#TOTTechs 🇹🇿 Profile picture
Washauri na wataalamu wa Teknolojia || 💻 Computers ||📱 Phones || 🎮 Games ||🎯 Softwares || ⚙️ICT Hardwares || 🛡ICT Security || 📧tottechstz@gmail.com
Sep 23, 2023 • 24 tweets • 5 min read
SABABU ZINAZOPELEKEA SIMU KULIPUKA.

Hivi karibuni tumeona matukio ya simu kulipuka zikiwemo simu za Oneplus Nord 2, Galaxy Note 7 na
baadhi ya simu ya nyingi zikiwemo simu kutoka kampuni ya iPhone, Oppo, Xiaomi, Vivo, n.k

Powered by #ElimikaWikiendi Ă— @fiidzsocial

UZI MFUPI 👇
Image
Image
Kati ya matukio makubwa ya simu kulipuka ilikuwa ni simu za
Galaxy note 7 hii ilipelekea Samsung kuomba simu hizo zirudishwe kiwandani kwa uchunguzi zaidi.

Matukio ya simu kulipuka yanajirudia kila siku japo kuna makosa ya kiufundi makosa na mtumiaji.

#ElimikaWikiendi
Image
Image
May 30, 2023 • 10 tweets • 3 min read
Maoni ya busara kwa leo.

Uzi mfupi

• Kama wewe ni Fan/shabiki wa kitu au kampuni flani, unatakiwa ujue kuheshimu mawazo ya watu wengine, unatakiwa ujue kutofautisha kizuri na kibaya, unatakiwa ujue kutofautisha Facts/ukweli na Opinions/maoni.  👇 ImageImageImageImage • Acha kuhoji na kubeza maamuzi ya watu, ingawa unaweza kutoa maoni yako kuhusu maamuzi yao.

• Unapoibeza kampuni nyingine kwa kufanya kitu, lakini unatetea kampuni unayoipenda kwa kufanya kitu kile kile, hiyo inamaanisha WEWE ndiye tatizo.
Dec 18, 2021 • 18 tweets • 9 min read
Wakati huu tunapo kwenda likizo za sikukuu za Christmas na mwaka mpya, huwa ni muda mzuri kukaa na familia zetu, ndugu, jamaa na marafiki kutafakari mwaka ulivyokuwa na kujiandaa na mwaka unaofuata.

#ElimikaWikiendi

STADI/SKILLS ZA MUHIMU KUJIFUNZA

UZI [THREAD] 👇 Pia ni kipindi ambacho watu wengi hupendelea kuwepo mitandaoni. Wakati unatumia mitandao ni vyema ukapata ujuzi mpya wa namna unaweza faidika na mitandao.

Tutakuelezea baadhi ya ujuzi wa mtandaoni unaoweza kuwa na faida kwako kwa namna moja ama nyingine.

#ElimikaWikiendi
Aug 21, 2021 • 23 tweets • 11 min read
ARTIFICIAL INTELLIGENCE (AI) [ AKILI BANDIA ]

Akili Bandia (AI) hii ni Teknolojia inayozipatia mashine uwezo wa akili ya kibinadamu ili kuweza kufikiria na kutenda matendo kama kibinadamu.

Je, hizi AI zikoje na zianatumika wapi?

THREAD [ UZI ] 👇

#ElimikaWikiendi Watu wengi wakiona neno AI ( Artificial Intelligence) hufikiria moja kwa moja ni roboti. Ili iwe AI inahitaji Software(Program endeshi) na Hardware. Software ndio kama ubongo unahitaji kupachikwa data ambazo zitakuwa zinatoka command/maelekezo kwenye hardware.

#ElimikaWikiendi
Aug 7, 2021 • 25 tweets • 11 min read
BITCOIN, BLOCKCHAIN AND CRYPTOCURRENCIES

Turudi nyuma mwaka 2008, Bwana mmoja aitwaye Santoshi Nakamoto mtaalamu wa Computer na Hesabu alitengeneza Program na kuiita jina la BITCOIN

Je, Bitcoins ni nini na zinafanyaje kazi ?

