HabariTech Profile picture
Mar 15, 2022 28 tweets 9 min read Read on X
🎁T O R R E N T S, Zinafanya vipi kazi?

Naweka dau langu kwamba ukisikia torrents, kitu kinakuja kichwani mwako ni software, video au audio za wizi (Pirated Files).

Uko sahihi lakini, torrent protocol haihusiana na hivyo tu.

#HabariTech
🎁Torrents ni nini?

Kwanini pirates wanatumia torrents kusambaza na kupakua files zao?

Huduma nyingine za internet zinazoendana na torrents kwanini hazitumiki katika sharing ya pirated files?

Haya maswali yote yanapatiwa majibu kupitia Bittorrent protocol.
🎁Unapofungua browser ili kuperuzi mtandao, browser inatuma request kwenda kwenye server yenye IP address ya website unayotaka kuifikia.

Request hii inaenda kuiomba server ikupe HTML za hiyo website ili uweze kuiona na kufanya kitu unataka.
🎁Ombi lako likikubalika, kwamba server iko hewani na website unataka kuifikia ipo, jibu linarudi kwako kwa mfumo wa picha, video na maneno (Kama websites zinavyo onekana).

Hapa kila unapotafuta website au kwenda page mpya, browser yako inapakua hizi data kutoka kwenye server.
🎁Mtandao umeundwa na WWW.

Kila website unayoona mtandaoni ipo katika server moja au zaidi katika maeneo tofauti tofauti duniani.

Unapotaka kuifikia website kama habaritech.com request inatumwa kwa moja wapo ya server ndipo majibu yarudi kwako.
🎁Uhusiano huu unaitwa Client-Server Model.

Yani ni sawa na pale mtaani kwenu kuna duka 1 la mangi ila wateja wengi.

Mangi = Server
Wateja = Clients

Kwa maana hiyo client hautakuwa wewe pekee unayetuma request kwenye server.

Inawezekana clients 1000 mkatuma request kwa pamoja
🎁Itakuwaje sasa kama duka la mangi likafungwa?

Watu wote mtashindwa kupata mahitaji yenu kwa siku hiyo. Maana yake server inapoacha kufanya kazi, request zote kwenda kwenye server hazitajibiwa.

Client-Server ni uhusiano ambao uko centralized, na hii ndiyo moja ya hasara yake.
🎁Torrents

Torrents zinatumia BitTorrent protocol.

Hii ni Peer-2-Peer (P2P) protocol. Yaani mteja na mteja mnahudumiana wennyewe moja kwa moja.

Mama chausiku akihitaji mafuta ya kula anaenda kwa Mama Majuto. Hakuna haja ya duka la mangi.
🎁P2P protocol inaruhusu kila computer kwenye mtandao kuwasiliana zenyewe moja kwa moja.

Hapo nadhani umeona utofauti uliopo kati ya Client-Server Network na hii Peer-2-Peer Nerwork.
🎁Tunapopakua files kutoka torrent. Kwanza huwa tunapakua torrent file ambayo tunaenda itumia kwenye torrent client kama uTorrent (Micro Torrent).

Wengi huwa mnaita u-Torrent, ile sio U. ni herufi ya kigiriki yenye maana ya Micro.
🎁Torrent client ndiyo inaanza pakua file yetu tunayotaka kama vile movie ya Batman 2022.

Ile .torrent file ya Batman tuliyo ipakua imebeba Metadata kuhusu movie ya Batman na sio movie yenyewe.

Metadata na ni taarifa kuhusu data zenyewe kabisa (eg file size, structure ya file)
🎁Metadata ndani ya .torrent file pia inabeba tracker addresses.

Trackers ni server inayobeba orodha ya computer zote ambazo tayari zina movie yetu ya Batman.

Computer hizi tunaziita seeders.

Bila shaka mtumiaji wa torrents umeshakutana na huu msamiati wa seeders.
🎁Seeding ni kitendo knachotokea mara baada ya kumaliza kupakua movie yako kupitia torrent client.

Unapofanya seeding unaruhusu watu wengine (Leechers) kupakua vipande vya movie hiyo kutoka kwako.

Nitaelezea mbele kwanini nasema vipande.
🎁Kabla hatujafika mbali ieleweke kwamba kutumia torrents ni kinyume cha sheria, na baadhi ya nchi kama Germany wana sheria kali kupinga torrents.

Ukiwa Germany na PC yako ikagundulika inafanya torrent seeding, utawekwa chini ya ulinzi wa polisi mara moja.
🎁Sasa unapofungua ile .torrent file kwa torrent client, ile client ya uTorrent kwanza itafanya connection na trackers zote ili kuunganika na computer zenye hilo file unapakua.

Baada ya hapo uTorrent itapakua file hiyo moja kwa moja kutoka kwenye hizo PC (seeders) kuja kwako.
🎁Seeders wataendelea kufanya upload ya file, endapo tu torrent client (uTorrent) yake inafanya kazi.

