kama Forest kwa kuwa kulikuwa na msitu mkubwa sana wa miti ya milingoti ambayo Kama huijui ni miti Image inayozalisha nguzo za umeme.

Huu msitu ndio Jaili aliutumia kuchinja watu ambao alikuwa akiwapiga kwanza na nyundo, Kisha huwapakia kwenye gari na kwenda kuwachinja Forest.

Mama yake Jaili alikuwa ni mchawi sana na alikufa na kufufuka Mara tatu kwenye uhai wake. Image
Apr 25, 2023 5 tweets 2 min read
MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA GEORGE FLOYD:
💔🙏🏾🕊

George alikatishwa uhai wake na Polisi wanne wa kizungu akiwa na umri wa miaka 46 .

George aliuawa baada ya kwenda kwenye mgahawa mmoja huko Minneapolis kwa ajili ya kupata Chakula na akiwa na mwenzake ghafla Polisi walimzunguka.. Image na kumfunga pingu wakimtuhumu kwa kughushi bili yake ya chakula/Forgery.

Licha ya kujitetea lakini Polisi hao waliendelea kumkandamiza George, ambae alikua hawezi kufanya chochote kutokana na kufungwa pingu mikononi mwake. Image