Habibu B. Anga Profile picture
Jul 15, 2021 β€’ 19 tweets β€’ 4 min read β€’ Read on X
π— π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—” #1: π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—žπ—’π——π—œ, π—¨π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π—•π—œπ—”π—¦π—›π—”π—₯𝗔

#7

Majukumu wakuu, mniwie radhi.

Tuendelee,

Mara ya mwisho nilisema, kuna Mtanzania ambaye mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu alidai kwamba alinyang'anywa passport na Idara ya Intelijensia Image
na kisha kupewa Hati ya Kusafiria ya nchi ya Afrika Kusini

Nikaeleza kwamba mtu huyu ambaye alikwenda Afrika Kusini kutafuta maisha mwanzoni mwa miaka ya tisini, mojawapo ya harakati zake kubwa za kwanza ni pale alipomshawishi Nelson Mandela na taasisi yake ya Mandela Foundation
kutuma ombi la kuandaa pambano la masumbwi la marudiano kati ya Evender Holyfield Vs Lennox Lewis yeye akiwa kama 'promota'.

Pia nikaeleza namna gani ambavyo kampuni ya Vodacom walimdondokea kumuomba awasaidie kuwatoa korokoroni wajumbe wao wa Bodi ya Wakurugenzi nchini Congo...
na pia kumaliza mgogoro wao na serikali ya Rais Kabila.

Nikaeleza pia kuhusu mkasa wa huduma ya "Please Call Me" ambayo kijana Nkosana Makate alikuwa anawashutumu Vodacom kwa kutumia wazo lake bila kumlipa.

Kwenye kuchimba skandali hiyo, ikatufikisha mpaka hapa Tanzania ambako
Moto Mabanga alifanya ujasusi adhimu wa kibiashara kwenye uuzaji wa vitalu vyetu vya gesi.
Nikaeleza namna ambavyo aliwakutanisha Tokyo Sexwale, Dr. Alan Stein na Jonatham Taylor na hatimaye kuunda kampuni ya Ophir Energy ambapo Moto Mabanga akafanya vikao vya siri na viongozi..
wa nchi waandamizi kuwashawishi kuwapa Ophir Energy vitalu

Baada wale vigogo waandamizi kukubaliana na Mabanga, ikaibuka changamoto, namna gani waandamizi wetu waliofanikisha dili hiyo watanufaika.
Ndipo nikasema kwamba Moto Mabanga akatoa 'mchoro' adhimu namna ambavyo watu wetu
watahongwa fedha katika namna ambayo ni almost impossible kwa mtu kushitukia kwamba wamehongwa au hata ku-trace fedha ambazo wamehongwa.

Nikaeleza kwamba Moto Mabanga akatoa wazo la serikali kuchukua mkopo
Tukaenda kukopa kiasi cha Shilingi bilioni 60 toka African Global Capital
Jambo ambalo bado lilikuwa halijulikani kipindi kile ni kwamba, African Global Capital ilikuwa inamilikiwa na kampuni inaitwa African Management Limited, AML. Ambapo hiyo AML ilikuwa ni joint venture ya kampuni mbili ambazo zinamilikiwa pia na Tokyo Sexwale (Mvelaphada Holdings Image
na Palladino Holdings).

Yaani kwa lugha nyepesi ni kwamba nchi yetu ilikuwa imesaini PSA Agreement ya uchimbaji wa gesi na Ophir Energy inayomilikiwa na Tokyo Sexwale, alafu wakati huo huo Tukaenda kuchukua mkopo wa Bilioni 60 African Global Capital ambayo nayo pia inamilikiwa..
na Tokyo Sexwale kupitia kampuni zake nyingine.

Umenifahamu.?

Sasa tuendelee tokea hapo, uone viroja vya namna ile bilioni 60 ilitumika.