Akizima uTorrent yake, utaendelea kupakua kutoka kwa wengine.

Zoezi hili litashindika iwapo hakuna seeder hata mmoja wa hiyo file.
🎁Unapopakua torrent file, wewe unaitwa "Leecher".

Huu mtandao wa Seeders & Leechers unaitwa Torrent Swarm.

Unapofanya leeching haupakui file lote kutoka kwa seeder mmoja. File inakuwa katika vipande ndani ya PC tofauti tofauti.

Hivyo wewe unapakua kipande kwa kila seeder.
🎁Baada ya kumaliza kupakua hivi vipande ndipo, torrent client yako inachukua jukumu la kuviweka pamoja hivi vipande ili kuunda file zima kama inavyotakiwa.

Kwa kufanya hivi download speed inakuwa kubwa, kwa kuwa unachukua vipande vipande kutoka kwa watu wengi.
🎁 Ukimaliza kupakua file yako, unageuka kuwa seeder. Unaanza upload file ili watu wengine wapakue kutoka kwako.

Sio lazima uwe seeder. Unaweza zima seeding ya file ili kutoendelea tumia bando lako.

Ila huo ni ubinafsi 😁 Wewe umepakua kwetu bure, ila hutaki wenzako wapate.
🎁Nasema hivyo kwa sababu, kadiri seeder wanavyokuwa wengi ndivyo ambavyo download speed inaongezeka.

Kama bando ni ya mawazo, sio mbaya zima tu seeding.
🎁Kwanini Pirates wanatumia torrents kusambaza files zao?

Pirates wengi hawaamini katika taarifa kuuzwa. Hivyo njia sahihi kwao kusambaza files ni torrents.

Lakini sababu kubwa ni kwamba ni ngumu sana kujua huyu pirate ni nani anapotumia torrents.
🎁Mwanzo kabisa huyu pirate ndiye atakuwa seeder wa kwanza na seeder pekee ambaye anafanya seeding ya hilo file.

Leechers watakuwepo wengi na kufanikiwa kuanza fanya seeding ndivyo idadi ya seeders inaongezeka.
🎁Seeders kuwa wengi tunapoteza ushahidi wa centralized source ya ile file yetu.

Kwa maana hiyo mamlaka husika watashindwa kujua msambazaji wa hiyo file ni nani.

Seeders tukiwa wengi mtu wa kwanza kufanya seeding anaweza kujitoa katika orodha ya seeders.
🎁Niibe msemo wa @NNgailo "Biashara sio utapeli, ila kuna matapeli katika biashara".

Ninachotaka kusema ni kwamba, torrents hazina shida na ni njia nzuri kufanya file sharing.

Shida ni kuna baadhi ya watu wanaotumia torrent vibaya.
@NNgailo 🎁Sijasema nakubaliana na piracy. Mimi mwenyewe sipendi kuona content zangu zinatumika bila ruhusa yangu.

Ila hatuna maisha ya kulipia $300 kununua genuine windows au kununua FIFA kila mara inapotoka mpya.

Bila kusahau kwenda kulipia Netflix na Spotify kila mwezi 😒
@NNgailo 🎁Ugumu wa maisha ndiyo unafanya tutumia torrents kupata pirated contents.

Muhimu ni kuwa makini na files unazopakua kwenye torrents. Kuna nyingine zinakuja na virusi vinavyoruhusu wadukuzi kuwa na control ya PC yako.
@NNgailo 🚀Habaritech Magazine Startup edition inapatikana katika @mPaperApp kupitia link hii bit.ly/3vDWwtE pamoja na Gumroad kupitia link hii habaritech.gumroad.com/l/habaritech5

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with HabariTech

HabariTech Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @HabariTech

Aug 30, 2022
⚡Unataka Kupunguza Muda Unaotumia kwenye Mitandao ya Kijamii? Soma Hii

Tunachoongelea ni mitandao ya kijamii. Huduma ambayo inafanya kazi yake vizuri mno.

Kazi yake ni kuhakikisha muda wote tunaangalia screen za simu zetu au PC.
⚡Wazo wa la kusema kwamba tunaweza kabisa kuacha mitandao ya kijamii, ni kama kuamini kwamba mwakani teknolojia ya time travel itakuwepo.

Ni ngumu na haiwezekani kuachana kabisa na mitandao ya kijamii, hivyo kilichobaki ni kujaribu kupunguza muda tunaotumia kwa kufanya haya.
1. Chagua siku moja kila wiki usiingie kabisa kwenye Mitandao ya kijamii

Ukisoma unaweza dhani ni rahisi kufanikisha hili jambo ila ni ngumu kama kushinda njaa zaidi ya siku mbili.
Read 19 tweets
May 31, 2022
🎭Kuona location, SMS & Calls bila yeye kujua

Unaweza kuhack simu/facebook/instagram ya mtu?

Bila shaka hili ni swali ambalo kila IT amewahi kusikia au kuulizwa yeye mwenyewe.

