Jamaa fulani anaona pikipiki mbili zinampita kwa mwendo wa kasi sana.
Kila pikipiki imebeba abiria wawili(mshikaki)
Hii ni baada ya kusikika milio mitano ya risasi
Yes A Dark day indeed
Baadae zikasambaa habari pale kisiwani kuwa Mlinzi mmoja wa mpaka wa shamba alikuwa “kalambwa vyuma” vitano na majambazi.
Naam!
It was a news tailored for journalists digest
Lakini nyuma ya pazia walinzi wa mipaka walikuwa wamegombana na bwana shamba two years back.
Kwanza walimchukia bwana shamba kwa kumleta kijana mdogo tu ndio awe kilanja wao lindoni.
Kijana huyo hakuwa na elimu dunia ya kutosha zaidi yao.
Yeye elimu dunia yake iliishia tu shule ya upili.
Elimu pekee aliyokuwa amebobea ni maswala ya mipaka.
Hakutegemewa kuwa Kilanja
Wakulima waliendelea kula ubwabwa na maharage na kwenda kulala.
Bila kujua mpakani mwa shamba kuna chess inachezwa.
Sasa Bwana shamba kuna maelekezo alitoa kwa kilanja akawaambie wenzake.
Ule haukuwa utaratibu
Namaanisha nini?
Yaani pale mpakani huwa kuna wazee ambao kiutaratibu kukiwa na jambo lolote, basi bwana shamba anatakiwa aongee nao pamoja akiwemo kilanja wao.
Sasa huu utaratibu wa kumtuma kilanja aongee nao hawakuupenda.
Na zaidi ya yote,
Maelekezo yaligusa maslahi yao
Unajua pale mpakani kulikuwa na Zabuni nyingi sana kuanzia catering services, Mafuta n.k
Zabuni hizi zilikuwa kiutaratibu zinachukuliwa na wazee ili nao wafurahie keki ya shamba kidogo.
Kwani wazee walikuwa wanaona wizi mkubwa tu pale shambani na kukaa kimya.
Zile zabuni angalau zilikuwa zinawafanya wazee wakae kimya na kutoingilia kwani uwezo wa kuingilia wanao na wanaweza kumweka bwana shamba yeyote kutokea kwenye kundi lao la wazee.
Sasa maelekezo yakatolewa kwa kilanja kwenda kwa wazee.
Kuwa zabuni sasa basi!
Yaani mchakato wa zabuni mpakani utakuwa unafanywa na bwana shamba kuanzia siku ya maelekezo hayo.
Mkutano ulikuwa wa moto!
Wazee wakafura!
Wakamuuliza kilanja huyo bwana shamba yuko wapi?
Kwa nini kakutuma wewe asije hapa azungumze hayo mbele yetu?
Wakamwambia unajua wewe ingawa ni kilanja lakini wewe ni bwana mdogo sana.
Wakamwabia kwanza wewe umeishia shule ya upili.. wewe sio size yetu, kamwite bwana shamba aje atueleze hayo.
Kilanja akarudisha zile taarifa kwa bwana shamba.
Bwana shamba alikuwa na tabia za ujeuri,
Hakuwa anapenda hata siku moja aonacho yeye ni sahii atokee mtu wa kukipinga.
Alishapewa ushauri na kilanja wa zamani kuwa kuna nyaya za kuchezea pale shambani lakini sio nyaya za transformer.
Hata bwana shamba wa zamani alimshauri hilo
Yeye hakutaka kusikia,
Sasa taarifa zile za mkutano wa mpakani zikamjia.
Akapuuzia kwenda mkutanoni.
Yeye akaanza kuwa anajihusisha na zabuni za watu wa mpakani.
Yaani wazee waliendelea kuhudumiwa bila wao kumtafuta muhudumu.
Bwana shamba hakujua kama swala lile ni nyeti.
Hakujua kama vikao vya usalama ndivyo vilivyoamua kuwa wazee wajipe zabuni wenyewe za kujihudumia.
Sababu kubwa ilikuwa kuwa kama mtu kutoka nje angewahudumia, angeweza kuwafanya chochote walinzi wa mpaka.
Mtu wa nje angeweza kuwa compromised akawawekea hata sumu kwenye chakula
Wazee walipoona tu Bwana shamba amewakwepa na kuanza kuwawekea watu wa nje kuwahudumia wakaamua kuandika barua kwa pamoja kuomba kuacha ulinzi.
This action a distress message security wise
Ikabidi bodaboda guy amfate bwanashamba.
Bodaboda guy without mincing words dared to inform Bwana shamba kuwa “Mzee hapa inamaanisha umeng’oa kiraka kwenye jeans ya bishoo”
Akamwambia “Find a way to resolve the matter before this deteriorated relationship with “wazee” sours much more.
Kama kawaida jamaa hapangiwi
Jamaa akaona hakuna threat yoyote
Lakini akawa ni mtu wa wasiwasi mwingi
Mara siku nyingine asilale kwenye nyumba ya bwana shamba.
Wiki hii tumeshuudia waliokuwa wanachama wa Chadema wakitangaza kuachana na chama hicho huku wakiahidi kuelezea hatima zao za kisiasa siku za mbeleni
Kati ya waliohama ni waliowahi kuwa viongozi waandamizi wa chama hicho
Hii inamaanisha nini?
