Kuduishe Kisowile Profile picture
Aug 23, 2020 18 tweets 6 min read Read on X
Mara ya kwanza nilimuona kwenye muvi ambapo kichwa chake kilikuwa dili.
Ni mwanamke mrembo, ingawa filamu nyingi humuonyesha tofauti na historia isemavyo.
Nywele zake ni nyoka na ukikutanisha macho yake na yako unageuka jiwe. Anaitwa MEDUSA! #UZI FUATILIA
#DaktariMwandishi Image
Historia yake inatoka kwenye hadithi za kigiriki, jina lake MEDUSA likimaanisha "mlinzi". Alikuwa binti mrembo, bikra na mtumishi wa mungu wa bikra, Athena. Alimtumikia kwenye helalu lake hadi mungu wa bahari, Poseidon alipombaka Medusa. Akapata mimba ya mapacha lkn hakuzaa. Image
Yule mungu Athena, akamlaani Medusa, akabadili nywle zake nzuri kuwa nyoka na kila kiumbe, binadamu, mnyama au miungu iliyokutanisha naye macho aligeuka jiwe.
Medusa akakimbia kwa hofu baada ya kushindwa kuishi na watu na miungu. Akaenda kuishi mapangoni. Akajificha. Image
Lakini je, Athena alimlaani Medusa au alimlinda? Baada ya kubakwa na mungu wa bahari Poseidon, baadhi ya wanaamini Athena alimbadili Medusa kuwa vile kama njia ya kumlinda asidhuriwe tena na miungu au wanadamu, wengine wanaamini alimlaani hivyo kwasababu ya wivu wa uzuri wake. Image
Medusa alijificha kwa miaka mingi, huku wanadamu na miungu ikijaribu kumtafuta ili kukata kichwa chake na kukitumia kama silaha dhidi ya maadui zao.
Alikuja kufanikiwa mungu-mtu (demigod), akamkata kichwa.
Alipomkata kichwa, wale watoto aliokuwa nao Medusa, walitoka, mmoja Image
anaitwa Chrysaor, aliyekuwa binadamu na Pegasus, farasi mwenye mabawa.
Kifo cha Medusa kilikuwa kama ishara ya uhuru wake baada ya maisha ya tabu, ya kujitenga ya mateso na ya kukosa haki.
Filamu nyingi na vitabu vinamuonyesha Medusa kama jini mwenye kudhuru watu lakini uhalisia
ni kwamba, Medusa alikuwa mhanga wa uovu wa miungu na wanadamu. Alikuwa mhanga wa ubakaji, na hata baada ya hapo, hakuna aliyemuelewa zaidi aligeuzwa kuwa kiumbe cha kutisha na kushindwa kuishi maisha ya kawaida tena.
Kwa wale walio wahanga wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia,
hadithi ya Medusa si kitu kigeni kwao. Ni hadithi ambayo wahanga wa vitendo vya ubakaji hukutana nayo. Wanapokwenda kuripoti waliyotendewa, jamii huanza kwa kuwahukumu na kuwalaumu wao, na mwisho wao huonekana ni tatizo na wale wabakaji kubaki huru wakilindwa na jamii.
Baada ya karne nyingi za mapokeo ya kumuona Medusa kama mtu muovu, sasa maandiko mbalimbali yanabadilisha namna ambavyo yanamuandika. Yanaandika ukweli. Yanamuandika kama mhanga aliyehukumiwa na jamii. Binti aliyejitoa kumtumikia mungu Athena, na bado alipopatwa na shida, dunia Image
ikamgeuka. Laana ya Athena, ilikuwa baraka kwa Maisha ya Medusa. Ilikuwa ni kinga dhidi ya mtu yeyote kumdhuru tena. Leo hii, nembo ya kichwa cha Medusa, hutundikwa kwenye makazi ya wanawake waliotoka kwenye ndoa za manyanyaso, wahanga wa vipigo na ubakaji.
Ni nembo ya UNYONGE Image
uliobadilishwa kuwa NGUVU. Nembo ya kuonyesha uhodari wa kuweza kushinda mapito.
