Gillsant v7.5 Profile picture
Sep 26, 2020 โ€ข 22 tweets โ€ข 4 min read โ€ข Read on X
๐‘ฑ๐‘ฐ๐‘ต๐‘บ๐‘ฐ ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐‘ฑ๐‘จ ๐‘ต๐‘จ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐’๐‘ผ๐‘น๐‘ฐ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ. Ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuwa na wazo zuri la biashara. Je unajua jinsi ya kupata wazo hilo zuri la biashara? ๐‘ผ๐’๐‘ฐ, ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 1
Watu wengi wamekuwa wakiniomba ushauri ni wazo gani zuri la biashara ambalo linaweza kuwapatia faida na mafanikio. Ukweli ni kwamba wazo ambalo ni bora kwa mtu fulani linaweza lisiwe bora kwako.
Moja ya sababu zinazofanya biashara nyingi kufa au kutokuendelea ni kuiga, yaani mtu akianza biashara leo baada ya muda unakuta watu wengine wameiga biashara ile ile, wanaifanya eneo lile lile na kwa mbinu zile zile. Hii ni njia rahisi sana ya kushindwa kwenye biashara.
Kuja na wazo la biashara kuna mambo mengi sana ya kuzingatia, hii ni pamoja na upo eneo gani, mkoa gani, elimu yako, watu waliokuzunguka, ujuzi, umri wako, muda, mtaji, resources, njaa yako, kiu ya kufanikiwa, connection, etc
Hivyo hakuna formula moja ambayo utatumia. Hapa chini nimejaribu tu kukupa njia mbali mbali kama muongozo. Unaweza chagua njia yoyote na kuanza nayo. Pia bilakusahau unaweza pitia uzi huu ukakuongezea madini
TUMIA UJUZI ULIO NAO
Ujuzi ulionao ndo sehemu ya kwanza kabisa ya kupata wazo la Biashara, Mfano kama wewe umejiriwa na ni fundi seremala, kwa nini usianze na wewe kuwa na biashara ya aina hiyo?
BADILISHA HOBBY YAKO KUWA PESA
Hobby ni moja ya maeneo ambayo watu hupata mafanikio, kama wewe hobby yako ni Kuogelea, kwa nini usifundishe watu kuogelea?
Kuna njia mbali mbali unaweza tumia kuanzisha biashara kutokana na hobby yako pitia uzi huu
NUNUA BIASHARA AMBAYO TAYARI IPO
Ukishindwa kabisa kupata wazo zuri unaweza nunua biashara ya mtu mwingine na kuindeleza, siku hizi kuna biashara kibao zinauzwa kwa sababu mbalimbali so unaweza nunua na kuendelea nayo. Kuna vigezo vya kuangalia kabla ya kununua.
NINI KINAKOSEKANA MTAANI?
Tazama ni kitu gani hakipo hapo mtaani, geuza kuwa opportunity, inaweza isiwe ni mtaani ikawa ni kazini kwako, Kijijini kwenu au maeneo unayo kwenda kustarehe.
-Ni kitu gani huwa kinaleta usumbufu kwako na kukuchukulia muda mwingi na pesa nyingi?
Ni huduma zipi hazipo kabisa mtaani kwako? Na ambazo ni za muhimu?
Ni bidhaa zipi ambazo ni vigumu kuzipata mtaani kwenu?
Ni kitu gani, wewe, Ndugu, Majirani huwa wanakilalamikia sana mtaani hapo?
Ni tatizo gani sugu ambalo wewe mwenyewe hua linakusumbua na hujapata solution?
