HabariTech Profile picture
Oct 12, 2021 19 tweets 5 min read Read on X
📡Mass Surveillance Afrika na Duniani kote.

Huu ni uchunguzi ambao unajikita kufatilia umati mkubwa wa watu na mara nyingi huwa kwa kigezo cha kupunguza uharifu na kuzuia ugaidi.

Mass surveillance inasemakana kuanza miaka ya 3800 kabla ya kristo huko Babylon.

#HabariTech Image
📡Kwa vizazi vya sasa Mass Surveillance haikuonekana mpaka miaka ya mwisho ya 1940s baada ya UK na USA walikubaliana kubadilishana taarifa za intelejensia.

Baadae katika makubaliano haya ziliongezeka Canada, Australia na New Zealand na kufanya muunganiko huu kuitwa “Five Eyes”. Image
📡Muungano huu baadae mwaka 1971 ulileta kitu kilichoitwa “Global Surveillance Network” ambayo ilipewa jina la “ECHELON”.

ECHELON ni mtandao maalum wa uliofuatilia mawasiliano ya kijeshi na kidiplomati ya Soviet Union na washirika wake wa Mashariki kipindi cha Vita Baridi. Image
📡Kufikia mwisho wa karne ya 20 “ECHELON” ilitoka kufatilia mawasiliano ya kivita na diplomati mpaka kuanza fatilia mawasiliano binafsi ya mtu mmoja mmoja nay a kampuni.

Turuke mbele mpaka karne ya 21. Bilas haka umeshasikia neno NSA?
📡NSA ni shirika la juu kabisa la intelejensia la USA. Shirika hili lilianzishwa na Raisi Harry Truman mwaka1952, lakini liliendeshwa kwa siri mpaka mwaka 1975. Image
📡Huku kwetu wengi walilifahamu/kusikia kuhusu NSA mwaka 2013 Edward Snowden alipotoa siri kwamba NSA wanafanya Mass Surveillance ya Wamarekani na watu wote duniani bila idhini yetu.

Baada ya kujulikana NSA waliacha kufanya hivyo? Hapana, kazi iliendelea kama kawaida. Image
📡Marekani waliipa hii kitu jina la Mass Surveillance State kwa kigezo cha kwamba wanafanya hivyo ili kujilinda dhidi ya matukio ya kigaidi kama lile la 9/11.

Sio Marekani pekee wanaofanya hivyo. China pia wanahusika na Mass Surveillance.
📡China mwaka 2005 walianzisha mtandao wa Camera za kufanya mass surveillance ulioitwa Skynet.

Serikali ya China ilikuja kuweka wazi kuhusiana na mtandao huu mwaka 2013 baada ya kufunga CCTV cameras 20 million ndani ya China. Image
📡Hizo ni zile tu zinazomilikiwa na serikali ya China bila kujumuisha za Kampuni na Watu binafsi.

Kufikia June mwaka huu serikali ya China ndiyo inayoongoza kumiliki camera za CCTV zinazofanya kazi ya kufatilia watu wake.
📡Dunia nzima kuna CCTV camera 770 million, kati ya hizo China inamiliki CCTV 415.8 Million (54% ya zilizopo).

Serikali hizi zikiulizwa maoni yao ni kwamba camera hizi zinawasaidia kupunguza uhaifu, Usalama barabarani na kufatilia uendashaji wa viwanda. Image
📡Wasichotuambia ni namna zinatumika kuchunguza maisha ya watu. CCTV za kisasa zinaweza kufanya mpaka facial recognition, kufanya video streaming remotely.

Hivi ni vitu ambavyo huko mbeleni vitaingilia privacy ya mtu.
📡Kwa namna moja zinasaida mfano Polisi wa New Delhi india walipoamua kutumia CCTV zenye facial recognition. Ndani ya siku 4 ziliwasaidia kuwapata watoto 3000 walioripotiwa kupotea.

Huko china CCTV za hivi zina historia mbaya kwa kiasi kikubwa.
📡Mara kadhaa zimekuwa zikiwatambua watu wenye ndevu nyingi na wanatumia milango ya nyuma kutoka majumbani mwao kama magaidi.

