My Authors
Read all threads
UKUAJI NA MAENDELEO YA MTOTO.

UKUAJI ni hali ya kuongezeka kwa ukubwa(size) ya mwili wa mtoto
 
Maendeleo ni hali ya mtoto kuweza kufanya jambo fulani kwa wakati fulani unaotarajiwa.

Mfano kutoka kutambaa hadi kutembea. 
#afyakwawote. Image
Ukuaji wa mtoto huanza baada ya mimba kutungwa.

Ukuaji na maendeleo ya mtoto huenda sambamba ila kwa kasi tofauti tofauti. 

#afyakwawote.
HATUA ZA UKUAJI WA MTOTO.

ukuaji wa mtoto unaweza gawanywa katika makundi makuu mawili ambayo ni

1. Baada ya mimba kutungwa (pre natal)

2. Baada ya mtoto kuzaliwa (post natal)

#afyakwawote.
BAADA YA MIMBA KUTUNGWA. 

Baada ya miezi mitatu ya mimba kutungwa ogani mbali mbali  kama ubongo, figo, mapafu moyo na nyinginezo huanza kutengenezwa.

#afyakwawote Image
Katika kipindi hiki mazingira hatarishi kwa mama yanaweza kumpelekea mtoto kuzaliwa na matatizo kama moyo, ukiziwi, upofu, na maambukizi mengine. 

Mazingira haya ni kama Uvutaji wa sigara,  mionzi (x rays) baadhi ya dawa na virus. 

#afyakwawote
Baada ya miezi sita ogani zote huwa zimetengenezwa na hukua kwa kasi sana.

Lishe duni, upungufu wa damu na malaria huathiri ukuaji wa mtoto katika kipindi hicho na mtoto huzaliwa na uzito mdogo au kudumaa akiwa angali tumboni kwa mama. 
#afyakwawote. Image
BAADA YA KUZALIWA. 
Hapa tunaweza kugawa kipindi hiki katika hatua nyingine ndogo tatu ambazo ni

1. Mtoto mchanga
2. Mtoto
3. Balehe.

#Afyakwawote ImageImageImage
Kipindi cha utoto uchanga huanza siku ya kwanza mtoto anapozaliwa hadi miezi 6 ya kwanza.

Kipindi hiki hutegemea sana hali ya lishe anayopata mtoto.

Katika miezi hii mtoto anatakiwa kupewa maziwa ya mama tu na si vinginevyo.

#afyakwawote.
Kipindi cha utoto huanza miezi sita na kuendelea ambapo dalili za mtoto kukua huwa ni za wazi wazi .

Kipindi hiki hutegemea sana vichocheo vya ukuaji katika mwili.

#afyakwawote
Kipindi cha balehe huwa ni kipindi cha kukua kimaumbile na via vya uzazi pia kukua.

Kwa wasichana huanza balehe Kati ya miaka 8_13 na kwa wavulana ni Kati ya 9_14.

#AfyaKwaWote
VIASHIRIA VYA UKUAJI WA MTOTO.

1. UZITO.

Baada ya mtoto kuzaliwa uzito wake hupungua kwa asilimia Kati ya 5% hadi 10% ndani ya wiki 2.
#afyakwawote. Image
#afyakwawote.

Kisha uzito huongezeka mara mbili yake ndani ya miezi 6, huongezeka tena mara 3 ndani ya miezi 9_12, huongezeka mara 4 ndani ya miaka miwili na baada ya hapo huongezeka kwa kilo 2 kila,mwaka.
#AfyaKwaWote
UREFU.

Urefu wakati wa kuzaliwa huwa ni 50cm kwa wastani,  Kisha 75cm baada ya mwaka mmoja na hufikia 100 cm baada ya miaka 5.
#afyakwawote Image
MZINGO WA KICHWA.
Huu huongezeka kwa kasi hadi kufikia 15 cm na kisha kuongezeka taratibu taratibu kadri muda unavozidi kwenda.
#afyakwawote. Image
SABABU ZINAZOCHANGIA UKUAJI WA MTOTO. 

