#TOTTechs Profile picture
Jukwaa la washauri na wataalamu wa Teknolojia || 💻 Computers ||📱 Phones | Softwares | ICT Hardwares | ICT Security || Partnership with Kukeke Gang and L.M.S

Aug 1, 2021, 11 tweets

VITU VYA KUZINGATIA KABLA YA KUNUNUA MacBook

Je! Unampango wa kununua MacBook mpya? Kabla ya kufanya ununuzi unahitaji kuielewa MacBook.

Aina nyingi za MacBook zinapatikana sokoni. Tutakusaidia kununua MacBook bora kulingana na mahitaji yako

Uzi mfupi 👇

Kabla ya kufanya ununuzi wowote angalia toleo la MacBook ambalo utaenda kununua. Kila Mwaka Apple hutoa toleo jipya la MacBook, unaweza kutembelea Apple’s official website, news, na social media kujua mda ambao Apple watatoa toleo Jipya

AINA ZA MacBook:

Kuna aina mbili za MacBook, MacBook Pro na MacBook Air: MacBook Air ni Nyembamba, nyepesi na ni rahisi kusafiri nayo wakati MacBook Pro ni nene kidogo.

Zote ni nzuri lakini zina utofauti sana kwenye Miundo ya ndani ( Internal Architecture & Specs)

MacBook Air ni basic version yaani ni toleo la Msingi lakini MacBook Pro ni toleo la hali ya juu ( Advanced version) na inapatikana kwa saizi mbili tofauti, Ikiwa ni mtumiaji wa kawaida basi MacBook Air itakufaa, Ikiwa wewe ni mtaalamu/Pro user basi Pro itakufaa zaidi.

SCREEN SIZE:

MacBook Air inapatikana kwa 13.3 inch screen size wakati MacBook Pro inapatikana kwa 13.3 na 16 inches screen sizes, MacBook Pro ina Options na Features nyingi kuliko MacBook Air, 16" Pro version inakuja na Intel UHD Graphics 630 wakati zingine hazina graphic card

Display kwenye MacBook Air ni 2560 X 1600 wakati kwenye 13.3" Pro Version ni 2560 X 1600 na kwenye 16" Pro version ni 3072 X 1920 pixels

BATTERY

Battery Life iko vizuri kwenye MacBook zote, MacBook Air ina 18hrs of Battery Life, Pro version 13.3" up to 20hrs, 16" up to 11hrs

INTERNAL SPECIFICATION

Apple wanatoa MacBook Specifications tofauti tofauti ni wewe tu kuchagua ipi ni bora kulingana na matumizi yako

🔸STORAGE
Storage ni kipengele muhimu sana kwenye kila Laptop, MacBook Air inakuja na Storage mpaka 2TB lakini kwa Pro version

13.3" ina hadi 4TB na kwa 16" Pro version ina hadi Storage ya 8TB SSD

Touch ID inapatikana kwenye versions zote lakini Touch Bar inapatikana kwenye Pro version pekee

Upande wa Processor na Chipset, zote 13.3" MacBook zina M1 Chip, 8 core CPU, 8 core GPU,16-core Neural Engine

MacBook Pro zina processors za aina tatu tofauti

🔸 2.6GHz 6-core Intel Core i7 🔸2.3GHz 8-core Intel Core i9 🔸2.4GHz 8-core Intel Core i9 with Turbo Boost 5.0GHz.

Hapo lazima uelewe unachukua Pro version yenye Processor ipi kulingana na mahitaji yako

MacBook Pro 16 inch inakuja na Intel UHD Graphics 630 Graphics card installed lakini zingine hazina Graphics Card

RAM ni kitu muhimu sana kwenye kuchagua Laptop, zote 13.3 inches MacBook zina 8GB - 16GB RAM lakini MacBook Pro ina RAM za aina tatu tofauti, kuna 16GB, 32GB, 64G

MacBook zote zina 720 Pixel FaceTime HD Camera:

MacBook Air inakuja na ports mbili za USB-C ikiwa Pro version ina Ports nne za USB-C

Hizo ni baadhi ya vitu vitakavyosaidia kuchagua MacBook nzuri kukingana na mahitaji yako

Hii naamini imesaidia

Share this Scrolly Tale with your friends.

A Scrolly Tale is a new way to read Twitter threads with a more visually immersive experience.
Discover more beautiful Scrolly Tales like this.

Keep scrolling