Fortunatus Buyobe Profile picture
Jan 24, 2022 14 tweets 4 min read Read on X
THIS CASE IS VERY COMPLICATED

Kwenye kesi za mauaji, ili kufikia hukumu ya haki, mahakama hutaka kujiridhisha kama elements mbili zimethibitishwa bila kuacha shaka.

1. Actus reus/ Tendo ovu (lazima liwe limetendeka)

2. Mens rea /dhamira ovu. Image
Dhamira ovu inaangaliwa kwenye angle mbalimbali...

Kwenye kesi hii naangazia matendo ya mshtakiwa kabla na baada ya kitendo kiovu.

Utetezi wake ungekuwa na nguvu sana, lakini matendo yake yalitia shaka.

Hapa namuongelea DAUDI KAPEJA.

Fatilia mkasa huu,

👇 Image
19/04/2014 UYUI, TABORA

Majira ya saa 4 usiku, BARESA RASHID aliambatana na DAUDI KAPEJA nyumbani kwake ambapo alichukua jacket na kumuaga mkewe kuwa wanakwenda kumuona jamaa aitwaye JUMA BUSEGA ili kufanya biashara ya tumbaku.

Wanatumia pikipiki mali ya BARESA RASHID Image
BARESA RASHID tena hakurudi nyumbani kwake usiku ule,

Baadae, mkewe ZAMDA ISSA akapewa taarifa za mwili wa mmewe kuokotwa pamoja na mwili wa mke wa JUMA BUSEGA yule yule ambaye marehemu mumewe na DAUD KAPEJA walisema wanaenda kufanya nae biashara ya tumbaku. Image
Maiti za watu hawa wawili zilikutwa kwenye vichaka katikati ya vijiji vya UFULUMA na MABAMA

Pikipiki ya BARESA RASHID ilikuwa pembeni yao huku miili yao ikiwa na majeraha sehemu mbalimbali.

Taarifa ile ikawafikia polisi

Usiku ule ule ikaanza nusa nusa
Ikiwa sasa siku imeshapinduka, tarehe 20/04/2014 ikafika pale timu ya makachero watatu waliotumwa na OC-CID msaidizi wa Uyui

Hawakuwa peke yao bali waliambatana na daktari kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu.

Jumla ya watu hawa wanne, kila mtu alikuwa na majukumu yake
1.Askari G.348 Detective Corporal OMARY MATESA ndiye alikuwa mpelelezi wa shauri hili.

2. G. 4876 Detective Corporal MATIKU alienda kuchora ramani ya eneo la tukio. Image
3. G.2269 D/Corporal RAJAB alikuwa na jukumu la kuimarisha ulinzi.

4. Dr. SINDABAKILA SEREJIO ailenda kufanya uchunguzi wa kitaalamu wa chanzo cha kifo akitokea hospitali ya wilaya ya Uyui. Image
Kwa mujibu wa daktari, ripoti yake ilisema maiti ya mwanaume ilikuwa na “fracture” kichwani ambapo mfupa wa “parietal” ulikuwa umevunjika kutokana na kupigwa na kitu kizito na kuvuja kwa damu.

Ripoti hii ilipelekwa kwa District Medical Officer Image
Lakini ripoti ilikuwa kimya juu ya maiti ya mwanamke.

Kwa nini?

Tutaona mbele ya safari....

.................................................

Katika nusanusa makachero wakabaini yafuatayo juu ya maisha ya nyuma ya marehemu BARESA baada ya kumuhoji mkewe,
BARESA alikuwa na mke mwingine mkubwa ambaye walikuwa na ugomvi naye.

Chanzo cha ugomvi ni kwamba marehemu alishamfumania mkewe akifanya “horizontal Engineering”na mtu aitwaye NDEBILE

Mwanamke huyu alishaondoka muda mrefu na hajulikani aliko.

