Kuduishe Kisowile Profile picture
Sep 20, 2020 20 tweets 10 min read Read on X
Oooh Mama Afrika! Tunakusifu kwa kuijaza Afrika. Kwa kutupa matunda bora ya mbegu zilizopandwa kwako.
Tumeona kilio chako kutoka nyikani. Kilio chako kwa matunda yako yaliyopotea kabla hayajaiva.
Mama Afrika, kilio chako tumekisikia. Futa machozi.
Kwani #MaamuziYakoKeshoYako #UZI
Ni siku nyingine tulivu, baada ya purukushani za daladala kuwahi hospitali, nilimsalimu nesi wa zamu huku nikivaa koti langu tayari kuandaa meza kwa ajili ya kliniki ya kina mama wajawazito.
Mlipuko wa homa ya virusi vya Korona ulikuwa umeanza, na siku ile #MaamuziYakoKeshoYako
Tulikuwa na mengi ya kuongea na kina mama wajawazito.
Nesi alitupa kila mmoja jukumu la kuelezea kitu kimoja.
Kabla ya kliniki, kabla ya kugawa namba kwa ajili ya kumuona daktari, ni lazima tutoe MASOMO mbalimbali kwa faida ya kina mama wajawazito.
#MaamuziYakoKeshoYako
Leo tulikuwa na masomo manne:
1. COVID19
2. Homa ya ini
3. Dalili za hatari kwa mama mjamzito
4. Umuhimu wa bima na maandalizi ya uzazi

