WatuNiStory Profile picture
By @djtee255 #ShujaazTZ / Simulizi halisi za vijana kuhusu kazi, maisha, ndoto, msukumo, nguvu na udhaifu kuhusu maisha yao. #WatuNiStory #Shujaaz #Hatukuchori
Mar 26, 2022 5 tweets 2 min read
"Harakati za shule na kusoma nikajikuta nimepangiwa shule moja huko Mtwara inaitwa Ndanda.

Kiukweli nilikuwa sijawahi kufika na sijui kabisa tamaduni za watu wa kule. Nikasema Tanzania ni moja hakuna sehemu nitashindwa kuishi, hivyo mwanaume nikajipanga tayari kwenda kuanza safari ya masomo huko.

Kumbuka ile likizo ya kusubiri matokeo ya kwenda kidato cha tano, nilikuwa mtu shamba. Yaani nilipiga sana jembe na kazi nzito kusaidia mishe za home. Hivyo nilikuwa nakula saaana.
Mar 8, 2022 4 tweets 1 min read
"Ipo hivi, mimi ni kijana wa miaka 25, nilikuwa na mpenzi wangu ana mtoto sio wangu. Kipindi nipo nae nilikuwa sina kazi na tulikuwa tumepanga tunaishi pamoja lakini yeye alikuwa na kazi. Sasa hakutaka kubeba mimba yangu akihofia hali ngumu ya maisha ambayo ninapitia. Kile kitendo kikaniumiza sana, nikaja Dar kutafuta maisha, ikawa kila baada ya miezi mitatu narudi nyumbani kumtembelea.

Sasa mwezi wa tisa nikashindwa kwenda kwa wakati, lakini tulikubaliana kwakuwa mkataba ulikuwa karibu kuisha, nimalizie mkataba ndio niende nyumbani.
Mar 7, 2022 10 tweets 2 min read
"Ilikuwa Jumapili weekend moja nimekaa ghetto kwangu nimefulia mbaya. Simu yangu inaita, kucheck alikuwa mwanangu.

Kupokea ananiambia ana msala inabidi nimsaidie kuu-solve. Inakuaje? nikauliza. Image Ndio ananiambia amempa mimba binti wa kidato cha nne hivyo anaomba aje kwangu kufanya harakati za kuitoa. Ashaongea na dokta, na dogo yupo tayari bado eneo la tukio tu sababu hawawezi kufanyia hospital.

Daah!nikicheck ni mwanangu sana. Na kwao ana mke na mtoto.
Mar 5, 2022 7 tweets 2 min read
"Ipo hivi mimi ni kijana wa miaka 28 sasa.

Nilipokua chuo mwaka 2018 nikisomea course ya IT nilibahatika kupata mdada ambaye niliishi nae kama mchumba na kumpa mahitaji yote na tulikubaliana tuzae. Image Basi nikampa kweli ujauzito huku nikimhudumia kwa kila kitu bila wazazi wangu kujua na hakuwahi kukosa kitu alichohitaji kwangu japo sikuwahi kuomba msaada kwa mtu, ila niliendeleza life langu kwa mishe zangu za kitaani(kwa wanaoelewa IT huwa hatukosi mishe za hapa na pale).
Dec 29, 2021 10 tweets 2 min read
"Kuna demu mmoja nina urafiki nae kiasi kwamba binafsi nikiwa na shida yoyote ananisaidia. Mara nyingi huwa anakuja home hata nguo zangu huwa anafua na usafi anafanya. Chochote nitakachomwambia anafanya. Alishaniweka wazi kuwa ana ngoma na mambo yake yote huwa hanifichi hata awe na mahusiano basi ataniweka wazi kwa kila kitu hata akalale na huyo mwanaume.

Tatizo linakuja sehemu moja, hatujawahi kuongelea swala la kuwa na mahusiano. Mimi na yeye huwa ni stori za kawaida tu.
Dec 28, 2021 9 tweets 2 min read
"Miaka kadhaa iliyopita Vijana mtaani kwetu waligundua kuwa Kuna mama huwa anaacha wazi madirisha ya nyumba yake pindi akiwa anabadilisha nguo. Ni mama mgeni ambae alikua kahamia miezi michache tu iliyopita. Alikua akifanya hivyo kila siku mida ya saa moja na nusu usiku akitoka kuoga.

Yule mama MashaAllah alijaliwa shape. Yani alikua na shape moja ya ukorofi sana. Alienda hewani.. huko nyuma ni kama pembe la ng'ombe tuu.. halifichiki.. hatari sana.
Oct 30, 2021 9 tweets 2 min read
"Tangu naanza Shule Ya Msingi, O level na A level Mungu alinijalia Uwezo Mkubwa Darasani. Nikafanikiwa kumaliza kidato cha Sita Vizuri na kuweza kuchaguliwa kujiunga na Chuo kikuu Cha Afya Muhimbili. Ndipo nilipo anza kuonja joto la kufeli masomo semester ya kwanza nikakamatwa kwenye moja ya somo gumu (Anatomy), second semester Nikapita vizuri, nikarudi October kuja kusapua.