Leo hii, MEDUSA si mwovu tena, bali ni shujaa mbele ya mamilioni ya wahanga wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia. Kila mmoja wao anaielewa vema stori ya Medusa, kwani ni stori yake #MimiNiMedusa🐍
Karne nyingi zilizopita huko Ugiriki, miungu na wanadamu walishindwa kumlinda Medusa. Bahati mbaya, hali haijabadilika hata leo. Tumeshindwa kuwalinda wahanga wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia. Wengine wamelazimishwa kuolewa na waliowabaka. Wengine wamegeuziwa vibao na
kushtakiwa, wengine wamelaumiwa kwa kuwa wahanga wa vitendo hivi na wengine wamepotea kama Medusa. Wamewekewa alama kuwa "fulani yule aliyebakwa", ilhali waliowabaka wanatembea huru mitaani. Ni kaka, baba, waume, wajomba, babu, wachumba, wapenzi, mabosi, walimu, madaktari wetu.
Tumewalinda kwasababu hatuna utu, hatuna ubinadamu, hatujali maumivu ya wengine, kwasababu bado tunakumbatia maovu kwa mlango wa familia, utajiri na vyeo.
Ndio maana kesi hizi haziishi wala hazipungui. Zinapunguaje wakati tuna madaktari wanabaka wagonjwa hospitalini na hatusikii
mwisho wa kesi zao? Zinaishaje wakati, mtoto akibakwa tunayamaliza kifamilia? Zinaishaje wakati tunaona ni sawa kulewesha watu kisha kuwabaka? Zinaishaje wakati tunawatazama watoto wadogo wanafunzi kwa macho ya matamanio na tunaona ni sawa kuwataka kimapenzi, huu nao ni ubakaji.
Jambo moja naloamini, tunahitaji mahakama ya kesi za unyanyasaji wa kijinsia itengwe kwa hiyo kazi tu.
Kesi hizi nyingi hazifiki popote, na takwimu zinaonyesha kuwa 99% ya wabakaji hawapewi adhabu yoyote.
Tunahitaji kutoa elimu kwa watoto, jamii kusimama pamoja na kupiga vita
vitendo hivi kwa pamoja.
Watoto wetu wa kike na wa kiume, na wanawake wetu hawana ulinzi.
Sheria yetu inabidi kubadilishwa, hasa katika kipengele cha nini maana ya mwanaume kubakwa, kwasababu sheria yetu inalinda wabakaji wa kike. Na kulinda wanaume wanaobaka wake zao.
Iwapo kila mtu aliyebakwa, au kufanyiwa kitendo cha unyanyasaji wa kijinsia akiandika #MimiPia au #MimiNiMedusa🐍, tutashangaa kuona ni wangapi & watu kutoka rika, jinsia, umri, dini, kabila na vyeo mbalimbali wataandika.
NI JANGA.
NI JINAMIZI TUNALOLIKUMBATIA.
#DaktariMwandishi Image

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Kuduishe Kisowile Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @Kudu_ze_Kudu

Jan 4
I woke up today with so much in my mind, and that Sylvia Plath quote pierced right through me and I felt every inch of it.
This made me think about the life cycle of a butterfly and how much it resonates with our lives. Female butterflies lay many eggs because not all will (1/?)
survive. Apparently, we are the eggs that survived long enough to become caterpillars. Oh the fun stage, probably the school years where we ate and ate and ate and ate again to grow and run around exploring everything. Then comes the pupa stage, the very uncomfortable (2/?)
one especially because hidden inside the coccoon is us knowing what we are cooking but outside it looks like we are stuck in a box for weeks, months and even years. This is a stage of patience and resilience. Depending on the species, the pupa may be suspended under a (3/?)
Read 9 tweets
Apr 23, 2023
A lot of people spend most of their lives away from their families and homes that they barely build a community around them. They become visitors of their own homes. Things that used to hold people who live around together don’t do that much anymore. Weddings, funerals conducted Image
far from home. Where one builds their house to call home is not where they live. So, you have this group of people who have spent most of their lives away from home for years and suddenly they have to build a home and make it work with those within it and around it.
Kids spend years in boarding schools away from home and holidays are for visiting relatives again away from home. For years & suddenly they get to university and have the new found freedom in their hostels and home becomes somewhere they visit when they can; again AWAY FROM HOME
Read 15 tweets
Mar 3, 2023
Mjadala uliofanyika leo katika mkutano mkuu wa MEWATA kuhusu afya ya akili baada ya kujifungua, umenikumbusha mbali.
