Habibu B. Anga Profile picture
Mar 22, 2021 20 tweets 4 min read Read on X
JIHADI JOHN: MCHINJAJI WA ISIS MIKONONI MWA WANAUSALAMA WA TANZANIA

PART 4 (HITIMISHO)

Kwa hiyo wakafanya uchambuzi wote ule kuunda "profile" ya mtu wanayemtafuta.
Kisha wakachukua hii profile na kuoanisha na orodha ya watu ambao kwa muda mrefu MI5 wamekuwa wanawashuku... Image
kujihusisha na mavuguvugu ya kigaidi.
Yaani wanaangalia kwamba kwenye watu ambao siku za nyuma wamekuwa wakiwalia rada pale London, ni nani ambaye ana-fit kwenye hii profile waliyotengeneza kuhusu yule mchinjaji wa ISIS anayeitikisa dunia.

Baada ya kufanya uoanishaji huu..
wakafikia conclusion kwamba mchinjaji wa ISIS ambaye alikuwa anaitikisa dunia alikuwa ni mtu anayeitwa Abdel Bary
Huyu Abdel alikuwa ni maarufu sana hapo London, kwa sababu alikuwa ni mwanamuziki wa Hip-hop anayechipukia kwa kasi sana akitumia jinan kisanii "L Jinny"

Hata kwenye
mtandao wa Youtube video zake za muziki zilikuwa zinapata mamilioni ya views.

Lakini mwishoni mwa mwaka 2012, Abdel Bary akapotea kusikojulikana na taarifa za kishushushu zilikuwa zinaonyesha kwamba alikwenda nchini Syria kujiunga na kikundi cha Daesh.

Ilikuwa ni almanusura..
serikali za Uingereza na Marekani watangaze kwa ulimwengu identity ya yule 'chinja chinja' anayejifunika manguo meusi kwamba ni Abdel Bary, lakini wakapata 'clue' mpya ambayo ikawafanya watafakari upya kama kweli Abdel ndiye yule mchinjaji.

Kuna baadhi ya watu waliochukuliwa...
mateka na ISIS walikuwa wameokolewa.

Mateka hao walitoa intelijensia muhimu sana.
Walisema kwamba mateka wote wa kimagharibi waliotekwa na ISIS kwenye jela yao walikuwa wanalindwa na wapiganaji wa ISIS wanne ambao wote wanaongea kingereza chenye lafudhi ya Uingereza...
Mateka hao wakawabatiza jina wapiganaji hao wanne wa ISIS na walikuwa wanawaita "The Beatles" (kikundi maarufu cha muziki toka Uingereza kilichotamba mno miaka ya sitini).

Kwa hivyo mateka waliwabatiza majina wapiganaji hao wa ISIS kila mmoja walimpa jina la mwanakikundi cha...
The Beatles (John, Paul, George na Ringo).

Mateka hao wakaeleza kwamba yule somo mchinjaji anayeonekana kwenye video mateka walikuwa wanamuita "John".

(Ndipo hapo vyombo vya habari wakalidaka jina hilo na kuliboresha kumuita yule mchinjaji "Jihadi John")

Mateka wale pia...
wakatoa clue muhimu sana ambayo ndio ilifanya serikali za Uingereza na Marekani wahisi Jihadi John hakuwa Abdel Bary kama walivyodhani.

Mateka walisema kwamba, yule mchinjaji, Jihadi John licha ya kwamba alikuwa mpiganaji wa ISIS lakini alikuwa na 'obsession' kubwa na Al-Shabaab
Alikuwa mara nyingi akiwalazimisha mateka kutazama video za Al-Shabaab. Alikuwa mara kadhaa akiwasimulia mikiki mikiki ya Al-Shabaab.