Kama unakumbuka nilisema kwamba mkopo huu tulichukua kwa ajili ya kuanzisha shughuli za taasisi na idara zinazosimamia sekta ya Nishati...
yani kama vile uanzishwaji wa TPDC n.k ambapo mkopo huu utatumika kununua vifaa pamoja na kugharamia huduma na utaalamu kwenye mchakato huu

Sasa, Ukipekua nyaraka utaona kwamba kampuni ambayo ililipwa fedha nyingi toka kwenye mkopo huu inaitwa Floras Bell ambayo imesajili visiwa
vya British Virgin Islands.

Nyaraka zinaonyesha kwamba wamiliki wa kampuni hii ni watu wawili wanaoitwa Mark Willcox na Ian Hannam.
Huyu Ian Hannam ni maarufu sana kwenye ulimwengu wa banking.
Kama umewahi kusoma makala yangu kuhusu mabilioni ya Roman Abramovich, huyu ndiye yule Image
somo ambaye alitaka kuandikisha 'float' za kampuni ya Rusal kwenye soko la hisa la London.

Mmiliki wa pili, Mark Willcox ndiye ana utata mkubwa, sababu huyu jamaa licha ya kwamba ni mmiliki wa kampuni hii ya Floras Bell, bali pia huyu somo alikuwa ni CEO wa Mvelaphanda Holdings
(Ile ya Tokyo Sexwale).

Yaani kwa lugha nyepesi ni kwamba, kampuni ambayo tuliilipa fedha nyingi toka kwenye ule mkopo tuliochukua, moja ya wamiliki wake ni mfanyakazi wa Tokyo Sexwale kupitia Mvelaphanda Holdings.

Sasa wataka kuona maajabu.?

Miezi michache baada ya serikali..
kuwalipa Floras Bell.. kampuni hii ikafanya malipo ya mabilioni ya shilingi kwenda kampuni ya usafirishaji mizigo majini ambayo imesajiliwa nchini Cyprus (tuhifadhi jina kwa sasa). Ajabu ni kwamba kampuni hii inamilikiwa na mtoto wa kiongozi mwandamizi wa enzi zile

Abracadabra..
And that my friend ndio namna gani watu wanakula "maziwa na asali" wakati sie wengine tunapigania "unga robo, dagaa fungu moja"..!!

Hiki nilichowaeleza hapa ni sehemu ndogo tu ya mchoro ambao Moto Mabanga alikuwa ameutoa wa namna gani mabilioni ya fedha yalizungushwa na kisha...
kupotelea hewani, yakiingia mifukoni mwa watu.

Sasa, baada ya mabilioni hayo kuzungushwa, hatimaye katikati ya mwaka 2005 serikali iliitisha 3rd Round ya mnada wa vitalu ambapo vitalu 7 viliwekwa sokoni.
Na kampuni ya Ophir Energy ya Tokyo Sexwale ikashinda mnada na kupatiwa..
Vitalu vya Block 1, Block 3 na Block 4.
Mwaka uliofuata 2006 wakaongeza kitalu kingine na mwaka 2007 wakaongeza tena kingine.
Vitalu viwili vilivyosalia walipewa kampuni za Petrobras na Dominion Petroleum kilatu kimoja kimoja.

Sasa, nimeeleza kwa upana kabisa.. namna gani...
Tokyo Sexwale alifaidika na huduma ya Moto Mabanga kwa kupata vitalu vya gesi. Pia vigogo waandamizi walivyo jizolea mabilioni.
Najua utabaki unajiuliza, Moto Mabanga alipata nini? Alinufaikaje.?

Naja kueleza.. be here!

Nisaidie Ku-Retweet

Habibu B. Anga
To Infinity and Beyond

β€’ β€’ β€’

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
γ€€

Keep Current with Habibu B. Anga

Habibu B. Anga Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @habibu_anga

Mar 25, 2023
Ukitaka kuelewa chanzo cha vita ya Ukraine basi unapaswa kufahamu mkasa wa huyu unaye muona pichani na Zitto… anaitwa Victor Yushchenko

Miaka kadhaa iliyopita huyu somo alikumbwa na kadhia ya kulishwa sumu na kupata madhara kama yale ambayo yalimkuta Dr. Mwakyembe..

