Madinidotcom Profile picture
Jun 23 23 tweets 9 min read
UMESIKIA MENGI KUHUSU MGOGORO WA #RWANDA NA #DRC LAKINI PENGINE UNASHINDWA KUELEWA WTF IZ GOING ON?🧐🤭
Kuna njia mbili za kuelewa,ya kwanza ni usome Uzi ufuatao.
Pili usikose show'Jmosi hii eastafricaradio.com
History iliyorahisishwa na #SabulaMaarifa wa #MadiniDigital.
Iko hivi!! Kitambo hicho Rwanda iliwahi ku-operate chini ya mwamvuli wa KIFALME uliokuwa ukiongozwa na mwamba wa kuitwa KIGELI IV RWABUGIRI.
Rwabugiri alikuwa ni jamaa fulani hivi kutokea Kabila la walio wachache (TUTSI) kule Rwanda.
na aliingia kwenye vitabu vya kihistoria kama kiongozi pekee wa taifa hilo aliyeamua kufanya mashirikiano na Serikali za KIKOLONI. By the way kama tunavyojua kuwa RWANDA kuna Makabila makuu mawili, na la 3 ni nyongeza, kuna walio wengi ambao tunawatambua kama Wa-HUTU
na walio wachache ambao ni TUTSI lakini kabila la 3 ni TWA ambao kihistoria ndio wa kwanza kuja Rwanda.Wahutu na Watutsi waliwakuta pale ila ni wachache na shughuli zao za kijamii haziwapi kiki sana.
Sasa huyu RWABUGIRI alikuwa kutokea upande huu wa jamii ya walio wachache ambao Wa-TUTSI (anapotokea Kagame)
RWABUGIRI aliongoza kwa muda mrefu na baadae alifariki lakini misingi yake iliendelea kuishi.Sasa ujue issue ya kushirikiana na MABEBERU,
haikuwapendezea kabisa jamaa zetu wa KI-HUTU na mara kadhaa walishakinukisha kujaribu kuuondosha madarakani UTAWALA wa KIFALME bila mafanikio.
Ujue walichokuwa wakifanya WAKOLONI kule Rwanda ni kwamba waliacha milango wazi kwa MACHIFU wote kuja na kufanya nao mashirikiano.
Wa-HUTU wao jambo hili lilionekana kupingwa vikali kwakuwa waliamini walikuwa na uwezo wa kujitawala wenyewe.
RWABUGIRI ambaye alikuwa akiongoza jamii ya walio wachache aliona ni fursa kuamua kutembea na HASHTAG ya JK 🇹🇿 kwamba 'Ukitaka kula lazima na wewe uliwe kidogo' 🥳
Kwa namna fulani mgogoro baina ya jamii hizi mbili Wa-HUTU & Wa-TUTSI ni kama ulianziaga hapa .Hii dillema ya machaguo ya kijamii wakati wa uhuru iliwapata pia NIGERIA tulikuletea saga la BIAFRA.
So Wa-HUTU walianzisha struggle za kuhakikisha wanauondoa UTAWALA wa KIFALME.
Mapinduzi yale yalifanya jamii kubwa ya Wa-TUTSI kuikimbia nchi na kwenda kutafuta hifadhi kwenye mataifa jirani kama Uganda,Congo na Tanzania ikiwemo.

