Kwenye kesi za mauaji, ili kufikia hukumu ya haki, mahakama hutaka kujiridhisha kama elements mbili zimethibitishwa bila kuacha shaka.
1. Actus reus/ Tendo ovu (lazima liwe limetendeka)
2. Mens rea /dhamira ovu.
Dhamira ovu inaangaliwa kwenye angle mbalimbali...
Kwenye kesi hii naangazia matendo ya mshtakiwa kabla na baada ya kitendo kiovu.
Utetezi wake ungekuwa na nguvu sana, lakini matendo yake yalitia shaka.
Hapa namuongelea DAUDI KAPEJA.
Fatilia mkasa huu,
👇
19/04/2014 UYUI, TABORA
Majira ya saa 4 usiku, BARESA RASHID aliambatana na DAUDI KAPEJA nyumbani kwake ambapo alichukua jacket na kumuaga mkewe kuwa wanakwenda kumuona jamaa aitwaye JUMA BUSEGA ili kufanya biashara ya tumbaku.
Wanatumia pikipiki mali ya BARESA RASHID
BARESA RASHID tena hakurudi nyumbani kwake usiku ule,
Baadae, mkewe ZAMDA ISSA akapewa taarifa za mwili wa mmewe kuokotwa pamoja na mwili wa mke wa JUMA BUSEGA yule yule ambaye marehemu mumewe na DAUD KAPEJA walisema wanaenda kufanya nae biashara ya tumbaku.
Maiti za watu hawa wawili zilikutwa kwenye vichaka katikati ya vijiji vya UFULUMA na MABAMA
Pikipiki ya BARESA RASHID ilikuwa pembeni yao huku miili yao ikiwa na majeraha sehemu mbalimbali.
Taarifa ile ikawafikia polisi
Usiku ule ule ikaanza nusa nusa
Ikiwa sasa siku imeshapinduka, tarehe 20/04/2014 ikafika pale timu ya makachero watatu waliotumwa na OC-CID msaidizi wa Uyui
Hawakuwa peke yao bali waliambatana na daktari kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu.
Jumla ya watu hawa wanne, kila mtu alikuwa na majukumu yake
1.Askari G.348 Detective Corporal OMARY MATESA ndiye alikuwa mpelelezi wa shauri hili.
2. G. 4876 Detective Corporal MATIKU alienda kuchora ramani ya eneo la tukio.
3. G.2269 D/Corporal RAJAB alikuwa na jukumu la kuimarisha ulinzi.
4. Dr. SINDABAKILA SEREJIO ailenda kufanya uchunguzi wa kitaalamu wa chanzo cha kifo akitokea hospitali ya wilaya ya Uyui.
Kwa mujibu wa daktari, ripoti yake ilisema maiti ya mwanaume ilikuwa na “fracture” kichwani ambapo mfupa wa “parietal” ulikuwa umevunjika kutokana na kupigwa na kitu kizito na kuvuja kwa damu.
Ripoti hii ilipelekwa kwa District Medical Officer
Lakini ripoti ilikuwa kimya juu ya maiti ya mwanamke.
Kwa nini?
Tutaona mbele ya safari....
.................................................
Katika nusanusa makachero wakabaini yafuatayo juu ya maisha ya nyuma ya marehemu BARESA baada ya kumuhoji mkewe,
BARESA alikuwa na mke mwingine mkubwa ambaye walikuwa na ugomvi naye.
Chanzo cha ugomvi ni kwamba marehemu alishamfumania mkewe akifanya “horizontal Engineering”na mtu aitwaye NDEBILE
Mwanamke huyu alishaondoka muda mrefu na hajulikani aliko.
Don’t you smell something?
Mtu pekee ambaye makachero walielekeza kwake vidole vya tuhuma ni alikuwa ni DAUD KAPEJA
Kwa sababu ndiye alikuwa the only last person known to be seen with the deceased.
Yes! Alikuwa ndiye mtu pekee aliyeonekana kwa mara ya mwisho na marehemu.
Msako dhidi yake ukaanza.
