Kuduishe Kisowile Profile picture
Aug 30, 2020 17 tweets 7 min read Read on X
Nilimpokea mtoto yule, alikuwa wa kiume, mkubwa, 4.4kgs lakini alikuwa amefariki. Nikamfunga vizuri, na kubandika karatasi kwenye kanga ile, "mtoto wa __"
Mama yake alikuwa nusu kaputi, kizazi kimechanika, daktari akifanya juu chini kuokoa maisha yake. #UZI
#MaamuziYakoKeshoYako Image
Alikuwa ni mtoto wake wa tano. Alikuwa amepoteza damu nyingi mno. Huku dripu ya damu ikishuka, daktari alisema, "leo, siku haijaanza vema"
Huyu ndio mgonjwa wa kwanza wa upasuaji kwa siku hiyo, aliletwa kwa upasuaji wa dharura.
Alipomaliza kushonwa, niliketi pembeni ya daktari
akijaza ripoti ya upasuaji. Kadi yake ya kliniki ilionyesha alihudhuria kliniki mara moja tu.
Daktari akasema, "Nilijua tu, lazima kuna kosa lilifanyika."
Alipomaliza ripoti hiyo, tukaendelea na mama mwingine, huyu aliletwa akiwa hajiwezi.
Mwili mzima umevimba, hawexi kusimama
wala haoni macho yamevimba.
Upasuaji mwingine wa dharura.
Mbio mbio, zikaletwa damu za kutosha kwasababu alikuwa anatokwa damu sana.
Akapigwa nusu kaputi, tukaingia kazini tena. Alikuwa binti mdogo miaka 20-22 tu, presha ya mimba ilikuwa ikimsumbua.
Daktari akasema, "jamani,
tuombeni huyu mtoto atoke salama"
Hali yake haikuwa nzuri hata kidogo. Mtoto alikuwa amefariki naye, hii ilikuwa mimba ya kwanza.
Tukamsafisha na kutoa damu iliyokuwa imetoka sana ndani, akashonwa vizuri.
Kila mtu kwenye chumba cha upasuaji alishusha pumzi.
#MaamuziYakoKeshoYako
Ripoti ikaandikwa, naye alionekana kuwa na presha ya mimba, lakini hakutumia dawa.
Daktari alipomaliza, aliketi akaongea na sisi, "hakuna kitu muhimu kama kuhudhuria kliniki na kupata vipimo vyote muhimu."
Akatueleza, kina mama wengi wakishazaa mara 2/3
#MaamuziYakoKeshoYako
Wanajisahau, wanakuwa sio wahudhuriaji wa kliniki kwasababu wanaamini wanafahamu kila kitu kuhusu ujauzito.
Hicho ndicho kilitokea kwa yule mama wa kwanza. Mwisho kumbe amepata mimba ya mtoto mwenye uzito mkubwa, amekaa nyumbani na uchungu, ameshindwa kuzaa
#MaamuziYakoKeshoYako
kwasababu njia ni ndogo tofauti na ukubwa wa mtoto. Mwisho mtoto amefariki na kizazi kimechanika, imebidi kitolewe.
Lakini pia, kwenda kliniki pekee haitoshi. Unaenda je, unahakikisha unapata huduma zote na unafuata hayo maelekezo?
Hicho ndio kimetokea kwa
#MaamuziYakoKeshoYako
yule binti wa pili. Licha ya kuhudhuria kliniki kama ilivyotakiwa, hakuwa akitumia dawa za presha kama maelekezo ya daktari. Naye amepoteza kifungua mimba wake.
Lakini je, kina mama na wenza wao wanafahamu ni huduma gani wanatakiwa kupata wakiwa wajawazito?
#MaamuziYakoKeshoYako
1. Kupima uzito, presha, urefu, kiwango cha damu, ultrasound(kujua maendeleo ya mtoto), UKIMWI, Kaswende, Malaria na mkojo.
Hivi vipimo ni muhimu SANA kwa afya ya mama na mtoto.

2. Kuchoma sindano ya tetenasi

3. Kuonana na daktari, ambapo ataangalia
#MaamuziYakoKeshoYako Image
ukubwa wa mimba, mapigo ya moyo ya mtoto na afya ya mama kwa ujumla.

