Gillsant v7.5 Profile picture
Sep 26, 2020 โ€ข 19 tweets โ€ข 3 min read โ€ข Read on X
๐‘ฐ๐‘ณ๐‘ฐ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐‘ณ๐‘จ๐‘ฒ๐‘ถ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ ๐‘ณ๐‘ฐ๐‘ญ๐‘จ๐‘ต๐‘ฐ๐‘ฒ๐‘ฐ๐‘พ๐‘ฌ ๐‘ฝ๐‘ฐ๐‘ป๐‘ผ ๐‘ฝ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐’๐‘ฐ๐‘ต๐‘ฎ๐‘จ๐‘ป๐‘ฐ๐‘จ: ๐‘ผ๐’๐‘ฐ ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 2
Vitu vingine vya kuzingatia wakati unakuja na wazo lako la biashara.
Yes unaweza fungua biashara kutokana na kitu unachokijua mfano Kinyozi ukafungua saluni yako au mpishi ukafungua restaurant yako. Kumbuka kwakua wewe ni mpishi mzuri sio kwamba utafahamu jinisi ya kuendesha restaurant yako vizuri. Kuna mambo mengi ya kuzingatia
Kama unataka biashara endelevu make sure huduma au bidhaa unayouza wateja wako watarudi kwako tena. Inabidi uwe na bidhaa au huduma ambayo wateja wataendelea kununua kwa muda mrefu. Mfano ni bora uwe na kampuni ya kusafisha swimming pool kuliko kua na kampuni ya ujenzi wa pool.
โ€œFanya kile unachopenda na pesa zitakufuata.โ€ Nafikiri ushawahi kusikia huu msemo. Mimi nitaweka msistizo tu sio kila unachokipenda kinaweza kua biashara yenye faida. Yes fanya unachokipenda but angalia kama kinaweza kua biashara yenye faida.
Kanuni mojawapo ya kufanikiwa katika kile unachokifanya ni kwa kupenda kile unachokifanya. Unapochagua wazo unalolipenda ni wazi kuwa utalifanya kwa moyo na kwa ufanisi mkubwa hata kama utakutana na changamoto.
Chagua wazo unalolifahamu na kulimudu
Watu wengi hufanya kosa la kuchagua wazo la biashara ambalo hawalifahamu vyema au kulimudu. Hii ni kutokana na kuiga, kukosa ubunifu au hata tamaa ya pesa.
Kumbuka ili wazo lifanikiwe ni lazima litekelezwe na mtu anayelifahamu vyema na kulimudu. Kwa mfano unaanzisha biashara ya hoteli huku ukiwa huna maarifa wa ujuzi wowote kuhusu uendeshaji wa hoteli; ni wazi kuwa hutoweza kufanikiwa.
Wataalamu wa biashara wanashauri ili uanze biashara inabidi uwe na Unique Selling Proposition (Utafauti katika soko) Bidhaa zako au huduma ziwe tofauti na washindani wako. Hii ni changamoto na inaweza kukwamisha, sio lazima bidhaa yako au huduma iwe tofauti.
Kuna baadhi ya bidhaa hazina USP, Badala ya kutafuta USP ya huduma au bidhaa yako tafuta jinsi gani utaiuza kiutofauti
Je una ujuzi au resources ambazo zinaweza kukusaidia kufanya wazo lako la biashara kua na faida? Kama hauna jifunze mpaka uwe na ujuzi au uwezo wa kufanya. Mfano nimeona kuna fursa nyingi kwenye graphics design na sina ujuzi huo, jifunze.
Zingatia swala la fedha
Kila biashara inahitaji fedha ili kujiendesha. Hivyo hakikisha wazo la biashara unalolichagua utaweza kupata fedha za kutosha ili kulitekeleza.
Lifahamu wazo vyema kabla ya kuamua kulifanyia kazi, fahamu gharama zote zinazohitajika katika kulitekeleza pamoja na faida itakayopatikana. Kwa njia hii utaweza kufanya maamuzi bora zaidi kama wazo linafaa au la.
Angalia uhitaji wa soko
Watu wengi hawafahamu umuhimu wa kuangalia uhitaji wa soko kabla ya kuchagua wazo la biashara. Unapoangalia uhitaji wa soko ni wazi kuwa utachagua wazo la biashara ambalo litauzika.
Tatua tatizo au changamoto ambayo mteja wako mlengwa anayo. Usichague tu wazo kwa sababu ni wazo au wengine wanalifanya, bali hakikisha wazo lako linahitajika sokoni katika wakati husika.
Ushindani
Ushindani ni jambo muhimu ambalo kila mtu anayechagua wazo la biashara anatakiwa kulizingatia, kwani kufanikiwa kwenye biashara kunategemea kiwango cha ushindani na jinsi utakavyokabiliana nacho.
Hakikisha unafahamu vyema ushindani kwenye wazo husika na unaweza kuumudu vyema. Hakuna haja ya kuchagua wazo ambalo unashindana na makampuni yaliyoenea ulimwenguni kote wakati wewe ni mjasiriamali unayeanza..
Wazo lako la biashara kabla ya kurukia na kuanza kufanya hakikisha umefanya utafiti wa kutosha na kikubwa umefanya majaribio kadhaa, Kuna njia za kufanya majaribio ya wazo lako la biashara, baadhi nimeelezea hapa
Kama nilivyoeleza hapo awali, uchaguzi wa wazo la biashara unahitaji utulivu na umakini mkubwa.