Hakuonekana eneo la tukio wala msibani
Baadae zikaja taarifa mpya kutoka kwa kichomi zikisaga kunguni.
Kichomi huyu ni JUMA BUSEGA yule yule ambaye marehemu na DAUDI walisema wanaenda kwake on the fateful night.
Lutueni Kanali E.A Sambila ambaye ndiye Commanding Officer wa 831 KJ anapokea taarifa nyeti ofisini kwake kutoka kwa askari wake wawili wahusikao na ulinzi amani kikosini (MPs)
Askari hawa wawili ambao ni P.12925 Captain Theresia Cylil Massawe na MT. 88710 Sergeant Mohammed Faki Haji walifika ofisini kwa Lt.Gen Msambila wakieleza kuwa wana taarifa ya dharula
Kuwa kuna uwezekano wa muda wowote amani kutoweka mle kikosini
Wakaruhusiwa kuingia
Taarifa inayotolewa mbele ya CO, inalazimu muda mfupi unaofuata, askari wale wawili, kwa maelekezo ya CO wavamie ofisini kwa serviceman MT. 85115 Sergeant Sahani
Askari yule anawekwa chini ya ulinzi, na kwenye upekuzi, wanachukua simu mbili anazomiliki
Tarehe 28 August 2025, chama tawala, CCM kilizindua kampeni zake za uchaguzi mkuu wa urais na wabunge katika viwanja vya Tanganyika packers
CCM walilazimika kutumia jukwaa hilo la uzinduzi wa kampeni kujibu mashambulizi kutoka kwa mwanachama wake mwandamizi Humphrey Polepole
Tangu kujiuzuru kwake July 13, mwaka huu kwa kile alichoeleza kama "kutoridhishwa na mienendo" ya serikali yake, balozi huyo wa zamani wa Tanzania nchini Cuba, amekuwa akitoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi waandamizi wa chama chake na serikali
Polepole ameeleza juu ya uwepo wa kikundi anachokiita "CCM mtandao" ambacho huakikisha wanaohodhi madaraka ya rais
Kuwa mtandao huo nchini tangu mwaka 1995 zilipoanza siasa za vyama vingi na mtandao huu una agenda ya kuhakikisha kila rais anakuwa chini ya himaya yao
Mwaka 2012, Blandine Nyoni akiwa katibu mkuu wizara ya afya, alinukuliwa akitoa kauli tata ya kuwabeza madaktari kuwa "wanajiona bora wakati ni wachafu na hawajui kiingeleza"
Katibu huyu akaendelea kusema kuwa hata yeye alisoma mchepuo wa PCB na kufaulu vizuri tu lakini kwa kutambua ubovu wa Medicine mzazi wake akamsomesha Accounts so hajui madaktari wanalalamikia nini.
Kauli hii ikang'oa kilaka kwenye jeans ya bishoo!
Ni kwamba mwaka huo, madaktari walikuwa katikati ya mgomo wa kihistoria
Kauli hii ikawatibua madaktari wakalianzisha upyaaaaa
Wiki hii tumeshuudia waliokuwa wanachama wa Chadema wakitangaza kuachana na chama hicho huku wakiahidi kuelezea hatima zao za kisiasa siku za mbeleni
Kati ya waliohama ni waliowahi kuwa viongozi waandamizi wa chama hicho
Hii inamaanisha nini?
Kabla sijajibu swali hilo ni vyema tukipitia kwa ufupi mtiririko wa matukio (A quick refresher)
1. Dec 12,2024, Tundu Lissu anatangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA taifa
Nia hii ya Lissu ilikuja baada ya kuwa uchokozi wa wazi dhidi yake ndani ya chama
Kabla ya uamuzi huu, Lissu aliyekuwa ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA, alishamwandikia barua katibu mkuu wake kumjuza nia yake ya kuendelea kugombea kubaki kwenye nafasi hiyo.
Ulikuwa ni utaratibu wa CHADEMA kwa viongozi wa juu kutoshindania nafasi moja endapo mmoja ataonesha nia