Don’t you smell something? Image
Mtu pekee ambaye makachero walielekeza kwake vidole vya tuhuma ni alikuwa ni DAUD KAPEJA

Kwa sababu ndiye alikuwa the only last person known to be seen with the deceased.

Yes! Alikuwa ndiye mtu pekee aliyeonekana kwa mara ya mwisho na marehemu.

Msako dhidi yake ukaanza. Image
Hakuonekana eneo la tukio wala msibani

Baadae zikaja taarifa mpya kutoka kwa kichomi zikisaga kunguni.

Kichomi huyu ni JUMA BUSEGA yule yule ambaye marehemu na DAUDI walisema wanaenda kwake on the fateful night.

Infomer huyu unamwamini ndugu msomaji? Image
Sogelea telegram link 👇

t.me/fbuyobe

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Fortunatus Buyobe

Fortunatus Buyobe Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @fbuyobe

Sep 6, 2025
Huko Harare, Zimbabwe katika barabara ya Borrowdale, kuna eneo la maduka makubwa maarufu kwa jina la Ballantyne Park Shopping Centre

Mwaka 2008, ilikuwa ukienda katika duka No. 19 kwenye maduka haya, ungekutana na mgahawa maarufu wa Millers Cafe

Mgahawa huu umebeba simulizi Image
Siku moja mchana mwaka 2008, nikiwa nimeboreka, niliingia kwenye mgahawa wa Millers

Niliongoza kwenye kiti kimojawapo ndipo nikasikia sauti ya mtu aliyekuwa ameketi nyuma yangu ikiniita

Nilipogeuka nikashtuka kubaini anayeniita ni mchungaji Uebert Angel Mudzanire Image
"Kijana, tangu ulipokuwa unaingia ndani ya mgahawa nimekuwa naona namba 33 kwenye paji la uso wako"

Aliniambia Mchungaji Angel

Sikumuelewa hivyo ikabidi nimuulize mchungaji:-

"Unataka kumaanisha nini?"

Jibu alilonipa lilikuwa mbali na uhalisia Image
Read 24 tweets
Sep 5, 2025
𝐒𝐨𝐦𝐞𝐭𝐢𝐦𝐞𝐬 𝟐𝟎𝟐𝟑

𝐋𝐨𝐠𝐢𝐬𝐭𝐢𝐜𝐬 𝐂𝐚𝐦𝐩
𝟖𝟑𝟏 𝐊𝐉
𝐌𝐆𝐔𝐑𝐀𝐍𝐈

𝟎𝟓𝟒𝟐 𝐇𝐑𝐒

Lutueni Kanali E.A Sambila ambaye ndiye Commanding Officer wa 831 KJ anapokea taarifa nyeti ofisini kwake kutoka kwa askari wake wawili wahusikao na ulinzi amani kikosini (MPs) Image
Askari hawa wawili ambao ni P.12925 Captain Theresia Cylil Massawe na MT. 88710 Sergeant Mohammed Faki Haji walifika ofisini kwa Lt.Gen Msambila wakieleza kuwa wana taarifa ya dharula

Kuwa kuna uwezekano wa muda wowote amani kutoweka mle kikosini

Wakaruhusiwa kuingia Image
Taarifa inayotolewa mbele ya CO, inalazimu muda mfupi unaofuata, askari wale wawili, kwa maelekezo ya CO wavamie ofisini kwa serviceman MT. 85115 Sergeant Sahani

Askari yule anawekwa chini ya ulinzi, na kwenye upekuzi, wanachukua simu mbili anazomiliki

Upekuzi ukahamia nyumbani Image
Read 13 tweets
Aug 30, 2025
Tarehe 28 August 2025, chama tawala, CCM kilizindua kampeni zake za uchaguzi mkuu wa urais na wabunge katika viwanja vya Tanganyika packers

