Madinidotcom Profile picture
Jul 11, 2022 25 tweets 9 min read Read on X
Nni kinaendelea SRILANKA? Sehemu 2

Uzi🧵🙌

#PichaLINAENDELEA anzia post ya jana.

Ankali GOTABAYA alipoingia madarakani 2019 aliahidi kodi za kibwege atazifutilia mbali,wananchi wakaona “eheee,huyu ndo mwaisa mtu mbadi wetu”km ujuavyo ujuavyo kila mtazamo hujengwa na historia Image
so shida ya wana SRI LANKA ilikuwa kuona nchi inarudi kusimama kwa miguu yake,mambo ya wewe ni nduguyakeNani wala hawajali sana. Alipoingia ankali GOTABAYA alionekana ni mtu wa kusimamia maneno yake, akapitisha panga la kupunguza kodi kwa wananchi ,kampeni ambayo ilipunguza 25% Image
yaani robo ya pato la taifa ili wananchi wafurahi.Wakati anafanya hili ni wakati ambao alikuwa akijiandaa na uchaguzi mkuu.Watalamu wa kiuchumi hawakushauri hili lakini yeye alisema anataka biashara ndogondogo za wananchi wanyonge wa hali ya chini zichipue,so wasilipe kodi . Image
Hawajakaa vizuri,GHAFLA ankali Gotabaya akaja na ajenda kwamba kuanzia sasa wakulima wote watatumia mbolea asilia ,waachane KABISA na mbolea za chemikali,ni mwendo wa maviYaNg’ombe,maviYaKuku na mimea. ndani ya usiku mmoja alitaka kuigeuza Sri lanka kuwa na kilimo organic 100% Image
yaani mbolea ya kiwandani ni kama ukutwe na bangi.Hakuna nchi duniani imefanikiwa kutegemea mbolea ya asili kwa chakula 100%,hata nchi kama ujerumani ni 10-15% tu ya chakula inategemea mbolea ya asili yaani ya wanyama na mimea. So ndani miaka michche kilimo cha mpunga kilishuka Image
50% (NUSU YA UZALISHAJI) na nchi ina watu zaidi ya milioni 21 .Hii ilifanya kulazimika kuagiza mchele nje ya nchi,jambo la ajabu kutokea kwenye nchi ambayo Mpunga ndo shughuli yao.
Ghafla ikaja COVID 19 kisiwa ambacho Utalii ulichangia 22% YA PATO LA TAIFA Image
liliyeyuka ndani ya muda mfupi. Hata hivyo kabla ya COVID,ndani ya 2019 kulitokea tukio la kigaidi kwenye mji mkuu COLOMBO,wahuni walilipua makanisa na majengo kadhaa kuua watu 269 palepale na 25 kati yao walikuwa raia wa kigeni,tukio hili lilishusha utalii kwa 70% nchini humo. Image
Covid ikamalizia mchezo. Chanzo kingine cha pesa za kigeni ilikuwa wananchi waishio nje ya nchi waliokuwa wanatuma pesa kwa ndugu zao, wanalipwa pesa za kigeni wanazituma nyumbani,covid ikaua hili. So hapa ndipo watu wakaanza kuhisi maumivu halisi na ukumbuke covid 19 iliingia Image
2019 ambapo GOTABAYA ndio kwanza amechaguliwa ,ndiyo maana akawa anafanya blandaz zote nilizokwambia, nchi iliishiwa pesa za kigeni kiasi kwamba alipiga marufuku mbolea za viwandani ili kuepuka kuagiza nje ambapo wangetumia pesa za kigeni.
mbali na hilo kuna blanda nyingine Image
iliyoharibu mambo,nadhani umewahi kusikia kuna nchi ambazo zina michezo au uhuni wa kupandisha thamani ya pesa zao kinyemela,yaani wanavaa kigodoro cha kiuchumi.Kama hujawahi kusikia au umewahi kusikia basi SRI LANKA ni moja ya nchi hizo.Kivip? Image
Mfano,Kama Tanzania tunaagiza mchele Kenya,na kilo 1 ya mchele KENYA inauzwa $1 (biashara duniani inafanyika kwa dola nilivyokwambia) na labda dola 1 ni sawa na buku 2 za kitanzania, serikali inaweza kutumia bank kuu yake kuaminisha kila mtu kwamba DOLLA 1 ndani ya Tanzania ni Image
sawa na 1,500, means mchele utauzwa kwa bei ya chini ya uhalisia.Mbinu hii hutumika na nchi zinazoingiza bidhaa nyingi kuliko inazouza nje ili kumaintain pesa yao lakini huwapunguzia wananchi mzigo wa gharama na hivyo serikali iliyo madarakani inajiweka pazuri kisiasa kwasababu Image
