#TOTTechs Profile picture
Jun 22, 2021 19 tweets 7 min read Read on X
DARASA LA CRYPTO:
SEASON 1: UZI/THREAD

MEME COINS/SHITCONS

Meme Coins au Shitcoins unaweza kuziita coins za majitaka au futuhi coins

Ni coins ambazo zimekua zikipendwa sana na watu wa Crypto kwa kuwa zinaweza kukupa faida hata mara 1000 ya mtaji wako kwa muda mfupi. 👇
Meme coins zimeundwa bila kuwa na matumizi yoyote muhimu kasoro kiki inayotokana na Jina la hiyo coin.

Katika msimu huu wa Crypto, shitcoins zimekua zikipatikana sana katika Blockchain inayoitwa Binance Smart Chain (BSC) kupitia website inayoitwa Pancakeswap
na kununua inabidi uwe na salio la coin ya BSC inayoitwa BNB na iwe ndani App ya TrustWallet...utatumia adress ya hiyo coin yako ili kuinunua

Kwa kawaida tumezoea Coin inakua na project fulani ili watu wawekeze.
Sasa hizi MemeCoins hazina project yoyote zaidi ya kupigiwa Kiki
Namna ya kununua Coins itaelezwa zaidi kwenye threads zijazo.

Meme Coins zipo nyingi, baadhi yake ni

Doge Coin
Mona Coin
Shiba Inu
Banano
Cum Rocket
Doge Swap
Safe Moon
Meme Coin kubwa kuliko zote ni Dogecoin na inaongozwa na kiki za tajiri Elon Musk

Dogecoin iliundwa kama utani kwa lengo la kuwatania watu kuwa sikuhizi watu wanaunda coin za kijinga kwahyo yeye ameunda yake inaitwa Dogecoin ikiwa na Picha ya mbwa wa kijapani anaeitwa Shiba Inu
Hii Dogecoin inapanda thamani tu pale inapokuwa inatangazwa na watu kwa lengo la kuwa watakuja kutajirika siku moja

Katika msimu huu wa Soko la Crypto (2021) tumeona hizi futuhi coins zikiingia sokoni kila leo zikiongozwa na Safemoon coin ambayo
walioiunda walikiri kuwa waliiunda bila kujua itatumika kufanyia nini na hawakujua itavuma kama ilivyovuma.

Hizi Meme Coins au Futuhi Coins, zinaweza kukupa faida kubwa ndani ya mda mfupi endapo ukiweza kuzifahamu siri zake na ukazinunua katika msimu wake na muhimu zaidi
ukijua ni muda gani wa kuziuza, Msimu wa Shitcoins huanza baada ya Bitcoin na coins nyingine nzuri kuingiza pesa na waliotajirika kuanza kutambia wenzio hapo ndio wale ambao hatujui kitu kuhusu crypto tunaingia tunakuta hakuna coin za kununua ili tutoboe
...sasa ndio shitcoin zinaundwa kutudanganya kuwa tutatoboa.

Futuhi Coins siku inavyoingia sokoni hua zinanunuliwa haraka na wamiliki na watu wanaitwa 'Whales' au 'Nyangumi' kwa kutumia software maalum zinaitwa 'trading bots' ambazo zinafanya manunuzi haraka kuliko binadamu
zinakuwahi kununua kabla yako

Whales au Manyangumi ni watu wenye pesa nyingi kiasi cha kufanya bei ya Coin ipande haraka kwa muda mfupi..hawa watu hua wanapanga dili na wamiliki wa coins Wakishanunua awali ndio sisi tunakuja kuskia coin fulani ina trend
imeongezeka thamani mara 5 au 10 hapo ndio muda watu wengi tunainunua Tukishainunua inapanda thamani tena kwa kua tupo wengi, ila sasa huu ndio muda wale Manyangumi na wamiliki hua wanauza hizo Coins zao.
Ukichelewa hapo utaambulia hasara kubwa kwa kuwa wakiuza wale wakubwa utapata hasara , njia pekee ya kuzuia hii hasara ni kuipigia promo hiyo coin wenzio wanunue ili bei isishuke...

