Baada ya kujua kwamba Wateja ndiyo bidhaa adimu Sokoni leo wacha nikupe ufunguo ambao watu na Makampuni mengi wanaudharau.....
Ufunguo huu utakuwezesha kunasa wateja kama Dan Bilzerian na madem zake... @nyandaAmosi anamfahamu huyu kamanda
UZIII TYM, YEEEAHH
Ngoja kwanza, unaweza ku ❤️ kisha Retweet 🔁 ku show support?... Eeh ndiyo hivyo, wengi watapata madini ukifanya hivyo...
Asante sana,
Twendezetu tukale
madini ⤵️
MASOKO au kwa Kizungu (MARKETING)
Ndiyo jibu litakalo kusaidia kuwashinda washindani wako badala ya kushindana kushuusha beeeiiii weee mpaka unaleta changamoto kwa biashara yako unauza bila faida.... Kuna mbinu za kufanya punguzo, uzi wa siku nyingine huo.....
Kwanza watu wengi wanadhani kufanya Marketing ni kujaribu au kusaidia kuuza bidhaa zao zilizokwama au kushindwa kuuzika sokoni...
Dhana hiyo ni potofu kabisa🙂
Badala yake leo utambue kwamba Marketing ni Kiwanda Maalum Kabisa cha kuzalisha Wateja wa bidhaa au huduma unayotoa...
Kitu kinacho fanya biashara au kampuni kufanikiwa ni mchakato na Mawazo ya Masoko (marketing) na utoaji huduma......
Yaani
Uzalishaji, Manunuzi, Utafiti na Uendelezaji, Idara ya Fedha pamoja na Idara nyinginezo zote kwenye kampuni hufanya kazi katika uwanja wa huduma kwa mteja wa bidhaa ya kampuni yako....
Marketing mara nyingi huchanganywa na Mauzo... hivi ni vitu viwili tofauti...
Mauzo yanaanza pale unapokuwa na bidhaa.... Au vipi?
Lakini Masoko au Marketing huanza kabla ya bidhaa kuwepo.... Eee, ndiyo hivyo!
Marketing ni zoezi ambalo unalifanya ili kujua Watu/Soko linataka nini na wewe unaweza kutoa nini ili kuziba hilo pengo!....
Umeona umuhimu wa marketing hapo...?
Enheee ndiyo hivyo,
Lakini Marketing itakusaidia kujua mambo yafuatayo pia
1. Jinsi ya kuitambulisha bidhaa yako 2. Bei gani itafaa sokoni 3. Jinsi utavyosambaza bidhaa yako 4. Jinsi utakavyo I promote bidhaa/huduma yako sokoni
5. Itakusaidia ku monita matokeo ya bidhaa yako na kujua wapi uongeze kiwango cha huduma ili kuboresha 6. Itakusaidia kujuA lini uache kutoa Offa
Marketing inatakiwa iwe ni mradi endelevu
Kabla hujatengeneza bidhaa yoyote au hujaingia soko lolote Na inaendelea muda mrefu hata baada mauzo....
Sikiliza....
Zama za mababu zetu walikuwa wanatengeneza bidhaa na wanasema...
"Hii ndiyo nimetengenezA, unaweza kununu tafadhali??? Eeh, we nunua tu hakuna namna, hutaki achaaa watanunua wenziooo"
Ila sasa ulimwengu ni tofauti, sasa mteja anasemA....
Fanya ku ❤️ kisha Retweet 🔁🔁 ku show love and Support
Tayari? Haya twendezetu tule madini⤵️
Naam...
Tatizo kubwa sana linalozikabiri biashara nyingi leo si ukosefu wa bidhaa bali ni....
ukosefu wa Wateja.....
Bidhaa unayouza/Kutengeneza unajua kabisa hauko peke yako sokoni ila una washindani kibao..
Lakini pia Makampuni mengi yanaweza kuzalisha bidhaa nyingi kuliko mahitaji ya wateja wanavyo weza kununua....
Na kutokana na uwezo huo, wanapotengeza bidhaa huweka makisio ya juu sana ya ukuaji wa biashara, wanapofika kwenye soko mambo huwa tofauti kwa ground...