Sasa, kwa intelijensia ambayo MI5 walikuwa wanayo ilikuwa haionyeshi kwa namna yeyote kama Abdel Bary alikuwa na mahaba hayo mazito na Al-Shabaab
Bali yuko mtu mwingine waliyewahi kumlia rada, tena mkazi wa London, ambaye si tu kwamba alikuwa na mahaba na Al-Shabaab bali aliwahi kujaribu kabisa kujiunga nao. Lakini kwa kushirikiana na idara ya ujasusi ya Tanzania wakatibua mpango huo.

Umeshamjua.?

Naam, Mohammed Emwazi.
Mohammed Emwazi ndiye alikuwa ana-fit hii profile ya kuwa na obsession na Al-Shabaab.

Wakachukua taarifa za kimo cha Emwazi, Kilo, mjengeko wa mwili, tone ya ngozi.. kila kitu kilikuwa kinamatch profile waliyoitengeneza awali.

Hawakuishia hapo. Wakachukua sauti za hotuba ambazo
mchinjaji huwa anazitoa kabla ya kuchinja wale mateka wake. Wakazichuja vyema hizo audio kisha wakamwita mama yake Emwazi asikilize. Mama Mohammed Emwazi aka-confirm kwamba hiyo ni sauti ya mwanaye Mohammed.

Kwa hiyo, sasa kwa 100% walikuwa wameng'amua yule mchinjaji alikuwa ni Image
Mohammed Emwazi.

Emwazi ambaye miaka kadhaa nyuma tu tulimsekwa selo pale kituo cha Polisi Stakishari Ukonga.
Emwazi ambaye alituomba karibia alie machozi tumruhusu aingie nchini Tanzania.

Kumbe.. kumbe..

Kumbe kama tungelimuacha siku ile aingie nchini, kisha akafanikiwa...
kwenda Somalia kujiunga na Al-Shabaab. Ule ubunifu wake wa kikatili wa kuchinja watu angekuwa anaufanya hapa Afrika.. angekuwa anawakata shingo wanajeshi wetu. Angekuwa anautetemesha ulimwengu kutokea hapa tu sebuleni kwetu.. Somalia.

Kwa umombo twasema "..we dodged a bullet.."
Baada ya CIA, MI6 na Mossad kumtambua yule mchinjaji kuwa ni Mohammed Emwazi wakaanza sasa kukusanya intelijesia kumuhusu.

Wakaanza kutazama 'topography' na landscape ya maeneo anayochinjia watu na kuoanisha na mwenendo wa vikosi vya ISIS ardhini.

Wakakusanya intelijensia ya...
Kutosha kwa mwaka mzima mpaka wakaja kujua mahala gani ambapo atakuwa kwenye siku fulani mahususi.

Pasipokujua kwamba CIA wamekwisha hesabu hatua zake na wamejua nyendo zake, siku hiyo Jihadi John na msafara wake walikuwa kwenye mji wa Raqqa nchini Syaria.

Jihadi John akiwa..
anatoka kwenye nyumba aliyofikia kuingia kwenye gari iliyokuwa inamsubiri nje.. Drone ya jeshi la Marekani ikafyatua kombora na kusambaratisha gari, Jihadi John na watu wote waliokuwepo kwenye msafara

Hiyo ilikuwa ni siku ya tarehe 12 November 2015.

Kesho yake, Pentagon wakatoa
taarifa kwa vyombo vya habari juu ya shambulio la mafanikio la kumuua Jihadi John. Mchinjaji wa ISIS aliyeutikisa ulimwengu na kupanda hofu kwa kila mtu ulimwenguni.
Jitu la maguo meusi ambaye aligeuka kufanyika kama nembo ya ISIS na ukatili.

Miezi miwili baadae ISIS kupitia.. Image
jarida lao la Dabiq walitoa taarifa juu ya kifo cha Mohammed Emwazi na kwa mara ya kwanza wakaweka picha yake sura ikiwa wazi na amevalia mavazi nadhifu.

Na huo ndio ulikuwa mwisho wa Jihadi John Mchinjaji.