4. Kupewa elimu ya dalili hatari za ujauzito. Mf: kuvimba mwili mzima, kifafa, homa kali, mapigo ya moyo kwenda kasi, n.k
Dalili hizi zinatokana na magonjwa yanayohatarisha ujauzito
#MaaamuziYakoKeshoYako
5. Kunywa dawa za kuongeza damu, dawa za malaria, dawa za minyoo na iwapo ana presha, basi dawa za presha, au magonjwa yoyote ambayo anaweza kuwa nayo mama.
NI MUHIMU SANA, mama kuzingatia dozi aliyoelekezwa na kumaliza dozi bila kuacha.
#MaamuziYakoKeshoYako
Katika matumizi ya dawa, mama anatakiwa kuhakikisha hatumii dawa YOYOTE ambayo hajaelekezwa na daktari ANAYEFAHAMU KUWA YEYE NI MJAMZITO. Yani iwapo mama ameenda kumuona daktari, lazima aseme kuwa ni mjamzito kwasababu baadhi ya dawa ni hatari kwa mimba
#MaamuziYakoKeshoYako Image
6. Elimu kuhusu homa ya ini, kunyonyesha, lishe ya mama, maandalizi ya uzazi na bima ya afya.
Elimu hii ni muhimu sana kwa mama, mtoto na baba hasa katika maandalizi ya kujifungua na kulea mtoto. Lishe ya mama inaamua mtoto akue vipi tumboni.
#MaamuziYakoKeshoYako
7. Usiri, mama anatakiwa kutambua kuwa, anapopimwa na kuonana na daktari ana haki ya kuwa na usiri. Yani, vipimo hivyo viwe kati yake na mwenza na daktari na nesi lakini taarifa zake ia zisiwekwe wazi kwa watu wengine zaidi ya wanaohusika.
#MaamuziYakoKeshoYako Image
Mwisho kabisa, ambacho ni muhimu zaidi. Ni mama kutambua kuwa ana haki juu ya yule kiumbe aliyembeba. Kwamba ushauri wa daktari unakuja kwanza kabla ya mengine yote. Kueleweshwa maana ya vipimo alivyofanyiwa na majibu yake. Na sababu za vipimo hivyo.
#MaamuziYakoKeshoYako
Afya ya mama mjamzito ni jukumu la jamii kiujumla, na NAKUMBUSHIA: Ewe BABA, kwenda KLINIKI na MAMA MJAMZITO sio OMBI, ni JUKUMU LAKO kufahamu hali ya mtoto na mama na kuwa sehemu ya MALEZI ya huyo mtoto tangu akiwa tumboni.
#MaamuziYakoKeshoYako Image

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Kuduishe Kisowile Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @Kudu_ze_Kudu

Jan 4
I woke up today with so much in my mind, and that Sylvia Plath quote pierced right through me and I felt every inch of it.
This made me think about the life cycle of a butterfly and how much it resonates with our lives. Female butterflies lay many eggs because not all will (1/?)
survive. Apparently, we are the eggs that survived long enough to become caterpillars. Oh the fun stage, probably the school years where we ate and ate and ate and ate again to grow and run around exploring everything. Then comes the pupa stage, the very uncomfortable (2/?)
one especially because hidden inside the coccoon is us knowing what we are cooking but outside it looks like we are stuck in a box for weeks, months and even years. This is a stage of patience and resilience. Depending on the species, the pupa may be suspended under a (3/?)
Read 9 tweets
Apr 23, 2023
A lot of people spend most of their lives away from their families and homes that they barely build a community around them. They become visitors of their own homes. Things that used to hold people who live around together don’t do that much anymore. Weddings, funerals conducted Image
far from home. Where one builds their house to call home is not where they live. So, you have this group of people who have spent most of their lives away from home for years and suddenly they have to build a home and make it work with those within it and around it.
Kids spend years in boarding schools away from home and holidays are for visiting relatives again away from home. For years & suddenly they get to university and have the new found freedom in their hostels and home becomes somewhere they visit when they can; again AWAY FROM HOME
Read 15 tweets
Mar 3, 2023
Mjadala uliofanyika leo katika mkutano mkuu wa MEWATA kuhusu afya ya akili baada ya kujifungua, umenikumbusha mbali.
Siku moja napita round wodi ya watoto wachanga nawahimiza kina mama kunyonyesha watoto, mama mmoja aliniita “dokta ukimaliza njoo” #UZI #MEWATA2023
Nilipoenda akamchukua mwanae akanikabidhi mkononi akasema, “shogaangu hebu niangalizie mwanangu, maana mie sijielewi”
Nikamuuliza, “unajiskiaje” nikidhani labda ana shida ya mwili ili tuwaite watu wa wodi ya kina mama waje kumhudumia. Akasema, “yani nikimbeba hivi mtoto kumpa
maziwa, kuna sauti zinaniambia kabisa nimnyonge. Yani nawaza nimzibe pumzi afe. Sasa mi sitaki kumdhuru mwanangu, naomba unilelee tu”

