Coach Ansey Profile picture
Digital Marketer | Content Creator | InfoPreneur Building @ThamaniAcademy
Apr 4, 2022 8 tweets 2 min read
SABABU 4 Kwanini wateja hawanunui BIDHAA zako.

~ Short Thread 👇 Image 1. Bado HAUELEWEKI.

Kosa kubwa unaloendelea kufanya, ni kujaribu kuuza bidhaa zako kwa kila mtu (Hauna Soko Maalumu).

Hali kama hii inaweza kukufanya utumie nguvu kubwa kuongea na watu wasioweza kabisa kununua bidhaa yako.
Mar 28, 2022 15 tweets 2 min read
MBINU zitakazokusaidia KUUZA Huduma zako kwa urahisi zaidi.

Siku zote, wateja huangalia ubora wa huduma wanayoipata bila kujali sekta ya biashara uliyopo.

Ndio maana, ni muhimu sana kufahamu ni kwa namna gani unaweza kuwafikia na kufikisha huduma zako kwa haraka.

#UZI Hizi ni Mbinu 5 zitakazokusaidia KUUZA huduma zako kwa urahisi, kupitia mitandao ya kijamii.

1. Hakikisha WANAKUTAMBUA mapema.

Ni rahisi kuuza huduma zako kama tu Audience watakuelewa mapema, na kufahamu THAMANI ya kile unachowapatia.
Oct 26, 2021 17 tweets 3 min read
MUHIMU: KAMA UNA ACCOUNT YA BIASHARA.

Huwa unajisikiaje pale unapowekeza juhudi & muda wako katika jambo flani, halafu usione matokeo?

Au

Umepanda mbegu zako vizuri, ukiwa na matumaini muda si mrefu zitaanza kuzaa matunda. Halafu gafla unaaza kuona zinanyauka/kufa? Enhee, sasa hiyo hali ndio utakayoipata pale unapoanza kuona followers wako wanapungua siku hadi siku katika Ukurasa wako wa Biashara.

Kama utagundua idadi ya followers wako inapungua, ni lazima uchunguze na kutafuta suluhu haraka sana!
Oct 14, 2021 13 tweets 3 min read
UNATESEKA KUPATA MAUZO KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII?

Inawezekana una Bidhaa nzuri, una Huduma bora kabisa, una post kila siku kwenye account zako, lakini huoni ukipata faida yoyote kupitia mitandao ya kijamii unayotumia

Nina Habari njema sana kwako siku ya leo

Are you ready?🤔 Kabla haujafanya uamuzi wa kufuta post zako, au kufunga kabisa kurasa za biashara yako...

Nataka kukuonyesha Hatua 5 muhimu sana zinazoweza kukusaidia ili kupata matokeo mazuri.

Twende wote taratibu sasa...
Oct 13, 2021 13 tweets 3 min read
UNASHINDWA KUANDIKA CAPTION NZURI KATIKA POST ZAKO?

Kama una Brand au unaendesha biashara yako kupitia Mitandao ya kijamii...

... basi utakuwa unafahamu ni ngumu kiasi gani kuja na mawazo ya kuandika kila siku katika kila post unayoweka kwenye ukurasa wako. Kutokana na jinsi unavyotaka watu wakutazame kupitia Brand/biashara yako...

...Unaweza kuchagua Tone ya sauti unayotaka watu wakutambue nayo.

Kupitia Caption zako, unaweza kuonekana Mcheshi, Mpole, au serious kiasi.

Sasa Social Media Entrepreneurs wengi ni WAVIVU mno...
Aug 18, 2021 21 tweets 5 min read
MBINU 5 ZITAKAZOKUSAIDIA KUKUZA BIASHARA YAKO KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII.

Inawezekana hapo ulipo umekwama, huoni maendeleo yoyote ya biashara yako, wakati huo huo unaona wapinzani wako wanaendelea kupiga hatua.

Upo katika hali hiyo? Usiwe na wasiwasi, kila mfanyabiashara au mjasiriamali kama wewe, amewahi kupitia hali kama hiyo.

Kama umeshindwa leo, haina maana utaendelea kushindwa kila siku.

Au unasemaje Brother @mafolebaraka ?
Aug 16, 2021 13 tweets 4 min read
JINSI YA KUTENGENEZA MAUDHUI (CONTENTS) YENYE KUONGEZA USHAWISHI KWA MTEJA.

Mara nyingi katika kutengeneza Maudhui, tunatumia mawazo, Ideas na ushawishi wetu binafsi...

..lakini, kuzingatia muonekano na aina ya Maudhui yanayoandikwa ni jambo muhimu mno. Ni rahisi sana kutengeneza mawazo na topic mbalimbali kwa ajili ya wateja wako...

..Lakini, kama muuzaji, ni lazima uwe na uelewa mkubwa wa namna ya kuwasilisha mawazo hayo kwa mteja wako.