CCM walilazimika kutumia jukwaa hilo la uzinduzi wa kampeni kujibu mashambulizi kutoka kwa mwanachama wake mwandamizi Humphrey Polepole Image
Image
Tangu kujiuzuru kwake July 13, mwaka huu kwa kile alichoeleza kama "kutoridhishwa na mienendo" ya serikali yake, balozi huyo wa zamani wa Tanzania nchini Cuba, amekuwa akitoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi waandamizi wa chama chake na serikali Image
Image
Polepole ameeleza juu ya uwepo wa kikundi anachokiita "CCM mtandao" ambacho huakikisha wanaohodhi madaraka ya rais

Kuwa mtandao huo nchini tangu mwaka 1995 zilipoanza siasa za vyama vingi na mtandao huu una agenda ya kuhakikisha kila rais anakuwa chini ya himaya yao Image
Read 45 tweets
Aug 2, 2025
Una uhakika kuwa wewe binafsi ulionana na IGP Sirro?

Unaweza kunieleza kwa ushaidi ni mara ngapi na wapi ulionana naye?

Unajua kuwa tuhuma unazotoa ni nzito ukihusisha watu wakubwa sana nchini?

Ilikuwa zamu yangu kuanza kumhoji mwanamama Jeannie Pollaert raia wa Netherlands Image
Nililazimika kumuuliza mama huyu maswali haya usiku wa manane baada ya kumaliza kusoma makabrasha mengi aliyonitumia kwa njia ya barua pepe.

Nilichokikuta ndani ya makabrasha yale kilifanya usingizi uliokwishaanza kunitongoza utoweke

Infact niliogopa sana

Nilihitaji ushaidi Image
Itakuwaje endapo Simon Sirro atakana kuwahi kukutana na wewe na kufanya na wewe kikao chochote?

Lilikuwa swali langu la kwanza.

Jeannie: Itakuwa vigumu sana kwa Sirro kukataa kuwa hajakutana nami

Akanipa ushaidi wa mawasiliano yao na jinsi Sirro alivyomjibu Image
Image
Read 25 tweets
Jun 27, 2025
Mwaka 2012, Blandine Nyoni akiwa katibu mkuu wizara ya afya, alinukuliwa akitoa kauli tata ya kuwabeza madaktari kuwa "wanajiona bora wakati ni wachafu na hawajui kiingeleza" Image
Katibu huyu akaendelea kusema kuwa hata yeye alisoma mchepuo wa PCB na kufaulu vizuri tu lakini kwa kutambua ubovu wa Medicine mzazi wake akamsomesha Accounts so hajui madaktari wanalalamikia nini.

Kauli hii ikang'oa kilaka kwenye jeans ya bishoo! Image
Ni kwamba mwaka huo, madaktari walikuwa katikati ya mgomo wa kihistoria

Kauli hii ikawatibua madaktari wakalianzisha upyaaaaa

Uzi👇

Dr. Ulimboka and total tools down

Nisome Image
Read 76 tweets
May 9, 2025
Wiki hii tumeshuudia waliokuwa wanachama wa Chadema wakitangaza kuachana na chama hicho huku wakiahidi kuelezea hatima zao za kisiasa siku za mbeleni

Kati ya waliohama ni waliowahi kuwa viongozi waandamizi wa chama hicho

Hii inamaanisha nini? Image
Kabla sijajibu swali hilo ni vyema tukipitia kwa ufupi mtiririko wa matukio (A quick refresher)

1. Dec 12,2024, Tundu Lissu anatangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA taifa

Nia hii ya Lissu ilikuja baada ya kuwa uchokozi wa wazi dhidi yake ndani ya chama Image
Kabla ya uamuzi huu, Lissu aliyekuwa ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA, alishamwandikia barua katibu mkuu wake kumjuza nia yake ya kuendelea kugombea kubaki kwenye nafasi hiyo.

Ulikuwa ni utaratibu wa CHADEMA kwa viongozi wa juu kutoshindania nafasi moja endapo mmoja ataonesha nia Image
Read 34 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(