Jamaa fulani anaona pikipiki mbili zinampita kwa mwendo wa kasi sana.
Kila pikipiki imebeba abiria wawili(mshikaki)
Hii ni baada ya kusikika milio mitano ya risasi
Yes A Dark day indeed
Baadae zikasambaa habari pale kisiwani kuwa Mlinzi mmoja wa mpaka wa shamba alikuwa “kalambwa vyuma” vitano na majambazi.
Naam!
It was a news tailored for journalists digest
Lakini nyuma ya pazia walinzi wa mipaka walikuwa wamegombana na bwana shamba two years back.
Kwanza walimchukia bwana shamba kwa kumleta kijana mdogo tu ndio awe kilanja wao lindoni.
Kijana huyo hakuwa na elimu dunia ya kutosha zaidi yao.
Yeye elimu dunia yake iliishia tu shule ya upili.
Elimu pekee aliyokuwa amebobea ni maswala ya mipaka.
Hakutegemewa kuwa Kilanja
Wakulima waliendelea kula ubwabwa na maharage na kwenda kulala.
Bila kujua mpakani mwa shamba kuna chess inachezwa.
Sasa Bwana shamba kuna maelekezo alitoa kwa kilanja akawaambie wenzake.
Ule haukuwa utaratibu
Namaanisha nini?
Yaani pale mpakani huwa kuna wazee ambao kiutaratibu kukiwa na jambo lolote, basi bwana shamba anatakiwa aongee nao pamoja akiwemo kilanja wao.
Sasa huu utaratibu wa kumtuma kilanja aongee nao hawakuupenda.
Na zaidi ya yote,
Maelekezo yaligusa maslahi yao
Unajua pale mpakani kulikuwa na Zabuni nyingi sana kuanzia catering services, Mafuta n.k
Zabuni hizi zilikuwa kiutaratibu zinachukuliwa na wazee ili nao wafurahie keki ya shamba kidogo.
Kwani wazee walikuwa wanaona wizi mkubwa tu pale shambani na kukaa kimya.
Zile zabuni angalau zilikuwa zinawafanya wazee wakae kimya na kutoingilia kwani uwezo wa kuingilia wanao na wanaweza kumweka bwana shamba yeyote kutokea kwenye kundi lao la wazee.
Sasa maelekezo yakatolewa kwa kilanja kwenda kwa wazee.
Kuwa zabuni sasa basi!
Yaani mchakato wa zabuni mpakani utakuwa unafanywa na bwana shamba kuanzia siku ya maelekezo hayo.
Mkutano ulikuwa wa moto!
Wazee wakafura!
Wakamuuliza kilanja huyo bwana shamba yuko wapi?
Kwa nini kakutuma wewe asije hapa azungumze hayo mbele yetu?
Wakamwambia unajua wewe ingawa ni kilanja lakini wewe ni bwana mdogo sana.
Wakamwabia kwanza wewe umeishia shule ya upili.. wewe sio size yetu, kamwite bwana shamba aje atueleze hayo.
Kilanja akarudisha zile taarifa kwa bwana shamba.
Bwana shamba alikuwa na tabia za ujeuri,
Hakuwa anapenda hata siku moja aonacho yeye ni sahii atokee mtu wa kukipinga.
Alishapewa ushauri na kilanja wa zamani kuwa kuna nyaya za kuchezea pale shambani lakini sio nyaya za transformer.
Hata bwana shamba wa zamani alimshauri hilo
Yeye hakutaka kusikia,
Sasa taarifa zile za mkutano wa mpakani zikamjia.
Akapuuzia kwenda mkutanoni.
Yeye akaanza kuwa anajihusisha na zabuni za watu wa mpakani.
Yaani wazee waliendelea kuhudumiwa bila wao kumtafuta muhudumu.
Bwana shamba hakujua kama swala lile ni nyeti.
Hakujua kama vikao vya usalama ndivyo vilivyoamua kuwa wazee wajipe zabuni wenyewe za kujihudumia.
Sababu kubwa ilikuwa kuwa kama mtu kutoka nje angewahudumia, angeweza kuwafanya chochote walinzi wa mpaka.
Mtu wa nje angeweza kuwa compromised akawawekea hata sumu kwenye chakula
Wazee walipoona tu Bwana shamba amewakwepa na kuanza kuwawekea watu wa nje kuwahudumia wakaamua kuandika barua kwa pamoja kuomba kuacha ulinzi.