Kutoka na maandalizi duni nikafeli tena nika carry.
Oct 29, 2021 10 tweets 2 min read
"Katika harakati za kutafuta maisha,wanaume huwa tunapitia mambo mengi kweli. Mengine yanabaki mioyoni na kuwa siri zetu.

Nakumbuka baada ya kukosa mishe na harakati za kuingiza hela, nilijikuta naingia kwenye kuuza bangi. Naweza kusema tabia yangu ilisanifu kazi yangu. Maana nilikuwa mbabe sana na mtu mwenye matukio mengi sana mtaani.

Ilikuwa ni ngumu sana kwangu kupitisha wiki na sijafanya tukio lolote la kibabe au kuogopwa. Hayo ndio yalikuwa maisha yangu.
Oct 27, 2021 6 tweets 2 min read
"Kuna story ambayo baba yangu Mzazi (Mzee Eugeni) alinisimulia kuwa kipindi cha nyuma akiwa kijana alikuwa anaishi mwanza kufanya kazi ndogo ndogo katika harakati zake alioa Mwanamke ambaye anaitwa Maria na alipata naye watoto wawili. Image Mtoto wa kwanza wa kike alikuwa anaitwa Agnes (Eugeni)alizaliwa 1979 na mtoto wa Pili alikuwa anaitwa Ana(Eugeni) alizaliwa 1983.

Mwaka 1984 baba alisafiri kusalimia Nyumbani kwake alipozaliwa ambapo ni Kilimanjaro.
Sep 24, 2021 4 tweets 1 min read
"Nimetokea kwenye familia maskini sana na kibaya zaidi ilidharaulika sana, tena kwa pande zote mbili yaani upande wa baba na mama.

Nimekuwa huku kauli za kejeri zinasikika na kuishi masikioni mwangu. Hilo kwangu ndio lilikuwa tatizo kubwa. Niliwachukia sana jamaa zangu mpaka nimekua mkubwa sikuwahi kuomba msaada wa aina yoyote kwao.

Hadi wazazi wangu niliwahi kuwakataza, niliwaambia shida zote na huduma wanibebeshe mimi.
Sep 23, 2021 5 tweets 1 min read
"Mwaka 2005 nilihitimu chuo cha ualimu Kabanga kilichopo mkoani Kigoma. Sikukaa muda mrefu mtaani, mwaka 2006 nilifanikiwa kupata ajira wilayani Moshi.

Nilifundisha pale miaka mitatu nikakutana na jamaa mmoja tukawa marafiki. Kumbe alikuwa mganga wa kienyeji. Katika harakati zake, akanishawishi nikawa chawa wake. Siku zilivyoenda nikajikuta na mimi nimetamani kuwa mganga.
Sep 22, 2021 7 tweets 2 min read
"Mwaka 2016 nilipoteza kazi niliyokuwa nimeajiriwa kwa makosa ambayo sikuhusika, lakini upepelezi ulipokuja kufanyika nilionekana ni kama na mimi nilihusika kwenye huo wizi ingawa ukweli sikuhusika.

Sikujua chochote na wala sikula hata sh 100. Wanasema siku ya kusurubiwa kwako manabii wa uongo watakuja ili kukutolea ushahidi wa uongo lengo uangamie, ndio kilichonitokea mimi.
Sep 21, 2021 6 tweets 2 min read
"Tulikuwa kwenye mahusiano miaka saba. Katika uhusiano wetu nilibahatika kupata mimba yake.

Aliikataa kabisa sio mimba yake. Niliumia sana. Ikabidi nilee mimba mwenyewe, hadi najifungua sikujua alipo na sikuwahi kumuona. Image Mtoto alipokuwa na mwaka na nusu nilipost picha yake Facebook. Alimuona na akaanza kunifuatilia.

Badae alinitafuta akaja hadi nyumbani na kwa ndugu zangu, akaomba msamaha. Hatukuwa na hiyana nae, tulimsamehe.
Aug 18, 2021 7 tweets 2 min read
“Wakati naanza mwaka wa kwanza pale IFM nilimpa mimba mpenzi wangu. Nilikua naye toka mimi nikiwa Form 5. Bahati mbaya alifeli Form 4 akaishia hapo hapo.

Aliniambia mimba ni yangu na nilikubali nikaanza kuilea ile mimba. Japo tulisumbuana sana kwenye pesa za matumizi kwa sababu sikua na pesa za kutosha kila kitu kwa wakati huo.

Chuki kwangu ikazidi balaa. Sikuiweka moyoni niliamini ni mimba inamsumbua.