Thread..
enzi zile za Richmond na Dowans mpaka akapelekwa India kutibiwa.
Ngozi ya mwili yote iliharibika na kuanza kupukutika kama unga

Huyu Yuschenko yeye kadhia hii ilimtokea mwaka 2004 kipindi hicho akiwa anagombea Urais wa Ukraine
Yushchenko alikuwa anachuana mwanasiasa Yanukovych..
ambaye alikuwa ni Waziri Mkuu wa serikali ambayo ilikuwa inamaliza muda wake

Uchaguzi huu wa Ukraine kwa kiasi kikubwa ulikuwa ni mchuano wa kiushawishi kati Marekani na Urusi wakitunishiana misuli.
Marekani walikuwa wanamuunga mkono huyu somo pichani Bw. Yushchenko wakati Urusi
Read 24 tweets
Aug 18, 2022
Roman Abramovich: Utajiri wa Damu Mpaka Kumuingiza Ikulu Putin

Thread,

Namna ambavyo mtoto yatima aliyelelewa katka umaskini ameweza kuibuka moja ya binadamu wenye ukwasi mkubwa duniani na mpaka kuweza kumuingiza Ikulu Vladmir Putin ni mkasa wa aina yake…

(Usisahu ku-Retweet) Image
Wazazi wake wote wawili licha ya kuishi maisha yao yote nchini Russian lakini asili yao ni Waisrael. Mama yake aliitwa Irina na alifariki kipindi Roman bado angali mchanga kabisa wakati baba yake ambaye aliitwa Arkady alifariki kwa ajali ya gari miaka michache baadae Roman akiwa
bado mtoto mdogo kabisa.

Hii ndio ilikuwa sababu ya Roman kwenda kulelewa kwa ndugu zake Komi kaskazini mwa Urusi ambako kuna baridi kali na umasikini uliokithiri

Ujanani mwake, Roman aliwahi kujiunga na jeshi kabla ya kuacha na kuamua kwenda Moscow kutafuta maisha
Akiwa Moscow
Read 23 tweets
Dec 21, 2021
TUMEWAHI KUWA NA CHANJO KWA MALENGO YA KISHUSHUSHU

Thread..

Kadiri ulimwengu unavyobadilika, stadi ya Ujasusi inazidi kuwa complex kwa kuhusisha mbinu ambazo nyingine ukizisikia unaweza kudhani labda watazama sinema au waota, lakini ndio uhalisia wa ulimwengu ulipo sasa katika
katika juhudi za mataifa na makampuni makubwa kupanua ushawishi wao juu ya dunia yote na kulinda maslahi.

Kuna kisa cha tofauti sana ningependa nikijadili leo hii. Kisa cha tofauti kabisa..

Wengi tutakuwa tumewahi kusikia shirika linaloitwa β€œSave the Children”. Ni moja ya…
Shirila kubwa zaidi la misaada ya kibinadamu ulimwenguni ambalo limejikita hasa kwenye kutoa misaada inayolenga kuboresha hali za maisha ya watoto wadogo.

Mwaka 2011 shirika hili lilikuwa kwenye shughuli zake mahala paitwa Khyber nchini Pakistan.
Save the Children walikuwa na…
Read 43 tweets
Oct 14, 2021
π—•π—œπ—‘π—§π—œ π—π—”π—¦π—¨π—¦π—œ π—ͺ𝗔 π— π—œπ—”π—žπ—” 25 π—”π—‘π—”π—¬π—˜π—œπ—§π—œπ—žπ—œπ—¦π—” 𝗔𝗙π—₯π—œπ—žπ—” 𝗠𝗔𝗦𝗛𝗔π—₯π—œπ—žπ—œ

Thread..

