Habibu B. Anga Profile picture
Apr 11, 2021 25 tweets 5 min read Read on X
MTANZANIA #1: JASUSI WA KUKODI, UJASUSI WA BIASHARA

Thread..

Si rahisi kuwa mahususi sana ni mwaka gani, lakini tunakadiria kwamba katikati ya miaka ya tisini hivi Mtanzania ambaye kwa sasa nimtaje kwa jina lake moja tu la Matiko aliondoka jiji Dar kwenda nchini Afrika Kusini Image
Kwa ajili ya kutafuta maisha. Lakini tofauti na Watanzania wengi wanaozamia SA ambako wakifika uanza kwa kufanya shughuli za hali ya chini, ilikuwa tofauti kabisa na bwana Matiko ambaye aliingia SA akiwa na mtaji wa kuridhisha kutokana na fedha ambazo alizipata toka kwenye mauzo
ya sehemu ya shamba lake la karibia Ekari 300 zilizoko kijiji cha Ghesaria Wilayani Serengeti.

Matiko akatumia mtaji huo akiwa hapo SA kuanzisha biashara ndogo ndogo
Moja ya biashara aliyoanzisha ambayo ilipanda mbegu ya kumbadilisha Matiko na kumfanya aingie kwenye ulimwengu wa
Ujasusi wa Kibiashara ilikuwa ni kampuni ndogo ya promotion aliyofungua iliyoitwa 80th Punch
Wahenga kama mie mnakumbuka kwamba hakujawahi kutokea nyakati bora kwa mchezo wa ngumi kama miaka ya tisini. Mapambano ya ngumi yalikuwa na msisimko na umaarufu kuzidi hata mechi za mpira
wa miguu.

Matiko hakutaka upepo huu umpite. Akaanzisha kampuni hiyo ndogo ili kuandaa mapambano ya ngumi pale Afrika Kusini

Mwaka 1999 kuna fursa adhimu sna ilijitokeza ambayo karbia kila mtu hakuiona
Mwaka ule lilifanyika moja ya pambano maarufu zaidi kuwahi kutoke. Pambajo la Image
ndondi kati ya Evender Holyfield vs Lennox Lewis. Pambano ambalo lilisha kwa majaji kutoa uamuzi unahosehabika wa hovyo zaidi kwenye historia ya ndondi, majaji hao wakisema matokeo ni Sare ingali ikiwa wazi kabisa Lennox Lewis alishinda pambano

Ulimwengu wote ulilpuka kwa hasira
watu wakitaka pambano lirudiwe na yatolewe maamuzi ya haki. Uhalali wa bodi zinazosimamia mchezo wa ngumi duniani ulikuwa uko rehani kwa kuonekana ni wala rushwa

Matiko akaona fursa. Na hii ilikuwa ni deal yake ya kwanza kubwa kabisa.

Nimesema huyu bwana alikuwa na kampuni yake
inaitwa 80th Punch inayoandaa mapambano ya ngumi. Hiki kikampuni chake kilikuwa kidogo cha mtaani. Hata kilikuwa hakijulikani wala hakina hadhi kubwa

Lakini akaona fursa.

Kipindi hicho Nelson Mandela alikuwa lulu ya dunia na ndio ametoka kupewa tuzo ya Nobel.
Nelson Mandela pia
alikuwa na NGO ya Nelson Mandela Foundation.
Mandela pia anajulikana alikuwa ni shabiki mkubwa haswa, shabiki kindakindani wa mchezo wa ndondi.

Matiko akamfuata Mkurugenzi Mtendaji wa Nelson Mandela Foundation. Akamweleza kwamba ana wazo adhimu.

Wazo lake lilikuwa kwamba..
Kwa kuwa ulimwengu mzima unapiga kelele kwamba lifanyike pambano la marudiano kati ya Evander na Lewis na haki safari hiyo itendeke wao kama Mandela Foundation wanaweza kutumia fursa hiyo.
Akamweleza kwamba ulimwengu ulikuwa hauna imani tena na vyombo vinavyosimamia mchezo huo.. Image
Kwa hiyo Mandela Foundation waandae ‘mkanda’ wao wa ubingwa wa uzito wa juu. Kisha watumie ushawishi wa Madiba kuandaa pambano la marudiano.

