Ishengoma Irene Profile picture
I am a solution|Women Football Welfare #sokalawanawaketz 🇹🇿|#AmaniHuanziaNyumbani|Online Safe Space| I work @globalpeacetz | Maisha Plus 2nd runner 2016.

Jun 6, 2022, 8 tweets

JIKO LA GESI LILIVYOONDOA UHAI WA FAMILIA YA ABEID FALHUM😭💔🙏🏽
‘Abeid alipokuwa kitandani NENO ambalo alisisitiza tuwe makini na Gesi, tufanye namna Gesi hata ikivuja na kulipuka isiweze kuleta madhara kiasi kilichoitokea familia yake.’
Enzi za uhai Abeid alisimulia…..👇🏽

IIikuwa mida ya saa1 usiku (18 May,J5) nipo nyumbani wife akiwa jikoni akaniita jiko linasumbua kuwaka ni jiko la plate, basi nikaenda jikoni na mwanangu wa mwisho akanifata, nilipofika jikoni bila kujali harufu ya Gesi nika'switch jiko, kaka! kiasi cha sekunde sifuri '0'….

Wote tukawa tunaogelea kwenye moto, Nikamshika mtoto kukimbia nae nje sababu mlango ulikuwa umerudishwa tu, wote tukiwa tunawaka nikambwaga nje, nikarudi tena ndani sebule imelipuka pia lakini binti yangu alikuwa chumbani nikaingia huko kote kunawaka mwanangu anawaka nikamvuta…

akiwa analia huku anaungua nikakimbia nae nje, Hilo tukio lote la kuungua ninalokuelezea limetokea hata dakika 5 hazifiki aisee Moto mkali....nikawa nimewabakiza Mke na dada wa kazi ndani nikiwa naungua nikaona zoezi la kuingia na kutoka ni gumu nikaenda jikoni nikaushika mtungi

wa Gesi nikauburuza kuelekea nje (huku nawaka moto).... Nikarudi tena ndani moto umepungua nikakuta Mke wangu na dada wa kazi wote wameungua sababu ya uoga walikuwa wanagalagala huku wanaungua, nikawavuta nje, Wote tukalala nje tunasubiri msaada wa majirani, wengine wakawa…..

wanatufunika na kutuzima moto wengine wanajaribu kuudhibiti moto kuunguza Nyumba.."
Anamalizia "...braza toa Gesi nje ndugu yangu ni hatari sana, hatari mnoo!!😭
Tarehe 23 May mtoto wa Abeid wa miaka 2 Akafariki dunia.
Tarehe 25 alfajiri Abeid Akafariki, tukasafirisha kuelekea…

Moshi- Usangi kumhifadhi Abeid, tupo njiani tarehe 26 tukapigiwa simu Dada wa kazi amefariki,...tarehe 31 May Mke wa Abeid Akafariki....na leo hii tarehe 6 Juni binti yao amefariki😭Familia yote imeteketea.

#ripabeidfalhum #restinheavenlypeace #ripabeidfamily #godisgood

Kibinadamu inaumiza, inaliza, usipokuwa makini unaweza muuliza muumba kwa nini? Ila kazi yake Mola haina makosa hatuna budi kumshukuru na kumuomba apumzishe roho za rafiki na ndugu zetu hawa kwa amani, pamoja na kuwapa tumaini wanafamilia waliobaki na kovu hili.
#Riprafiki 💔😭❤️

Share this Scrolly Tale with your friends.

A Scrolly Tale is a new way to read Twitter threads with a more visually immersive experience.
Discover more beautiful Scrolly Tales like this.

Keep scrolling