Ushuhuda

Kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja nimekuwa nikiugua na kutibiwa ugonjwa wa #COVID19 unaotokana na virusi vya #Corona (SARS-CoV-2). Ni jinsi gani niliweza kuambukizwa ugonjwa huu kijijini kwetu Lufilyo, Busokelo, Mbeya, pamoja na kuzingatia tahadhari zote dhidi ya (1/7)
maradhi haya ni kitendawili. Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya uhai, zawadi ya Pasaka. Nawashukuru pia mke wangu Lucy Akiiki, watoto na wajukuu, familia za Kahigwa na Mwandosya, Madaktari na Wauguzi wangu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, na (2/7)
Hospitali ya Nairobi (Nairobi Hospital), @AMREFFlyingDocs, Uongozi wa @StanbicBankTZ na @StanbicKE ,Balozi Chirau na Rose Mwakwere wa Nairobi, Mheshimiwa Jaji Paul na Grace Mugamba wa Uganda, na ndugu na marafiki wote wanaoendelea kunitakia heri na afya njema. Asanteni sana.(3/7)
Huu ni ushuhuda wangu kwamba Corona/Covid 19 ipo #Tanzania .
Tumebahatika kuvuka kipindi cha mpito salama na kumpata Rais mpya Mheshimiwa @SuluhuSamia . Mwenyezi Mungu amjalie neema na baraka tele. Mheshimiwa @DrPhilipMpango , Makamu wa Rais, ambaye nampongeza kwa uteuzi, (4/7)
amepitia hayo yaliyonisibu.

Nawaomba, tena kwa unyenyekevu mkubwa, Mhe.@SuluhuSamia , Mhe.@DrPhilipMpango na Mhe,@DrHmwinyi , Rais wa #zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwamba, tuongozwe na sayansi, na tuungane na tushirikiane na wenzetu duniani kote katika (5/7)
kupambana na ugonjwa huu kama tunavyofanya katika milipuko ya magonjwa mengine. Kwani katika mlipuko wowote, hakuna anayeweza kuwa salama mpaka wote duniani tumekuwa salama.

Maombi yangu kwa Mwenyezi Mungu ni kwamba, ikiwezekana, Mtanzania mwingine awaye yote aepushwe na (6/7)
mateso na taabu za kukabiliana na maradhi haya.

Hakika siwezi kumtakia mtu mwingine yeyote, hata aliye adui yangu mkubwa namna gani, kama yupo, apate ugonjwa huu.

Tutakiane Pasaka njema. Mwenyezi Mungu ibariki Tanzania. Pro Deo et patrina. (7/7)

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Mark J. Mwandosya

Mark J. Mwandosya Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!