Na pambano lisihusishe chama chochote cha ngumi duniani kwa kuwa watu hawana imani navyo tena, bali lisimamiwe 100% na Mandela Foundation
Kampuni yake yeye ya promotion (yaani 80th Punch) watalipwa commission tu ya kuandaa pambano.Mapato mengine yote yatakwenda kwa Mandela Foundation.

Mkurugenzi wa Mandela Foundation akalipenda hili wazo. Akalipeleka kwa Mzee Mandela. Mandela naye akalipenda wazo.

Watu wa Mandela
Wakakaa na Matiko kuandaa proposal ya kupeleka kwa Lennox Lewis na Evender Holyfield.

Wakaandaa na design ya mkanda utakaoshindaniwa. Mkanda utapambwa na vito vya thamani tofauti tofauti vya thamani ya dola milioni 3.Katikati ya mkanda kutakuwa na picha ya Mandela

Walipo maliza
Kuandaa hii proposal wakaipeleka Wizara ya Michezo ipewe baraka. Wizara ikakubali.

Kwa hiyo ikaandaliwa barua maalumu ambayo iliambatanishwa na ile proposal. Barua hii ilikuwa na signatures za Waziri wa Michezo na Katibu wa Rais (Rais alikuwa ni Mandela mwenyewe).

Baada ya hapo
Matiko akiwa kama Mkurugenzi wa 80th Punch ambao walikusudiwa kuwa waandaaji wa hilo pambano, akasafiri kwenda London kuonana na Meneja wa Lennox Lewis aliyeitwa Panos Eliades.

Menejiment ya Lennox wakalipenda wazo na kukubali.
Kama wakumbuka mwaka huo 1999 mwezi March, Lennox..
Lewis akafanya mkutano na wanahabri akiwa begani amebeba mkanda ambao katikati una sura ya Mandela. Akatangaza kutaka rematch na Evander na pambano hilo lifanyike Afrika Kusini na lisimamiwe na Mandela Foundation.
Press ile maarufu ya Lennox waafrika wengi tuliifurahia, kwamba...
hatimaye pambano la ngumi la kihistoria linakuja kufanyika kwenye ardhi yetu

Lakini menejiment ya Evander Holyfield lilikataa ile proposal. Na baada ya majadiliano ya menejiment ya mabondia hawa wawili,pambano lilikwenda kufanyika Las Vegas Marekani bila kuwahusisha Mandela wala
Matiko na 80th Punch yake.

Sasa,

Japo dili hii ilifeli, lakini ilipanda mbegu ndani ya Matiko. Kitendo cha kuishawishi serikali nzima ya Nelson Mandela, na menejimenti ya moja ya bondia mashuhuri kuwahi kutokea, kukubali wazo lake.. ilikuwa ni hatua kubwa ambayo ilimbadili..
Matiko kutoka kuwa promoter mganga njaa pale SA na kugeuka kuwa jasusi bora wa kibiashara barani Afrika.Akawa mtu ambaye anaweza kukupatia kitu chochote, au dili lolote alimradi tu uwe na uwezo wa kumudu fee yake.
Karibia kila madili makubwa makubwa unayoyaona kati ya serikali..
na kampuni binafsi, kuna mkono wa Matiko (nitasimulia deals kadhaa na uhusika wa Matiko)

Huyu Matiko nina imani wengi mmewahi kumsikia. Majina yake kamili ni Moto Matiko Mabanga.. au maarufu kama Moto Mabanga.

Kwa ambao mmewahi kumsikia lazima mtashangaa nilivyosema kwamba huyu Image
somo ni Mtanzania. Wengine watasema wamewahi kusikia huyu bwana ni Mrundi. Wengine watasema ni Mkongo. Wengine Mzulu na kadhalika.

Swali kama hilo pia limewahi kuulizwa na Jaji Kassim Nyangarika wa Mahakama Kuu ya Tanzania divisheni ya Biashara mwaka 2014. Alimuuliza Matiko...
inakuwaje yeye Mtanzania awe na passport ya Afrika Kusini.??
Moto Mabanga akiongozwa na wakili wake Mabere Marando akajibu kwamba Idara ya Intelijensia ya Afrika Kusini (NIA) walimlazimisha kuchukua passport ya South Africa.