1. Genetics /urithi. Wazazi wenye vimo vifupi huzaa watoto wenye vimo vifupi,  hivyo hivyo kwa wazazi warefu.

#afyakwawote.
2.  Lishe bora.  Lishe bora hupelekea mtoto kukua kwa kasi nzuri. 
3.  Vichocheo vya ukuaji 
4.  Magonjwa. Magonjwa wakati wa utoto hupelekea mtoto kupungua uzito na kudumaa pia.
#afyakwawote.
HATUA ZA MAENDELEO YA MTOTO.

Maendeleo ya mtoto ni jumla ya shughuli zote( kijamii, kitabia na kimatendo) anazoweza kufanya mtoto kutokana na umri alionao.

Hatua hizi huitwa developmental milestones na hugawanywa kwa miezi.
#AfyaKwaWote
MAENDELEO YA MTOTO WA MIEZI 2.

KIJAMII
1.Huanza kutabasamu anapowaona watu au unapocheza nae. Hasa watu wa karibu anaokaa nao kila siku.

2. Anaweza kujituliza mwenyewe kwa kuleta mkono wake mdomoni na kuunyonya.

3.Anaweza kuanza kutazama wazazi au mlezi wake.
#afyakwawote . Image
KIMATENDO
Anaweza kumfuata mtu kwa kugeuza kichwa

Kwa kiasi kidogo anaweza kukaza shingo, pale anapoinuliwa kwa mikono.

#afyakwawote.
KUONGEA NA LUGHA 
Huanza kutoa sauti ndogo ndogo kama anacheka (cooing and gurgling)

Anaweza kugeuza kichwa kuelekea upande sauti inapotoka.
#afyakwawote.
KIAKILI
Anaweza kuanza kutambua uso. Atapendelea zaidi nyuso za watu aliowazoea.

Anaanza kufuata vitu kwa macho. Anaweza akapendelea kutazama upande wenye televisheni au vitu vingine.

Atalia iwapo hajisikii vizuri au hafurahii kitu kinachofanyika. #afyakwawote.
MIEZI 4.
Hucheka mara kwa mara, huanza kuiga maneno anayosikia, huanza kuvifata vitu kwa mkono mmoja, huanza kupelekea mikono kinywani na huanza kumtambua mama.
#AfyaKwaWote Image
MIEZI 6.
Huweza kutambua sura ngeni na aliowazoea.

Huanza kuonyesha muitikio akiitwa jina lake.

Huweza kukaa bila msaada.

Huanza kuvifata vitu vilivyo mbali

#AfyaKwaWote Image
MIEZI 9.

Huanza kutamka neno kama mamamaaaaa.

Hutambaa na kuanza kusimama bila msaada.
Hutumii kidole kuonyesha vitu.
#AfyaKwaWote Image
MIEZI 18.
Hutamka baadhi ya maneno

Huanza kuvitambua baadhi ya vitu vya kawaida

Hutembea pekee yake bila msaada. Image
SABABU ZINAZOCHANGIA MAENDELEO YA MTOTO.

1.Lishe

2.Msaada wa kihisia. Ili mtoto aendelee vizuri lazima ahisi anapendwa na wazazi na jamii inayomzunguka,  ajihisi yupo salama wakati wote, ajihisi yupo huru,  ajihisi anathaminiwa na anakubalika kama mtu.

#afyakwawote.
Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh.

Enjoying this thread?

Keep Current with njole julian

Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

Twitter may remove this content at anytime, convert it as a PDF, save and print for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video

1) Follow Thread Reader App on Twitter so you can easily mention us!

2) Go to a Twitter thread (series of Tweets by the same owner) and mention us with a keyword "unroll" @threadreaderapp unroll

You can practice here first or read more on our help page!

Follow Us on Twitter!

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just three indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!