wananchi wanaona vitu vinashuka bei au atleast hakuna mfumuko wa bei,hata kama duniani kwingine mambo yamebadilika.Utajiuliza sasa kwanini nchi nyingine hazitumii mbinu hii kabambe?well,jibu ni simpo, kwasababu ya hiki kilichoitokea SRI LANKA leo.🥳 Image
So sri lanka walifanya uhuni huu na kumaintain pesa yao (Rupee) tangu APRIL 2021 wakifanya mchezo wa wakiaminisha watu kwamba dola 1=buku jero wakati kiuhalisia ni buku 2.Utajiuliza inafanyaje kazi kwenye mazingira halisi?
Iko hivi..mfano unaenda bank unawapa dola 1 ya kimarekani Image
then wanakupa buku jero(1500), Ukienda kwenye duka binafsi la kubadilisha pesa wanakupa BUKU 2.Bila shaka haichukui muda mrefu sana watu wataanza kuambiana kwamba usibadilishe au usiweke pesa zako za kigeni kwenye bank kwasababu wananunua kwa bei chee. Image
so wale raia wa kigeni hawatumi tena pesa kwa ndugu zao kupitia bank au njia rasmi ambazo zitaingia serikalini.Kupitia hili bank kuu ambapo mzunguko wa pesa zote huishia inakosa pesa za kigeni kumaintain UCHUMIwaKati FEKI waliojitengenezea. Image
So ni mambo 3 yaliyojimix yameishusha sri lanka ,Kwanza hazina imeishiwa pesa za kigeni kwa uongozi mbaya ,pili waliotunza pesa zao zina thamani ndogo kuliko ilivyokuwa mwanzo kutokana na mfumuko wa bei duniani,so kama ulikuwa na pesa inayoweza kununua kilo 10 jana, Image
leo pesa yako inaweza kununua kilo 5 pekee za mchele.Hivyohivyo kwenye bidhaa nyingine kama mafuta.
Hawajakaa vizuri Vita ya UKRAINE ikaanza na kwa nchi inayotegemea kuingiza zaidi kama SRI LANKA ilipigwa na kitu chenye ncha kali kwasababu UKRAINE na URUSI zinasambaza 28% Image
ya mahindi na ngano yote duniani. Ukraine tu yenyewe inalisha watu milioni 400 duniani kwa export yake ya chakula.Russia inasambaza 15% ya mbolea za mazao duniani na mafuta yanayotumika kutengeneza hizo mbolea pia yanapatikana Russia. Image
Mbali na hilo BEI ya mafuta ikapanda duniani na katika kupambana na hali ya kupanda kwa vyakula,nchi nyingi duniani zimepiga marufuku kuuza nje baadhi ya bidha za vyakula,so kwa nchi kama SRI LANKA ambayo mbolea hakuna,chakula na vitu vingi wanaagiza nje, Image
bila shaka sio ajabu kusikia yanayo wapata. So uchumi huwa una collapse kwa namna hii lakini kuna njia ya kutatua hili linapotokea,kwasababu nchi kushindwa kulipa madeni yake na kukosa sifa ya kukopesheka lkn kukosa hazina ya pesa ya pesa ya kigeni sio mchongo mpya dunia Image
imeshaweka njia ya kupambana nayo,na hapa ndipo mashirika ya kimataifa huingia kama IMF shirika la fedha na kutoa msaada wanaziita BAILOUT.
SRI LANKA ishapokea mpunga wa aina hii mwaka 2006 na nchi kibao hukopeshwa kwa namna hii kuokoa uchumi,unakumbuka UGIRIKI pia, Image
lkn kuna KIPENGELE ambacho kinafanya SRI LANKA inashindwa kusaidika.Hizo BailOUT sio pesa zinazotolewa hovyo tu kwasabab nchi ina matatizo,ila kuna vigezo maalum ikiwemo uimara wa serikali,sera za nchi kuhusu maendeleo na kifupi IMF hutaka kujiridhisha kwamba situation ya nchi Image
kwamba situation ya nchi husika ni salama kuwapa pesa hizo au ndo watajikuta kwenye same situation miezi 6 baadaye.Hiki kigezo ndo SRI LANKA inakikosa,kwasababu wananchi wapo barabarani wakiandamana na wana sababu kwa wanachokifanya,lkn wanazidi kuchelewesha msaada wa kimataifa Image
Mfumuko wa bei duniani,vita na covid 19 vimekutana na uongozi mbaya/dhaifu ndani ya nchi na hii ndio UN waliita A PERFECT STORM. hope umepata idea ya kinachotokea Sri SRI LANKA

