Habibu B. Anga Profile picture
Author
Henry Profile picture Hangi πŸ“Ώ Profile picture Mjukuu Profile picture peter August Profile picture Micky leony Profile picture 6 subscribed
Mar 25, 2023 β€’ 24 tweets β€’ 6 min read
Ukitaka kuelewa chanzo cha vita ya Ukraine basi unapaswa kufahamu mkasa wa huyu unaye muona pichani na Zitto… anaitwa Victor Yushchenko

Miaka kadhaa iliyopita huyu somo alikumbwa na kadhia ya kulishwa sumu na kupata madhara kama yale ambayo yalimkuta Dr. Mwakyembe..

Thread.. enzi zile za Richmond na Dowans mpaka akapelekwa India kutibiwa.
Ngozi ya mwili yote iliharibika na kuanza kupukutika kama unga

Huyu Yuschenko yeye kadhia hii ilimtokea mwaka 2004 kipindi hicho akiwa anagombea Urais wa Ukraine
Yushchenko alikuwa anachuana mwanasiasa Yanukovych..
Aug 18, 2022 β€’ 23 tweets β€’ 5 min read
Roman Abramovich: Utajiri wa Damu Mpaka Kumuingiza Ikulu Putin

Thread,

Namna ambavyo mtoto yatima aliyelelewa katka umaskini ameweza kuibuka moja ya binadamu wenye ukwasi mkubwa duniani na mpaka kuweza kumuingiza Ikulu Vladmir Putin ni mkasa wa aina yake…

(Usisahu ku-Retweet) Image Wazazi wake wote wawili licha ya kuishi maisha yao yote nchini Russian lakini asili yao ni Waisrael. Mama yake aliitwa Irina na alifariki kipindi Roman bado angali mchanga kabisa wakati baba yake ambaye aliitwa Arkady alifariki kwa ajali ya gari miaka michache baadae Roman akiwa
Dec 21, 2021 β€’ 43 tweets β€’ 11 min read
TUMEWAHI KUWA NA CHANJO KWA MALENGO YA KISHUSHUSHU

Thread..

Kadiri ulimwengu unavyobadilika, stadi ya Ujasusi inazidi kuwa complex kwa kuhusisha mbinu ambazo nyingine ukizisikia unaweza kudhani labda watazama sinema au waota, lakini ndio uhalisia wa ulimwengu ulipo sasa katika katika juhudi za mataifa na makampuni makubwa kupanua ushawishi wao juu ya dunia yote na kulinda maslahi.

Kuna kisa cha tofauti sana ningependa nikijadili leo hii. Kisa cha tofauti kabisa..

Wengi tutakuwa tumewahi kusikia shirika linaloitwa β€œSave the Children”. Ni moja ya…
Oct 14, 2021 β€’ 98 tweets β€’ 25 min read
π—•π—œπ—‘π—§π—œ π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π— π—œπ—”π—žπ—” 25 π—”π—‘π—”π—¬π—˜π—œπ—§π—œπ—žπ—œπ—¦π—” 𝗔𝗙π—₯π—œπ—žπ—” 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗔π—₯π—œπ—žπ—œ

Thread..

Siku ya 30 May 2019, maafisa Usalama Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JKIA, Nairobi walimuweka kizuizini abiria mmoja mwenye hati ya kusafiria ya kidiplomasia, mwanaume.. Image wa asili ya kisomali. Japokuwa watu wenye diplomatic passport wapata exemptions kadhaa kwenye kaguzi za uwanja wa ndege, lakini ilikuwa ni lazima kwa maafisa hawa kumuhoji abiria huyu kutokana na utata wa mzigo ambao alikuwa nao.

Huyu somo alikuwa na briefcase ambalo ndani yake
Sep 4, 2021 β€’ 41 tweets β€’ 10 min read
π—žπ—”π—•π—Ÿπ—” 𝗬𝗔 π—œπ—žπ—¨π—Ÿπ—¨.. π—žπ—ͺ𝗔𝗑𝗭𝗔 𝗔𝗗𝗛𝗔𝗕𝗨 𝗬𝗔 π—žπ—œπ—™π—’

Thread..

Ukiwa unatoka Lusaka kwenda Jimbo la Magharibi, kabla hujaingia mji wa Mongu kuna kipande cha barabara kinajulikana kama Limulunga Road.
Kipande hiki cha barabara mwaka juzi kimetupa tukio la kipekee Image ambalo kwa kiwango kikubwa tukio hili limebadili mwelekeo wa siasa la bara zima la Afrika na hasa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara.

Pengine pasipo tukio hili huyu Hichilema tunayemuona leo asingelikuwa Rais. Lilikuwa tukio la kipekee kabisa..

