Hii ilikuwa ni miaka ya '90 mwanzoni, tukitokea pembezoni mwa mgodi wa Mwadui, tulifahamika kwa jina la "Wabeshi".
Zana zetu za kazi ilikuwa ni sululu, chepe na majembe yaliyonolewa sana, tulikabiliana na jeshi la polisi la mgodi wa Mwadui waliokuwa na kikosi cha farasi na mbwa wenye uweredi mkubwa sana na mafunzo ya hali ya juu.
Nakumbuka siku rafiki zangu wawili walivyouwawa kwa kuumwa na mbwa sehemu za siri na jirani yangu Jilingumika Masufulia alivyopigwa risasi ya kichwa akivuka fensi ya mgodi wa Mwadui.
Almasi tuliibatiza jina la "ng'ana", na ilikuwa hauwezi kwenda kuiba bila kuchanjwa chale za kwapani na matakoni. Mganga wetu mkubwa alikuwa ni Mzee maarufu sana wa Kijiji cha MWIGUMBI, Nje kidogo ya mgodi, huyu ndio mzee aliyetupa dawa na kinga wakati wa kwenda kuiba almasi,
Nilikuwa na miaka 16 nimemaliza darasa la saba shule ya msingi Luhumbo.Tajiri wetu mkubwa alikuwa mwarabu wa Maganzo maarufu kwa jina la Abeid,huyu alitupikia vitumbua na chai kabla ya kwenda mgodini kuiba almasi, na chote tulichokipata tulipeleka kwake kama tajili na kulipa
Tajiri Abeid hakuwa mtu "rahisi rahisi", yeye mganga wake alikuwa anatokea kijiji cha Idukilo, mganga hatari sana aliyekuwa na madawa ya kisukuma ambayo yaliwabadilisha watu na kuwa mbwa mwitu au nyani pindi walipoingia ndani ya mgodi kuiba,
tajiri Abeid alikuwa anaishi kijiji cha Maganzo, akiwa na duka la bidhaa la kuzugia,lakini deal zake kubwa ilikuwa ni kununua almasi na kuziuza kwa matajili wakubwa wa Mwanza na Shinyanga mjini.
Almasi zote tulizopeleka kwa Abaeid zilikuwa zinatunzwa na mbuzi dume, beberu mkubwa aliyekuwa anazimeza na kuzihifadhi tumboni hadi mteja atakapokuja,hata polisi wakifika na ku-search vipi,wasiongeziona almasi kwani beberu alikuwanazo tumboni,
hakuwa beberu wa kawaida maana alikuwa na chumba chake na alilala ktk godoro. Mbuzi hakula nyasi wala majani ya miti, bali vitumbua, chai na "maparage". Kipindi hicho hatukuwa na ruhusa ya kuongea juu ya mbuzi yule, tulimuogopa na kumtii zaidi hata ya kiongozi wetu.
Tajiri wa uhakika alikuwa Fantomu wa maeneo ya Mipa,huyu hakuonana na sisi wabeshi maana tulikuwa watu "wadogo" sana, bali alipitia kwa Abeid na waarabu wengine wa Maganzo.
Maisha ya kuwa "mbeshi" yalikuwa magumu sana,maana kifo na kujeruhiwa ilikuwa ni njenje,tuliuwa na kuuwawa.
Polisi, mbwa na farasi waliokuja bila tahadhari waliuwawa kwa chepe zilizonolewa na mapanga. Tukio moja nalokumbuka ni la mwenzetu Masunga kumuua mbwa wa polisi kwa kumkata na chepe mdomoni na kuutenganisha mdomo pande mbili.
Wenzetu wengi walikufa tukiwa bwawani tukiiba,wengi walizama kwenye tope liliotokana na mabaki ya kusafishwa kwa almasi ambayo sisi tulikuwa tunakwenda kuchota na kuchekecha upya,
bwawa hili la tope zito lilukuwa karibu na "sorting area" ambayo ililindwa kwa kiasi kikubwa sana. Lakini kwa imani ya chale za mganga wa MWIGUMBI na Idukilo watu wengi tulikuwa na ujasiri wa kukatiza kila mahali bila hofu.
Wengi waliojeruhiwa na kuumizwa walilazwa ktk hospitali ya Mwadui.Siku nilipoamua kuacha "kazi" hii na kurudi shule,ilikuwa ni siku hatari sana... binamu yangu kipenzi Luhende alipigwa risasi ya kichwa na ubongo kutawanyika, mbele ya macho yangu Luhende alikufa bila kuomba maji.
Askari wakiwa umbali wa kama mita 100,sisi tukiwa na makarai yetu na chekecheke tukiambaaambaa pembeni ya reli maeneo ya SONGWA ktk njia ya mzunguko kuelekea Maganzo tuliwekwa katikati yao na kuuliwa baadhi yetu.
Katika kundi la wabeshi kumi, saba walikufa hapo hapo..watatu walifia hospitali na mimi pekee nilipona baada ya kujitumbukiza kwenye bwawa la maji ya kunywea mifugo, niliogolea chinichini kwa chini na kuibukia upande wa matete, ambapo nilikaa ndani ya maji zaidi ya masaa 12
Tuendelee na wahabeshi?
• • •
Missing some Tweet in this thread? You can try to
force a refresh
Wakili Fatuma Karume alisafiri kutoka Dar kwenda mkoani Kilimanjaro.
Wakili huyu alikuwa amesafiri akiwa amebeba nyaraka furani ya muhimu.
Nyaraka ile alikuwa anaenda kumsomea na kumkabidhi mzee fulani aliyefahamika kwa jina la Juma
Actually, Mzee Juma naye alikuwa ni wakili ambaye sasa amestaafu akiwa amefanikiwa kurithisha taaluma hiyo pia kwa mwanae ambaye alikuja kuwa ni wakili maarufu sana mkoni Arusha.