Sasa wakiwa huko bhn Wa TUTSI hawakulaza damu,wakaanza kujipanga kwa kutoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana wao...
LENGO KUU likiwa ni kuona siku moja wanarejesha UTAWALA wao ndani ya Rwanda 🇷🇼
Hapo katikati (Toka Mapinduzi ya mwaka 1960) kulifanywa majaribio kadhaa ya kupindua nchi by Wa-TUTSI ambayo yalifeli.
Ni katika kipindi hichi ndipo neno COCKROACHES (Mende) nchini Rwanda.
Wa-HUTU walitumia neno hili kuyaelezea makundi mbalimbali ya Wa-TUTSI yaliyokuwa yakijaribu kupindua Nchi. baadaye lilitumika kwenye Media wakati wa mauaji.
Mfululizo wa majaribio haya ya ki-mapinduzi yaliyokuwa yakifanywa na vikundi vya Wa-TUTSI uliendelea bila mafanikio.
Then ukafika mwaka 1990 Paul Kagame akiwa na kikundi Chake cha waasi Rwanda Patriotic Front (RPF) wakafanya Uvamizi wa NGUVU ulioitikisa Serikali.KIKAUMANA HASWA!
Wakati huu jamaa walikuja na nguvu kiasi cha kufanikiwa kushikilia baadhi ya miji na kushikilia mateka wa kivita
Kitendo cha kikundi kufikia kushikilia wapiganaji wa serikali,you can see walikua walikuwa zaidi ya kundi la waasi.Ikamlazimu Rais Juvenal Habyarimana kukubali kurudi mezani kwa mazungumzo.
Eneo la mazungumzo likawa ni CHUGANISTAN kwa Machalii wa R (Arusha-Tanzania)
na haikushangaza kuona trip za Kigali to Tanzania kwa Rais Habyarimana pamoja na delegation yake zikiongezeka maradufu kwa wakati huo
Huku mazungumzo baina ya Upinzani ambao ni ulikuwa ni Rwanda Patriotic Front (RPF) na Serikali ya Rwanda yakionekana kwenda vizuri kule ARUSHA.
Ghafla #PichaLinaanza taarifa zikaja, ndege ya Rais Habyarimana imetunguliwa ilipokuwa ikijaribu kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kigali(Rwanda) na kuuwa watu wote waliokuwa ndani ya ndege hiyo akiwemo rais wa Burundi ambaye aliomba Lift! ukawa ukaribisho wa RWANDA GENOCIDE!!
Jamii ya Wa-HUTU ililihusisha tukio hili la kutunguliwa kwa ndege ya wao Habyarimana na jamii za Wa-TUTSI so KIKAUMANA.
Yakafanyika mauaji dhidi ya jamii ya walio wachache (TUTSI) lakini hatimaye RPF chini ya Rais Paul Kagame wakafanikiwa kuyatwaa madaraka na kukomesha yote.
Utakumbuka tulikuletea Deep kuanzia hapa na kuendelea kwenye episodes zetu kuhusu visa na mikasa ya tukio hili.
AND THAT WAS THE BEGINNING OF THE NEW TUTSI SUPREMACY IN RWANDA.
Upande wa pili baadaye wengi ilibidi waikimbie nchi na kwenda nchi jirani ya CONGO.
Huko walikwenda kufanya makazi katika miji mbalimbali iliyopo Mashariki mwa nchi hiyo 🇨🇩Sasa wakiwa huko bhn ni kama nao wanaonekana kuendelea na mipango ya chini kwa chini ya kuona namna siku moja watarejesha tena UTAWALA wao ndani ya taifa la RWANDA 🇷🇼
Wanachofanya RPF (RWANDA) ni kuzuia uwezekano wa hawa jamaa kujipanga upya na kufanya kile walikifanya wao 1994 .Ukumbuke hadi leo kuna vikundi na watu binafsi wengi wanaopambana kumng'oa rais Kagame,na yeye ameshasema na kuonyesha mipango yake ya kupambana nao MAADUI WA TAIFA.
#Taarifa ya hivi majuzi iliyotolewa na Serikali ya Kongo imeonyesha kuishutumu moja kwa moja Serikali ya Rwanda kwamba inasapoti kikundi cha UASI cha M23 .Ni kwasababu kuna story ya MASLAHI ya jamii za wanyarwanda ndani ya DRC na maeneo hayo ambayo yana utajiri mkubwa
Jambo ambalo pengine utakuwa hulifahamu ni kuwa hawa wa M23 ni aina ya Wa-TUTSI wapatikanao CONGO ingawa kwa kule huwa wanaitwa BANYAMULENGE kwasababu ni jina(bandia)walilolitumia wakati wanaoung'oa utawala wa MOBUTU SESE SEKO wakisaidiana na LAURENT KABILA.
Usaidizi huu wa BANYAMULENGE wa MCHONGO yalikua makubaliano ya SIRI kati ya LAURENT KABILA na WANYARWANDA hao wakimbizi wakati huo,na unafahamika kama MAKUBALIANO ya Lemera ya mwaka I996.
Mkataba huu wa siri ...
Tunaujadili kiundani na YERICO NYERERE,mwandishi wa kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI.Ukitufuatilia utagundua unaunganisha doti nyingi za matukio ya dunia kwa lugha ya kishkaji.Usikose Eastafricaradio kila jumamosi saa 9alasiri hadi 10jioni .