Namna gani? Kwa nini wamlazimishe.? Kwa maslahi gani.?
Niwape mikasa kadhaa kuhusu huyu jasusi wa kibiashara. Mikasa kadhaa ili tuone namna gani biashara kubwa kubwa unazoziona, dili kubwa kubwa.. zina siri nzito na ujasusi mwingi nyuma yake.
Niwasimulie ni namna gani hata vitalu vyetu vya gesi tunavyoringia kule mikoa ya kusini..
Huyu bwana ndiye ambaye ameviuza..ameviuza kwa watu awatakao kana kwamba anauza karanga. Yes, kiuhalisia huyu bwana ndiye ameuza sio serikali yenu

Tuanze na mkasa huu..

Mwezi May 2007 Kampuni ya Vodacom iliingia kwenye moja ya skandali mbaya zaidi kuwahi kuwapata. Mkurugenzi wa
Vodacom na Wajumbe wote wa Bodi walikuwa wamesekwa lupango kwa amri ya mahakama.
Katika kutapatapa kutafuta suluhu ndipo wakaelezwa kwamba yuko mtu mmoja tu hapa barani Afrika mwenye uwezo wa kuwaokoa.. mtu huyo waliambiwa ni Moto Mabanga

Nitaweka PART 2..

Nisaidie Ku-Retweet

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Habibu B. Anga

Habibu B. Anga Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @habibu_anga

Mar 25, 2023
Ukitaka kuelewa chanzo cha vita ya Ukraine basi unapaswa kufahamu mkasa wa huyu unaye muona pichani na Zitto… anaitwa Victor Yushchenko

Miaka kadhaa iliyopita huyu somo alikumbwa na kadhia ya kulishwa sumu na kupata madhara kama yale ambayo yalimkuta Dr. Mwakyembe..

Thread..
enzi zile za Richmond na Dowans mpaka akapelekwa India kutibiwa.
Ngozi ya mwili yote iliharibika na kuanza kupukutika kama unga

Huyu Yuschenko yeye kadhia hii ilimtokea mwaka 2004 kipindi hicho akiwa anagombea Urais wa Ukraine
Yushchenko alikuwa anachuana mwanasiasa Yanukovych..
ambaye alikuwa ni Waziri Mkuu wa serikali ambayo ilikuwa inamaliza muda wake

Uchaguzi huu wa Ukraine kwa kiasi kikubwa ulikuwa ni mchuano wa kiushawishi kati Marekani na Urusi wakitunishiana misuli.
Marekani walikuwa wanamuunga mkono huyu somo pichani Bw. Yushchenko wakati Urusi
Read 24 tweets
Aug 18, 2022
Roman Abramovich: Utajiri wa Damu Mpaka Kumuingiza Ikulu Putin

Thread,

Namna ambavyo mtoto yatima aliyelelewa katka umaskini ameweza kuibuka moja ya binadamu wenye ukwasi mkubwa duniani na mpaka kuweza kumuingiza Ikulu Vladmir Putin ni mkasa wa aina yake…

(Usisahu ku-Retweet) Image
Wazazi wake wote wawili licha ya kuishi maisha yao yote nchini Russian lakini asili yao ni Waisrael. Mama yake aliitwa Irina na alifariki kipindi Roman bado angali mchanga kabisa wakati baba yake ambaye aliitwa Arkady alifariki kwa ajali ya gari miaka michache baadae Roman akiwa
bado mtoto mdogo kabisa.

Hii ndio ilikuwa sababu ya Roman kwenda kulelewa kwa ndugu zake Komi kaskazini mwa Urusi ambako kuna baridi kali na umasikini uliokithiri

Ujanani mwake, Roman aliwahi kujiunga na jeshi kabla ya kuacha na kuamua kwenda Moscow kutafuta maisha
Akiwa Moscow
Read 23 tweets
Dec 21, 2021
TUMEWAHI KUWA NA CHANJO KWA MALENGO YA KISHUSHUSHU

Thread..

Kadiri ulimwengu unavyobadilika, stadi ya Ujasusi inazidi kuwa complex kwa kuhusisha mbinu ambazo nyingine ukizisikia unaweza kudhani labda watazama sinema au waota, lakini ndio uhalisia wa ulimwengu ulipo sasa katika
katika juhudi za mataifa na makampuni makubwa kupanua ushawishi wao juu ya dunia yote na kulinda maslahi.

Kuna kisa cha tofauti sana ningependa nikijadili leo hii. Kisa cha tofauti kabisa..

Wengi tutakuwa tumewahi kusikia shirika linaloitwa “Save the Children”. Ni moja ya…
Shirila kubwa zaidi la misaada ya kibinadamu ulimwenguni ambalo limejikita hasa kwenye kutoa misaada inayolenga kuboresha hali za maisha ya watoto wadogo.

