Leo tunaendelea na experience yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro ambapo machozi, jasho na damu ni sehemu ya safari hii inayohitaji ujasiri na moyo wa chuma kweli kweli..

Mfululizo wa matukio niliyopitia unaweza kukufundisha na kukuandaa vyema ewe Mtalii mtarajiwa 😅😅

UZI 👇🏾
Kituo 1: MLIMA URUGURU

Urefu wa Mlima Uluguru ni kama 8600ft. Na huu ulikuwa ni moja ya mlima wa majaribio kabla ya kupanda Mlima Kilimanjaro.

Kiukweli hili lilikuwa ndio jaribio rahisi kuliko yote hadi tukaona kumbe mambo ni mepesi hivi! Tungejua 😃😃
Nakumbuka tulienda siku ya Ijumaa. Jumamosi tukapanda Mlima. Jumapili tukarudi Dar.

Mandhari ya Uluguru ni bomba sana. Kuna memories nyingi nzuri ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls 🤩🤩

Waluguru mmebarikiwa ndugu zetu. Hii ni moja ya kumbukumbu yangu bora pale!
Jambo ambalo sikupenda Uluguru ni hali ya choo pale. Nakumbuka nilibanwa haja kubwa ila mzigo wangu niliubana hadi nilivyorudi town maana kushusha gogo porini nilikuwa siwezi. Sijui kwanini SUA hawarekebishi 😬

Hiz ni tents tulizotumia kulala muda wote tukiwa pale. Usalama 100%.
Na hapa ni camp tulikofikia. Panaitwa Morning Site. Jengo fulani amazing sana!

Humo ndani kuna machata ya watu wengi sana. Panavutia mno kusema ukweli.

Palinikumbusha yale machata tuliyokuwa tunayaona shuleni enzi hizo tunasoma!
Hapa MORNING SITE naamini kina @BarakaSaimon3
@Eric_Bernard94 @officielsalome @kigogo2014 @rollymsouth
@MiriamMkanaka @YourFrenchFry @chapo255 @Roma_Mkatoliki na ndugu zangu wengine siku wakipita lazima waache alama!!

Mambo ya #ChapoWasHere #DearCoco 😜😜
Muonekano nikiwa nabarizi maeneo mbalimbali ya Milima ya Uluguru mkoani Morogoro..

🇹🇿#Tanzania ni nchi nzuri sana sana. Tuilinde na kuitunza kwa wivu mkubwa!

Nazipongeza @MaliasiliUtalii na @TTBTanzania kwa kazi nzuri wanazozifanya kutunza haya maeneo ya kujidai!
Kwa leo naomba niishie hapa. Kesho nitaendelea na kituo kinachofuata ambacho ni Moshi kuelekea Marangu. Huko sasa ndio picha linapoanzia 😃

Ikumbukwe hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwenda kupanda Mlima Kilimanjaro, hivyo kila nilichokutana nacho kilikuwa kipya kwangu.. Acheni tu!
Marangu ilikuwaje? Tulikutana na wakina nani? Tulipokelewaje?

Haya yote nitayajibu kesho mapema. Unaweza kuweka notification on ili upate taarifa punde tu nitakapopanda hewani.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Habiba Mtanzania 🇹🇿

Habiba Mtanzania 🇹🇿 Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @habibamtanzania

13 Apr
SAFARI YA MOSHI

Tunaingia Moshi usiku saa 2 na kupokelewa na wenyeji wetu wakarimu kishenzi. Wale ma-guide sijui walidhani tumetoka nchi gani hatujui Kiswahili, kumbe ni wabongo tu😅😅

Nadhani walishazoea wanaoenda kupanda Mlima ni foreigners tu. Hii kidogo ilinisikitisha.. Image
Hoteli tuliyofikia kulikuwa na wazungu kibao. Wengi wametoka mlimani wakipongezana kwa dinner, wines na kupeana vyeti..

Nikawa nawatizama kwamba can I do this? Unaona watu wanachechemea miguu, sura hazitamaniki wamebabuka, wengi wako hoi.

Nikaguna, mambo yenyewe ndio hivi!!!
Basi, ule usiku tukafanyiwa training na rescue team ya ile kampuni.

Tukapewa maelekezo yote muhimu yaliyohitajika. Asubuhi safari ya Mlimani.

Nilikuwa na shauku na hofu kwa wakati mmoja. Nikasali na kuamua liwalo na liwe. Kesho ndio kesho!
Read 7 tweets
10 Apr
Miaka kadhaa iliyopita nilipata mzuka wa kwenda kutimiza moja ya ndoto zangu kubwa - kupanda Mlima Kilimanjaro.

Siku zote nilitamani kufika juu kabisa ya "Paa la Afrika". Nikasema ipo siku tu!

Hatimaye siku zikawadia za kuitimiza ndoto yangu hii kongwe.

Ilikuwaje?

THREAD👇🏾
Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails. Sikusafiri peke yangu, kundi letu tulikua 21. Njia tuliyotumia ni Marangu.

Gharama ilikuwa ni USD 560 kwa kila mmoja na hii ilihusisha kila kitu kuanzia usafiri Dar-Moshi, chakula, hoteli, vifaa, ada za getini, personal guides n.k.
MAANDALIZI YA SAFARI

Baada ya kuthibitisha ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro, jambo la kwanza nilifanya medical checkup. Nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni.

Basi, nikaanza mazoezi. Nakimbia uwanja huki nazunguka mara 7-10 kila siku kuuandaa mwili..
Read 8 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!