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Madinidotcom

Madinidotcom Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @madinidotcom

Apr 9
KUTENGANA KWA KOREA KUSINI NA KASKAZINI ,CHANZO NA MATOKEO
YAKE

#PichaLinaendelea Wote tunajua kuna KOREA 2,Wale wa kaskazini kama Johmakini na wa kusini kama konde boy .Sasa STRAIGHT To the point, nini sababu ya wao kutengana?JIBU fupi Ni vita vya pili vya dunia.Ilikuwaje?
Korea ilikuwa nchi moja tangu karne ya 7 means tangu miaka ya 1700 mpaka
1945.Karne za kutosha wamekaa pamoja chini ya HIMAYA YA SILLA
WANAITA SILLA DYNASTY(sila dainasti).Mwanzo ulisikia chanzo cha ketengana ni VITA VYA PILI VYA
DUNIA(1945) lakini story kidoogo
ilianzia nyuma ya hapo.Kuna ‘ndondi’ flani zishawahi kupigwa kati ya JAPAN na CHINA,hii vita inaitwa First Sino -Japanese war,imagine wanasema ni vita kati ya CHINA na JAPAN lakini picha halisi ni tofauti kabisa.JAPAN alikua ndo Baba lao miaka hyo kutokana na walichukua mfumo
Read 25 tweets
Apr 7
CORONA VIRUS NI KAZI YA MAABARA? WHY CHINA?
#PichaLinaendelea sehemu 2

Lakini SIDE B kuna issue ya LABARATORY THEORY niliyokugusia mwanzoni ambayo mataifa mengi
yameanza kurudi kujiuliza na CHINA inatumia POWER yote kuhakikisha hilo halifanyiki. Ni Theory gani
hii?
Kwanini kuna hizi maabara za VIRUSI hatari duniani?By the way leo tunaongelea CHINA tu lakini
marekani pia wana mahabara kama hizi kibao na zimejaa virusi hatari kibao,vya faida gani?Kwanini MAREKANI na CHINA wanatupiana mpira?.PICHA LINANOGA
So kama tulivyosikia dunia ina maswali mengi kuhusu Corona na kubwa linalojitokeza ni LAB THEORY
ambayo imeanza kuuliziwa vikali na wakubwa.Kabla haijathibitika kama kweli ni kazi ya maabara ama
lah,Kuna mwingine utauliza kwani tukijua ndo isaidie nini?Well
Read 25 tweets
Apr 7
CORONA VIRUS NI KAZI YA MAABARA? WHY CHINA?

#PichaLinaanza CORONA VIRUS!True story hatimaye tumepata HIT SONG iliyosikilizwa na wote wazee,vijana,
watoto,wanasiasa,madaktari na wahuni wa skani.Mara ya mwisho tumepata hit song ya aina hii ilikuwa #MUZIKI ya Darassa ft Benpol. Image
Kabla ya hapo CONGO WALITULETEA ‘’TWANGA PHOTO WAAAAH,
ekotiteee,ekotiteee’’ ya Kofii olomide. au Mbele tukasikia DESPACITO…
Hii sio mara ya kwanza na huenda isiwe ya mwisho kusikia virusi kusambaa duniani kutoka nchi china. So
why CHINA?
Dunia imeshaingia kwenye process ya CHANJO na mjadala wake ni mkubwa na mzito .We unaamini nini?Ni hiari na maamuzi yako.Kwanini China ndo chanzo cha haya yote?
PICHA LINAANZA #2019 China wakijiandaa kudamshi na mwaka mpya ,BREAKING NEWZ watu walianza
kupata kikohozi kikavu
Read 25 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(