Twende na uzi 👇

#ElimikaWikiendi Bitcoin ni toleo la pesa taslimu ya ki-mtandao ( peer-to-peer version of electronic cash ) ambayo unaweza kutuma moja kwa moja kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine pasipo kupitia taasisi za fedha kama benki, Mobile money etc, unahitaji kuwa na internet tu

#ElimikaWikiendi
Aug 1, 2021 • 11 tweets • 4 min read
VITU VYA KUZINGATIA KABLA YA KUNUNUA MacBook

Je! Unampango wa kununua MacBook mpya? Kabla ya kufanya ununuzi unahitaji kuielewa MacBook.

Aina nyingi za MacBook zinapatikana sokoni. Tutakusaidia kununua MacBook bora kulingana na mahitaji yako

Uzi mfupi 👇 Kabla ya kufanya ununuzi wowote angalia toleo la MacBook ambalo utaenda kununua. Kila Mwaka Apple hutoa toleo jipya la MacBook, unaweza kutembelea Apple’s official website, news, na social media kujua mda ambao Apple watatoa toleo Jipya
Jul 31, 2021 • 5 tweets • 2 min read
Tesla Motors ni moja ya kampuni zenye ubunifu zaidi katika magari. Elon Musk, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo kwa sasa ni mmoja wa watu wenye ushawishi mkubwa ulimwenguni. Hivi karibuni, C.E.O wa Tesla na SpaceX alisema kwamba alijaribu kuuza kampuni yake ya gari kwa Apple 👇 Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Apple, Tim Cook aliripotiwa kukataa kupanga mkutano kujadili ofa hiyo. Hiyo ilibainika baada ya Musk Ku-tweet kwenye Page yake juzi alipoulizwa na Mwandishi wa BBC Kuhusu Habari iliyovuma kuwa alitaka kuwa CEO wa Apple mwaka 2016
Jul 24, 2021 • 25 tweets • 12 min read
NAMNA YA KUTENGENEZA PESA MTANDAONI

Kutoka michezo ya Betting mpaka uuzaji wa nguo katika mitandao. Kuna namna nyingi sana za kutengeneza pesa mtandaoni, nyingine zina ahadi ya kukupa utajiri mkubwa ndani ya muda mfupi., lakini je, ni kweli zinafanya kazi? 👇

#ElimikaWikiendi Jibu: Sio siku zote.
Je, Utatengeneza pesa ukifata njia hizo?
Jibu: Labda, maana ni kitu kimekaa kimtego sana. Inawezekana kabisa kwamba ile kazi yako inayokupa mshahara kila mwisho wa mwezi ikakupa pesa zaidi ya hizi njia za mitandaoni au kinyume chake

#ElimikaWikiendi
Jul 10, 2021 • 18 tweets • 12 min read
UZI:

RADAR NA MATUMIZI YAKE

RADAR
Radar ni kifupisho cha (Radio Detection and Ranging)
Ni mfumo ambao unatuma signal/ishara kwenye kitu (object) na kuchambuliwa kisha kurudisha majibu ya hicho kifaa kwa mfumo huo wa signal kupitia hewa 👇

#ElimikaWikiendi Ili kugundua uwepo, mwelekeo, umbali, na kasi ya ndege, meli, na vitu vingine

Signal ni mawimbi (radio waves) ambayo hutumwa kwa kifaa kilicho kwenye coverage ya Radar/eneo Radar inapofika na kukichambua hicho kifaa na kurudisha majibu kwenye chanzo/muongozaji

#ElimikaWikiendi
Jun 22, 2021 • 19 tweets • 7 min read
DARASA LA CRYPTO:
SEASON 1: UZI/THREAD

MEME COINS/SHITCONS

Meme Coins au Shitcoins unaweza kuziita coins za majitaka au futuhi coins

Ni coins ambazo zimekua zikipendwa sana na watu wa Crypto kwa kuwa zinaweza kukupa faida hata mara 1000 ya mtaji wako kwa muda mfupi. 👇 Meme coins zimeundwa bila kuwa na matumizi yoyote muhimu kasoro kiki inayotokana na Jina la hiyo coin.

