Una umri gani?
Umewahi kuwasikia watu hawa? 1. Bokoman Mkongoman 2. Limonga Justin Limonga 3. Chidi chidi Chitenda 3. Wajadi Fundi 4. Mwalimu Mashaka Sabuni 5. Alafa Kapilima 6. Thomas Mushi Kimboka
Na Zakaria Ndemfoo wakiwa safarini kuelekea Mahuta Newala?
Nazungumzia enzi zileee za post kadi kipindi cha Jambo, Mchana Mwema, Salam za mchana, Shambani, na pole kwa kazi...
Story kidogo kuhusu hawa jamaa ni siku walipomchezee mtu mzima Charles Hilary akiwa redio one
Alipiga simu Muhiru Obare na kuweka kikorombwezo Niambriiiiiiieeeee
Charles Hilary akakasirika sana akamkandia kiaina na akaweka wazi kuwa hapendi hiyo tabia ya watu kutamka hivyo (Niambriiiieee!). Akapiga simu Mkaudi Mkaudo Tingisha naye akaweka vikorombwezo hivyo hivyo Charles akamkatia cm akachukia sana .👇
Mtu wa tatu kupiga simu ni Ima Kulaya, akatuma salama kama kawaida ila mwisho akamwambia Charles ;
IMA KULAYA: Brother Charles eeh!
CHARLES HILARY: Ndio Ima kulaya
IMA KULAYA: Watu wengine sio wastaarabu kabisa
👇
CHARLES HILARY: Kweli kabisa Ima kulaya,kwa nini wasiige watu wastaarabu kama wewe!
IMA KULAYA: Huwa nawachukia sana hawa jamaa wanaosema Niambriiiiiiiiiiiiiiiiieeeeeeiii
Charles Hilary alicheka sana mwenyewe kwani Imma naye alifanya yale yale ila kwa style nyingine.
Tokea hapo ikabidi awe anawaacha wazee wa niambriiiieeee koma koma,sela sela,nukta nukta.
Mkasa mwingine ulikuwa ule wa kutuma salamu kwa zaidi ya watu 3,👇
Charles Hilary aliwashindwa kabisa jamaa kwani kitendo cha kupokea simu tu, mtu kama Papaa Osama alikuwa ameshataja watu kama 6. Walikwa na swaga za aina yake
Charles Hilary : Karibu Papaa Osama ,tuma salaam
Papaa Osama : Charles Hilary! Nipo na Mwiri Obare,Mamka Mushi,....
... Chesco Mzee wa Matunda wakusalimu sana.Chidi Chitenda anamuuguza Maalim Litumbi hivyo hatafika . Kaka Charles Natuma Salaam kwa watu watatu kama ifuatavyo moja Chivalavala akiwa pale kwa Makabureta Pili kwa David Bekham Onana na Mwisho kwa Mohamed Kiyai yai ambaye..
.. ametapeliwa saa na Baba Dula 1.
Charles Hilary : Haya bwana..!
Kuwadhibiti ilikuwa inashindikana kwani walikuwa wanaspeed kali sana hawa jamaa katika kutaja majina haswa Muhiri Obare na Limonga J. Limonga
Kuna mmoja alikua anajiita 'Jemedari Mkuu aliyevuka maji ya shingo bila mgongoni kuloa'
Enzi za call box za TTCL,enzi za Tritel na mwanzo wa BUZZ,Long time sana. Mwingine unakuta anapiga simu hadi BBC anampa ushauri al asad sasa sijui ujumbe ulikuwa unawafikia?
• • •
Missing some Tweet in this thread? You can try to
force a refresh
Kwenye kesi za mauaji, ili kufikia hukumu ya haki, mahakama hutaka kujiridhisha kama elements mbili zimethibitishwa bila kuacha shaka.
1. Actus reus/ Tendo ovu (lazima liwe limetendeka)
2. Mens rea /dhamira ovu.
Dhamira ovu inaangaliwa kwenye angle mbalimbali...
Kwenye kesi hii naangazia matendo ya mshtakiwa kabla na baada ya kitendo kiovu.
Utetezi wake ungekuwa na nguvu sana, lakini matendo yake yalitia shaka.
Hapa namuongelea DAUDI KAPEJA.
Fatilia mkasa huu,
👇
19/04/2014 UYUI, TABORA
Majira ya saa 4 usiku, BARESA RASHID aliambatana na DAUDI KAPEJA nyumbani kwake ambapo alichukua jacket na kumuaga mkewe kuwa wanakwenda kumuona jamaa aitwaye JUMA BUSEGA ili kufanya biashara ya tumbaku.
Mahakama ya Kinondoni imemwandikia Christian Makonda kufika mahakamani tarehe 3 February 2022 kujibu Miscellaneous Criminal Application Na. 1 ya mwaka 2022 na imepangwa kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi, Aron Lyamuya.
👇
Makonda anashitakiwa kwa kuvamia kituo cha clouds tarehe 17 March 2017 saa nne usiku.
Siku ya tukio alifika akiendesha gari yake mwenyewe yenye usajili T 553 BFM akiwa na Askari wanne waliovaa sare za majeshi mbalimbali.
👇
Lengo lilikuwa ni kushinikiza watangazaji warushe kwenye kipindi video ya mwanamke aliyefahamika kwa jina la GRACE ATHUMANI akifanya tendo la ndoa na Askofu Gwajima.
Hii ilikuwa ni miaka ya '90 mwanzoni, tukitokea pembezoni mwa mgodi wa Mwadui, tulifahamika kwa jina la "Wabeshi".
Zana zetu za kazi ilikuwa ni sululu, chepe na majembe yaliyonolewa sana, tulikabiliana na jeshi la polisi la mgodi wa Mwadui waliokuwa na kikosi cha farasi na mbwa wenye uweredi mkubwa sana na mafunzo ya hali ya juu.
Nakumbuka siku rafiki zangu wawili walivyouwawa kwa kuumwa na mbwa sehemu za siri na jirani yangu Jilingumika Masufulia alivyopigwa risasi ya kichwa akivuka fensi ya mgodi wa Mwadui.