Ni kitu gani umeona inaweza kua tatizo mbeleni? Mfano kwa sasa watu wanakula junk food bila kuangalia afya zao hili ni tatizo unaweza kuja na solution yake
Huduma au bidhaa gani inaweza kuokoa pesa/muda wa mteja wako mtarajiwa?
Huduma gani inaweza rahisisha maisha ya mtu?
ANGALIA MAKAMPUNI MAKUBWA WANAHITAJI NINI?
Unaweza tumia uwepo wa makampuni Fulani au taasisi Fulani maeneo yako kutengeneza wazo la biashara, taasisi kama Shule, vyuo, Hospitali, Makampuni kama Viwanda Migodi na kadhalika, angalia ni kipi hawa watu wanaweza kuwa wanahitaji.
UNAWEZA KUANGALIA KUHUSU KUUZA BIDHAA ZA WENGINE
Unaweza ukawa unauza bidhaa za watu wengine, unachukua na kuuza. Fanya utafiti kabla ya kuanza kuuza bidhaa hizi. Mfano miezi miwili mitatu nyuma kuna mafuta ya wanawake yanaitwa Snail yameuzwa sana. Hii ilikua bidhaa nzuri
ANGALIA HABARI NA MAKALA MBALIMBALI
Kuna chaneli huwa zina makala mazuri sana ya kiuchumi na biashara, kitaifa na kimataifa siku huzi kazi yao ni hiyo tu, ni kuonyesja ubunifu wa wajasirimali, TV, radio na magazeti yanaweza toa mchango wakutosha kwa wewe kupata wazo la biashara
COPY BUSINESS IDEA AMBAYO IMEFANIKIWA KWINGINEKO
Hii ni moja ya njia zinazo tumika kwa sasa, unaweza copy idea kutoka hata India, China, na kwingineko na ukaja kuifanyia kazi huku kwa kufanya marekebisho madogo kulingana na mahitaji ya eneo husika
TUMIA NJIA ZOTE ZA KIUTAFITI KUPATA WAZO LA BIASHARA
- Maonyesho ya biashara
- Kwenye taasisi za uma zinazo husika na biashara
- Kwa marafiki.
MITANDAO YA KIJAMII
Watu kwenye mitandao ya kijamii ni rahisi sana kupost kuhusu matatizo na kero zao kuhusu huduma au bidhaa flani. Wachache hua wanafuatilia na kutatua matatizo hayo. Matatizo hayo yanaweza kua chanzo cha wazo bora la biashara.
WEBSITE ZA BIASHARA
Kuna kurasa za Instagram ambazo hua wanauza vitu mbali mbali au mitandao kama ebay, AliExpress, AliBaba, Kikuu, Inalipa, etc pendelea kuitembelea na kuangalia bidhaa zinazouzwa humo ni chanzo kizuri cha mawazo ya biashara
TEMBELEA MASOKO MAKUBWA
Kwa kutembelea masoko makubwa kama Kariakoo na mengine kama hayo. Yanaweza kukufungua akili kufahamu biashara gani ya kufanya. Kwa kuangalia bidhaa aina gani zinatoka au wateja wanazikimbilia.
UNAWEZA GUNDUA KITU?
Unaweza ukaja na ugunduzi wako kama kuna jamaa nilimuona TBC katengeneza mashine zake za kukunia nazi kwa umeme. Jamaa anauza mashine 300,000 mashine hizo nikakuta kariakoo vijana wanatumia kukunia nazi moja 200. Kwa siku jamaa wanakuna nazi hadi 500
Kama tulivyoona hapo juu hizo ni baadhi tu ya njia unazoweza kuzifanya ukiwa unatafuta wazo la biashra. Kama kunayoyote nimeisahau unawea kuiongezea hapa chini. Vitu 20 vya kuzingatia wakati unatafuta wazo la biashara.
๐™„๐™‰๐˜ผ๐™€๐™‰๐˜ฟ๐™€๐™‡๐™€๐˜ผ ๐™‹๐˜ผ๐™๐™ 2