Na kuna baadhi mpaka sasa wapo chini ya ulinzi baada ya kukutwa na app ya Whatsapp kwa sababu imezuiliwa nchini China.
📡Baadhi ya nchi za Afrika zimeanza kuingia katika mfumo huu polepole kwenye baadhi ya miji yao.

Miji kama Nairobi (Kenya), Johannesburg (South Africa), Addis Ababa(Ethiopia) na Kampala (Uganda).
📡Africa inatumia teknolojia tofauti tofauti kutoka mataifa ya nje kufanya mass surveillance.

Teknolojia kutoka Israel, Germany na China ndizo zinatumika kwa wingi zaidi. Kutoka Israel teknolojia za kutfatilia mawasiliano wa watu ndizo zinatumika zaidi Afrika. Image
📡Nchi za Afrika zilizoonekana kutumia hizi teknolijia zaidi ni Botswana, Nigeria na Zimbabwe.

Katika nchi 13 za Afrika zinazofanya Mass Surveillance ikiwemo Tanzania kulingana na taarifa ya “Africa Center” zote bado zinashida kubwa ya demokrasia.
📡Serikali za nchi hizi zinafanya uhalifu wa kufatilia mawasialiano ya wanachi wao kinyume na sharia za mitandao.

Na mbaya zaidi ni kwamba katika nchi hizi hakuna hata moja yenye sharia za ulinzi wa data za kimtandao na kama inazo basi bado zina mianya mingi.
📡Utumiaji wa bidhaa za ufuatiliaji Africa unahiska zaidi na project ya Huawei ya Safe cities. Kulingana na Huawei wamesema kwa Kenya imesadia kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa.

Lakini polisi wa kenya walisema ni kinyume cha hivyo. Image
📡Afrika kwa sasa ipo katika mabadiliko ya kidijitali. Kuna haja ya kuwa na uelewa wa haki zetu za kidijitali, lakini pia kujua namna tunaweza kulinda haki zetu mtandaoni. Image

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with HabariTech

HabariTech Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @HabariTech

Aug 30, 2022
⚡Unataka Kupunguza Muda Unaotumia kwenye Mitandao ya Kijamii? Soma Hii

Tunachoongelea ni mitandao ya kijamii. Huduma ambayo inafanya kazi yake vizuri mno.

Kazi yake ni kuhakikisha muda wote tunaangalia screen za simu zetu au PC.
⚡Wazo wa la kusema kwamba tunaweza kabisa kuacha mitandao ya kijamii, ni kama kuamini kwamba mwakani teknolojia ya time travel itakuwepo.

Ni ngumu na haiwezekani kuachana kabisa na mitandao ya kijamii, hivyo kilichobaki ni kujaribu kupunguza muda tunaotumia kwa kufanya haya.
1. Chagua siku moja kila wiki usiingie kabisa kwenye Mitandao ya kijamii

Ukisoma unaweza dhani ni rahisi kufanikisha hili jambo ila ni ngumu kama kushinda njaa zaidi ya siku mbili.
Read 19 tweets
May 31, 2022
🎭Kuona location, SMS & Calls bila yeye kujua

Unaweza kuhack simu/facebook/instagram ya mtu?

Bila shaka hili ni swali ambalo kila IT amewahi kusikia au kuulizwa yeye mwenyewe.

Kwanini watu wanatamani kuwafatilia ndugu/rafiki/wapenzi wao?
🎭Kisayansi hata mimi sijui. Binafsi nadhani ni hali tu ya ubinadamu kutaka kujua nini kinaendelea katika maisha mwingine.

Ni wazi kwamba binadamu tunapenda kuwa wa kwanza kujua kitu na kuwa juu kuzidi mwingine muda wote.
🎭Hii ni kwa sababu ya ubinafsi unaoishi ndani ya kila mmoja wetu.

Je, gharama ya kuwa na hali hii na kuingilia faragha ya mtu ni ipi?

Kulingana na sheria za mitandao za Tanzania “Cyber Act (2015)” ni kinyume cha sheria kutumia kifaa cha mawasiliano cha mtu bila ruhusa yake.
Read 5 tweets
Mar 15, 2022
🎁T O R R E N T S, Zinafanya vipi kazi?