Unajua hivi vitu ukivisoma kwenye vitabu vinaonekanaga kama utani fulani hivi hadi siku unakutana navyo. Nikawasiliana na in charge tukatoa
Read 13 tweets
Oct 3, 2022
When I saw a stream of blood down my leg, I knew right there and then; it’s happening! My worst nightmare was coming true and I couldn’t believe it because it was already days after delivery. I have NEVER been that terrified ALL MY LIFE.
This is my story: SURVIVING PPH #Thread 🧵
I tried to be calm, but I could hear my heart pounding in my ears. It felt like someone ripped out my heart and put it in speaker right next to my ears. I felt dizzy, so I sat down. I can’t tell if I was dizzy because of blood loss or the fear of becoming a statistic.
As we prepared to go back to the hospital, I tried so hard to appear calm; a big smile on my face but in my heart I was terrified. I knew it very well, PostPartum Hemorrhage is no joke. In a matter of seconds EVERYTHING COULD GO WRONG.
I asked for ONE thing: my rozary ring.
Read 24 tweets
Sep 26, 2022
Kuna safari hata ziwe fupi vipi, hazisahauliki. Hazisahauliki kwa mengi; watu uliosafiri nao, watu uliokutana nao, experience ya safari na mengine mengi.
Mimi safari hii pichani sitaisahau.
Nilipata wasaa wa kushare na @buguzi @NormanJonasMD @DrArabiFrank na @JuliethSebbaMD #UZI Image
Ilianza kama utani hivi, nikafahamishwa nimepata nafasi ya kufanya mafunzo Morogoro ambayo yaliandaliwa na @sikika1 na @tacaidsinfo
Na mimi mpenda safari na mpenda afya, naanzaje kukosa? Nikafungasha kibegi changu uelekeo mji kasoro bahari.
Moro bwana! Moro PAZURI NYIE! Basi tu. ImageImageImageImage
Katika mengi nilojifunza siku hizo mbili, kuna kitu kimoja kilichonivutia zaidi ya mandhari nzuri ya Morogoro, maana mara ya mwisho nilikuwa hapa ilikuwa ni trip ya Udzungwa na Mto Mawe.
Kitu hicho ni Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (ATF). Leo naomba niwashirikishe Image
Read 16 tweets
Jul 28, 2021
SEHEMU YA PILI #IjueChanjoNaDaktariMwandishi
Leo, saa 3 asubuhi, Rais SSH atazindua chanjo pale ikulu kwa kupata chanjo hiyo.
Wakati huo, tuendelee kujifunza kuhusu chanjo za COVID19 haswa aina ya Johnson&Johnson ambayo ndio imepokelewa. #UZI FUATILIA
#DaktariMwandishi
3. JE, NIKIPATA CHANJO YA COVID19 KUTANIFANYA NIWE NA SUMAKU (MAGENTIC)?

Hapana. Chanjo za COVID19 hazina uwezo wa kutengeneza "electromagnetic field" (uwezo wa wewe kuwa sumaku) na chanjo zote hazina metals.
Unaweza kuangalia nini kimo kwenye chanjo katika ukurasa wa CDC.
4. KWANINI BAADHI YA TAARIFA ZINASEMA TUMEPOKEA CHANJO YA JOHNSON&JOHNSON NA NYINGINE ZINASEMA "JANSSEN"?
Jina kamili la chanjo iliyopokelewa Tanzania kupitia mpango wa COVAX ni "Johnson&Johnson's Janssen(J&J/Janssen) COVID19 Vaccine" kwahiyo ni kitu kimoja wala si chanjo tofauti
Read 18 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(