Masomo yalifundishwa lkn somo la tatu lilitakiwa kuwa la majadiliano.
Nesi alichagua mama kila benchi ataje dalili hizo #MaamuziYakoKeshoYako
Kina mama wengi ambao waliweza kujibu walikuwa na mimba ya pili au zaidi, wale wa mimba ya kwanza wengi walikosea.
Nesi akawaita wale kina baba wote walioandamana na wake zao wajawazito, akawaambia, "kila mmoja ataje dalili moja ya hatari kwa mama mjamzito"
#MaamuziYakoKeshoYako
Kila mmoja alikuwa kimya.
Nesi akasema, "nyie kina baba ndio wasimamizi wa wake zenu wajawazito, nyie ndio mnalala na kuamka nao, haya hamjui dalili za hatari, unamsaidiaje huyo mkeo sasa? Unajuaje kwamba anacholalamika sasa hivi ni hatari au kawaida?"
#MaamuziYakoKeshoYako
Kimya kikatawala. "Kakaeni", akawaambia sura yake ikionyesha wazi kukwazwa na kilichotokea.
Huku akipanga kadi za kliniki aanze kuita majina alinong'ona, "watu wanadhani kuja kliniki ni ili tu wahudumiwe mapema basi"
Zoezi likaendelea, tukipima uzito, presha #MaamuziYakoKeshoYako
Na kuwaelekeza kuingia kwa daktari.
Nikiwa najaza taarifa zao, alikuja mama mmoja wa makamo, ilikuwa mimba yake ya tano lakini zote nne zilikuwa zimeharibika. Alikuwa amekuja na mumewe, mtoto hachezi tumboni. Akaruhusiwa kuingia kwa daktari akiwa na mumewe. #MaamuziYakoKeshoYako
Nilipoingia kwa daktari kukabidhi kadi zao, walikuwa wanampa majibu ya ultrasound. Kwa bahati mbaya mtoto alikuwa amefariki.
Mama yule aliinama, mume wake akamshikilia, akamkumbatia. Wote wakalia. Huyu ni mtoto wa TANO wamempoteza. Ilisikitisha.
#MaamuziYakoKeshoYako
Baada ya kushauriwa na daktari walitoka akaingia dada mmoja wa miaka 20 hivi, yeye alikuwa peke yake
Alianza, "Daktari, mimi hii ni mimba yangu ya kwanza, nina presha na nimekuwa natumia dawa lakini tangu majuzi mtoto hachezi, nikaambiwa ni kawaida inatokea"
#MaamuziYakoKeshoYako
Daktari akampandisha kitandani akapima tumbo kusikiliza mapigo ya moyo ya mtoto. Hakuyasikia.
Akamuuliza, "ni mtoto hachezi tu, au kuna hali yoyote ya tofauti umeisikia hapo kabla ya kuona mtoto hachezi?"
Akasema, "Wiki ilopita nilitokwa na damu kidogo, wifi
#MaamuziYakoKeshoYako
alisema inatokeaga kwenye ujauzito wa kwanza, kwahiyo sikutilia maanani. Lakini kutokea hapo mtoto alipunguza kucheza. Pia nimekuwa naumwa sana kichwa, wakati mwingine uso unavimba yani mwili mzima. Nakunywa dawa zangu za presha basi"
Akaelekezwa kupima
#MaamuziYakoKeshoYako
Ultrasound. Baada ya muda akarudi, ultrasound ikionyesha mtoto amefariki, amekuwa mummified. Daktari akamueleza kinachoonekana. Yule dada alilia sana, akagalagala pale chini, tukambeba tukamuingiza kwenye chumba cha ushauri akaongea na daktari kutulizwa
#MaamuziYakoKeshoYako
Hawa wawili ni mifano ya wanawake wengi wanaopoteza watoto kwasababu ya kutofahamu dalili za hatari, na wanaowazunguka kutofahamu pia.
Je, unafahamu ni dalili gani hizo?
-Homa kali, Degedege, kutokwa na damu ukeni, mwili kuvimba, maumivu makali ya kichwa
#MaamuziYakoKeshoYako
Lakini zaidi ya zile za wakati wa ujauzito, kuna dalili za hatari wakati wa kujifungua, ambazo zinaweza kusababisha kifo cha mama, mtoto au wote.
Dalili hizi ni kama zinavyoonekana hapo chini.
Ni muhimu kwa wanaomjali mama mjamzito kuzifahamu hizi.
#MaamuziYakoKeshoYako
Lakini haya yote yanawezekana tu iwapo wanaomjali mama mjamzito haswa kina baba watahudhuria kliniki pamoja na wenza wao, na kujifunza yanayofundishwa huko.
Pia kuwahi kuanza kliniki na kwenda pale unapoona mabadiliko yoyote katika mwili.
#MaamuziYakoKeshoYako
Muhimu zaidi ni kuhakikisha kama mama mjamzito ana magonjwa ya muda mrefu kama presha, kisukari, magonjwa ya moyo n.k anaendelea na dawa hizo kama anavyoelekezwa na daktari.
Na kuhakikisha anachoma chanjo na kunywa dawa zote anazotakiwa wakati wa ujauzito
#MaamuziYakoKeshoYako
Iwapo ataumwa ugonjwa wowote, ni lazima amfahamishe daktari kuwa yeye ni mjamzito ili kuepuka dawa zinazoweza kumdhuru mtoto tumboni.
Kuepuka matumizi ya mitishamba, na dawa zisizothibitishwa na wataalamu ambayo yanaweza kusababisha mimba kuharibika
#MaamuziYakoKeshoYako
Kina baba kuja kliniki na mwenzi wako ni JUKUMU lako, sio OMBI.
Ni JUKUMU lako kufahamu dalili za hatari.
Ni JUKUMU lako kutoa sapoti ya kihisia kwa mama mjamzito wakati wote hasa wakati anapopitia hali ngumu kama mimba kuharibika, kuumwa n.k
#MaamuziYakoKeshoYako
Ooh Mama Afrika. Nimefikisha ujumbe kwa matunda ya tumbo lako. Nimefikisha ujumbe kwa wapanda mbegu. Nimefikisha ujumbe kwa mataifa.
Nitakulinda Mama Afrika hadi uijaze dunia.
Nchi ipambwe na matunda ya tumbo lako.
Tuponye maumivu ya wale uliowapoteza.
#MaamuziYakoKeshoYako

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Kuduishe Kisowile Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @Kudu_ze_Kudu

Jan 4
I woke up today with so much in my mind, and that Sylvia Plath quote pierced right through me and I felt every inch of it.
This made me think about the life cycle of a butterfly and how much it resonates with our lives. Female butterflies lay many eggs because not all will (1/?)
survive. Apparently, we are the eggs that survived long enough to become caterpillars. Oh the fun stage, probably the school years where we ate and ate and ate and ate again to grow and run around exploring everything. Then comes the pupa stage, the very uncomfortable (2/?)
one especially because hidden inside the coccoon is us knowing what we are cooking but outside it looks like we are stuck in a box for weeks, months and even years. This is a stage of patience and resilience. Depending on the species, the pupa may be suspended under a (3/?)
Read 9 tweets
Apr 23, 2023
A lot of people spend most of their lives away from their families and homes that they barely build a community around them. They become visitors of their own homes. Things that used to hold people who live around together don’t do that much anymore. Weddings, funerals conducted Image
far from home. Where one builds their house to call home is not where they live. So, you have this group of people who have spent most of their lives away from home for years and suddenly they have to build a home and make it work with those within it and around it.
Kids spend years in boarding schools away from home and holidays are for visiting relatives again away from home. For years & suddenly they get to university and have the new found freedom in their hostels and home becomes somewhere they visit when they can; again AWAY FROM HOME
Read 15 tweets
Mar 3, 2023
Mjadala uliofanyika leo katika mkutano mkuu wa MEWATA kuhusu afya ya akili baada ya kujifungua, umenikumbusha mbali.
Siku moja napita round wodi ya watoto wachanga nawahimiza kina mama kunyonyesha watoto, mama mmoja aliniita “dokta ukimaliza njoo” #UZI #MEWATA2023
Nilipoenda akamchukua mwanae akanikabidhi mkononi akasema, “shogaangu hebu niangalizie mwanangu, maana mie sijielewi”
Nikamuuliza, “unajiskiaje” nikidhani labda ana shida ya mwili ili tuwaite watu wa wodi ya kina mama waje kumhudumia. Akasema, “yani nikimbeba hivi mtoto kumpa
maziwa, kuna sauti zinaniambia kabisa nimnyonge. Yani nawaza nimzibe pumzi afe. Sasa mi sitaki kumdhuru mwanangu, naomba unilelee tu”

