Gillsant v7.5 Profile picture
Aug 29, 2020 16 tweets 3 min read Read on X
JINSI YA KUANZISHA BIASHARA UKIWA UMEAJIRIWA: Biashara yoyote iwe mpya au ya zamani ina changamoto zake especially kwenye mazingira yetu. 50% Ya biashara zote ndogo zinakufa katika mwaka wake wa kwanza kuanzishwa. UZI #ElimikaWikiendi
Mtandao wa Investopedia ulitoa sababu ya biashara ndogo kufa, 1. Mtaji Mdogo, 2. Uendeshaji Mbovu, 3. Mpangilio Mbovu wa Biashara na Bidhaa yako au huduma yako haihitajiki sokoni (Hakuna wateja wanahitaji bidhaa zako). Pamoja na sababu zingine nyingi.
Sasa kama tulivyoona hapo juu changamoto ni nyingi. Kabla ya kufikiria kuanzisha biashara ukiwa umeajiriwa inabidi ujipange. Kitu kimoja kikubwa ambacho Ajira itakusaidia kipindi unataka kuanzisha biashara ni MTAJI pamoja na muda wa kujipanga kabla ya kuanza biashara full time.
Kuna watu hua wanafikiria kuacha kazi ndio waanzishe biashara. Ndio unatakiwa kufuata ndoto zako lakini sikushauri hicho kitu. Asilimia kubwa ya biashara mpaka zianze kuingiza pesa inachukua hata mwaka mzima. So its either uwe ume save hela za kutosha kukusaidia muda wote huo
Hizi ni hatua chache za kufuata ili uanzishe biashara ukiwa umeajiriwa. Kwanza hakikisha mkataba wako na mwajiri wako unakuruhusu kufanya biashara ukiwa mwajiriwa wake. Kuna baadhi ya makampuni huwezi kuanzisha biashara ukiwa bado mwajiriwa wao. Soma Mkataba wako wa kazi
MUDA: Tambua kwamba biashara mpya inahitaji muda wako wa kutosha. Kuna muda wa kazi yako na muda wa biashara yako. Panga muda wako vizuri. Punguza au ondoa vitu ambavyo vinakumalizia muda wako na sio vya maana mfano Kuangalia Netflix, Social Media, Video Games, etc
WAZO LA BIASHARA: Usichague wazo la biashara na aina ya biashara ambayo hutaweza kuifanya part time. Mfano umefungua mgahawa au bar kama hautokuepo hapo full time kipindi cha mwanzo au huna msaidizi. UTALIA. Kama tulivyoona hapo juu moja ya sababu biashara kufa ni usimamizi mbovu
Kuna mawazo ya biashara (Business Ideas) na mfumo wa biashara (Business Models) nyingi sana ambazo unaweza kuchagua na kufanya on side ukiwa umeajiriwa full time. Kwa mawazo machache unaweza ingia hapa adesanmivictor.com/business-ideas…
Kabla hujachagua wazo la biashara uchague au ufanye jipime skills, abilities, and weaknesses zako. Kisha focus biashara ambayo itakufanya utumie strength zako. Kama huna hio skill ambayo biashara unayotaka kuifanya tumia muda wako kujifunza au mpe hio kazi mtu mwingine akusaidie.
Tuseme ushachagua wazo lako la biashra. Kibinadamu ni rahisi kuona wazo lako ni zuri na litakufanya upige hela. That’s the TRAP. UTAFELI. Kabla ya kutumia muda wako mwingi VALIDATE your idea first. Fanya utafiti, Market research. Soma Uzi Huu hapa
Malengo yako ni kuanzisha biashara ambayo inaongeza thamani kwa watu. Haitakua namaana kama utakua na bidhaa ambayo hakuna mtu anahitaji. Kusanya maoni kutoka kwa watu/wateja wako walengwa tokea unaanza biashara na usiache kuwaskiliza.
Tengeneza detailed, measurable, and realistic goals. Ni ngumu kwenda popote kama hufahamu unakwenda wapi. Panga mipango yako ya siku, wiki, mwezi. Kisha panga mkakati jinsi gani jinsi utayafikia malengo yako.
Biashara ina mahitaji mengi ili ifanikiwe na wewe kwa sababu umeajiriwa huna muda wa kutosha kuyafikia mahitaji yote. Mfano unahitaji Social Media Makerting kwa biashara yako na wewe huna muda. Hio kazi mpe mtu mwingine. Focus kwenye vitu muhimu vinavyokuza biashara yako
Faida inayopatikana kwenye Side Business yako Re Invest kwenye biashara yako na kiasi kingine kinachopatikana SAVE itakusaidia pale ambapo utaamua kuacha kazi na kufanya biashara full time. Hakikisha umeweka mipango na bajeti ya jinsi utatumia hela zako.
ANGALIZO: Usitumie mali za kampuni/mwajiri wako kwa kazi zako binafsI. Usitume email, printer, laptop, etc. Hii ni pamoja na muda wa mwajiri wako usitumie kwa biashra zako.
Kuanzisha biashra ukiwa umeajiriwa sio kazi ndogo lakini INAWEZEKANA. Kuna njia nyingi za kua mjasiriamali hii ni moja wapo. #ElimikaWikiendi

