ZOLENDRONIC Profile picture
May 8 22 tweets 4 min read
Sicarios - Wauaji maalum wanaotumiwa na magenge ya madawa ya kulevya kupanua himaya zao Amerika kusini

#UZI 👇
Mwaka 1993 tajiri namba moja duniani alikuwa m-Japan mmoja wakuitwa Yoshiaki Tsutsumi

Huyu somo mwaka huo alikuwa na utajiri wa dola za kimarekani bilioni 9
Mwaka 1993 pia ndio mwaka aliokufa mbabe wa cocaine kutoka pande za Medellin Columbia kwa jina Pablo Escobar Gaviria (don Pablo)

Data zinaonesha kwamba wakati somo wetu huyu anaaga dunia alikuwa na mkwanja unaokadiriwa kuwa dola za kimarekani bilioni 30
Sasa ukiangalia hizo namba unaona kabisa kwamba somo wetu Pablo alikuwa na mkwanja mnene kuliko bwana Yoshiaki mara tatu na ushee

Kwa hiyo kimsingi don Pablo ndiye alikuwa Elon Musk wa zama hizo ila kwa sababu chanzo cha hela zake ni ngada, forbes wakawa wanamvungia
Katika historia ya biashara ya madawa ya kulevya, Pablo Escobar Gaviria anatajwa km binadamu wa kwanza kuifanya kwa ufanisi mkubwa sana..

Hii ilimpelekea kufikia kiwango cha juu cha utajiri duniani wakati wa kifo chake
Pablo baada ya kudrop chuo miaka ya 60 mwishoni, alianza kufanya biashara za magendo na wizi wa pikipiki.

Alianza biashara ya dawa mwaka 1970 akifanya kazi na makundi mengine. Huu muda alifanya sana mishe za kuteka watu na kudai fidia kabla ya kuwaachia, akafanikiwa sana
Mwaka 1976 Pablo akaanzisha genge lake kwa jina Medellin Cartel

Baadaye Pablo akaanzisha njia ya kwanza kabisa ya kuingiza cocaine US, akipitia jimbo la Miami..
1976 baada ya kuanzisha Medellin Cartel, Pablo akaanza kutafuta namna ya kupanua empire yake ya kuuza ngada

Ndipo hapo akapata wazo la kutengeneza kikosi cha kusafisha njia kabla hajaanza kuingiza mzigo kwenye empire alizokuwa anafikiria
Yaani iko hivi, wauza madawa wakipata eneo zuri la ku-push-ia bizinea yao, ni lazima walisafishe kwanza

Kusafisha eneo ni kuondoa watu wote wanaoweza kuwavutia askari kwenye hilo eneo

Empire ya cartel haitakiwi kuwa na vibaka, machangudoa, wauza ngada wengine wadogo wadogo n.k
Hawa watu hawahamishwi km wamasai wanavyohamishwa Ngorongoro

Hawa wanauawa.

Pablo akaanzisha kikosi cha mauaji, kikiwa na lengo la kuwaua watu wote walioonekana kuwa kikwazo kwenye maeneo waliyotaka kuweka mzigo wa kutosha
Pablo alitumia baadhi ya walinzi wake aliowaamini sana kufanya recruitment ya vijana wadogo (miaka 13-17) kwenye mitaa maskini mjini Medellin..

Vijana waliopewa kipaumbele ni wale waliokuwa na record za uhalifu, wavuta bangi, walioacha shule na wenye vipaji maalum
Walipopatikana walipelekwa kwa Pablo kuapishwa kiapo cha utii, wakishaapa wanaenda kambini sasa kwenye mafunzo

Kambi za mafunzo ya sicarios ni milimani, mbali na makazi ya watu. Kwenye misitu minene
Wakishafika kambini wanafanyiwa interview - practical

Interview zinagawanyika kutokana na rekodi za uhalifu wako

Kwa kijana aliyewahi kuua mtu kabla (intentionally) anaweza kupewa bunduki akaambiwa amuue mwenzake waliyekuja naye.. akishindwa anauawa yeye
Kwa wale ambao hawajawahi kuua kabla wanaanza na brainwashing kwanza

Wanafundishwa kuwa kuua ni kazi km kazi zingine, wanafundishwa kuwa hata hivyo sio wao wanaoua ila yule anayetoa order - boss wao
Wale wanaofuzu kwenye hizi interview za kwanza wanaanza mafunzo sasa

Wale wanaofeli wanauawa afu wanatundikwa mtini wanatumika km target kwenye kujifunza kulenga shabaha
Kuna sicario mmoja alihojiwa na gazeti la NYT akasema kwenye hii interview ya pili kwa sababu yeye alikuwa ameshaua mtu kabla, basi alipewa kisu afu akaoneshwa mwili wa mtu aliyeuawa. Akaambiwa aukate vipande vipande.. anasema ukionesha kusita au kuogopa unakula bullet ya kichwa
Mafunzo yanaendelea sasa, mnakuwa na mafunzo ya shabaha, kukimbia, kujificha, kutambua target, kusoma mazingira iliyoko target yako n.k

Inasemekana kuwa kwenye haya mafunzo kosa dogo sana linakupatia adhabu ya kifo..
Kuna hatua mkifika mnaenda field, mara nyingi field zao huwa ni kuwawinda maafisa wa polisi na kuwachalisha

Anayeshindwa kutii order ya mkufunzi hufanywa target pia. Yaani mnaweza kuamka asubuhi mwenzako akapewa mission ya kukuua, au wawili mkapewa mission moja - kuuana
Atakayemuwahi mwenzake ndo anakuwa amesave

Mnaweza kwenda 20 kwenye mafunzo, mkahitimu 6

Baada ya kuhitimu mnarudi kwa boss, mnasaini mkataba wa kazi afu mnarudi mtaani kwenye maisha yenu ya kawaida. Ikitokea mission unaitwa chap unapiga unapata bonus unaendelea na maisha
Sicario akishapewa oda huua yeyote anayeonekana kikwazo kwenye biashara..