Unajua hivi vitu ukivisoma kwenye vitabu vinaonekanaga kama utani fulani hivi hadi siku unakutana navyo. Nikawasiliana na in charge tukatoa
Read 13 tweets
Oct 3, 2022
When I saw a stream of blood down my leg, I knew right there and then; it’s happening! My worst nightmare was coming true and I couldn’t believe it because it was already days after delivery. I have NEVER been that terrified ALL MY LIFE.
This is my story: SURVIVING PPH #Thread 🧵
I tried to be calm, but I could hear my heart pounding in my ears. It felt like someone ripped out my heart and put it in speaker right next to my ears. I felt dizzy, so I sat down. I can’t tell if I was dizzy because of blood loss or the fear of becoming a statistic.
As we prepared to go back to the hospital, I tried so hard to appear calm; a big smile on my face but in my heart I was terrified. I knew it very well, PostPartum Hemorrhage is no joke. In a matter of seconds EVERYTHING COULD GO WRONG.
I asked for ONE thing: my rozary ring.
Read 24 tweets
Sep 26, 2022
Kuna safari hata ziwe fupi vipi, hazisahauliki. Hazisahauliki kwa mengi; watu uliosafiri nao, watu uliokutana nao, experience ya safari na mengine mengi.
Mimi safari hii pichani sitaisahau.
Nilipata wasaa wa kushare na @buguzi @NormanJonasMD @DrArabiFrank na @JuliethSebbaMD #UZI Image
Ilianza kama utani hivi, nikafahamishwa nimepata nafasi ya kufanya mafunzo Morogoro ambayo yaliandaliwa na @sikika1 na @tacaidsinfo
Na mimi mpenda safari na mpenda afya, naanzaje kukosa? Nikafungasha kibegi changu uelekeo mji kasoro bahari.
Moro bwana! Moro PAZURI NYIE! Basi tu. ImageImageImageImage
Katika mengi nilojifunza siku hizo mbili, kuna kitu kimoja kilichonivutia zaidi ya mandhari nzuri ya Morogoro, maana mara ya mwisho nilikuwa hapa ilikuwa ni trip ya Udzungwa na Mto Mawe.
Kitu hicho ni Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (ATF). Leo naomba niwashirikishe Image
Read 16 tweets
Jul 28, 2021
SEHEMU YA PILI #IjueChanjoNaDaktariMwandishi
Leo, saa 3 asubuhi, Rais SSH atazindua chanjo pale ikulu kwa kupata chanjo hiyo.
Wakati huo, tuendelee kujifunza kuhusu chanjo za COVID19 haswa aina ya Johnson&Johnson ambayo ndio imepokelewa. #UZI FUATILIA
#DaktariMwandishi
3. JE, NIKIPATA CHANJO YA COVID19 KUTANIFANYA NIWE NA SUMAKU (MAGENTIC)?

Hapana. Chanjo za COVID19 hazina uwezo wa kutengeneza "electromagnetic field" (uwezo wa wewe kuwa sumaku) na chanjo zote hazina metals.
Unaweza kuangalia nini kimo kwenye chanjo katika ukurasa wa CDC.
4. KWANINI BAADHI YA TAARIFA ZINASEMA TUMEPOKEA CHANJO YA JOHNSON&JOHNSON NA NYINGINE ZINASEMA "JANSSEN"?
Jina kamili la chanjo iliyopokelewa Tanzania kupitia mpango wa COVAX ni "Johnson&Johnson's Janssen(J&J/Janssen) COVID19 Vaccine" kwahiyo ni kitu kimoja wala si chanjo tofauti
Read 18 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(