Usichague wazo kwa kuwa wengine wamelichagua au wengine linawapa faida; bali chagua lile linalokufaa wewe na mazingira yako.
UZI ujao nitaleta mfano wa mawazo 50 ya biashara unayoweza anzisha bila mtaji au mtaji mdogo. Comment YES kama unahitaji uzi huu.

โ€ข โ€ข โ€ข

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
ใ€€

Keep Current with Gillsant v7.5

Gillsant v7.5 Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @GillsaInt

Jan 18, 2023
Kwa vile bado ni January, Tujikumbushe zile shule 10 zenye ada(Fees) ghali Tanzania 2023 Update. Mtoto wako utampeleka shule ipi? #UZI ๐Ÿงต
Morogoro International School (MIS)

Location: Morogoro
Curriculum: Cambridge.
Nursery: 6.4 Million Tshs Per Year
Secondary: 18 Million Tshs Per Year
Michango Mingine: Not Included
International School Moshi (ISM)/ UWC East Africa

Location: Kilimanjaro
Curriculum: International Baccalaureate (IB).
Nursery: 17.5 Million Tshs Per Year
Secondary: 43.8 Million Tshs Per Year
Michango Mingine: Not Included
Read 14 tweets
May 1, 2021
๐™‰๐™…๐™„๐˜ผ 9 ๐˜ฝ๐™Š๐™๐˜ผ ๐™•๐™„๐™๐˜ผ๐™†๐˜ผ๐™•๐™Š๐™†๐™๐™๐˜ผ๐™‰๐™”๐˜ผ ๐™๐˜ผ๐™‰๐™•๐™€ ๐™…๐˜ผ๐™ˆ๐˜ฝ๐™Š ๐™‰๐˜ผ ๐™๐™๐˜ผ๐™‰๐™„๐™†๐™„๐™’๐™€ ๐™†๐˜ผ๐™๐™„๐™†๐˜ผ ๐™ˆ๐˜ผ๐™„๐™Ž๐™ƒ๐˜ผ ๐™”๐˜ผ๐™†๐™Š. #๐™€๐™ก๐™ž๐™ข๐™ž๐™ ๐™–๐™’๐™ž๐™ ๐™ž๐™š๐™ฃ๐™™๐™ž - ๐™๐™๐™ง๐™š๐™–๐™™ (๐™๐™•๐™„)
Kila siku tunajishughulisha ili tutimize malengo yetu. Katika maisha kuna watu ambao wanafanikiwa katika mambo yao na kuna watu ambao hawafanikiwi. Tunajishughulisha kila siku kuyatimiza malengo hayo. Malengo yanaweza yakawa ni maswala ya Elimu, Kazi, Biashara, Uongozi nk.
Tafiti zinaonyesha ni watu wachache sana wanaotimiza malengo yao duniani kote, inawezekana ukawa miongoni mwa watu ambao hawajafanikiwa kutimiza malengo yao. Zifuatazo ni njia 9 bora zitakazokufanya ufanikiwe katika maisha yako.
Read 17 tweets
Sep 26, 2020
๐‘ฑ๐‘ฐ๐‘ต๐‘บ๐‘ฐ ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐‘ฑ๐‘จ ๐‘ต๐‘จ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐’๐‘ผ๐‘น๐‘ฐ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ. Ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuwa na wazo zuri la biashara. Je unajua jinsi ya kupata wazo hilo zuri la biashara? ๐‘ผ๐’๐‘ฐ, ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 1
Watu wengi wamekuwa wakiniomba ushauri ni wazo gani zuri la biashara ambalo linaweza kuwapatia faida na mafanikio. Ukweli ni kwamba wazo ambalo ni bora kwa mtu fulani linaweza lisiwe bora kwako.