Kuanzia polisi, wanasiasa, wanaharakati, waandishi wa habari, wanachama na viongozi wa cartels nyingine, viongozi au wanachama wa cartel yenu wanaokaidi amri au wanaoanza kuwa na ushawishi kupitiliza n.k
Pia sicario anaweza kupewa mission ya kumuua sicario mwenzake ambaye haonekani kueleweka kwa wakuu

Baada ya Pablo kuanzisha matumizi ya Sicarios 1970's na kuonekana ni idea nzuri, baadaye cartels nyingine zikaanza kutumia sicarios pia.

Wakapanda bei
Kwenye late 1980's sicario mbali na mshahara wake alikuwa anapata hadi US $2000 km bonus akiua mtu mmoja

Kuna sicarios wana rekodi za kuua mpaka watu 300 na kuendelea

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with ZOLENDRONIC

ZOLENDRONIC Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @_zolendronic

May 3
DO or DIE - A Tale of an INTRUDER in North Mara Gold Mine (Nyamongo) - (True Story) - Thread
1. Kwanza kabisa mimi ZOLENDRONIC ni mzaliwa wa wilaya ya Tarime mkoa wa Mara..

Japo maisha yangu kiasi kikubwa nmekulia nje ya Mara, nlitoka nikiwa mdogo ila najua culture kiasi (lugha na baadhi ya vitu)

20** nmemaliza zangu F6. Nikarudi nyumbani wakati nasubiria matokeo
2. Pale home kuna mwana alikuwa anazama mgodini - as intruder kufukuzia madini..

Intruder - Ni wale watu wanaoruka ukuta na kwenda kutafuta dhahabu mgodini - mostly Usiku

Huyu jamaa sio ndg yangu wa damu japo ni amekulia pale home mpaka ana familia yake now, (mke na watoto)
Read 25 tweets
Feb 6
BEEF YA NAS NA JAY Z

#UZI

April 30, 2021 mwanetu DJ Khaled aliachia album yake ya 12..

Ndani ya ile album kuna ngoma inaitwa 'SORRY NOT SORRY'

Ndani ya hiyo ngoma kuna ma-legendary wawili wa Rap, wazaliwa wa New York. Wana wanachana ki-boss sana kuelezea mafanikio yao mle
Hapa kuna Nasir Jones aka Nas, kule kuna Sean Carter au Jay Z.. kiitikio kimegongwa na James Fauntleroy

Ni ngoma ya kitajiri sana. Wana hawajatumia nguvu nyingi, wanatiririka tu ki-boss sana na wanaeleweka (si unajua tena tajiri hata akikohoa kuna kitu anakuwa anamaanisha😁😁)
Sasa ule wimbo ni sehemu ya udhihirisho wa mapatano kati ya Nas na Jay Z kufuatia beef yao nzito sana miaka ya mwishoni ya 90 na 2000 mwanzoni

Shuka na huu uzi upate ABC za hii beef iliotikisa muziki wa Hip Hop miaka ya 90 mpaka 2000 mpaka mama mzazi wa Jay Z akaingilia Kati👇
Read 22 tweets
Jan 23
BEEF YA LIL WAYNE NA BIRDMAN

#UZI

Mwaka 2017 Rick Ross aliachia album yake ya tisa kwa jina 'Rather You Than Me'

Ndani yake kulikuwa na ngoma kali kali pamoja na diss track moja kali sana kwa jina "Idols Become Rivals"

Hii ni diss track maalum kwa ajili ya Birdman
Rosey alimdiss sana mle ndani kutokana na jinsi mwana alivyokuwa anam-treat mshkaji wake wa muda mrefu Lil Wayne

Mle ndani Ross anasema kabla hajatoka alikuwa anawaangalia Birdman na Wayne anatamani maisha yao. Hakutegemea Birdman anaweza kumtenda Wayne vibaya
Sasa kuhusu story ya Rick Ross the Boss, achana nayo!

Lil Wayne alikutana na Birdman kwa mara ya kwanza mwaka 1991 wakati huo ka-Wayne kana miaka 8 tu..

Wayne alikuwa anaishi na mama yake na baba yake wa kambo muda huo

Mama'ake na baba'ake walitengana akiwa na miaka miwili
Read 25 tweets
Jan 17
BEEF YA KANYE WEST NA JAY - Z
#UZI

Kama ulishawahi kusikiliza ile album ya Kanye kwa jina Graduation bila shaka unaujua wimbo unaitwa 'Big Brother'

Ule ni wimbo spesho kabsa ambao mwana alimuimbia mshkaji wake wa faida (yaani km ile tattoo ya Mondi kwa mmakonde😃)
Ndani ya ule wimbo kuna line inasema 'But he got me out my mama crib'

Kanye hajapiga hustle sana mtaani km wenzake waliotusua kupitia game ya rap

Jamaa ni wa kishua tu, mama'ake (Donda West) alikuwa professor wa chuo kikuu cha Chicago akiwa mkuu wa idara kabisa
...lakini pia Kanye ni mtoto wa pekee kwa mama'ake, ko tunaweza kusema jamaa ni 'mtoto wa mama' dizaini km @mchachu_ hivi😃

Japo mama'ake alikuwa prof., Kanye na shule ni km Zambarau na #KatibaMpya .. hawakupatana kbs. Jamaa ali-drop college ili afukuzie ndoto zake kwa game
Read 24 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(