Kila mwaka pale Zambia huwa wana
Aug 10, 2021 β€’ 25 tweets β€’ 6 min read
π—¨π—§π—”π—π—œπ—₯π—œ π—ͺ𝗔 π— π—”π—¦π—›π—”π—žπ—” π—ͺ𝗔 π—ͺπ—”π—Ÿπ—œπ—‘π—­π—œ π—ͺ𝗔 π—©π—œπ—’π—‘π—šπ—’π—­π—œ

Thread..

Mwaka juzi kwenye hafla ya mapokezi ya ndege kwenye nchi fulani hivi hapa Afrika Mashariki kuna incident ndogo tu ilitokea lakini wengi ikatufikirisha sana.

Dakika chache baada ya Rais wa... nchi hiyo kumaliza kuongoza hafla hiyo ya mapokezi ya ndege akashuka jukwaani na akianza kuandoka.
Lakini kabla hajakwenda kupanda gari, kama ambavyo ilikuwa ada kwa Rais yule akaelekea upande waliokaa wananchi wake na ili awasalimie.
Na kusalimia huku akaanza jukwaa ambalo...
Jul 20, 2021 β€’ 25 tweets β€’ 7 min read
UZI
πŸ‘‡πŸ‘‡

Tujadili kidogo Executive Protection.
Hapa chini nimeweka picha za inner cycle za ulinzi wa Rais JPM, Samia, Ndayishimiye (Burundi) na Mnangagwa (Zim).

Kwa kila Rais utaona 'First Ring' zao (hao walinzi wanaomzunguka Rais muda wote) lazima kuna afisa mmoja au wawili.. amebeba begi la mkononi

Umewahi kujiuliza hilo begi lina dhumuni gani.?

Hiyo picha hapo juu, JPM alikuwa chato na hapo alikuwa anakwenda kwenye kibanda cha simu kusajili line yake kwa alama ya vidole
Kwa hiyo hakuwa kwenye ziara au anakwenda kikaoni.. sasa hilo begi ni la nini?
Jul 17, 2021 β€’ 25 tweets β€’ 5 min read
π—‘π—”π—‘π—œ π—”π—Ÿπ—œπ— π—§π—˜π—žπ—” 𝗠𝗧𝗒𝗧𝗒 π—ͺ𝗔 π—₯π—”π—œπ—¦, π— π—”π—­π—œπ— π—•π—¨, 𝗠𝗒π—₯π—’π—šπ—’π—₯𝗒.?

FINALE

Naam, niwamalizie sasa hiki kisa. Kama haujasoma sehemu ya kwanza, angalia kwenye profile yangu juu kabisa pinned tweet.

Sasa,

Wale wakimbizi waliorejea SA, tokea hapa Morogoro... wakaeleza namna ambavyo waliishi kambini Mazimbu na kijana anayeitwa Louis Mathakoe ambaye sasa hivi wanaonyeshwa picha kwamba identity halisi kijana huyo ni mtoto wa Rais Mbeki.

Wajumbe wa Tume ya TRC walivyo endelea kuhoji kuhusu nyendo za kijana Kwanda akiwa hapo Mazimbu..
Jul 16, 2021 β€’ 25 tweets β€’ 5 min read
π—‘π—”π—‘π—œ π—”π—Ÿπ—œπ— π—§π—˜π—žπ—” 𝗠𝗧𝗒𝗧𝗒 π—ͺ𝗔 π—₯π—”π—œπ—¦, π— π—”π—­π—œπ— π—•π—¨, 𝗠𝗒π—₯π—’π—šπ—’π—₯𝗒.?

Kuna masuala huwa yanakuwa salama yakiachwa bila kuzungumzwa. Sababu ukianza kuhoji kuhusu ukweli na undani wake, unajikuta unafungua mlango wa hatari ambazo pengine hauko tayari kuzikabili... Mojawapo ya masuala haya ni madhira ambayo yanafanywa na watu tuliowapa madaraka. Nyendo zao, na siri zao ni kana kwamba haupaswi kutamani kuzifahamu.

Lakini binadamu tumeumbwa na kiu ya kutaka kujua, na kiu hii ni kama upele, hauachi kuwasha mpaka uukune
Na pia historia ya nchi
Jul 15, 2021 β€’ 19 tweets β€’ 4 min read
π— π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—” #1: π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—žπ—’π——π—œ, π—¨π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—•π—œπ—”π—¦π—›π—”π—₯𝗔

#7

Majukumu wakuu, mniwie radhi.

