MBINU 5 ZITAKAZOKUSAIDIA KUKUZA BIASHARA YAKO KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII.

Inawezekana hapo ulipo umekwama, huoni maendeleo yoyote ya biashara yako, wakati huo huo unaona wapinzani wako wanaendelea kupiga hatua.

Upo katika hali hiyo?
Usiwe na wasiwasi, kila mfanyabiashara au mjasiriamali kama wewe, amewahi kupitia hali kama hiyo.

Kama umeshindwa leo, haina maana utaendelea kushindwa kila siku.

Au unasemaje Brother @mafolebaraka ?
Siku zote SILAHA kubwa katika biashara na MAARIFA!

Maarifa ndio silaha yako kubwa, ndio maana leo unapaswa kunisikiliza kwa makini kwa sababu ninaenda kukupa MAARIFA (Mbinu) takazokusaidia kufufua tena matumaini yako.
Bahati nzuri, inawezekana washindani wako hawajui chochote kuhusu kile ninachotaka kukuambia leo.

Sasa, nisikilize kwa makini...

Hizi ni mbinu 5 Muhimu zitakazusaidia kukuza Biashara yako hasa kupitia mitandao ya kijamii.
1. Tafuta Eneo moja, kisha TULIA.

Changamoto kubwa ya wajasiriamali wengi, ni kutaka kuweka Biashara zao katika kila mtandao.

Kama na wewe unafanya hivyo, badilika mara moja!

Kutangatanga katika kila mtandao, ni njia rahisi ya kudhorotesha ukuaji wako.
Kama ndio kwanza unaanza, focus zaidi katika mtandao mmoja.

Maana yake, juhudi zako elekeza katika mtandao unaoufahamu vizuri na unaweza kuutumia.

Lakini kikubwa zaidi, angalia mtandao unaotumiwa na kundi kubwa la wateja wako.
Sasa, baada ya kutumia mtandao huo kwa muda, fanya analysis. Angalia kama unapata matokeo unayoyahitaji

Kama hakuna ukuaji wowote, basi unaweza kuongeza mtandao mwingine

Lengo hapa ni kupata mtandao mmoja utakaokupa matokeo mazuri zaidi na kukuletea wateja katika biashara yako
2. Tengeneza LIST yako

@NyandaAmosi anasema, pesa ipo kwenye list yako.

List inaweza kuwa namba za simu za wateja wako, whatsapp contact zako , au whatsapp groups unazosimamia wewe.
Sikiliza, huna guarantee ya follower wa mtandaoni kununua bidhaa yako, lakini una uhakika wa kuuza bidhaa kutoka kwa mteja uliye save namba yake

Why?

Kwa sababu huna umiliki wa followers wako ( You dont own them), lakini katika LIST yako una umiliki wa jina & namba zao za simu
Ni kweli, kuna faida kubwa ya kuwa na followers wengi.

Lakini, linapokuja suala la kubadili followers wako (@NyandaAmosi anawaita cold traffic) kuwa mteja (hot traffic), LIST yako ndio ufunguo wako.
3. Tumia kanuni ya 80 - 20 katika Maudhui.

Sasa, wafanyabiashara wengi ni wavivu wa kutengeneza maudhui (contents), wavivu mno kuandika.

Kama huwezi kuandika, unapoteza wateja wengi mno!

Mtafute @NyandaAmosi akufundishe!

Turudi kwenye kanuni ya 80 - 20.

Kanuni hii inasema,
"Asilimia 80 ya mafanikio yako, yatatokana na asilimia 20 ya juhudi zako katika kujitangaza."