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Gillsant v7.5

Gillsant v7.5 Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @GillsaInt

Jan 18, 2023
Kwa vile bado ni January, Tujikumbushe zile shule 10 zenye ada(Fees) ghali Tanzania 2023 Update. Mtoto wako utampeleka shule ipi? #UZI 🧵
Morogoro International School (MIS)

Location: Morogoro
Curriculum: Cambridge.
Nursery: 6.4 Million Tshs Per Year
Secondary: 18 Million Tshs Per Year
Michango Mingine: Not Included
International School Moshi (ISM)/ UWC East Africa

Location: Kilimanjaro
Curriculum: International Baccalaureate (IB).
Nursery: 17.5 Million Tshs Per Year
Secondary: 43.8 Million Tshs Per Year
Michango Mingine: Not Included
Read 14 tweets
May 1, 2021
𝙉𝙅𝙄𝘼 9 𝘽𝙊𝙍𝘼 𝙕𝙄𝙏𝘼𝙆𝘼𝙕𝙊𝙆𝙐𝙁𝘼𝙉𝙔𝘼 𝙐𝘼𝙉𝙕𝙀 𝙅𝘼𝙈𝘽𝙊 𝙉𝘼 𝙐𝙁𝘼𝙉𝙄𝙆𝙄𝙒𝙀 𝙆𝘼𝙏𝙄𝙆𝘼 𝙈𝘼𝙄𝙎𝙃𝘼 𝙔𝘼𝙆𝙊. #𝙀𝙡𝙞𝙢𝙞𝙠𝙖𝙒𝙞𝙠𝙞𝙚𝙣𝙙𝙞 - 𝙏𝙝𝙧𝙚𝙖𝙙 (𝙐𝙕𝙄)
Kila siku tunajishughulisha ili tutimize malengo yetu. Katika maisha kuna watu ambao wanafanikiwa katika mambo yao na kuna watu ambao hawafanikiwi. Tunajishughulisha kila siku kuyatimiza malengo hayo. Malengo yanaweza yakawa ni maswala ya Elimu, Kazi, Biashara, Uongozi nk.
Tafiti zinaonyesha ni watu wachache sana wanaotimiza malengo yao duniani kote, inawezekana ukawa miongoni mwa watu ambao hawajafanikiwa kutimiza malengo yao. Zifuatazo ni njia 9 bora zitakazokufanya ufanikiwe katika maisha yako.
Read 17 tweets
Sep 26, 2020
𝑰𝑳𝑰 𝑾𝑨𝒁𝑶 𝑳𝑨𝑲𝑶 𝑳𝑨 𝑩𝑰𝑨𝑺𝑯𝑨𝑹𝑨 𝑳𝑰𝑭𝑨𝑵𝑰𝑲𝑰𝑾𝑬 𝑽𝑰𝑻𝑼 𝑽𝒀𝑨 𝑲𝑼𝒁𝑰𝑵𝑮𝑨𝑻𝑰𝑨: 𝑼𝒁𝑰 𝑷𝑨𝑹𝑻 2
Vitu vingine vya kuzingatia wakati unakuja na wazo lako la biashara.
Yes unaweza fungua biashara kutokana na kitu unachokijua mfano Kinyozi ukafungua saluni yako au mpishi ukafungua restaurant yako. Kumbuka kwakua wewe ni mpishi mzuri sio kwamba utafahamu jinisi ya kuendesha restaurant yako vizuri. Kuna mambo mengi ya kuzingatia
Kama unataka biashara endelevu make sure huduma au bidhaa unayouza wateja wako watarudi kwako tena. Inabidi uwe na bidhaa au huduma ambayo wateja wataendelea kununua kwa muda mrefu. Mfano ni bora uwe na kampuni ya kusafisha swimming pool kuliko kua na kampuni ya ujenzi wa pool.
Read 19 tweets
Sep 26, 2020
