D A L A L I Profile picture
■Half Genious ■Half Dumb
Mar 5 18 tweets 3 min read
Kijana alikuwa amekaa dukani kwa boss wake, mara akaja mwamba flani hivi

Kijana: Karibu kaka

Mwamba: Asante dogo, Mambo vipi

Kijana: Poa bro, karibu sana

Mwamba: Okay.. naona una bidhaa zote ambazo boss wangu anahitaji

Kijana: Ndio kaka, bidhaa zipo zipo Image Mwamba: Okay

Mwamba akaanza kuuliza bei ya vitu anaandika kwenye kikaratasi..

Mwamba: Sasa mi ni daktari wa mifugo, Kuna boss wangu mmoja namsimamia nguruwe wake hapo Mapinga, ndo nataka niwachukulie virutubisho kwa ajili ya chakula....
Feb 25, 2023 16 tweets 4 min read
THE EAST AFRICAN KINGMAKER

Always in a position to score the winning goal.. June mwaka 2021 kampuni ya mtanzania mzalendo aliyeanza biashara kwa kuuza sigara na pipi kifua kwenye sinia. Namaanisha Taifa Gas ya Rostam Aziz ilipewa kibali cha kuanza ujenzi wa plant yake maeneo ya Dongo Kundu mjini Mombasa..
May 23, 2022 16 tweets 3 min read
Story ya KITAPELI

Wakati niko Advance ile likizo kabla ya mitihani ya utani (MOCK) nikarudi zangu home. Nikapewa hela za tuition nisome prac. nijiandae na paper

Kuna jamaa yangu akaniomba nimkopeshe zile hela atanirudishia in one week period, with interest. Nikaona ni BINGO, nika-buy in.. nikampa zote (km 70k hivi) kwa makubaliano kuwa atanirudishia 100k

Jamaa akapotea mazima. Nikashindwa kusoma practical. Ile likizo inaisha nikaona kabsa kwa jinsi nlivyo mweupe nitaaibisha ukoo kwenye MOCK. Ikabidi nitengeneze plot nisifanye MOCK
May 8, 2022 22 tweets 4 min read
Sicarios - Wauaji maalum wanaotumiwa na magenge ya madawa ya kulevya kupanua himaya zao Amerika kusini

#UZI 👇 Mwaka 1993 tajiri namba moja duniani alikuwa m-Japan mmoja wakuitwa Yoshiaki Tsutsumi

Huyu somo mwaka huo alikuwa na utajiri wa dola za kimarekani bilioni 9
May 3, 2022 25 tweets 6 min read
DO or DIE - A Tale of an INTRUDER in North Mara Gold Mine (Nyamongo) - (True Story) - Thread 1. Kwanza kabisa mimi ZOLENDRONIC ni mzaliwa wa wilaya ya Tarime mkoa wa Mara..

Japo maisha yangu kiasi kikubwa nmekulia nje ya Mara, nlitoka nikiwa mdogo ila najua culture kiasi (lugha na baadhi ya vitu)

20** nmemaliza zangu F6. Nikarudi nyumbani wakati nasubiria matokeo
Feb 6, 2022 22 tweets 5 min read
BEEF YA NAS NA JAY Z

#UZI

April 30, 2021 mwanetu DJ Khaled aliachia album yake ya 12..

Ndani ya ile album kuna ngoma inaitwa 'SORRY NOT SORRY'

Ndani ya hiyo ngoma kuna ma-legendary wawili wa Rap, wazaliwa wa New York. Wana wanachana ki-boss sana kuelezea mafanikio yao mle Hapa kuna Nasir Jones aka Nas, kule kuna Sean Carter au Jay Z.. kiitikio kimegongwa na James Fauntleroy

Ni ngoma ya kitajiri sana. Wana hawajatumia nguvu nyingi, wanatiririka tu ki-boss sana na wanaeleweka (si unajua tena tajiri hata akikohoa kuna kitu anakuwa anamaanisha😁😁)
Jan 23, 2022 25 tweets 6 min read
BEEF YA LIL WAYNE NA BIRDMAN

#UZI

Mwaka 2017 Rick Ross aliachia album yake ya tisa kwa jina 'Rather You Than Me'

Ndani yake kulikuwa na ngoma kali kali pamoja na diss track moja kali sana kwa jina "Idols Become Rivals"

Hii ni diss track maalum kwa ajili ya Birdman Rosey alimdiss sana mle ndani kutokana na jinsi mwana alivyokuwa anam-treat mshkaji wake wa muda mrefu Lil Wayne

Mle ndani Ross anasema kabla hajatoka alikuwa anawaangalia Birdman na Wayne anatamani maisha yao. Hakutegemea Birdman anaweza kumtenda Wayne vibaya
Jan 17, 2022 24 tweets 6 min read
BEEF YA KANYE WEST NA JAY - Z
#UZI

Kama ulishawahi kusikiliza ile album ya Kanye kwa jina Graduation bila shaka unaujua wimbo unaitwa 'Big Brother'

Ule ni wimbo spesho kabsa ambao mwana alimuimbia mshkaji wake wa faida (yaani km ile tattoo ya Mondi kwa mmakonde😃) Ndani ya ule wimbo kuna line inasema 'But he got me out my mama crib'

Kanye hajapiga hustle sana mtaani km wenzake waliotusua kupitia game ya rap

Jamaa ni wa kishua tu, mama'ake (Donda West) alikuwa professor wa chuo kikuu cha Chicago akiwa mkuu wa idara kabisa