Imeandaliwa na @Gplanet5
Usikose kutuskiliza kila jumamosi kuanzia saa 9 alasiri mpk saa 10 jioni

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Madinidotcom

Madinidotcom Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @madinidotcom

Dec 22, 2022
MAFUTA YANATOKA-GA WAPI?🤔
#PICHALINAANZA...
Mpaka sasa jibu la kisayansi juu ya chanzo cha uwepo wa mafuta, hata mimi sipendagi sana kumuaminisha mtu😅,Tho nitakuelewesha wanasega nini ,ukiona haikuingii basi tuishie kukubali tu MUNGU FUNDI.Lakini wanasema...
ni matokeo ya mgandamizo(presha) wa mimea,viumbe waliowahi kuishi duniani na mazagazaga kibao yaliyovunda-ga ardhini ambapo vilitengeneza hewa ya HYDROCARBON.
Hii HAIDRO-KABONI wala isikuogopeshe,hili jina ni kitu kinachotokeaga pale...
Kemikali za asili wanaita Organic chemical yaani unajua kuna zile kemikali za maabara za mikonoYaWatu na hizi za Asili zinaweza kujiumba zenyewe tu labda umetupa takataka na vyakula sehemu moja,then zinajimix zikivunda huenda kuna chemical zinajitengeneza.
Read 25 tweets
Aug 25, 2022
SAKATA LA MAUAJI YA RAIS WA CONGO.
🧵🔥

#PichaLinaanza Hili ni picha kuhusu tukio la kuuawa kwa rais wa Congo Laurent-Désiré Kabila,ni kama movie la kutisha lakini BASED ON TRU EVENT. Mwamba ambaye ni Stelingi wetu anaitwa RASHIDI MIZELE,baadaye mastelingi watabadilika. Image
hii ndio story,ambayo tulikugusia episode zilizopita za rais aliyeingia mkataba maarufu wa kuigawa Congo MKABA WA LEMERA.HADI leo Congo juzi kati imekubaliwa kuwa sehemu ya africa mashariki,ni nchi yenye historia nyeusi.Licha ya kwamba imebarikiwa madini... Image
ANZIA HAPA......agiza popcorn kabisa

Acha turewind mkanda ,Lets go back hadi siku ya TUKIO lenyewe la mwamba aliyempiga risasi kadhaa Rais wa nchini na akatoka zake mbio akitarajia kutoroka.Huyu ndo mwenye siri hii nzito ya KWANINI alimuua rais wa Congo Laurent-Désiré Kabila Image
Read 20 tweets
Aug 23, 2022
SAKATA LA BILIONEA JEFF BEZOS NA KING SALMAN WA SAUDIA.