Tukutane tena kwenye simulizi nyingine hapa hapa.

- Habibu B. Anga

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Habibu B. Anga

Habibu B. Anga Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @habibu_anga

May 15
TISS| MAPINDUZI| MTIHANI MKUU WA KIKWETE

Mwaka wa mwisho wa utawala wa Kikwete ulikuwa ni mgumu kuliko umma unavyofahamu.

Alikuwa anapambana na mpasuko ndani ya chama, kushamiri kwa upinzani… lakini zito zaidi ilikuwa ni changamoto iliyotokea siku ya 13 May 2015.

Thread… Image
Hii picha hapa chini ni picha halisi ikimuonyesha Mkurugenzi wa Idara ya Ujasusi Tanzania kipindi kile Bw. Othman Rashid akifanya suala ambalo si la kawaida na hatukuwahi kuliona hapo kabla kwa Mkurugenzi Mkuu wa TISS kufanya jukumu la ‘VIP Protection’

(Niliyemzungushia duara) Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa - TISS, akiongoza msafara wa wa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza toka Hoteli ya Serena, Dar es Salaam
Pichani DGIS Othman alikuwa anamuongoza Rais Nkurunziza na msafara wake kuwaondoa kwa dharura toka Serena Hotel kuwapeleka uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere.

Siku hii 13 May 2015 ilikuwa moja ya siku mbaya sana katika ulingo wa usalama, ujasusi na diplomasia ya Afrika Mashariki
Read 25 tweets
Mar 25, 2023
Ukitaka kuelewa chanzo cha vita ya Ukraine basi unapaswa kufahamu mkasa wa huyu unaye muona pichani na Zitto… anaitwa Victor Yushchenko

Miaka kadhaa iliyopita huyu somo alikumbwa na kadhia ya kulishwa sumu na kupata madhara kama yale ambayo yalimkuta Dr. Mwakyembe..

Thread..
enzi zile za Richmond na Dowans mpaka akapelekwa India kutibiwa.
Ngozi ya mwili yote iliharibika na kuanza kupukutika kama unga

Huyu Yuschenko yeye kadhia hii ilimtokea mwaka 2004 kipindi hicho akiwa anagombea Urais wa Ukraine
Yushchenko alikuwa anachuana mwanasiasa Yanukovych..
ambaye alikuwa ni Waziri Mkuu wa serikali ambayo ilikuwa inamaliza muda wake

Uchaguzi huu wa Ukraine kwa kiasi kikubwa ulikuwa ni mchuano wa kiushawishi kati Marekani na Urusi wakitunishiana misuli.
Marekani walikuwa wanamuunga mkono huyu somo pichani Bw. Yushchenko wakati Urusi
Read 24 tweets
Aug 18, 2022
Roman Abramovich: Utajiri wa Damu Mpaka Kumuingiza Ikulu Putin

Thread,

Namna ambavyo mtoto yatima aliyelelewa katka umaskini ameweza kuibuka moja ya binadamu wenye ukwasi mkubwa duniani na mpaka kuweza kumuingiza Ikulu Vladmir Putin ni mkasa wa aina yake…

(Usisahu ku-Retweet) Image
Wazazi wake wote wawili licha ya kuishi maisha yao yote nchini Russian lakini asili yao ni Waisrael. Mama yake aliitwa Irina na alifariki kipindi Roman bado angali mchanga kabisa wakati baba yake ambaye aliitwa Arkady alifariki kwa ajali ya gari miaka michache baadae Roman akiwa
bado mtoto mdogo kabisa.

Hii ndio ilikuwa sababu ya Roman kwenda kulelewa kwa ndugu zake Komi kaskazini mwa Urusi ambako kuna baridi kali na umasikini uliokithiri

Ujanani mwake, Roman aliwahi kujiunga na jeshi kabla ya kuacha na kuamua kwenda Moscow kutafuta maisha
Akiwa Moscow
Read 23 tweets
Dec 21, 2021
TUMEWAHI KUWA NA CHANJO KWA MALENGO YA KISHUSHUSHU

Thread..