โ€ข โ€ข โ€ข

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
ใ€€

Keep Current with Gillsant v7.5

Gillsant v7.5 Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @GillsaInt

Jan 18, 2023
Kwa vile bado ni January, Tujikumbushe zile shule 10 zenye ada(Fees) ghali Tanzania 2023 Update. Mtoto wako utampeleka shule ipi? #UZI ๐Ÿงต
Morogoro International School (MIS)

Location: Morogoro
Curriculum: Cambridge.
Nursery: 6.4 Million Tshs Per Year
Secondary: 18 Million Tshs Per Year
Michango Mingine: Not Included
International School Moshi (ISM)/ UWC East Africa

Location: Kilimanjaro
Curriculum: International Baccalaureate (IB).
Nursery: 17.5 Million Tshs Per Year
Secondary: 43.8 Million Tshs Per Year
Michango Mingine: Not Included
Read 14 tweets
May 1, 2021
๐™‰๐™…๐™„๐˜ผ 9 ๐˜ฝ๐™Š๐™๐˜ผ ๐™•๐™„๐™๐˜ผ๐™†๐˜ผ๐™•๐™Š๐™†๐™๐™๐˜ผ๐™‰๐™”๐˜ผ ๐™๐˜ผ๐™‰๐™•๐™€ ๐™…๐˜ผ๐™ˆ๐˜ฝ๐™Š ๐™‰๐˜ผ ๐™๐™๐˜ผ๐™‰๐™„๐™†๐™„๐™’๐™€ ๐™†๐˜ผ๐™๐™„๐™†๐˜ผ ๐™ˆ๐˜ผ๐™„๐™Ž๐™ƒ๐˜ผ ๐™”๐˜ผ๐™†๐™Š. #๐™€๐™ก๐™ž๐™ข๐™ž๐™ ๐™–๐™’๐™ž๐™ ๐™ž๐™š๐™ฃ๐™™๐™ž - ๐™๐™๐™ง๐™š๐™–๐™™ (๐™๐™•๐™„)
Kila siku tunajishughulisha ili tutimize malengo yetu. Katika maisha kuna watu ambao wanafanikiwa katika mambo yao na kuna watu ambao hawafanikiwi. Tunajishughulisha kila siku kuyatimiza malengo hayo. Malengo yanaweza yakawa ni maswala ya Elimu, Kazi, Biashara, Uongozi nk.
Tafiti zinaonyesha ni watu wachache sana wanaotimiza malengo yao duniani kote, inawezekana ukawa miongoni mwa watu ambao hawajafanikiwa kutimiza malengo yao. Zifuatazo ni njia 9 bora zitakazokufanya ufanikiwe katika maisha yako.
Read 17 tweets
Sep 26, 2020
๐‘ฐ๐‘ณ๐‘ฐ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐‘ณ๐‘จ๐‘ฒ๐‘ถ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ ๐‘ณ๐‘ฐ๐‘ญ๐‘จ๐‘ต๐‘ฐ๐‘ฒ๐‘ฐ๐‘พ๐‘ฌ ๐‘ฝ๐‘ฐ๐‘ป๐‘ผ ๐‘ฝ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐’๐‘ฐ๐‘ต๐‘ฎ๐‘จ๐‘ป๐‘ฐ๐‘จ: ๐‘ผ๐’๐‘ฐ ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 2
Vitu vingine vya kuzingatia wakati unakuja na wazo lako la biashara.
Yes unaweza fungua biashara kutokana na kitu unachokijua mfano Kinyozi ukafungua saluni yako au mpishi ukafungua restaurant yako. Kumbuka kwakua wewe ni mpishi mzuri sio kwamba utafahamu jinisi ya kuendesha restaurant yako vizuri. Kuna mambo mengi ya kuzingatia
Kama unataka biashara endelevu make sure huduma au bidhaa unayouza wateja wako watarudi kwako tena. Inabidi uwe na bidhaa au huduma ambayo wateja wataendelea kununua kwa muda mrefu. Mfano ni bora uwe na kampuni ya kusafisha swimming pool kuliko kua na kampuni ya ujenzi wa pool.
Read 19 tweets
Aug 29, 2020
JINSI YA KUANZISHA BIASHARA UKIWA UMEAJIRIWA: Biashara yoyote iwe mpya au ya zamani ina changamoto zake especially kwenye mazingira yetu. 50% Ya biashara zote ndogo zinakufa katika mwaka wake wa kwanza kuanzishwa. UZI #ElimikaWikiendi
Mtandao wa Investopedia ulitoa sababu ya biashara ndogo kufa, 1. Mtaji Mdogo, 2. Uendeshaji Mbovu, 3. Mpangilio Mbovu wa Biashara na Bidhaa yako au huduma yako haihitajiki sokoni (Hakuna wateja wanahitaji bidhaa zako). Pamoja na sababu zingine nyingi.
Sasa kama tulivyoona hapo juu changamoto ni nyingi. Kabla ya kufikiria kuanzisha biashara ukiwa umeajiriwa inabidi ujipange. Kitu kimoja kikubwa ambacho Ajira itakusaidia kipindi unataka kuanzisha biashara ni MTAJI pamoja na muda wa kujipanga kabla ya kuanza biashara full time.
Read 16 tweets
Aug 8, 2020
NJIA (Business Models) 10 ZA KUPATA PESA ONLINE. UZI Nimeshindwa kupata kiswahili cha Business Model (Mtanisaidia) Kwa uzoefu wangu watu wengi wanapotaka kuanza kufanya biashara Online or Offline. Hua wanafikiria njia moja au Mbili. #GillMadini
Kununua Bidhaa kutoka sehemu fulani au Kutengeneza hio bidhaa na kuiuza dukani or ikizidi sana mtandaoni kupitia Instagram au Facebook wachache kwenye website. Leo nimewaletea Business Models zingine 10. Ambazo unaweza kutumia kupiga hela.
Tukirejea kwenye UZI nilioandika mara ya mwisho. Kama bado haujausoma tafadhali usome Halafu rudi kumalizia Uzi huu. Leo nitatoa mfano wa wazo moja la biashara mbalo unaweza tumia njia zaidi ya 10 (10 Business Models) tofauti kuweza kufanikisha kujipatia pesa.
Read 24 tweets
Jul 23, 2020
BIASHARA MTANDAONI: Kuna njia nyingi za kuanza kufanya biashara mtandaoni (Facebook, Twitter, Instagram). Watu wengi hua tunakwama ni wazo gani la biashara au bidhaa gani niuze itakua na wateja. Nimekuletea UZI huu ukusaidie njia fupi ya kupata bidhaa ya uhakika kuuza #GillMadini
Kuna njia 2 ambazo ntazielezea kwa ufupi. 1. Kama tayari ushafahamu ni bidhaa gani utaenda kuuza mtandaoni 2. Hufahamu bidhaa au huduma gani uchague na kuuza mtandaoni.
Last time niliongelea hili swala lakini leo pia ningependa kutoa msisitizo, Idea za bidhaa za kuuza zipo nyingi sana lakini kuna maeneo haya ukipata bidhaa zake unatoboa faster Afya, Urembo, Passion, Hobby, Interest, Activities, Self Improvement, Wealth and Money, fitness.
Read 42 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(