Kabla sijajibu swali hilo ni vyema tukipitia kwa ufupi mtiririko wa matukio (A quick refresher)
1. Dec 12,2024, Tundu Lissu anatangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA taifa
Nia hii ya Lissu ilikuja baada ya kuwa uchokozi wa wazi dhidi yake ndani ya chama
Kabla ya uamuzi huu, Lissu aliyekuwa ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA, alishamwandikia barua katibu mkuu wake kumjuza nia yake ya kuendelea kugombea kubaki kwenye nafasi hiyo.
Ulikuwa ni utaratibu wa CHADEMA kwa viongozi wa juu kutoshindania nafasi moja endapo mmoja ataonesha nia
Polisi katika upelelezi wao wakatajiwa kuwa gari ile imeonekana akiwa nayo jambazi mmoja sugu sana ambaye alikuwa kwenye radar za polisi kwa muda mrefu.
Jambazi huyu si mwingine bali ni Ernest Joseph Sambua Mushi maarufu kwa jina la White
Taarifa zikadokeza jambazi lile lipo mkoni Kilimanjaro kwa wakati ule
Yule mfanyabiashara akajulishwa juu ya hili na akatoa gari lake na dereva ili kwenda Kilimanjaro
Jan 22, 2024 kwenye kikao cha baina ya CDF na makamanda kwa upande mmoja, na Amiri Jeshi mkuu kwa upande mwingine,Mkuu wa majeshi alitoa kauli iliyoibua udadisi
"Kuna wakimbizi wameteuliwa serikalini kwenye nafasi za maamuzi"
Kauli hii ilikuwa ni nzito kutoka kwa mtu mzito.
Nasema mtu mzito kwa kuwa, mtu aliyetoa kauli hii ni mwenye nafasi ya kupata taarifa zote za intelejensia za nchi hii
Kwanza kama mwenyekiti wa kamati ya majeshi ya ulinzi
Pili akiwa kama kiongozi kwenye taasisi yenye chombo kinachofanya "military intelligence" siku zote.
Kwa hiyo CDF Mkunda alikuwa anajua anachokizungumza ni sahii kutoka vyanzo sahii
Undisputed and not farfetched facts
Kauli hii kwa mtu asiyeutumia ubongo wake vizuri, ataisoma tu kwenye magazeti na kuachana nayo bila kuusumbua ubongo kuona yale yasiyoonekana.
Kumekuwepo na taarifa za kukamatwa kwa wahusika wa kampuni ya LEO BENEATH LONDON (LBL) inayoendesha biashara ya upatu, kukusanya amana, na kutoa riba kwa wanachama wake.
Victims wengi wa kampuni hii wakiwa ni watumishi wa kada ya ualimu
Pia Benki kuu imetoa taarifa ya kutoitambua wala kuipatia leseni kampuni hiyo.
Hapa ndipo napata maswali kuhusu umakini wa taasisi zetu zinazohusika na ukusanyaji wa taarifa za kiitelejensia
Taasisi hizi huwa hazipati fununu ya uwepo wa kampuni hizi kabla watu hawajatepeliwa?
Sasa hivi kuna kampuni nyingine inayojiita FIC
Kampuni hii inajinadi kuwa imesajiliwa BRELA na kupata cheti No. 177461385
Imepata TIN ya TRA No. 177-461-385 na kupewa cheti cha Tax Clearance
Sometimes March 2013 Wakili Fatuma Karume alisafiri kutoka Dar kwenda mkoani Kilimanjaro. Wakili huyu alikuwa amesafiri akiwa amebeba nyaraka furani ya muhimu. Nyaraka ile alikuwa anaenda kumsomea na kumkabidhi mzee fulani aliyefahamika kwa jina la Juma
Actually, Mzee Juma naye alikuwa ni wakili ambaye sasa amestaafu akiwa amefanikiwa kurithisha taaluma hiyo pia kwa mwanae ambaye alikuja kuwa ni wakili maarufu sana mkoni Arusha. Fatma hakujua kama nyaraka aliyobeba ingeleta taflani kubwa ndani ya familia ya Mzee Juma.
Fatma aliwasili nyumbani kwa ambako alikuta waombolezaji ambao walikusanyika baada ya kusambaa taarifa za msiba za mmoja wa watoto wa Mzee Juma. Fatma alitegemea kuikuta hali hii nyumbani pale na hata safari yake ilitokana na yeye kupata taarifa hizi.
Ni mara ngapi tumesikia watu wakitoa shuuda kuwa gari fulani lilimuacha na kisha mbeleni gari hilo likapata ajali? Hili ndilo lililomtokea Moses John miaka miwili iliyopita. kijana huyu ni muuza simu katika jengo la CHINA PLAZA lililoko mtaa wa Aggrey Kariakoo. Thread👇
Kuna wakati unaweza unaweza kushindwa kusafiri kwa sababu tu basi ulilopanga kusafiria limekuacha baada ya kuchelewa. Hupaswi kujilaumu kama hili litakutokea. Mara nyingine Mungu huwa anaingilia kati ili kukuepusha na baya ambalo lingeweza kukutokea ndani ya basi hilo.
Tarehe 26 December mwaka 2021, vijana kadhaa ambao wote wanajishughurisha kuuza simu kwenye jengo hilo, walikubaliana waende wakasherehekee sikukuu ya Christmas katika fukwe za Kigamboni.