Kadiri ulimwengu unavyobadilika, stadi ya Ujasusi inazidi kuwa complex kwa kuhusisha mbinu ambazo nyingine ukizisikia unaweza kudhani labda watazama sinema au waota, lakini ndio uhalisia wa ulimwengu ulipo sasa katika
katika juhudi za mataifa na makampuni makubwa kupanua ushawishi wao juu ya dunia yote na kulinda maslahi.

Kuna kisa cha tofauti sana ningependa nikijadili leo hii. Kisa cha tofauti kabisa..

Wengi tutakuwa tumewahi kusikia shirika linaloitwa “Save the Children”. Ni moja ya…
Shirila kubwa zaidi la misaada ya kibinadamu ulimwenguni ambalo limejikita hasa kwenye kutoa misaada inayolenga kuboresha hali za maisha ya watoto wadogo.

Mwaka 2011 shirika hili lilikuwa kwenye shughuli zake mahala paitwa Khyber nchini Pakistan.
Save the Children walikuwa na…
Read 43 tweets
Oct 14, 2021
𝗕𝗜𝗡𝗧𝗜 𝗝𝗔𝗦𝗨𝗦𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗜𝗔𝗞𝗔 25 𝗔𝗡𝗔𝗬𝗘𝗜𝗧𝗜𝗞𝗜𝗦𝗔 𝗔𝗙𝗥𝗜𝗞𝗔 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗔𝗥𝗜𝗞𝗜

Thread..

Siku ya 30 May 2019, maafisa Usalama Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JKIA, Nairobi walimuweka kizuizini abiria mmoja mwenye hati ya kusafiria ya kidiplomasia, mwanaume.. Image
wa asili ya kisomali. Japokuwa watu wenye diplomatic passport wapata exemptions kadhaa kwenye kaguzi za uwanja wa ndege, lakini ilikuwa ni lazima kwa maafisa hawa kumuhoji abiria huyu kutokana na utata wa mzigo ambao alikuwa nao.

Huyu somo alikuwa na briefcase ambalo ndani yake
alikuwa amebeba fedha cash dola za Kimarekani milioni moja na nusu.

Mtu huyu nyaraka zake zilikuwa zinaonyesha kwamba alikuwa safarini kuelekea nchini Ethiopia.

Maafisa hawa wa Usalama. Wakaanza kumuhoji abiria huyu sababu za kusafiri na kiwango kikubwa hivyo cha fedha na pia.. Image
Read 98 tweets
Sep 4, 2021
𝗞𝗔𝗕𝗟𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗞𝗨𝗟𝗨.. 𝗞𝗪𝗔𝗡𝗭𝗔 𝗔𝗗𝗛𝗔𝗕𝗨 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗙𝗢

Thread..

Ukiwa unatoka Lusaka kwenda Jimbo la Magharibi, kabla hujaingia mji wa Mongu kuna kipande cha barabara kinajulikana kama Limulunga Road.
Kipande hiki cha barabara mwaka juzi kimetupa tukio la kipekee Image
ambalo kwa kiwango kikubwa tukio hili limebadili mwelekeo wa siasa la bara zima la Afrika na hasa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara.

Pengine pasipo tukio hili huyu Hichilema tunayemuona leo asingelikuwa Rais. Lilikuwa tukio la kipekee kabisa..

Kila mwaka pale Zambia huwa wana
sherehe maarufu zinaitwa "Kuomboka Ceremony".
Wenzetu mpaka leo hii bado wanatambua cheo cha asili cha "Litunga" ambaye ni Mfalme wa kabila la Walozi.
Kila mwaka mwishoni mwa msimu wa mvua mfalme huwa anahama kutoka makazi yake ya bondeni ya Lealui na kuhamia makazi yake yaliyo..
Read 41 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(