, 13 tweets, 2 min read
My Authors
Read all threads
Weekend hii nimesoma kitabu kuhusu kesi iliyomkabili Nyerere ya mwaka 1958. Huenda historia ya Tanzania ingekuwa tofauti kama kesi hii ingeamuliwa vinginevyo.

Kuna vitu vingine vizuri nimejifunza kuhusu wakati huo vyenye mafunzo kwetu leo - THREAD
Julius Nyerere alishtakiwa kwa makosa matatu ya kukashfu ma-DC wakikoloni.

Kwenye gazeti la Sauti ya TANU la Tar. 7 Mei 1958, Nyerere alitumia maneno kama 'washenzi', 'maharamia' na 'magava wa mistuni' kuwaelezea ma-DC wakikoloni, DC Weeks wa Geita na DC Scott wa Songea.
Tarehe 5 Juni 1958, ofisi za TANU mtaa wa New Street Na. 25 (sasa Lumumba) zilivamiwa na polisi wakiongozwa na Kamishna wa Polisi M. T. Mackinley.

Nyerere alihojiwa na ofisi za TANU kupekuliwa. Tarehe 9 Juni 1959 alisomewa mashtaka rasmi.
Nyerere alitetewa na mwanasheria maarufu wa kiingereza, D. N. Pritt, ambaye pia alisimamia kesi ya Jomo Kenyatta (Mau Mau) na Ho Chi Minh (Vietnam). Gharama za Pritt zilikua Sh. 23,700 (mshahara wa Nyerere wakati huo ulikua Sh 500 kwa mwezi)
Moja ya malalamiko ya Nyerere kwenye makala ya sauti ya TANU ilikua kuwa ma-DC wa kikoloni wananyanyasa wananchi na kufukuza kazi machifu kiholela, pamoja na kufunga ofisi za TANU mikoani bila kufuata utaratibu.
Serikali ya mkoloni ilipata shida kidogo kuthibitisha madai yake, ikambidi mwanasheria mkuu wa serikali kwenda mahakamani kuondoa shitaka moja kati ya yale matatu.
Kwenye hukumu, hakimu wa mahakama ya mwanzo L.A. Davies alisema Nyerere alikuwa mjumbe wa tume ya kutunga sheria (LEGCO) na angeweza kufikisha malalamiko yake kwa serikali bila kutumia gazeti na kutumia maneno kama 'washenzi' na 'maharamia'.
Nyerere alitiwa hatiani na kuhukumiwa faini ya Sh. 3,000 au kifungo cha miezi sita. Nyerere alilipa faini hio ndani ya siku mbili.

Kwa hali ya kisiasa wakati huo, endapo angelazimishwa kifungo, mapambano ya uhuru wa Tanganyika yangehamia kwenye silaha na vita.
Mengine madogo niliyojifunza.

Ulipo uwanja wa taifa sasa ulikua uwanja wa ndege. Nyerere alianza kuutumia baada ya mnazi mmoja kujaa mno.

Baraza la machifu wa Tanganyika wakati wa mkoloni lilikua linakutania Mzumbe, Morogoro (niliposoma sekondari lakini hili nilikua silijui).
Nyerere alikuwa mwekezaji, mpaka mwaka 1958 aliiambia mahakama kuwa alimiliki hisa kwenye makampuni tofauti zenye thamani ya Sh. 2,000. Nahisi aliziuza kabla ya Azimio la Arusha.
Inaaminika jalada la kesi hii ya Nyerere lilichukuliwa au kuchomwa na serikali ya mkoloni kipindi kifupi kabla ya uhuru kwani halikuonekana tena.
Kitabu kimeandikwa na Simon Ngh'waya, akipata msaada toka kwa Benjamin Mkapa, wakati huo waziri wa mambo ya nje wa Tanzania na mjumbe wa NEC, CCM (1990).
Sehemu ya majibu ya Nyerere akiwa Kizimbani.
Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh.

Enjoying this thread?

Keep Current with Samwel Ndandala

Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

Twitter may remove this content at anytime, convert it as a PDF, save and print for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video

1) Follow Thread Reader App on Twitter so you can easily mention us!

2) Go to a Twitter thread (series of Tweets by the same owner) and mention us with a keyword "unroll" @threadreaderapp unroll

You can practice here first or read more on our help page!

Follow Us on Twitter!

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just three indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!