Tuendelee,

Mara ya mwisho nilisema, kuna Mtanzania ambaye mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu alidai kwamba alinyang'anywa passport na Idara ya Intelijensia Image na kisha kupewa Hati ya Kusafiria ya nchi ya Afrika Kusini

Nikaeleza kwamba mtu huyu ambaye alikwenda Afrika Kusini kutafuta maisha mwanzoni mwa miaka ya tisini, mojawapo ya harakati zake kubwa za kwanza ni pale alipomshawishi Nelson Mandela na taasisi yake ya Mandela Foundation
May 25, 2021 β€’ 9 tweets β€’ 2 min read
πŒπ“π€ππ™π€ππˆπ€ #1: π‰π€π’π”π’πˆ 𝐖𝐀 πŠπ”πŠπŽπƒπˆ, π”π‰π€π’π”π’πˆ 𝐖𝐀 ππˆπ€π’π‡π€π‘π€

#6

Nikasema kwamba kwenye ule mchoro wa Motto Mabanga aliowapa vigogo wetu. Sehemu ya mchoro huu ilikuwa ni kuchukua mkopo wa karibia shilingi bilioni 60 toka taasisi ya African Global.. Image Capital.

Hapa tafadhali soma kwa makini sana,

Yule Walter Hennig niliyewaeleza jana mwenye kuandaa sherehe za mwaka mpya pale Clifton, Cape Town.. huyu bwana ni CEO wa kampuni inaitwa African Management Limited.

Sasa hawa African Management Limited ndio wanaomiliki taasisi ya
May 24, 2021 β€’ 22 tweets β€’ 5 min read
πŒπ“π€ππ™π€ππˆπ€ #1: π‰π€π’π”π’πˆ 𝐖𝐀 πŠπ”πŠπŽπƒπˆ, π”π‰π€π’π”π’πˆ 𝐖𝐀 ππˆπ€π’π‡π€π‘π€

#5

Mara ya mwisho nikaeleza namna ambavyo Motto Mabanga aliwakutanisha Mwanasiasa wa South Africa, Tokyo Sexwale na mtaalamu wa jiolojia Dr. Alan Stein na Swahiba wake Jonathan Taylor.. Image na hatimaye kuunda kampuni ya Ophir Energy Plc.

Nikaeleza kwamba Motto Mabanga alipewa kamisheni ya 5% ya umiliki wa kila kitalu ambacho atafanikiwa kuwapatia Ophit Energy kwa mkataba mnono.

Na Motto Mabanga alipoingia kazini, target yake ya kwanza ya vitalu ilikuwa ni Tanzania
May 10, 2021 β€’ 23 tweets β€’ 5 min read
π— π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—” #1: π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—žπ—’π——π—œ, π—¨π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—•π—œπ—”π—¦π—›π—”π—₯𝗔

#4

Mara ya mwisho nikasema kwamba minada yetu yote ya vitalu vya mafuta ilidoda. 1st, 2nd na 4th Round.
Mwaka 2005 pekee kwenye 3rd Round kutokana na uhusika wa Motto Mabanga ndipo mnada Image Ule mpaka leo umeweka rekodi ya vitalu vyote 7 kuchukulia na PSA Agreement kusainia kati ya serikali na wawekezaji.

Sasa ni namna gani ambavyo Motto Mabanga alisuka mipango kufanya mnada wetu uchangamke, ndipo hapo sasa nikaanza kueleza.

Kwanza kwa kifupi sana niseme kwa nini..
May 1, 2021 β€’ 26 tweets β€’ 5 min read
π— π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—” #1: π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—žπ—’π——π—œ, π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—•π—œπ—”π—¦π—›π—”π—₯𝗔

PART 3

Wakuu, mnisamehe bure, majukumu yalibana mno. Niko na muda wa kutosha sasa.
Nitaweka Parts kadhaa mfululizo kuwafidia uraibu niliowaachia muda wote huu.

Tuendelee

Mara ya mwisho Image Nilieleza kuhusu mgogoro ambao ulitokea pale Vodacom Congo.
Ambapo Vodacom Group walikuwa wameingia ubia na kampuni ya Congolese Wireless Network kuunda kampuni ya Vodacom Congo ambapo kwenye ubia huo Vodacom Group walikuwa na 51% ya umiliki huku CWN wakiwa na 49%.

Lakini baada,
Apr 11, 2021 β€’ 25 tweets β€’ 5 min read
MTANZANIA #1: JASUSI WA KUKODI, UJASUSI WA BIASHARA

Thread..

Si rahisi kuwa mahususi sana ni mwaka gani, lakini tunakadiria kwamba katikati ya miaka ya tisini hivi Mtanzania ambaye kwa sasa nimtaje kwa jina lake moja tu la Matiko aliondoka jiji Dar kwenda nchini Afrika Kusini Image Kwa ajili ya kutafuta maisha. Lakini tofauti na Watanzania wengi wanaozamia SA ambako wakifika uanza kwa kufanya shughuli za hali ya chini, ilikuwa tofauti kabisa na bwana Matiko ambaye aliingia SA akiwa na mtaji wa kuridhisha kutokana na fedha ambazo alizipata toka kwenye mauzo
Apr 5, 2021 β€’ 18 tweets β€’ 4 min read
Kuna uzi niliandika hapa Mwezi March kuhusu dhana nzima ya Ulinzi wa viongozi wa juu.
Nikasisitiza sana kwamba sula la ulinzi wao sio tu kulinda wasidhuriwe kimwili bali pia kulinda hadhi zao, heshima zao na siri zao.