Did you know unaweza kuhack an Iphones? Unafahamu ndicho chanzo cha tajiri namb 1 duniani Jeff Bezos kuachwa na mkewe?unafahamu aliyefanya hilo tukio ni King Salman kiongozi wa Saudi Arabia? #PICHALINAANZA Image
Kuna imani kwamba iphones zina strong security ni ngumu kuichezea,yes inawezekena bhanaa lakini kudakwa ni njenje.Sasa hacking inahitaji vitu flani ambavyo sometimes ni teknolojia ghali au lazima uwe na connections kali .
Juzi kati ikatangazwa BREKING NYIUZ Image
WhatsApp imeishtaki kampuni flani inayodevelp computer programs kutoka Israel. Sababu inashtumiwa kumpa Paul Kagame wa Rwanda program ya computer iliyowezesha kudukua "WhatsApp conversation” za wapinzani wa serikali ya Rwanda wanaoishi uhamishoni wanaojiita 'wanaharakati' Image
Read 37 tweets
Jul 13, 2022
MAUAJI YA Mohsen Fakhrizadeh KAMA MOVIE.

Uzi 🧵

Kuiadhibu Iran kama taifa kwa adhabu za vikwazo vya kiuchumi hakujaweza
kuzuia hatari inayosemwa na mataifa makubwa, na 'NEXT' mbinu ni kudeal namtu mmoja kwasababu kuivamia kijeshi pia ni jambo linalowezekana lakini... Image
unahitaji kujipanga sawa sawa kama asemavyo Rose mhando.Kuna mauaji ya wanasayansi wa nyuklia yameshafanyika lakini huyu aliyeuawa Mohsen Fakhrizadeh,tunasema wahuni wamegonga ikulu. Iran sio mgeni wa hiki kinachowakuta kwasababu kilianzia IRAQ Image
aliyekuwa rais wa marekani George W bush sababu KUU aliyotoa ya kuanzisha vita na Iraq 2003, alisema Iraq ilikua inarutubisha na kununua kiwango kikubwa cha Uranium inayochimbwa Africa.Haya madini tuseme ni kama ndizi ambazo unaweza kuMIX ndizi moja na maziwa ukasaga kwenye Image
Read 25 tweets
Jul 10, 2022
Nini kinaendelea SRILANKA..?

Uzi🧵

#Trustory labda umeshaona story nyingi kuhusu SRI LANKA na labda hujui tumefikaje hapa na ndiyo sababu unasoma hapa,au unajiuliza hivi nchi inawezaje ku collapse kiasi cha kukosa hela?kwanza nchi inakosaje hela?inamaana noti zimepotea? Image
Mwingine hata huelewi SRI LANKA yenyewe ndo wapi. So twende nikupe historia simpo yenye MASUALA Mazima ya uchumi ndani yake. Sri lanka ni kisiwa kipo kusini mwa INDIA zamani sana inasemekana kulikuwa na barabara kabisa kutoka INDIA hadi SRI LANKA ya sasa Image
lakini #Trustory maji yalifukia hilo eneo na sasa wana mpaka wa kwenye maji,ni sawa na kusema SRI LANKA zamani ilikuwa #peninsula na sasa ni kisiwa, ukiangalia watu wake wanafanana na jamii ya wahindi.Ushaskiaga wahuni wanaitwa Tamil Tigers? ImageImage
Read 25 tweets
Jun 23, 2022
UMESIKIA MENGI KUHUSU MGOGORO WA #RWANDA NA #DRC LAKINI PENGINE UNASHINDWA KUELEWA WTF IZ GOING ON?🧐🤭
Kuna njia mbili za kuelewa,ya kwanza ni usome Uzi ufuatao.
Pili usikose show'Jmosi hii eastafricaradio.com
History iliyorahisishwa na #SabulaMaarifa wa #MadiniDigital.
Iko hivi!! Kitambo hicho Rwanda iliwahi ku-operate chini ya mwamvuli wa KIFALME uliokuwa ukiongozwa na mwamba wa kuitwa KIGELI IV RWABUGIRI.
Rwabugiri alikuwa ni jamaa fulani hivi kutokea Kabila la walio wachache (TUTSI) kule Rwanda.
na aliingia kwenye vitabu vya kihistoria kama kiongozi pekee wa taifa hilo aliyeamua kufanya mashirikiano na Serikali za KIKOLONI. By the way kama tunavyojua kuwa RWANDA kuna Makabila makuu mawili, na la 3 ni nyongeza, kuna walio wengi ambao tunawatambua kama Wa-HUTU
Read 23 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(