Siku moja napita round wodi ya watoto wachanga nawahimiza kina mama kunyonyesha watoto, mama mmoja aliniita “dokta ukimaliza njoo” #UZI #MEWATA2023
Nilipoenda akamchukua mwanae akanikabidhi mkononi akasema, “shogaangu hebu niangalizie mwanangu, maana mie sijielewi”
Nikamuuliza, “unajiskiaje” nikidhani labda ana shida ya mwili ili tuwaite watu wa wodi ya kina mama waje kumhudumia. Akasema, “yani nikimbeba hivi mtoto kumpa
maziwa, kuna sauti zinaniambia kabisa nimnyonge. Yani nawaza nimzibe pumzi afe. Sasa mi sitaki kumdhuru mwanangu, naomba unilelee tu”

Unajua hivi vitu ukivisoma kwenye vitabu vinaonekanaga kama utani fulani hivi hadi siku unakutana navyo. Nikawasiliana na in charge tukatoa
Read 13 tweets
Oct 3, 2022
When I saw a stream of blood down my leg, I knew right there and then; it’s happening! My worst nightmare was coming true and I couldn’t believe it because it was already days after delivery. I have NEVER been that terrified ALL MY LIFE.
This is my story: SURVIVING PPH #Thread 🧵
I tried to be calm, but I could hear my heart pounding in my ears. It felt like someone ripped out my heart and put it in speaker right next to my ears. I felt dizzy, so I sat down. I can’t tell if I was dizzy because of blood loss or the fear of becoming a statistic.
As we prepared to go back to the hospital, I tried so hard to appear calm; a big smile on my face but in my heart I was terrified. I knew it very well, PostPartum Hemorrhage is no joke. In a matter of seconds EVERYTHING COULD GO WRONG.
I asked for ONE thing: my rozary ring.
Read 24 tweets
Sep 26, 2022
Kuna safari hata ziwe fupi vipi, hazisahauliki. Hazisahauliki kwa mengi; watu uliosafiri nao, watu uliokutana nao, experience ya safari na mengine mengi.
Mimi safari hii pichani sitaisahau.
Nilipata wasaa wa kushare na @buguzi @NormanJonasMD @DrArabiFrank na @JuliethSebbaMD #UZI Image
Ilianza kama utani hivi, nikafahamishwa nimepata nafasi ya kufanya mafunzo Morogoro ambayo yaliandaliwa na @sikika1 na @tacaidsinfo
Na mimi mpenda safari na mpenda afya, naanzaje kukosa? Nikafungasha kibegi changu uelekeo mji kasoro bahari.
Moro bwana! Moro PAZURI NYIE! Basi tu. ImageImageImageImage
Katika mengi nilojifunza siku hizo mbili, kuna kitu kimoja kilichonivutia zaidi ya mandhari nzuri ya Morogoro, maana mara ya mwisho nilikuwa hapa ilikuwa ni trip ya Udzungwa na Mto Mawe.
Kitu hicho ni Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (ATF). Leo naomba niwashirikishe Image
Read 16 tweets
Jul 28, 2021
SEHEMU YA PILI #IjueChanjoNaDaktariMwandishi
Leo, saa 3 asubuhi, Rais SSH atazindua chanjo pale ikulu kwa kupata chanjo hiyo.
Wakati huo, tuendelee kujifunza kuhusu chanjo za COVID19 haswa aina ya Johnson&Johnson ambayo ndio imepokelewa. #UZI FUATILIA
#DaktariMwandishi
3. JE, NIKIPATA CHANJO YA COVID19 KUTANIFANYA NIWE NA SUMAKU (MAGENTIC)?

Hapana. Chanjo za COVID19 hazina uwezo wa kutengeneza "electromagnetic field" (uwezo wa wewe kuwa sumaku) na chanjo zote hazina metals.
Unaweza kuangalia nini kimo kwenye chanjo katika ukurasa wa CDC.
4. KWANINI BAADHI YA TAARIFA ZINASEMA TUMEPOKEA CHANJO YA JOHNSON&JOHNSON NA NYINGINE ZINASEMA "JANSSEN"?
Jina kamili la chanjo iliyopokelewa Tanzania kupitia mpango wa COVAX ni "Johnson&Johnson's Janssen(J&J/Janssen) COVID19 Vaccine" kwahiyo ni kitu kimoja wala si chanjo tofauti
Read 18 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(