Fatma hakujua kama nyaraka aliyobeba ingeleta taflani kubwa ndani ya familia ya Mzee Juma.
Fatma aliwasili nyumbani kwa ambako alikuta waombolezaji ambao walikusanyika baada ya kusambaa taarifa za msiba za mmoja wa watoto wa Mzee Juma.
Fatma alitegemea kuikuta hali hii nyumbani pale na hata safari yake ilitokana na yeye kupata taarifa hizi.
Nimesikiliza hotuba ya leo ya mheshimiwa rais, na hii ndio analysis yangu.
1. Hotuba hii imekuja siku chache baada ya rais kuviagiza vyombo vyake vya ilinzi vimpelekee taarifa ya nini kilicho nyuma ya matukio ya utekaji na mauaji hasa baada ya kifo cha Ali Kibao
2. Inaonekana rais alipokea ripoti hii mapema kama alivyoagiza na yafuatayo ndiyo yalikuwa ndani ya ripoti hiyo:
(a)Kuwa haya yote anayoyasikia juu ya mauaji na utekaji, ni zao ya kikao cha siri kililichofanyikia Ngurero mkoani Arusha mnamo Sept 11, 2024
(b) Maazimio ya kikao kile yaliamua kutumia vibaya 4R alizoziasisi mheshimiwa rais ili kuzua ghasia nchini, kufitini jeshi la polisi na kufanya fujo misibani.
Kama ripoti hii ni sahii, kuna mambo yanayohitaji ufafanuzi..
Satiiva ammedai kumtambua Mafwele kama mtu aliyeenda usiku kwa Land Cruiser kwenye karakana ya polisi Oysterbay alipotekwa
Kuwa ndiye mtu mwembamba, mkakamavu, aliyekuwa kavaa Jezi ya Simba na pensi
Amemtambua baada ya kuona picha ya Mafwele ikisambaa mtandaoni.
Pia Sativa ameshaujulisha uongozi wa Jeshi la polisi juu ya utayari wake wa kuhojiwa na jeshi hilo ili kuwashirikisha anachokifahamu nyuma ya kutekwa kwake.
Jeshi limemjibu likipata nafasi litamuita kumuhoji
Lakini ni jeshi hilihili, lilipata nafasi ya kunitumia timu ya makachero watatu, mmoja akiwa wa cheo kikubwa cha SACP, Mwingine akiwa ni katibu wa DCI, kusafiri kutoka makao makuu ya polisi Dodoma hadi Central DarEsSalaam kunihoji habari za ASP Fatuma Kigondo.
Kifo cha Ali Kibao kimekuwa ni kama sauti ya wote waliokuwa wanabeza kuwa hakuna matendo ya utekaji na summary executions nchini.
Ni sauti iliyowasemea victims wote wa matendo haya.
Lakini pia kinaweza kuleta mwanga kwa kuwa sasa watu wameanza kugusia jambo fulani muhimu.
Jambo la kwanza kugusiwa ni dai la kuundwa kwa chombo huru kinachotakiwa kuufatilia utendaji wa jeshi la polisi.
Majirani zetu nchini Kenya wanacho chombo hiki kwa jina la IPOA
Independent Policing Oversight Authority
Nini umuhimu wa kuwa na chombo hiki?
Ni kwa sababu si rahisi kujichunguza kwa uhuru dhidi ya tuhuma unazotuhumiwa wewe mwenyewe.
Watu wanaojitambulisha kama askari polisi, ndio wanaotuhumiwa kwa utekaji na mauji hivyo haiwezekani hata kidogo chombo hiki kikaachwa kijichunguze chenyewe kisha tutarajie majibu chanya.
Imeshathibitika kuwa, watu wanaojitambulisha kuwa ni askari wanaweza kumkamata mtu mbele ya watu, kuondoka naye na baadaye unakuja kupatikana mwili wake usio na uhai au asionekane kabisa.
Pia kwa kuwa @tanpol wameishia kutoa matamko bila suluhisho..
Yafuatayo ndiyo mambo tutakiwayo kufanya wote kwa pamoja ili kuokoa maisha ya wengine.
Kwani wakimaliza kwa huyo, wewe ndie utakayefata
1. Kataa kabisa kukamatwa kwa sasa hata kama utatolewa kitambulisho. Piga kelele zote uwezavyo, fanya fujo kwani upole wako hautakusaidia.
2. Kama mtu anakamatwa eneo la watu wengi, wengine saidieni kwa kuongeza fujo, kuhoji makosa yake na kuwarekodi kwa simu zenu wakamataji.
MSIOGOPE: Ni wao ndio wametufikisha kwenye ujeuri kwa ajili ya maisha yetu.
Kuna kitu fulani wataalamu wa siasa hukiita "Political Paranoia"
Paranoia ni ugonjwa wa akili ambapo mgonjwa huwa na wasiwasi mkubwa kuwa kuna watu wanamfatilia mambo yake, wanapanga kibaya juu yake, wanamdanganya etc
UZI👇
CHOCHORO ZA MADARAKA -2
Mgonjwa wa Paranoia mara nyingi hutuhumu watu fulani wana njama fulani dhidi yake.
Hata jambo fulani ambalo linaweza kutokea kwa bahati mbaya (just coincidence) ambavyo hata watu wengine huamini hivyo, lakini mgonjwa wa paranoia huamini si bahati mbaya bali makusudi.
Viongozi wengi barani Afrika, ni Paranoid.
Muda wote hutembea na hisia kuwa kundi fulani linakula njama za kuwatoa madarakani
Hii ndio maana unaona wengi wa viongozi hawa hupanga na kupangua safu za wasaidizi wao.