Katika msimu huu wa Crypto, shitcoins zimekua zikipatikana sana katika Blockchain inayoitwa Binance Smart Chain (BSC) kupitia website inayoitwa Pancakeswap
Jan 1, 2021 • 13 tweets • 5 min read
APPLE

Mwaka 2021 unatabiriwa kuwa na mapinduzi ya Tekinolojia, Apple wao wamejipanga kufanya yafuatayo

UZI

◾️Apple silicon iMac

Apple wanakuja na iMac ambayo itakuwa na Apple silicon chip, kama walivyofanya kwenye MacBook, itakuwa na16 high-power cores& 4 efficiency cores ImageImage ◾️AirPods

2021 Apple wanategemea kutoa third-generation AirPods ambayo itakuwa na replaceable silicone air tips, pia wataboresha wireless chip na battery life Image
Dec 19, 2020 • 25 tweets • 10 min read
UZI

SOCIAL ENGINEERING
[ utumiaji wa madhaifu ya Mwanadamu kufanya wizi]

◾️Social engineering huchukua faida ya kitu dhaifu kabisa katika ulinzi wa taarifa za kila aina ya taasisi ambacho ni MTU

Social engineering ni "PEOPLE HACKING" na inahusisha 👇

#ElimikaWikiendi Image Madhaifu ambayo binadamu tunayajenga sisi kwa sisi na kuweza kuyatumia hayo madhaifu kupata taarifa ambazo hutumika kwa faida binafsi

◾️Social engineering ni moja ya wizi mgumu kufanyika, kwa Dunia ya sasa imekuwa ni vigumu sana mtu kumwamini mtu mgeni kwake

#ElimikaWikiendi Image
Oct 27, 2020 • 7 tweets • 4 min read
TWITTER FOR VPN

◾️kumekuwa na sintofahamu baina yetu na kulazimika kutumia VPN ili kuweza kupata access ya twitter

◾️Hii inasababishwa na kitu kinaitwa OUTAGE kwa jina jingine ni DOWNTIME

◾️Twende na uzi uelewe inatokeaje na kwa nini unatumia VPN/TOR/PROXIES

Uzi mfupi ◾️Outage kwa jina jingine ni Downtime ambapo ni ukosefu wa huduma flani au network, Hii inakuwa imegawanyika kwa namna mbili

👉 Unplanned outage
👉 Planned outage

◾️Unplanned outage ni ukosefu wa huduma flani au network nzima kutokana na mambo kadhaa kama vile
Oct 24, 2020 • 18 tweets • 7 min read
iPhone 12 Pro Max VS Samsung Note 20 Ultra

◾️Hizi ni simu zinazotamba kwa sasa Duniani ikiwa ni matoleo mapya kwa Samsung na Apple

◾️Nakuletea ulinganifi wa hizi simu, hii ni kulingana na majarida mengi kama AndroidAuthority, CNet, GSMArena, Gadget360 n.k

Twende na uzi👇 Image ◾️Samsung Galaxy Note 20 Ultra ilitoka Aug 5 na iPhone 12 Pro Max ilitoka Oct 13 lakini hii bado ni Pre-order

◾️Kila kampuni inasifia simu yake kuwa ni bora zaidi Duniani kwa sasa kutokana na teknologia ya hali ya juu iliyotumika kwenye hizo simu

◾️Tuzichambue taratibu ImageImage
Sep 19, 2020 • 25 tweets • 9 min read
ENCRYPTION

Najua unasikia sana neno "Encryption" lakini kuna mengi ya kujifunza ili uelewe zaidi kuhusu encryption

◾️Encryption ni nini na aina zake ni zipi ?

