SAFARI YA MOSHI

Tunaingia Moshi usiku saa 2 na kupokelewa na wenyeji wetu wakarimu kishenzi. Wale ma-guide sijui walidhani tumetoka nchi gani hatujui Kiswahili, kumbe ni wabongo tu๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…

Nadhani walishazoea wanaoenda kupanda Mlima ni foreigners tu. Hii kidogo ilinisikitisha..
Hoteli tuliyofikia kulikuwa na wazungu kibao. Wengi wametoka mlimani wakipongezana kwa dinner, wines na kupeana vyeti..

Nikawa nawatizama kwamba can I do this? Unaona watu wanachechemea miguu, sura hazitamaniki wamebabuka, wengi wako hoi.

Nikaguna, mambo yenyewe ndio hivi!!!
Basi, ule usiku tukafanyiwa training na rescue team ya ile kampuni.

Tukapewa maelekezo yote muhimu yaliyohitajika. Asubuhi safari ya Mlimani.

Nilikuwa na shauku na hofu kwa wakati mmoja. Nikasali na kuamua liwalo na liwe. Kesho ndio kesho!
SAFARI YA MARANGU

Alfajiri tukaamka!

Mimi pamoja na kununua vifaa vya mlimani lakini bado nilikuwa nahitaji kukodi baadhi ya vifaa kama vile hiking boot, balaclava, walking stick, sleeping bags zile zenye joto maana huko juu tushaambiwa kuna baridi la kufa mtu..
Saa 3 asubuhi tukaanza safari ya Marangu. Si umbali mrefu.

Usajili getini tukamaliza saa 9 mchana.

Mwezi ule ulikuwa ni ile miezi ya high season, hivyo kuna watu kutoka nchi mbalimbali walikuwa wamekuja kupanda mlima. Yaani kulikuwa na nyomi la kufa mtu!
Jambo nililopenda Marangu getini kuna ramani ya njia unayotumia kufika kileleni.

Pia kuna picha za kumbukumbu za watu waliofanikiwa kupanda mlima kwa muda mchache. Kuna mmoja alipanda kwa 5hrs tu. Huyu hadi leo najiuliza aliwezaje? Masaa 5 hadi kileleni is not a joke!

๐Ÿ“ธGetini
Leo naomba niweke kituo hapa. Kesho nitaelezea kwa kirefu yaliyojiri kuanzia hapo getini hadi Mandara huko na ugumu wake.

Nitamtambulisha na personal guide wangu Freddy๐Ÿ˜๐Ÿ˜

Huyu kaka alinisaidia sana sana. Sitamsahau! Safari ingenishinda mapema isingekuwa yeye.

Kesho jameni ๐Ÿ˜…

โ€ข โ€ข โ€ข

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
ใ€€

Keep Current with Habiba Mtanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

Habiba Mtanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @habibamtanzania

14 Apr
MANDARA

Hii ndio ilikuwa point yangu ya kwanza baada ya kutoka getini. Nilikuwa na personal porter anaitwa Fredy. Mwenyewe alinipokea bag (back pack) na kujitambulisha kwangu.

Ukiwa na personal guide ina maana yeye atakua na wewe bega kwa bega, achana na wale guide wa group..
Tulianza kwa story akanielezea safari zake milimani. Yeye keshapanda mara 6 hadi Uhuru Peak. I was excited!

Mwanzo story zilikolea baadae zikakata ule uchovu.

Tunavyopanda tulikuwa tunakutana na makundi ya watu wanarudi na wengi walikua wanatuambia โ€œpole poleโ€..
..nadhani huu ndio msemo maarufu ukifuatiwa na โ€œJamboโ€.

Nilianza kuchoka jinsi masaa yanavyokwenda. Nikawa kama siwezi kupumua vizuri. Muda mwingi Fred alikuwa ananisitiza kunywa maji.

Kuna muda wenzangu walikuwa mbele..
Read 13 tweets
12 Apr
Leo tunaendelea na experience yangu ya kupanda Mlima Kilimanjaro ambapo machozi, jasho na damu ni sehemu ya safari hii inayohitaji ujasiri na moyo wa chuma kweli kweli..

Mfululizo wa matukio niliyopitia unaweza kukufundisha na kukuandaa vyema ewe Mtalii mtarajiwa ๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…

UZI ๐Ÿ‘‡๐Ÿพ
Kituo 1: MLIMA URUGURU

Urefu wa Mlima Uluguru ni kama 8600ft. Na huu ulikuwa ni moja ya mlima wa majaribio kabla ya kupanda Mlima Kilimanjaro.

Kiukweli hili lilikuwa ndio jaribio rahisi kuliko yote hadi tukaona kumbe mambo ni mepesi hivi! Tungejua ๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ
Nakumbuka tulienda siku ya Ijumaa. Jumamosi tukapanda Mlima. Jumapili tukarudi Dar.

Mandhari ya Uluguru ni bomba sana. Kuna memories nyingi nzuri ila mojawapo ni kuoga alfajiri katika water falls ๐Ÿคฉ๐Ÿคฉ

Waluguru mmebarikiwa ndugu zetu. Hii ni moja ya kumbukumbu yangu bora pale!
Read 9 tweets
10 Apr
Miaka kadhaa iliyopita nilipata mzuka wa kwenda kutimiza moja ya ndoto zangu kubwa - kupanda Mlima Kilimanjaro.

Siku zote nilitamani kufika juu kabisa ya "Paa la Afrika". Nikasema ipo siku tu!

Hatimaye siku zikawadia za kuitimiza ndoto yangu hii kongwe.

Ilikuwaje?

THREAD๐Ÿ‘‡๐Ÿพ
Kampuni niliyotumia inaitwa Origin Trails. Sikusafiri peke yangu, kundi letu tulikua 21. Njia tuliyotumia ni Marangu.

Gharama ilikuwa ni USD 560 kwa kila mmoja na hii ilihusisha kila kitu kuanzia usafiri Dar-Moshi, chakula, hoteli, vifaa, ada za getini, personal guides n.k.
MAANDALIZI YA SAFARI

Baada ya kuthibitisha ushiriki wangu kupanda Mlima Kilimanjaro, jambo la kwanza nilifanya medical checkup. Nikawa 100% fit kupanda mlima na hadi kufika kileleni.

Basi, nikaanza mazoezi. Nakimbia uwanja huki nazunguka mara 7-10 kila siku kuuandaa mwili..
Read 8 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!