WatuNiStory Profile picture
Sep 28, 2020 9 tweets 2 min read Read on X
Nimeona bora niongee na kuomba ushauri wenu kwani nimekaa kimya siku nyingi. Hali inazidi kuwa mbaya. Nazidi kudhoofika kisaikolojia na imefikia hatua Kuna mawazo mabaya yananijia kichwani.
Ni hivi, nilikua na biashara zangu kama tatu hivi nilizokua naziendesha zikiwa eneo moja. Kwa kuwa mimi ni mwalimu wa shule binafsi (private school) muda mwingi nashinda kazini, Hivyo msimamizi mkuu wa biashara zangu alikuwa mke wangu.
Mwezi wa 7 wakati wa likizo ya Corona mke wangu alisafiri kwenda nyumbani kusalimia.

Nikawa nasimamia mimi mwenyewe.

Shule zikafunguliwa huku mke wangu akiwa bado hajarudi.
Hapo ndipo hali ilianza kuwa tofauti.

Wafanyakazi wakaamua kutumia hiyo nafasi kuniumiza kwa kushirikiana na mtu wangu wa karibu, ambaye kwangu alikuwa kama ndugu na rafiki.

Aliwashawishi wafanyakazi wangu pasipo mimi kujua.
Kwanza ikatokea hasara kubwa, hadi biashara ikayumba, kisha kwa pamoja wakaomba wote kuacha kazi. Kabla sijajua cha kufanya nikamwambia mke wangu awahi kurudi.
Kwa huo muda nikaamua nifunge ili kumngoja mke wangu.

Gafla nikapokea simu kutoka kwa mwenye fremu akisema anataka abadilishie matumizi ya sehemu hiyo hivyo natakiwa nihamishe biashara zangu na atanilipa gharama zangu za usumbufu.
Nikaamua kutoa vitu vyangu, kumbe yule jamaa yangu kanizunguka.

Niliporudi kufuatilia gharama zangu, nikamkuta nae kafungua biashara Kama zile zangu, na wafanyakazi wangu wote amewaajiri.

Sikufanya chochote, kumbe walishirikiana na mwenye fremu pia.
Sasa kibaya kabisa kinachoniuma, nilitoka kuchukua mkopo mwezi wa tano, nikaiweka kwenye biashara. Na sasa biashara imesimama.

Nilijipa muda sana wa kutomshirikisha mtu hiki kitu, ila sasa nimeona nashindwa kulihimili, akili yangu sasa hivi siielewi, inanipa mawazo mabaya.
Nifanye nini? nianzie wapi? kila mahesabu nayopiga yanakataa, nalipaje mkopo? kila nikifikilia kichwa kinauma kwa mawazo. Kahama.
#WatuNiStory

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with WatuNiStory

WatuNiStory Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @watunistory

Mar 26, 2022
"Harakati za shule na kusoma nikajikuta nimepangiwa shule moja huko Mtwara inaitwa Ndanda.

Kiukweli nilikuwa sijawahi kufika na sijui kabisa tamaduni za watu wa kule. Nikasema Tanzania ni moja hakuna sehemu nitashindwa kuishi,
hivyo mwanaume nikajipanga tayari kwenda kuanza safari ya masomo huko.

Kumbuka ile likizo ya kusubiri matokeo ya kwenda kidato cha tano, nilikuwa mtu shamba. Yaani nilipiga sana jembe na kazi nzito kusaidia mishe za home. Hivyo nilikuwa nakula saaana.
Sasa kufika shule, nakuta dishi la msosi yaani ugali ambao ningeweza kumaliza mimi na dada yangu, tunakula wanaume kama saba.

Hili lilinitesa sana aisee kipindi cha kwanza. Nakumbuka ilipita miezi kama mitatu mwanaume sijawahi kushiba.
Read 5 tweets
Mar 8, 2022
"Ipo hivi, mimi ni kijana wa miaka 25, nilikuwa na mpenzi wangu ana mtoto sio wangu. Kipindi nipo nae nilikuwa sina kazi na tulikuwa tumepanga tunaishi pamoja lakini yeye alikuwa na kazi. Sasa hakutaka kubeba mimba yangu akihofia hali ngumu ya maisha ambayo ninapitia.
Kile kitendo kikaniumiza sana, nikaja Dar kutafuta maisha, ikawa kila baada ya miezi mitatu narudi nyumbani kumtembelea.