◾️Encryption salama na zisizo salama

◾️Matumizi ya Encryption

◾️Faida za kufanya Encryption

Cc: @Kimkayndo ◾️ Encryption ni kitendo cha kubadili maneno au jumbe za kawaida kutoka kwenye mfumo unaosomeka kwenda kwenye mfumo ambao hausomeki, ambapo huzalisha kitu kinaitwa "cipher text"

Mfano kipindi cha utoto, watoto huongea kwa kuchanganya maneno ili watu wazima wasielewe wanaongea
Sep 15, 2020 • 14 tweets • 6 min read
ANDROID 11

Android 11 imetoka, ni jambo zuri kwa watumiaji wa Android, simu za mwanzo Kabisa zilizoanza kupokea Android 11 updates ni Google pixels, OnePlus, Oppo, Xiaomi na Nokia. Simu zingine zitapata Android updates week chache zijazo

Tuangalie features zilizomo [ uzi ]👇 ◾️ MEDIA CONTROL

Media players zitakuwa zinaonyesha media controls zote ( prev, stop, next etc) moja kwa moja kutoka kwenye "toggle bar" ( Sehemu ya juu ya simu kwenye notification pannel ambapo itaonyesha wimbo, media husika na control zake)
Aug 23, 2020 • 25 tweets • 10 min read
ELON MUSK

Alizaliwa South Africa akiwa na miaka 17 alihamia Canada na baadae America, ni mfanyabiashara na mwanzilishi wa makampumi makubwa kama SpaceX, PayPal, Tesla Motors

Leo nimekuletea kila kitu kuhusu Elon Musk

✴️ Historia yake na familia yake

✴️ Biashara zake

Uzi Image ELON MUSK NI NANI

Ni mzaliwa wa South Africa lakini sasa ana uraia wa Marekani na Canada, ni mfanyabiashara na mwanzilishi wa makampumi ya PayPal, SpaceX na Tesla Motors, alipata pesa akiwa na umri mdogo (20's) baada ya kuuza kampuni yake ya kwanza (Zip2) kwa Compaq computers Image
Jun 28, 2020 • 15 tweets • 8 min read
JINSI YA KUIFANYA SIMU YAKO IWE NA NAFASI ( SPACE) YA KUTOSHA

Kwa watumiaji wa Android devices nimepata maswali mengi, simu zinajaa pasipo kuwa na vitu vingi kwenye simu

Leo tuangalie namna gani unaweza kuifanya simu yako iwe na nafasi ya kutosha

Twende na uzi Wewe ni mtumiaji wa Android phone na umekuwa ukipata shida kwenye suala la storage, unaona kama una vitu vichache lakini storage imejaa

Basi jifunze vitu hivi ambavyo vimesaidia wengi katika kuifanya simu kuwa safi katika suala la storage
Jun 10, 2020 • 11 tweets • 5 min read
Je umewahi kujiuliza haya maswali ?

✴️ Taarifa na vitu vyote kwenye mtandao huwa vinatunzwa wapi?

✴️ Serikali na makampuni binafsi yanatunza wapi taarifa zao?

Jibu: Taarifa na vitu vyote vya kimtandao duniani vinatunzwa sehemu inaitwa DATA CENTER

DATA CENTER NI NINI?

Uzi DATA CENTER ni nini na inafanyaje kazi?

Data center ni sehemu maalumu ambapo vifaa vya computer na mawasiliano vimewekwa kwa ajili ya kukusanya, kutunza, kuchakata (processing) na kusambaza (distribute) taarifa zote za kimtandao Duniani
Apr 27, 2020 • 11 tweets • 4 min read
Zijue sheria za uhalifu wa mitandao (cyber crimes) na adhabu zake nchini Tanzania

Leo tuangazie sheria mbalimbali za uhalifu wa mitandao na adhabu zake kwa mtu anayekwenda kinyume

Hizi ni Sheria zilizopitishwa mwaka 2015 na Raisi mstaafu Mh J.M Kikwete

Uzi 👇 Act No. 14 ya 2015
Hizi sheria zinatumika Tanzania bara na visiwani

1. Illegal access (upatikanaji wa taarifa kinyume na sheria)

Mtu hapaswi kwa makusudi kuingilia taarifa au kufanya mifumo ya computer kupatikana (accessed) ili kupata taarifa bila kufuata sheria