Kwa kua hiyo coin haina matumizi yoyote ni ngumu mno kuhamasisha watu wainunue..
hivhyo mbinu chafu hutumika mfano kukuambia kuwa utatajirika kwa muda mfupi pale utakaponunua na usiuze(hodl) hadi bei itakapopanda kufika mwezini au "To the moon" .
Mbinu nyingine chafu ni wamiliki walivogundua kuwa wakiweka thamani ya coin iwe na bei ndogo watu ndio watanunua
....zaidi wakiwa na imani kuwa itafika dola $1 au $10 Hivyo Shitcoins hizi hua na bei kama $0.00000001 na kwa kuwa watu hawajui basi hununua wakitegemea kuwa wamewahi ipo siku itafika dola moja watatajirika
Ukweli ni kuwa ukinunua Meme Coin mfano ShibaInu, ili ifike thamani ya $10 inahitaji fedha zote duniani tena uzidishe mara sita , zitumike kuinunue hiyo coin ndo itafika $10
Wengi hawajui haya mambo wanashindwa kujua ni muda gani sahihi wa kuuza hivyo hupata hasara mno
Hizi meme coins hua zina majina yanayovutia wageni wa hili soko na pia zinakuwa na majina yanayofanana au yanayoendana na Coin maarufu.

Pia kuna muda unaweza kuuziwa shitcoin ambayo utashindwa kuiuza pale faida zinapopatikana
kwakuwa wamiliki wanakua wamesepa na pesa zote zilizopo kwenye 'Float' (Liquidity) ya kubadlishia fedha zako
Shitcoins zina faida kubwa mno ila jua muda wa kuingia na wa kutoka, Pia watu wakubwa na ma rolimodo wako wanaweza kulipwa au kukudanganya makusudi ununue hiyo Shitcoin
ili yeye atajirike kwa kua anayo tayari Mara nyingine hata hao watu maarufu hili soko hawalijui watakuhamasisha ununue tu na kwa kua unawaamini unainunua...utaumia ndugu yangu. Usiamini sana watu kwenye cryptocurrency bila kufanya tafiti zako binafsi
TO THE MOOOOOOOOOOOOOOOOOOON!!!!

Imeandaliwa na @NNgailo [ Nicky ] pamoja na @TOTTechs

Cc: @BankOfTanzania
@wizaraMTH
@TanzaniaSA
@ZMuhaji

SOMO 2. TUTAELEZA KUHUSU BITCOIN.

SOMO 3. NAMNA YA KUNUNUA NA KUUZA COINS

STAY TUNED, WEKA NOTIFICATION ON

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with #TOTTechs

#TOTTechs Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @TOTTechs

Sep 23, 2023
SABABU ZINAZOPELEKEA SIMU KULIPUKA.

Hivi karibuni tumeona matukio ya simu kulipuka zikiwemo simu za Oneplus Nord 2, Galaxy Note 7 na
baadhi ya simu ya nyingi zikiwemo simu kutoka kampuni ya iPhone, Oppo, Xiaomi, Vivo, n.k

Powered by #ElimikaWikiendi × @fiidzsocial

UZI MFUPI 👇
Image
Image
Kati ya matukio makubwa ya simu kulipuka ilikuwa ni simu za
Galaxy note 7 hii ilipelekea Samsung kuomba simu hizo zirudishwe kiwandani kwa uchunguzi zaidi.

Matukio ya simu kulipuka yanajirudia kila siku japo kuna makosa ya kiufundi makosa na mtumiaji.

#ElimikaWikiendi
Image
Image
SABABU KWANINI SIMU ZINALIPUKA.

1. Kasoro za utengenezaji.

Moja ya sababu au kasoro inayofanya simu zilipuke ni kutoka kwa watengezaji (kiwandani), Betri ya Lithium-ion ambayo hutumika kwenye smartphone inahitaji kujaribiwa vizuri kabla kusafirishwa.

#ElimikaWikiendi Image
Read 24 tweets
May 30, 2023
Maoni ya busara kwa leo.

Uzi mfupi

• Kama wewe ni Fan/shabiki wa kitu au kampuni flani, unatakiwa ujue kuheshimu mawazo ya watu wengine, unatakiwa ujue kutofautisha kizuri na kibaya, unatakiwa ujue kutofautisha Facts/ukweli na Opinions/maoni.  👇 ImageImageImageImage
• Acha kuhoji na kubeza maamuzi ya watu, ingawa unaweza kutoa maoni yako kuhusu maamuzi yao.

• Unapoibeza kampuni nyingine kwa kufanya kitu, lakini unatetea kampuni unayoipenda kwa kufanya kitu kile kile, hiyo inamaanisha WEWE ndiye tatizo.
• Wakati mtu X anakejeli kikundi cha watu flani, usitarajie hicho kikundi cha watu kusema kitu cha busara kujibu taarifa ya mtu X.

