“Hii siri nitaitunza mpaka lini? Nibaki nayo au nijisalimishe?

Nilikuja Dar kutokea kijijini kupambania ugali. Mungu mwema mitikasi ilikubali. Kama unavyojua tena jiji la Dar wanawake warembo kila kona. Ni kama nilikua na ngekewa kila nilipotupa ndoano ilinasa. Nilijichanganya
nilitembea na kila aina ya mwanamke niliyemtamani.

Katika haya mahangaiko nilikutana na dada mmoja wa Songea. Huyu dada alikuja kunieleza amepata mjamzito. Ila akawa ameenda kwao Songea. Nilikua nikituma matumizi ila ilifika mahali mawasiliano yalikufa. Sikumpata tena. Ni miaka
mitano sasa sina mawasiliano yoyote sijui alipoteleaga wapi.

Maisha yaliendelea huku Dar nikakutana tena na mwanamke kutoka Kahama. Na yeye akapata ujauzito. Alirudi kwao Kahama pia ila mawasiliano yaliendelea kuwepo.

Ulifika muda nikaona hii njia sio sahihi. Nikabadilika
nikapata mwanamke nikamuoa. Mungu alinipendelea nimeoa mke mzuri sanaaa. Na ninamshukuru Mungu ndoa inaendelea vizuri na tumebarikiwa watoto wawili.
Sasa kinachonitatiza, sikuwahi kumuambia mke wangu kuhusu hawa watoto wawili. Hajui nilizaa nje ya ndoa. Nimwambie? Nikaushe? Nifanyeje?”
Sam, Dar Es Salaam. #WatuNiStory.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with WatuNiStory

WatuNiStory Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @watunistory

8 Aug
"Wakati nakutana na mpenzi wangu ambaye kwa sasa ni mchumba wangu na tutaoana sio mda mrefu, nilimwambia kabisa mimi sina mapenzi ya maonyesho.

Sinaga habari za mitoko wala kupostiana kuandikiana caption za makopakopa. Wewe ukitaka kutoka, toka na rafiki zako. Wala sitajalii. Image
Me nifanyie vitu vya kawaida tu kabsa nitafurahi sana.

Nina amini katika mahusiano ya siri na yenye staha. Kupostiana watu huleta chuki na maneno ambayo hayapo.
Wengine wana vijicho, wanataka mazuri unayopata wewe na yeye ayapate. Mpenzi wako anakupost kwa mapenzi tu ila unakuta mtu wivu unamshika anaanza kujipendekeza kwake.

Na wanaume sio wa kustahimili vishawishi na hapo ndoa ndio inaanza kuwa ngumu.
Read 4 tweets
29 May
Baada ya kumaliza shule nilimpata binti niliyeamini atakuwa wa maisha yangu alikuwa anaitwa Mwajuma, hapo ndio kwanza nilikuwa ninaanza kuingia katika ulimwengu wa mapenzi.
Sikuwa ninaelewa kabisa kuhusu maana ya neno penzi, watu waliotabiri mwisho wangu na Mwajuma niliamini kuwa ni wanafiki na walikuwa na malengo mabaya dhidi yetu.
Siku zilivyozidi kusonga penzi letu lilizidi kustawi kama bustani iliyokuwa inasimamiwa vizuri, tulipanga hadi kutambulishana kwa wazazi.
Read 7 tweets
27 May
"Tulifanya interview kutafuta mtu wa finance katika kampuni yetu. Tulipokea maombi mengi, watu tano ndio walifanikiwa kupigiwa simu na kuitwa kwa ajili ya usahili.

Wote walifika. Kila mtu alipangiwa muda wake. Image
Nakumbuka kuna kijana alikuja amependeza, yuko smart na alikuwa na vigezo vyote vya kupata ajira.

Alikuwa na madaha na majivuno ya hapa na pale wakati tunafanya nae interview. Alitaka mshahara wake usishuke si chini ya milioni moja na laki tano.
Alisema bila mshahara huo hawezi kutoka kwenye kampuni anayoifanyia kazi.

Hatukuwa na hiyo hela. Hivyo tulimchagua mtu mwingine ambaye tulielewana nae.
Read 5 tweets
29 Sep 20
1/10 “Naitwa William Adam Lukoo ,mzaliwa wa mkoa wa Morogoro. Mwaka 2003 familia yetu ilihamia jijini Tanga kwa ajili ya harakati za kimaisha. Haikua rahis kwa sababu ya ugeni lakini wazazi walipambana kuhakikisha napata elimu bora. Licha ya kutoka kwenye familia ya kimaskini...
2/10 ..nilihakikisha nafanya vizuri kwenye masomo kiasi cha kuwavutia walimu na kujizolea umaarufu shuleni. Nilifanikiwa kuhitimu mwaka 2010 shule ya msingi Majani Mapana wilayani Tanga mjini. Mwaka 2011 nilianza kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Usagara..
3/10 ..lakini kutokana na ugumu wa maisha, wazazi wangu wote hawakuwa na kazi. Ikawalazimu kufikia hatua ya kuuza vitu vya ndani ili kuweza kunilipia ada. Maisha yalikuwa magumu mno nyumbani kiasi cha kufikia hatua ya kushindwa kupata chakula na kodi.
Read 8 tweets
29 Sep 20
"Kipindi nipo nyumbani Mwanza, nilikuwa napigiwa simu na Kaka mmoja ambaye nilikuwa nafahamiana nae sana. Alikuwa ananiomba nije sana Kahama akiwa na ahadi ya kunipa kazi, kunipangishia nyumba na ahadi nyingine nyingi nzuri.
Siku niliyofika kahama, nilifikia guest house. Yule kaka ndiye aliyenipokea, hivyo nililala nae na mambo mengine ya chumbani yalifanyika.

Alivyoondoka asubuhi ndio ilikuwa mwisho kunipigia simu. Nikawa kila nikimtafuta naambulia matusi tu. Hakunipa chochote kama alivyoniahidi.
Kwa bahati nzuri nilivyotoka nyumbani Mwanza nilikuwa na akiba ya kama elfu 60.

Ilibidi niingie mtaani kutafuta kazi mimi mwenyewe, kwa maana nisingeweza kurudi tena Mwanza, Ningeambia nini watu maana nilikuwa nimeshaaga.
Read 4 tweets
28 Sep 20
Nimeona bora niongee na kuomba ushauri wenu kwani nimekaa kimya siku nyingi. Hali inazidi kuwa mbaya. Nazidi kudhoofika kisaikolojia na imefikia hatua Kuna mawazo mabaya yananijia kichwani.
Ni hivi, nilikua na biashara zangu kama tatu hivi nilizokua naziendesha zikiwa eneo moja. Kwa kuwa mimi ni mwalimu wa shule binafsi (private school) muda mwingi nashinda kazini, Hivyo msimamizi mkuu wa biashara zangu alikuwa mke wangu.
Mwezi wa 7 wakati wa likizo ya Corona mke wangu alisafiri kwenda nyumbani kusalimia.

Nikawa nasimamia mimi mwenyewe.

Shule zikafunguliwa huku mke wangu akiwa bado hajarudi.
Read 9 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(