Mwaka 2011 shirika hili lilikuwa kwenye shughuli zake mahala paitwa Khyber nchini Pakistan.
Save the Children walikuwa na…
Read 43 tweets
Oct 14, 2021
𝗕𝗜𝗡𝗧𝗜 𝗝𝗔𝗦𝗨𝗦𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗜𝗔𝗞𝗔 25 𝗔𝗡𝗔𝗬𝗘𝗜𝗧𝗜𝗞𝗜𝗦𝗔 𝗔𝗙𝗥𝗜𝗞𝗔 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗔𝗥𝗜𝗞𝗜

Thread..

Siku ya 30 May 2019, maafisa Usalama Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JKIA, Nairobi walimuweka kizuizini abiria mmoja mwenye hati ya kusafiria ya kidiplomasia, mwanaume.. Image
wa asili ya kisomali. Japokuwa watu wenye diplomatic passport wapata exemptions kadhaa kwenye kaguzi za uwanja wa ndege, lakini ilikuwa ni lazima kwa maafisa hawa kumuhoji abiria huyu kutokana na utata wa mzigo ambao alikuwa nao.

Huyu somo alikuwa na briefcase ambalo ndani yake
alikuwa amebeba fedha cash dola za Kimarekani milioni moja na nusu.

Mtu huyu nyaraka zake zilikuwa zinaonyesha kwamba alikuwa safarini kuelekea nchini Ethiopia.

Maafisa hawa wa Usalama. Wakaanza kumuhoji abiria huyu sababu za kusafiri na kiwango kikubwa hivyo cha fedha na pia.. Image
Read 98 tweets
Sep 4, 2021
𝗞𝗔𝗕𝗟𝗔 𝗬𝗔 𝗜𝗞𝗨𝗟𝗨.. 𝗞𝗪𝗔𝗡𝗭𝗔 𝗔𝗗𝗛𝗔𝗕𝗨 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗙𝗢

Thread..

Ukiwa unatoka Lusaka kwenda Jimbo la Magharibi, kabla hujaingia mji wa Mongu kuna kipande cha barabara kinajulikana kama Limulunga Road.
Kipande hiki cha barabara mwaka juzi kimetupa tukio la kipekee Image
ambalo kwa kiwango kikubwa tukio hili limebadili mwelekeo wa siasa la bara zima la Afrika na hasa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara.

Pengine pasipo tukio hili huyu Hichilema tunayemuona leo asingelikuwa Rais. Lilikuwa tukio la kipekee kabisa..

Kila mwaka pale Zambia huwa wana
sherehe maarufu zinaitwa "Kuomboka Ceremony".
Wenzetu mpaka leo hii bado wanatambua cheo cha asili cha "Litunga" ambaye ni Mfalme wa kabila la Walozi.
Kila mwaka mwishoni mwa msimu wa mvua mfalme huwa anahama kutoka makazi yake ya bondeni ya Lealui na kuhamia makazi yake yaliyo..
Read 41 tweets
Aug 10, 2021
𝗨𝗧𝗔𝗝𝗜𝗥𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗔𝗞𝗔 𝗪𝗔 𝗪𝗔𝗟𝗜𝗡𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗩𝗜𝗢𝗡𝗚𝗢𝗭𝗜

Thread..

Mwaka juzi kwenye hafla ya mapokezi ya ndege kwenye nchi fulani hivi hapa Afrika Mashariki kuna incident ndogo tu ilitokea lakini wengi ikatufikirisha sana.

Dakika chache baada ya Rais wa...
nchi hiyo kumaliza kuongoza hafla hiyo ya mapokezi ya ndege akashuka jukwaani na akianza kuandoka.
Lakini kabla hajakwenda kupanda gari, kama ambavyo ilikuwa ada kwa Rais yule akaelekea upande waliokaa wananchi wake na ili awasalimie.
Na kusalimia huku akaanza jukwaa ambalo...
walikuwa wamekaa wageni VIP.

Wageni wale mashuhuri wakasimama na Rais akawa anapita akiwapa mkono.

Mojawapo ya wageni wale mashuhuri alikuwa ni mfanyabiashara maarufu sana mwenye asili ya kihindi.
Rais alipopita mbele yake, mfabiashara huyu akanyoosha mkono ili asalimiane na...
Read 25 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(