This action a distress message security wise
Ikabidi bodaboda guy amfate bwanashamba.
Bodaboda guy without mincing words dared to inform Bwana shamba kuwa “Mzee hapa inamaanisha umeng’oa kiraka kwenye jeans ya bishoo”
Akamwambia “Find a way to resolve the matter before this deteriorated relationship with “wazee” sours much more.
Kama kawaida jamaa hapangiwi
Jamaa akaona hakuna threat yoyote
Lakini akawa ni mtu wa wasiwasi mwingi
Mara siku nyingine asilale kwenye nyumba ya bwana shamba.
Lutueni Kanali E.A Sambila ambaye ndiye Commanding Officer wa 831 KJ anapokea taarifa nyeti ofisini kwake kutoka kwa askari wake wawili wahusikao na ulinzi amani kikosini (MPs)
Askari hawa wawili ambao ni P.12925 Captain Theresia Cylil Massawe na MT. 88710 Sergeant Mohammed Faki Haji walifika ofisini kwa Lt.Gen Msambila wakieleza kuwa wana taarifa ya dharula
Kuwa kuna uwezekano wa muda wowote amani kutoweka mle kikosini
Wakaruhusiwa kuingia
Taarifa inayotolewa mbele ya CO, inalazimu muda mfupi unaofuata, askari wale wawili, kwa maelekezo ya CO wavamie ofisini kwa serviceman MT. 85115 Sergeant Sahani
Askari yule anawekwa chini ya ulinzi, na kwenye upekuzi, wanachukua simu mbili anazomiliki
Tarehe 28 August 2025, chama tawala, CCM kilizindua kampeni zake za uchaguzi mkuu wa urais na wabunge katika viwanja vya Tanganyika packers
CCM walilazimika kutumia jukwaa hilo la uzinduzi wa kampeni kujibu mashambulizi kutoka kwa mwanachama wake mwandamizi Humphrey Polepole
Tangu kujiuzuru kwake July 13, mwaka huu kwa kile alichoeleza kama "kutoridhishwa na mienendo" ya serikali yake, balozi huyo wa zamani wa Tanzania nchini Cuba, amekuwa akitoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi waandamizi wa chama chake na serikali
Polepole ameeleza juu ya uwepo wa kikundi anachokiita "CCM mtandao" ambacho huakikisha wanaohodhi madaraka ya rais
Kuwa mtandao huo nchini tangu mwaka 1995 zilipoanza siasa za vyama vingi na mtandao huu una agenda ya kuhakikisha kila rais anakuwa chini ya himaya yao
Mwaka 2012, Blandine Nyoni akiwa katibu mkuu wizara ya afya, alinukuliwa akitoa kauli tata ya kuwabeza madaktari kuwa "wanajiona bora wakati ni wachafu na hawajui kiingeleza"
Katibu huyu akaendelea kusema kuwa hata yeye alisoma mchepuo wa PCB na kufaulu vizuri tu lakini kwa kutambua ubovu wa Medicine mzazi wake akamsomesha Accounts so hajui madaktari wanalalamikia nini.
Kauli hii ikang'oa kilaka kwenye jeans ya bishoo!
Ni kwamba mwaka huo, madaktari walikuwa katikati ya mgomo wa kihistoria
Kauli hii ikawatibua madaktari wakalianzisha upyaaaaa
Wiki hii tumeshuudia waliokuwa wanachama wa Chadema wakitangaza kuachana na chama hicho huku wakiahidi kuelezea hatima zao za kisiasa siku za mbeleni
Kati ya waliohama ni waliowahi kuwa viongozi waandamizi wa chama hicho
Hii inamaanisha nini?
Kabla sijajibu swali hilo ni vyema tukipitia kwa ufupi mtiririko wa matukio (A quick refresher)
1. Dec 12,2024, Tundu Lissu anatangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA taifa
Nia hii ya Lissu ilikuja baada ya kuwa uchokozi wa wazi dhidi yake ndani ya chama
Kabla ya uamuzi huu, Lissu aliyekuwa ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA, alishamwandikia barua katibu mkuu wake kumjuza nia yake ya kuendelea kugombea kubaki kwenye nafasi hiyo.
Ulikuwa ni utaratibu wa CHADEMA kwa viongozi wa juu kutoshindania nafasi moja endapo mmoja ataonesha nia