Siku ya 30 May 2019, maafisa Usalama Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JKIA, Nairobi walimuweka kizuizini abiria mmoja mwenye hati ya kusafiria ya kidiplomasia, mwanaume.. Image
wa asili ya kisomali. Japokuwa watu wenye diplomatic passport wapata exemptions kadhaa kwenye kaguzi za uwanja wa ndege, lakini ilikuwa ni lazima kwa maafisa hawa kumuhoji abiria huyu kutokana na utata wa mzigo ambao alikuwa nao.

Huyu somo alikuwa na briefcase ambalo ndani yake
alikuwa amebeba fedha cash dola za Kimarekani milioni moja na nusu.

Mtu huyu nyaraka zake zilikuwa zinaonyesha kwamba alikuwa safarini kuelekea nchini Ethiopia.

Maafisa hawa wa Usalama. Wakaanza kumuhoji abiria huyu sababu za kusafiri na kiwango kikubwa hivyo cha fedha na pia.. Image
Read 98 tweets
Sep 4, 2021
π—žπ—”π—•π—Ÿπ—” 𝗬𝗔 π—œπ—žπ—¨π—Ÿπ—¨.. π—žπ—ͺ𝗔𝗑𝗭𝗔 𝗔𝗗𝗛𝗔𝗕𝗨 𝗬𝗔 π—žπ—œπ—™π—’

Thread..

Ukiwa unatoka Lusaka kwenda Jimbo la Magharibi, kabla hujaingia mji wa Mongu kuna kipande cha barabara kinajulikana kama Limulunga Road.
Kipande hiki cha barabara mwaka juzi kimetupa tukio la kipekee Image
ambalo kwa kiwango kikubwa tukio hili limebadili mwelekeo wa siasa la bara zima la Afrika na hasa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara.

Pengine pasipo tukio hili huyu Hichilema tunayemuona leo asingelikuwa Rais. Lilikuwa tukio la kipekee kabisa..

Kila mwaka pale Zambia huwa wana
sherehe maarufu zinaitwa "Kuomboka Ceremony".
Wenzetu mpaka leo hii bado wanatambua cheo cha asili cha "Litunga" ambaye ni Mfalme wa kabila la Walozi.
Kila mwaka mwishoni mwa msimu wa mvua mfalme huwa anahama kutoka makazi yake ya bondeni ya Lealui na kuhamia makazi yake yaliyo..
Read 41 tweets
Aug 10, 2021
π—¨π—§π—”π—π—œπ—₯π—œ π—ͺ𝗔 π— π—”π—¦π—›π—”π—žπ—” π—ͺ𝗔 π—ͺπ—”π—Ÿπ—œπ—‘π—­π—œ π—ͺ𝗔 π—©π—œπ—’π—‘π—šπ—’π—­π—œ

Thread..

Mwaka juzi kwenye hafla ya mapokezi ya ndege kwenye nchi fulani hivi hapa Afrika Mashariki kuna incident ndogo tu ilitokea lakini wengi ikatufikirisha sana.

Dakika chache baada ya Rais wa...
nchi hiyo kumaliza kuongoza hafla hiyo ya mapokezi ya ndege akashuka jukwaani na akianza kuandoka.
Lakini kabla hajakwenda kupanda gari, kama ambavyo ilikuwa ada kwa Rais yule akaelekea upande waliokaa wananchi wake na ili awasalimie.
Na kusalimia huku akaanza jukwaa ambalo...
walikuwa wamekaa wageni VIP.

Wageni wale mashuhuri wakasimama na Rais akawa anapita akiwapa mkono.

Mojawapo ya wageni wale mashuhuri alikuwa ni mfanyabiashara maarufu sana mwenye asili ya kihindi.
Rais alipopita mbele yake, mfabiashara huyu akanyoosha mkono ili asalimiane na...
Read 25 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(