Kitimbwi ambacho kimetokea leo cha Rais wa nchi

ThreadπŸ‘‡πŸ‘‡ Image Kuteua na kufukuza Mkurugenzi wa TPDC ndani ya masaa machache kabisa... ni failure kubwa ya kitengo cha intelijensia ya nchi ambao wana jukumu la kulinda hadhi na heshima ya Rais.
Mtu yule aliyeteuliwa huku akionekana kwamba hana sifa kabisa ya kushika wadhifa ule, ina reflect..
Apr 2, 2021 β€’ 5 tweets β€’ 1 min read
Mkuu @abuu_adam anauliza nini ilikuwa hatma ya yule "Mtanzania" Al-Asad aliyekuwa anashikiliwa kwenye black site ya CIA hapo Djibouti?

Jibu: CIA baada ya kumaliza kumuhoji na Asad kutoa siri zote anazozijua, wakataka kumrudisha hapa nchini, lakini tukamkataa kwa sababu hakuwa.. raia halali wa nchi hii bali alikuwa akiishi hapa kwa nyaraka za kugushi.

Kwa hiyo CIA wakamdeport al-Asad kwenda nchini Yemen.

Huko vyombo vya usalama wakamshikilia kwa miezi michache na kisha kumuachia huru mwaka 2005.

Baada ya kuachiwa huru al-Asad alitumia muda wake wote..
Apr 2, 2021 β€’ 11 tweets β€’ 3 min read
"ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA"

Nyongeza...

Mwanzoni mwa makala kabisa nilieleza kuhusu wale vijana watatu ambao walikuwa wanasafiri toka Afgooye kwa gari kuelekea Mogadishu na njiani wakakutana na check point ya jeshi na baadae kumiminiwa risasi.

Nikasema kijana mmoja Image Fouad (yule msomali aliyekaa siti ya nyuma) kwa mujibu wa CIA wanasema kwamba alifanikiwa "kutoroka" akiwa hai.

Sasa,

Kuna vitu viwili hapo nivieleza kwa haraka haraka.

Jambo la Kwanza; kama ambavyo ilikuwa kule Kenya ambavyo waliunda Renditions Operations Team ndivyo hivyo...
Apr 2, 2021 β€’ 25 tweets β€’ 6 min read
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 5 (HITIMISHO)

Nikiwa nahitimisha ni vyema kusisitiza kwamba, kikosi hiki cha makomando wa Kenya ambacho kinaendeshwa kwa amri ya CIA na NIS (Idara ya Ujasusi Kenya) kwa sasa kimegawanywa kwenye vitengo viwili.. Image Kitengo cha kwanza ndio ile Rendition Operations Team; hawa wanahusika sana kama target anatakiwa kukamatwa akiwa hai

Alafu siku hizi kuna RRT (Rapid Response Team) hawa wanatumika zaidi kama target anatakiwa kuwaneutralized (kuuwawa) au kuhusika kuokoa mateka kama watekaji wana
Apr 1, 2021 β€’ 16 tweets β€’ 4 min read
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 4

Ile taarifa ambayo Asad aliwapatia ilikuwa ya maana sana kwa CIA.

Mpaka muda huu ambapo Asad alikuwa anahojiwa (kumbuka hiyo ni mwaka Oct 2003) huyo "bwana somba" Odeh tayari alikuwa ameshakamatwa Image na yuko gerezani Guatanamo Bay (alikamatwa tangu mwaka 1998).

Taarifa hii ya Asad iliwapa CIA kitu kimoja muhimu sana.. walithibitisha intelijensia yao kuhusu shirika la al-Haramain kutumiwa na al-Qaida kusambaza fedha ulimwenguni kwa watu wao.
Ushahidi huu ulitumiwa na Marekani
Apr 1, 2021 β€’ 26 tweets β€’ 5 min read
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 3

Mara ya mwisho nikasema kwamba, maafisa wawili wa CIA walifika kwenye jela ya siri ya shirika hilo la Ujasusi iliyopo ndani ya kambi ya Kijeshi ya Camp Lemonnier nchini Djibouti ambako "Mtanzania" al-Asad.. Image alikuwa anashikiliwa.

Maafisa hawa wa CIA swali pekee ambalo walikuwa wanamuhoji Asad ni kuhusu shughuli zake ndani ya shirika la Kiislamu la al-Haramain ambalo yeye alikuwa kama muhasibu hapa Tanzania

Kwa muda wa siku tatu nzima, Asad alikuwa akihojiwa kwa mtindo ambao wenyewe