𝑱𝑰𝑵𝑺𝑰 𝒀𝑨 𝑲𝑼𝑱𝑨 𝑵𝑨 𝑾𝑨𝒁𝑶 𝒁𝑼𝑹𝑰 𝑳𝑨 𝑩𝑰𝑨𝑺𝑯𝑨𝑹𝑨. Ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuwa na wazo zuri la biashara. Je unajua jinsi ya kupata wazo hilo zuri la biashara? 𝑼𝒁𝑰, 𝑷𝑨𝑹𝑻 1
Watu wengi wamekuwa wakiniomba ushauri ni wazo gani zuri la biashara ambalo linaweza kuwapatia faida na mafanikio. Ukweli ni kwamba wazo ambalo ni bora kwa mtu fulani linaweza lisiwe bora kwako.
Moja ya sababu zinazofanya biashara nyingi kufa au kutokuendelea ni kuiga, yaani mtu akianza biashara leo baada ya muda unakuta watu wengine wameiga biashara ile ile, wanaifanya eneo lile lile na kwa mbinu zile zile. Hii ni njia rahisi sana ya kushindwa kwenye biashara.
Read 22 tweets
Aug 8, 2020
NJIA (Business Models) 10 ZA KUPATA PESA ONLINE. UZI Nimeshindwa kupata kiswahili cha Business Model (Mtanisaidia) Kwa uzoefu wangu watu wengi wanapotaka kuanza kufanya biashara Online or Offline. Hua wanafikiria njia moja au Mbili. #GillMadini
Kununua Bidhaa kutoka sehemu fulani au Kutengeneza hio bidhaa na kuiuza dukani or ikizidi sana mtandaoni kupitia Instagram au Facebook wachache kwenye website. Leo nimewaletea Business Models zingine 10. Ambazo unaweza kutumia kupiga hela.
Tukirejea kwenye UZI nilioandika mara ya mwisho. Kama bado haujausoma tafadhali usome Halafu rudi kumalizia Uzi huu. Leo nitatoa mfano wa wazo moja la biashara mbalo unaweza tumia njia zaidi ya 10 (10 Business Models) tofauti kuweza kufanikisha kujipatia pesa.
Read 24 tweets
Jul 23, 2020
BIASHARA MTANDAONI: Kuna njia nyingi za kuanza kufanya biashara mtandaoni (Facebook, Twitter, Instagram). Watu wengi hua tunakwama ni wazo gani la biashara au bidhaa gani niuze itakua na wateja. Nimekuletea UZI huu ukusaidie njia fupi ya kupata bidhaa ya uhakika kuuza #GillMadini
Kuna njia 2 ambazo ntazielezea kwa ufupi. 1. Kama tayari ushafahamu ni bidhaa gani utaenda kuuza mtandaoni 2. Hufahamu bidhaa au huduma gani uchague na kuuza mtandaoni.
Last time niliongelea hili swala lakini leo pia ningependa kutoa msisitizo, Idea za bidhaa za kuuza zipo nyingi sana lakini kuna maeneo haya ukipata bidhaa zake unatoboa faster Afya, Urembo, Passion, Hobby, Interest, Activities, Self Improvement, Wealth and Money, fitness.
Read 42 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(