Kwa watengeneza Maudhui kama @fotty__ kanuni hii inasema,

"Hakikisha 80% ya maudhui yako yanatoa VALUE kwa Audience wako, na 20% kufanya promotion ya biashara yako."
Wafundishe watu kuhusu huduma au bidhaa yako;

Kama unauza saa, wafundishe faida zake, jinsi ya kutofautisha saa original na fake, nk. Chochote unachouza, unaweza kukitengenezea maudhui yenye kuongeza VALUE kwa wafuasi/wateja wako watarajiwa.
Halafu tumia 20% zilizobaki kulipia Ads na kufanya promotion ya bidhaa zako bora na zenye demand kubwa kwa wateja wako.
4. Fanya Matangazo.

Nimegusia kidogo hapo juu.

Waswahili wanakuambia "Biashara, Matangazo"

Sasa kuna kitu natamani kukuambia....

Kabla ya kufanya Tangazo lolote, hakikisha unatengeneza FUNNEL.
Funnel ni mfumo unaweza kukusaidia kumvutia mtu asiyekufahamu kabisa, kushawishika kununua bidhaa yako.

Brother @GillsaInt ni mtaalamu sana wa kutengeneza funnels. Ongea nae vizuri.

Unapotangaza, maana yake unataka watu wengi (wasiokufahamu) waone na kununua bidhaa yako.
Kumbuka, HAWAKUFAHAMU!

Sasa kosa kubwa la wafanyabiashara wengi ni kujaribu kuuza kwa siku moja.

Ni sawa na kukutana na binti mrembo kwa mara ya kwanza, halafu ukataka ufunge nae ndoa. ATAKUKIMBIA tu!🙊
Ili tangazo lako livutie, hakikisha unaanza kutoa kitu flani BURE.

Mfano; Ushauri, Darasa online au short Ebook.

Ndani yake, sasa ndio unaweza kuweka ofa ya kile unachotaka kuuza.

Hapo unakuwa umetumia 80% Maudhui, halafu unamalizia 20% kuuza bidhaa yako.
5. Kuwa na Muendelezo (CONSISTENCY)

Kuna wakati utapata like 2, wakati mwingine 0 kabisa.

Kuna wakati utalipia matangazo, na kuishi kupata likes tu. Hupati simu wala DMs.

Haya yote ni kawaida huku mtandaoni.

Kikubwa ni kujitahidi kufanya Improvements kila wakati.
Always weka room ya kufanya Improvements. As you improve l, ndivyo utakavyozidi kukua.

Changamoto zisikufanye uishie njiani.

Endelea kutoa VALUE, endelea kupost, endelea kujitangaza, endelea kubadili strategies zako, mpaka pale utakapoona umeanza kupata matokeo mazuri.
Mbinu ya Nyongeza,

6. RETWEET Post hii.

Mafanikio yapo katika kusaidia watu wengine pia.

Hebu Retweet Post hii ili tuwasaidie watu wengine kupata Maarifa haya.

Asante kwa kusoma #UZI
huu mpaka mwisho.

Rafiki yako,

Anselmo.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Anselmo

Anselmo Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @CoachAnsey

16 Aug
JINSI YA KUTENGENEZA MAUDHUI (CONTENTS) YENYE KUONGEZA USHAWISHI KWA MTEJA.

Mara nyingi katika kutengeneza Maudhui, tunatumia mawazo, Ideas na ushawishi wetu binafsi...

..lakini, kuzingatia muonekano na aina ya Maudhui yanayoandikwa ni jambo muhimu mno.
Ni rahisi sana kutengeneza mawazo na topic mbalimbali kwa ajili ya wateja wako...

..Lakini, kama muuzaji, ni lazima uwe na uelewa mkubwa wa namna ya kuwasilisha mawazo hayo kwa mteja wako.
Ndio maana ni muhimu sana kufahamu namna mbalimbali ya kuandika maudhui yanayokidhi mahitaji ya mteja wako.

Kupitia mchanganyiko huu wa maudhui, itakusaidia kuongeza wafuasi wako zaidi, kufikia wateja wapya, na kutengeneza mazingira rafiki ya kuuza Bidhaa au huduma yako.
Read 13 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(