Eng. Mbwambo Profile picture
Sep 11, 2020 13 tweets 3 min read Read on X
HISTORIA YA SIKU YA LEO MIAKA 19 ILIYOPITA USA NA DUNIA KWA UJUMLA...
Siku kama ya leo 2001 Dunia ilitawala huzuni na simanzi kubwa kutokana na Shambulio la September 11 2001 Shuka nao... 👇👇
Retweet ifike mbalii
#ElimikaWikiendi
#WajumbeTuinuane ImageImageImage
Siku ya Jumanne, tare 11 mwezi September mwaka 2001 majira ya saa 2 na dakika 46 asubuhi mpaka saa 4 na dakika 28 asubuhi lilifanyika shambulio kubwa na baya zaidi kuwahi kutokea na kufanywa na adui katika ardhi ya nchi ya Marekani.
Majira ya saa 2 na dakika 46, ndege aina ya Boeing 767-223ER (A.A. Flight 11) iliyosajiliwa kwa namba N334AA, mali ya shirika la American Airlines ambayo iliruka kutoka Boston katika uwanja wa ndege wa Logan International Airport ikitegemewa kutua katika uwanja wa ndege
Los Angels International Airport ambamo ndani yake kulikuwa na abiria 81 na wafanyakazi 11 ilijibamiza na kulipua jijini New York kwenye jengo la Kaskazini (North Tower) la kituo cha kibiashara cha kimataifa (World Trade Center) jengo ambalo lilikuwa na ghorofa 110
Dakika chache baadae, ndege nyingine aina ya Boeing 767-222 (U.A Flight 175) iliyosajiliwa kwa namba N6126UA inayomilikiwa na shirika la United Airlines ambayo pia iliruka kutoka Boston katika uwanja wa ndege wa Logan International Airport
Ikitegemewa pia ikatue katika uwanja wa ndege wa Los Angeles International Airport ambamo ndani ilikuwa na abiria 56 na wafanyakazi 9 ilinibamiza na kujilipua pia jijini New York South Tower la kituo hicho hicho cha biashara cha kimataifa. Jengo hili pia lilikuwa na ghorofa 110.
Kujibamiza kwa kwa ndege hizi na kulipua majengo haya kulisababisha maghorofa haya kudondoka kabisa (total collapse) na yalisababisasha kudondoka kwa majengo mengine kama vile ghorofa la 7 WTC Tower na maghorofa mengine kumi yaliyomo ndani ya kituo cha cha kimataifa (WTC Complex)
Wakati haya yakitokea jijini New York, ndege nyingine aina ya Boeing 757-223 (A.A. Flight 77) iliyosajiliwa kwa namba N644AA inayomilikiwa na shirika la American Airlines ambayo iliruka kutoka katika uwanja wa ndege wa Washington Dulles International Airport ikitegemewa
Ikatue kwenye uwanja wa Los Angels International Airport ambmo ndani yake ilikuwa na abiria 58 na wafanyakazi iligeuza njia na kurudi nyuma na kwenda kujibamiza na kulipua jengo la Pentagon, ambalo ndio Makao Makuu ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (US Department of Defense).
Muda huo huo pia, ndege nyingine aina ya Boeing 757-222 (U.A Flight93) iliyosajiliwa kwa namba N591UA mali ya shirika la United Airlines ambayo iliruk
a kutoka Newark Intenational Airport ikiwa na abiria 37 na wafanyakazi 7 na ikitegemewa ikatue
katika uwanja wa San Fransisco International Airport ilidondoka karibu na eneo la Shanksville, Pennsylvania na inasadikiwa ndege hii ilikuwa njiani kwenda kujibamiza katika Ikulu ya marekani.
Mfululizo wa mashambuluo haya ya
siku hii yalikuwa ni tukio baya zaidi katika historia kwa Marekani kushambuliwa na adui katika ardhi yake mwenyewe.

Jumla ya watu 2997 walifariki na watu 6000 wengine walijerehiwa vibaya mno.
Hasara hii inafikia jumla ya shilingi za kitanzania Quadrillion 6 (Trilioni elfu sita za kitanzania).