• Unapomwambia mtu jambo la hovyo/ajabu usitegemee kukuheshimu au kupata majibu ya heshima kutoka kwake
Read 10 tweets
Dec 18, 2021
Wakati huu tunapo kwenda likizo za sikukuu za Christmas na mwaka mpya, huwa ni muda mzuri kukaa na familia zetu, ndugu, jamaa na marafiki kutafakari mwaka ulivyokuwa na kujiandaa na mwaka unaofuata.

#ElimikaWikiendi

STADI/SKILLS ZA MUHIMU KUJIFUNZA

UZI [THREAD] 👇
Pia ni kipindi ambacho watu wengi hupendelea kuwepo mitandaoni. Wakati unatumia mitandao ni vyema ukapata ujuzi mpya wa namna unaweza faidika na mitandao.

Tutakuelezea baadhi ya ujuzi wa mtandaoni unaoweza kuwa na faida kwako kwa namna moja ama nyingine.

#ElimikaWikiendi
ONLINE SHOPPING

huu ni ununuzi wa bidhaa na huduma mtandaoni bila ya wewe kuwepo katika duka au biashara husika kimwili.

Ni rahisi sana kujifunza namna ya kununua vitu mtandaoni kutoka sehemu yoyote ile Duniani na malipo hufanyika kwa njia ya mtandao.

#ElimikaWikiendi
Read 18 tweets
Aug 21, 2021
ARTIFICIAL INTELLIGENCE (AI) [ AKILI BANDIA ]

Akili Bandia (AI) hii ni Teknolojia inayozipatia mashine uwezo wa akili ya kibinadamu ili kuweza kufikiria na kutenda matendo kama kibinadamu.

Je, hizi AI zikoje na zianatumika wapi?

THREAD [ UZI ] 👇

#ElimikaWikiendi
Watu wengi wakiona neno AI ( Artificial Intelligence) hufikiria moja kwa moja ni roboti. Ili iwe AI inahitaji Software(Program endeshi) na Hardware. Software ndio kama ubongo unahitaji kupachikwa data ambazo zitakuwa zinatoka command/maelekezo kwenye hardware.

#ElimikaWikiendi
AI ina jifunza (learning), Fikiri (reasoning) na mtazamo (perception). Ndivyo hivyo sehemu ya akili ya binadamu inafanya kazi. Kwa miaka ya sasa hii Teknolojia inakuwa kwa kasi sana.

Imefikia hatua wataalamu wanataka AI iwe na uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi kama mwanadamu,
Read 23 tweets
Aug 7, 2021
BITCOIN, BLOCKCHAIN AND CRYPTOCURRENCIES

Turudi nyuma mwaka 2008, Bwana mmoja aitwaye Santoshi Nakamoto mtaalamu wa Computer na Hesabu alitengeneza Program na kuiita jina la BITCOIN

Je, Bitcoins ni nini na zinafanyaje kazi ?

Twende na uzi 👇

#ElimikaWikiendi
Bitcoin ni toleo la pesa taslimu ya ki-mtandao ( peer-to-peer version of electronic cash ) ambayo unaweza kutuma moja kwa moja kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine pasipo kupitia taasisi za fedha kama benki, Mobile money etc, unahitaji kuwa na internet tu

#ElimikaWikiendi
Kitu muhimu kwenye Bitcoin huwezi kugushi/forge, miamala fake haiwezi kufanyika, siyo lazima uwe na kitambulisho cha Taifa ( National ID) wala Bank account, Bitcoin iko decentralized ( imegawanyika ), mwamala ukifanyika hauwezi kubadilishwa na ina ulinzi sana

#ElimikaWikiendi
Read 25 tweets
Aug 1, 2021
VITU VYA KUZINGATIA KABLA YA KUNUNUA MacBook

Je! Unampango wa kununua MacBook mpya? Kabla ya kufanya ununuzi unahitaji kuielewa MacBook.

Aina nyingi za MacBook zinapatikana sokoni. Tutakusaidia kununua MacBook bora kulingana na mahitaji yako

Uzi mfupi 👇
Kabla ya kufanya ununuzi wowote angalia toleo la MacBook ambalo utaenda kununua. Kila Mwaka Apple hutoa toleo jipya la MacBook, unaweza kutembelea Apple’s official website, news, na social media kujua mda ambao Apple watatoa toleo Jipya
AINA ZA MacBook:

Kuna aina mbili za MacBook, MacBook Pro na MacBook Air: MacBook Air ni Nyembamba, nyepesi na ni rahisi kusafiri nayo wakati MacBook Pro ni nene kidogo.

Zote ni nzuri lakini zina utofauti sana kwenye Miundo ya ndani ( Internal Architecture & Specs)
Read 11 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(