Sasa mwezi wa tisa nikashindwa kwenda kwa wakati, lakini tulikubaliana kwakuwa mkataba ulikuwa karibu kuisha, nimalizie mkataba ndio niende nyumbani.
Kweli, nikaenda mwezi wa 12 ila cha ajabu namkuta na mimba ya mwezi na ananieleza kuwa aliempa mimba hakuwa na mahusiano nae na hamtaki tena.

Kwa hasira nikaondoka, nikamwacha. Ety katoa mimba ananiomba msamahe na turudiane.
Read 4 tweets
Mar 7, 2022
"Ilikuwa Jumapili weekend moja nimekaa ghetto kwangu nimefulia mbaya. Simu yangu inaita, kucheck alikuwa mwanangu.

Kupokea ananiambia ana msala inabidi nimsaidie kuu-solve. Inakuaje? nikauliza. Image
Ndio ananiambia amempa mimba binti wa kidato cha nne hivyo anaomba aje kwangu kufanya harakati za kuitoa. Ashaongea na dokta, na dogo yupo tayari bado eneo la tukio tu sababu hawawezi kufanyia hospital.

Daah!nikicheck ni mwanangu sana. Na kwao ana mke na mtoto.
Nikaona sio mbaya nilibebe hili nimsaidie mshkaji. Nikamwabia njoo haina noma.

Walipofika ikabidi niwapishe wafanye yao. Nikakaa zangu nje.

Nikiwa na mawazo mengi na dakika nyingi kupita, mshkaji anakuja kunishtua dogo amezima. Haelewi anayeingia wala anayetoka.
Read 10 tweets
Mar 5, 2022
"Ipo hivi mimi ni kijana wa miaka 28 sasa.

Nilipokua chuo mwaka 2018 nikisomea course ya IT nilibahatika kupata mdada ambaye niliishi nae kama mchumba na kumpa mahitaji yote na tulikubaliana tuzae. Image
Basi nikampa kweli ujauzito huku nikimhudumia kwa kila kitu bila wazazi wangu kujua na hakuwahi kukosa kitu alichohitaji kwangu japo sikuwahi kuomba msaada kwa mtu, ila niliendeleza life langu kwa mishe zangu za kitaani(kwa wanaoelewa IT huwa hatukosi mishe za hapa na pale).
Ilipofika mwezi mmoja na nusu kabla ya binti kujifungua alisema anaenda jifungulia nyumbani.

Sikumkataza kwa vile na mimi niliona sitaweza ghaili masomo nisaidie malezi. Hivyo nikamruhusu aende na kumpatia vitu vyote muhimu alivyohitaji kwa ajili ya safari na mambo mengine.
Read 7 tweets
Dec 29, 2021
"Kuna demu mmoja nina urafiki nae kiasi kwamba binafsi nikiwa na shida yoyote ananisaidia. Mara nyingi huwa anakuja home hata nguo zangu huwa anafua na usafi anafanya. Chochote nitakachomwambia anafanya.
Alishaniweka wazi kuwa ana ngoma na mambo yake yote huwa hanifichi hata awe na mahusiano basi ataniweka wazi kwa kila kitu hata akalale na huyo mwanaume.

Tatizo linakuja sehemu moja, hatujawahi kuongelea swala la kuwa na mahusiano. Mimi na yeye huwa ni stori za kawaida tu.
Mimi nina mahusiano na demu mwingine na anamfahamu hata nikikosana na demu wangu anakuwa wa kwanza kutusuluhisha. Alishawahi kuolewa wakaachana na mume wake kisa huyo mwanaume alimwambia aache mazoea na mimi akakataa.
Read 10 tweets
Dec 28, 2021
"Miaka kadhaa iliyopita Vijana mtaani kwetu waligundua kuwa Kuna mama huwa anaacha wazi madirisha ya nyumba yake pindi akiwa anabadilisha nguo. Ni mama mgeni ambae alikua kahamia miezi michache tu iliyopita.
Alikua akifanya hivyo kila siku mida ya saa moja na nusu usiku akitoka kuoga.

Yule mama MashaAllah alijaliwa shape. Yani alikua na shape moja ya ukorofi sana. Alienda hewani.. huko nyuma ni kama pembe la ng'ombe tuu.. halifichiki.. hatari sana.
Basi Vijana ndo ukawa mchezo wao.. Taarifa ziliponifikia nikawa natamani nikamwambie yule mama kuna raia wanamla chabo maana alikua ni jirani yangu na ananifahamu vizuri tunaheshimiana halafu alikua mwalimu wa shule ya msingi.
Read 9 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(