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Eng. Mbwambo

Eng. Mbwambo Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @iAlfordMbwambo

Oct 1, 2020
Leo Tumjue Mnyama Nyegere
RT iwafikie wengi
Ongezea unalojua zaidi
Nyegere ni moja kati ya wanyama wenye wivu sana hapa duniani.
Chakula chake kikubwa ni asali,yeye hupanda juu ya mzinga wa asali na kuujambia, baada ya mashuzi yake nyuki wote hulewa na yeye kupakua asali na masega yake na kula.
Mwili wake una ngozi ngumu sana kiasi hata nyuki akimuuma hakuna chochote kinatokea.
Ni mnyama mwenye wivu na mapenzi makubwa sana kwa jike lake,hutembea nyuma ya jike huku akiwa ameziba sehemu za siri za jike,hata jani tu likiigusa sehemu ya siri ya jike litararuliwa na kupokea kichapo cha hatari,maana wivu wake ni kuwa jani laitakuwa "limefaidi utamu" wa jike
Read 11 tweets
Sep 23, 2020
FURSA YA KILIMO CHA NYOKA
Achana connection za ifm njoo connection hii...

Kilimo cha nyoka ni moja ya kilimo chenye faida sana ,mmoja anaweza akaanzisha kilimo hichi ukizingatia thamani ya "snake venom" ipo juu sana.
Sumu ya nyoka inatumik kwa wingi kwenye viwanda vya famasia na viwanda vya vipodozi thamani ya "snake venom " ipo juu sana kutokana na uhitaji wake

Gram moja ya "snake venom" kwa soko la kimataifa inauzwa $1880 ,na kwenye soko la Afrika kusini inauzwa kwa makadirio ya Rand 25K
Kama unafikiria kuanzisha shamba lako la nyoka ,yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia ili uweze kupata faida ya kutosha kutokana na venom wanayozalisha Nyoka

1.Zingatia hali ya joto na hewa.
Nyoka wanahitaji joto ya kiwango cha 24-29°C nyakati ya siku na 21-24 nyakati za usiku
Read 7 tweets
Sep 17, 2020
MASKINI & TAJIRI:-
1.Maskini hudhani utajiri ni bahati,tajiri hudhani umaskini hutokana na uvivu na uzembe. Maskini ni mdogo kuliko matatizo yake,tajiri ni mkubwa kuliko matatizo yake.
2.Tajiri bila masikini ni maskini lakini maskini bila tajiri ni tajiri.Umaskini ni matokeo ya fursa zote ambazo hazikutumika kwa usahihi,utajiri ni jumla ya fursa zote zilizotumika kwa usahihi
3.Maskini huwaza kulima mchicha,tajiri huwaza kulima miti ya mbao.Maskini huamini unahitaji pesa kupata pesa,tajiri huamini atapata pesa kupitia pesa za wengine.Maskini hudhani tajiri ana tabia ya kuringa,tajiri hudhani maskini ana tabia ya kuombaomba.
Read 5 tweets
Sep 14, 2020
MWL.JULIUS KAMBARAGE NYERERE NI BABA WA TAIFA LA TANZANIA.
Kuelekea Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa .Tujue machache kumhusu
1.Alizaliwa tarehe 13/04/1922 Butiama na kufariki tarehe 14/10/1999 kule London. Ni Raisi wa kwanza Afrika kuachia madaraka kwa hiari yake mwenyewe. Image
2.Ni Raisi wa kwanza kuhama Ikulu na kwenda kuishi kwenye nyumba aliyoijenga kwa mkopo akiwa bado Raisi.
3.Ni kati ya Raisi aliyekuwa analipwa mshahara mdogo duniani na pia raisi aliyewahi kulipwa mshahara mdogo barani Afrika mpaka sasa.
4. Ni Mtanganyika wa kwanza kusoma chuo kikuu nchini Uingereza na Muafrika wa pili kupata Degree nje ya Afrika, akisomea English, Political Economy, Social Anthropology, British History, Economic History, Constitutional Law, and Moral Philosophy.
Read 21 tweets
Sep 14, 2020
Mambo Ya Msingi Unayopaswa Kufahamu Kuhusu Nidhamu Ya Pesa.
Ni bora tuwe wakweli katika somo linalohusu pesa kwani ndilo somo ambalo watu wengi hufeli sana hasa pale wanapozipata,wapo baadhi ya watu wakizipata pesa hujikuta hawana kitu au zimeisha pasipo kufanya mambo ya msingi
Wengi wao wamesahau ya kwamba pesa zina kanuni na misingi yake ambapo kila mwenye kuzihitaji ni lazima aweze kuzielewa kanuni hizo, na pia kanuni hizo ni lazima aendane na misingi pamoja na nidhamu ili ziweze kujizalisha.
Hivyo ili uweze kumiliki pesa unatakiwa kufahamu mambo haya ya msingi yahusuyo pesa kama ifuatavyo:-

1. Ongeza kiwango cha uzalishaji.
Ukitaka kuishi katika kiwango kizuri cha umiliki wa pesa unatakiwa kuzingatia misingi itayokusaidia wewe kuweza kuwa hivyo, na miongoni mwa
Read 15 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(