Naweka dau langu kwamba ukisikia torrents, kitu kinakuja kichwani mwako ni software, video au audio za wizi (Pirated Files).

Uko sahihi lakini, torrent protocol haihusiana na hivyo tu.

#HabariTech
🎁Torrents ni nini?

Kwanini pirates wanatumia torrents kusambaza na kupakua files zao?

Huduma nyingine za internet zinazoendana na torrents kwanini hazitumiki katika sharing ya pirated files?

Haya maswali yote yanapatiwa majibu kupitia Bittorrent protocol.
🎁Unapofungua browser ili kuperuzi mtandao, browser inatuma request kwenda kwenye server yenye IP address ya website unayotaka kuifikia.

Request hii inaenda kuiomba server ikupe HTML za hiyo website ili uweze kuiona na kufanya kitu unataka.
Read 28 tweets
Mar 15, 2022
👽Russia hawataweza kuvuka vikwazo vya Teknolojia

24 February 2022, baada ya Russia kuvamia Ukraine, serikali ya Marekani ilitangaza vikwazo vya kwanza Russia.

Katika vikwazo hivyo vilikuwemo vinavyogusia teknolojia.

#HabariTech
👽Moja ya kikwazo kilisema, "Kuzuia zaidi ya nusu ya uagizaji wa Russia kuingiza teknolojia ya juu nchini mwao, Kuzuia Russia kupata pembejeo muhimu za kiteknolojia, Kudhoofisha msingi wao wa viwanda...
👽...na kudhoofisha matarajio ya kimkakati ya Russia ya kuwa na Ushawishi katika jukwaa la ulimwengu." -mwisho wa nukuu.

Inawezekana ilionekana ni kikwazo kikubwa kwa muda huo. Ila ni kidogo sana ukilinganisha na yaliyofata baada ya hapo.
Read 33 tweets
Mar 14, 2022
🍿Nini Kiliwakuta Founders wa Pirates Bay

Pirates bay ni kati ya website bora za kufanya piracy ya Games, Softwares, Movies, Music na aina nyingi ya files zinazokuwepo online.

Ni website ambayo iko kinyume na sheria za hakimiliki na haikutakiwa kuwepo.

#HabariTech
🍿Kampuni nyingi na wanasheria duniani wamejaribu sana kuhakikisha website hii haipatikani mtandaoni bila mafanikio.

Kwa kuwa content zinazokuwepo huko hazikutakiwa kuwepo na mara nyingi zinawakosesha mauzo kwa kuwa ni usambazaji wa content usio sahihi.
🍿Kuna miaka ya nyuma waliwahi fanikiwa kuiondoa online. Bahati mbaya mafanikio yao hayakudumu kwa muda mrefu.

Saa chache baada ya kuondolewa online website ya Pirates bay ilirudi online. Hivyo wakaona wabadili namna ya mashambulizi yao.
Read 41 tweets
Jan 24, 2022
🚀Sifa Kuu ya MATAPELI

Kwa sasa teknolojia imefanya kupata pesa iwe rahisi sana, lakini kupoteza ni rahisi zaidi 😁.

Kutapeliwa ni dakika 0.

Kila unapogusa mtandaoni sasa hivi kuna haya maneno NFT, Cryptocurrency, Bitcoin.

Lengo ni PESA.
🚀Bahati mbaya wengi mnaishia kuumia kwa sababu mnakosa maarifa.

Mnaingia kichwa kichwa katika biashara msizoelewa haswa ziko vipi.

Kwa sababu hiyo unajikuta unajitapeli wewe mwenyewe. Ulikosea mwanzo kutotaka kusoma inakuaje wengine wanapata faida.
🚀Siri kubwa ya matapeli hata sio kubwa kivile. Ila tu kwa kuwa wengi hatuumizi akili huwa tunaipita tu.

Tapeli guru kabisa ana siri moja.

Kipindi ambacho dhahabu inapatikana kwa wingi yeye huwa hajishughulishi na uchimbaji.

Image Credit: @MaujanjaCrypto
Read 9 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(