Moja ya sababu zinazofanya biashara nyingi kufa au kutokuendelea ni kuiga, yaani mtu akianza biashara leo baada ya muda unakuta watu wengine wameiga biashara ile ile, wanaifanya eneo lile lile na kwa mbinu zile zile. Hii ni njia rahisi sana ya kushindwa kwenye biashara.
Read 22 tweets
Aug 29, 2020
JINSI YA KUANZISHA BIASHARA UKIWA UMEAJIRIWA: Biashara yoyote iwe mpya au ya zamani ina changamoto zake especially kwenye mazingira yetu. 50% Ya biashara zote ndogo zinakufa katika mwaka wake wa kwanza kuanzishwa. UZI #ElimikaWikiendi
Mtandao wa Investopedia ulitoa sababu ya biashara ndogo kufa, 1. Mtaji Mdogo, 2. Uendeshaji Mbovu, 3. Mpangilio Mbovu wa Biashara na Bidhaa yako au huduma yako haihitajiki sokoni (Hakuna wateja wanahitaji bidhaa zako). Pamoja na sababu zingine nyingi.
Sasa kama tulivyoona hapo juu changamoto ni nyingi. Kabla ya kufikiria kuanzisha biashara ukiwa umeajiriwa inabidi ujipange. Kitu kimoja kikubwa ambacho Ajira itakusaidia kipindi unataka kuanzisha biashara ni MTAJI pamoja na muda wa kujipanga kabla ya kuanza biashara full time.
Read 16 tweets
Aug 8, 2020
NJIA (Business Models) 10 ZA KUPATA PESA ONLINE. UZI Nimeshindwa kupata kiswahili cha Business Model (Mtanisaidia) Kwa uzoefu wangu watu wengi wanapotaka kuanza kufanya biashara Online or Offline. Hua wanafikiria njia moja au Mbili. #GillMadini
Kununua Bidhaa kutoka sehemu fulani au Kutengeneza hio bidhaa na kuiuza dukani or ikizidi sana mtandaoni kupitia Instagram au Facebook wachache kwenye website. Leo nimewaletea Business Models zingine 10. Ambazo unaweza kutumia kupiga hela.
Tukirejea kwenye UZI nilioandika mara ya mwisho. Kama bado haujausoma tafadhali usome Halafu rudi kumalizia Uzi huu. Leo nitatoa mfano wa wazo moja la biashara mbalo unaweza tumia njia zaidi ya 10 (10 Business Models) tofauti kuweza kufanikisha kujipatia pesa.
Read 24 tweets
Jul 23, 2020
BIASHARA MTANDAONI: Kuna njia nyingi za kuanza kufanya biashara mtandaoni (Facebook, Twitter, Instagram). Watu wengi hua tunakwama ni wazo gani la biashara au bidhaa gani niuze itakua na wateja. Nimekuletea UZI huu ukusaidie njia fupi ya kupata bidhaa ya uhakika kuuza #GillMadini
Kuna njia 2 ambazo ntazielezea kwa ufupi. 1. Kama tayari ushafahamu ni bidhaa gani utaenda kuuza mtandaoni 2. Hufahamu bidhaa au huduma gani uchague na kuuza mtandaoni.
Last time niliongelea hili swala lakini leo pia ningependa kutoa msisitizo, Idea za bidhaa za kuuza zipo nyingi sana lakini kuna maeneo haya ukipata bidhaa zake unatoboa faster Afya, Urembo, Passion, Hobby, Interest, Activities, Self Improvement, Wealth and Money, fitness.
Read 42 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(