Alienda kwao kujifungua mkoa mwingine. Na akajifungua mtoto wa kiume. Baada ya siku tatu akaniambia mtoto amefariki na baada ya hapo hakupokea simu
Aug 16, 2021 4 tweets 1 min read
“Nakumbuka nikiwa shule ya msingi maisha hayakua mazuri. Biashara ya mama yangu ya bagia ikawa ndio inaendesha maisha yetu. Mimi ndio mkubwa na ndiye mtoto wa kiume kwetu. Kwa kipindi hicho mdogo wangu wa kike alikua bado mdogo sana.

Ilinibidi nisaidiane na mama kuuza bagia. Image Nikitoka shule nakuta zimeshatayarishwa nabeba sufuria natembeza mpaka vijiji vya jirani. Nahakikisha zimeisha ndipo narudi nyumbani.

Utaratibu ulikua ni huo huo tangu darasa la tatu hadi form three. Nakumbuka wenzangu walikua wananicheka. Nilikosa marafiki.
Aug 10, 2021 5 tweets 1 min read
“Hii siri nitaitunza mpaka lini? Nibaki nayo au nijisalimishe?

Nilikuja Dar kutokea kijijini kupambania ugali. Mungu mwema mitikasi ilikubali. Kama unavyojua tena jiji la Dar wanawake warembo kila kona. Ni kama nilikua na ngekewa kila nilipotupa ndoano ilinasa. Nilijichanganya nilitembea na kila aina ya mwanamke niliyemtamani.

Katika haya mahangaiko nilikutana na dada mmoja wa Songea. Huyu dada alikuja kunieleza amepata mjamzito. Ila akawa ameenda kwao Songea. Nilikua nikituma matumizi ila ilifika mahali mawasiliano yalikufa. Sikumpata tena. Ni miaka
Aug 8, 2021 4 tweets 1 min read
"Wakati nakutana na mpenzi wangu ambaye kwa sasa ni mchumba wangu na tutaoana sio mda mrefu, nilimwambia kabisa mimi sina mapenzi ya maonyesho.

Sinaga habari za mitoko wala kupostiana kuandikiana caption za makopakopa. Wewe ukitaka kutoka, toka na rafiki zako. Wala sitajalii. Image Me nifanyie vitu vya kawaida tu kabsa nitafurahi sana.

Nina amini katika mahusiano ya siri na yenye staha. Kupostiana watu huleta chuki na maneno ambayo hayapo.
May 29, 2021 7 tweets 2 min read
Baada ya kumaliza shule nilimpata binti niliyeamini atakuwa wa maisha yangu alikuwa anaitwa Mwajuma, hapo ndio kwanza nilikuwa ninaanza kuingia katika ulimwengu wa mapenzi. Sikuwa ninaelewa kabisa kuhusu maana ya neno penzi, watu waliotabiri mwisho wangu na Mwajuma niliamini kuwa ni wanafiki na walikuwa na malengo mabaya dhidi yetu.
May 27, 2021 5 tweets 1 min read
"Tulifanya interview kutafuta mtu wa finance katika kampuni yetu. Tulipokea maombi mengi, watu tano ndio walifanikiwa kupigiwa simu na kuitwa kwa ajili ya usahili.

Wote walifika. Kila mtu alipangiwa muda wake. Image Nakumbuka kuna kijana alikuja amependeza, yuko smart na alikuwa na vigezo vyote vya kupata ajira.

Alikuwa na madaha na majivuno ya hapa na pale wakati tunafanya nae interview. Alitaka mshahara wake usishuke si chini ya milioni moja na laki tano.
Sep 29, 2020 8 tweets 2 min read
1/10 “Naitwa William Adam Lukoo ,mzaliwa wa mkoa wa Morogoro. Mwaka 2003 familia yetu ilihamia jijini Tanga kwa ajili ya harakati za kimaisha. Haikua rahis kwa sababu ya ugeni lakini wazazi walipambana kuhakikisha napata elimu bora. Licha ya kutoka kwenye familia ya kimaskini... 2/10 ..nilihakikisha nafanya vizuri kwenye masomo kiasi cha kuwavutia walimu na kujizolea umaarufu shuleni. Nilifanikiwa kuhitimu mwaka 2010 shule ya msingi Majani Mapana wilayani Tanga mjini. Mwaka 2011 nilianza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Usagara..
Sep 29, 2020 4 tweets 2 min read
"Kipindi nipo nyumbani Mwanza, nilikuwa napigiwa simu na Kaka mmoja ambaye nilikuwa nafahamiana nae sana. Alikuwa ananiomba nije sana Kahama akiwa na ahadi ya kunipa kazi, kunipangishia nyumba na ahadi nyingine nyingi nzuri. Siku niliyofika kahama, nilifikia guest house. Yule kaka ndiye aliyenipokea, hivyo nililala nae na mambo mengine ya chumbani yalifanyika.

Alivyoondoka asubuhi ndio ilikuwa mwisho kunipigia simu. Nikawa kila nikimtafuta naambulia matusi tu. Hakunipa chochote kama alivyoniahidi.