Kwanini watu wanatamani kuwafatilia ndugu/rafiki/wapenzi wao?
🎭Kisayansi hata mimi sijui. Binafsi nadhani ni hali tu ya ubinadamu kutaka kujua nini kinaendelea katika maisha mwingine.

Ni wazi kwamba binadamu tunapenda kuwa wa kwanza kujua kitu na kuwa juu kuzidi mwingine muda wote.
🎭Hii ni kwa sababu ya ubinafsi unaoishi ndani ya kila mmoja wetu.

Je, gharama ya kuwa na hali hii na kuingilia faragha ya mtu ni ipi?

Kulingana na sheria za mitandao za Tanzania “Cyber Act (2015)” ni kinyume cha sheria kutumia kifaa cha mawasiliano cha mtu bila ruhusa yake.
Read 5 tweets
Mar 15, 2022
👽Russia hawataweza kuvuka vikwazo vya Teknolojia

24 February 2022, baada ya Russia kuvamia Ukraine, serikali ya Marekani ilitangaza vikwazo vya kwanza Russia.

Katika vikwazo hivyo vilikuwemo vinavyogusia teknolojia.

#HabariTech
👽Moja ya kikwazo kilisema, "Kuzuia zaidi ya nusu ya uagizaji wa Russia kuingiza teknolojia ya juu nchini mwao, Kuzuia Russia kupata pembejeo muhimu za kiteknolojia, Kudhoofisha msingi wao wa viwanda...
👽...na kudhoofisha matarajio ya kimkakati ya Russia ya kuwa na Ushawishi katika jukwaa la ulimwengu." -mwisho wa nukuu.

Inawezekana ilionekana ni kikwazo kikubwa kwa muda huo. Ila ni kidogo sana ukilinganisha na yaliyofata baada ya hapo.
Read 33 tweets
Mar 14, 2022
🍿Nini Kiliwakuta Founders wa Pirates Bay

Pirates bay ni kati ya website bora za kufanya piracy ya Games, Softwares, Movies, Music na aina nyingi ya files zinazokuwepo online.

Ni website ambayo iko kinyume na sheria za hakimiliki na haikutakiwa kuwepo.

#HabariTech
🍿Kampuni nyingi na wanasheria duniani wamejaribu sana kuhakikisha website hii haipatikani mtandaoni bila mafanikio.

Kwa kuwa content zinazokuwepo huko hazikutakiwa kuwepo na mara nyingi zinawakosesha mauzo kwa kuwa ni usambazaji wa content usio sahihi.
🍿Kuna miaka ya nyuma waliwahi fanikiwa kuiondoa online. Bahati mbaya mafanikio yao hayakudumu kwa muda mrefu.

Saa chache baada ya kuondolewa online website ya Pirates bay ilirudi online. Hivyo wakaona wabadili namna ya mashambulizi yao.
Read 41 tweets
Jan 24, 2022
🚀Sifa Kuu ya MATAPELI

Kwa sasa teknolojia imefanya kupata pesa iwe rahisi sana, lakini kupoteza ni rahisi zaidi 😁.

Kutapeliwa ni dakika 0.

Kila unapogusa mtandaoni sasa hivi kuna haya maneno NFT, Cryptocurrency, Bitcoin.

Lengo ni PESA.
🚀Bahati mbaya wengi mnaishia kuumia kwa sababu mnakosa maarifa.

Mnaingia kichwa kichwa katika biashara msizoelewa haswa ziko vipi.

Kwa sababu hiyo unajikuta unajitapeli wewe mwenyewe. Ulikosea mwanzo kutotaka kusoma inakuaje wengine wanapata faida.
🚀Siri kubwa ya matapeli hata sio kubwa kivile. Ila tu kwa kuwa wengi hatuumizi akili huwa tunaipita tu.

Tapeli guru kabisa ana siri moja.

Kipindi ambacho dhahabu inapatikana kwa wingi yeye huwa hajishughulishi na uchimbaji.

Image Credit: @MaujanjaCrypto
Read 9 tweets
Jan 24, 2022
⚡Namna ya (ku)bypass restrictions za Channels na bots telegram

Kila mara whatsapp isipopatikana watu wengi hutumia telegram kwa muda.

Ukiacha hivyo telegram imekuwa sehemu nzuri ya kuendesha biashara kama anavyofanya @itzjacton na group la Soko Letu

#HabariTech
Au wanavyofanya @CipherdotM na channel yao ya movies. Kwa wengine telegram ni sehemu ya kupakua miziki ya Spotify, YouTube au Apple Music bila kuwa na account katika platform hizo.

Na wengine wanatumia kupakua movies za Netflix ama Amazon Prime
Bahati mbaya channel & bots nyingi zinazotumia majina na content za kampuni kubwa huwa zinafungiwa na telegram kwa sababu ya ukiukaji wa hakimiliki (copyright infringement).

Telegram wapo kulinda maslahi yao na ya kampuni nyingine, hivyo ni lazima wafanye hivi.
Read 7 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(