"Nimetokea kwenye familia maskini sana na kibaya zaidi ilidharaulika sana, tena kwa pande zote mbili yaani upande wa baba na mama.

Nimekuwa huku kauli za kejeri zinasikika na kuishi masikioni mwangu.
Hilo kwangu ndio lilikuwa tatizo kubwa. Niliwachukia sana jamaa zangu mpaka nimekua mkubwa sikuwahi kuomba msaada wa aina yoyote kwao.

Hadi wazazi wangu niliwahi kuwakataza, niliwaambia shida zote na huduma wanibebeshe mimi.
Kuwaeleza shida zetu, ilikuwa kama kuwalilia njaa kwao.

Leo Mungu amesaidia tunakula kwa muda sahihi na tunalala pazuri. Kiukweli sitamani hata kuwapigia simu. Sasa hivi wamenibadilisha jina wanasema mimi ni jeuri.
Je kuna ubaya kutokuwahesabu wao kama ndugu zangu na kuwakataa mazima?

Ukumbuke hapo tunawasiliana kwenye maafa tu. Wanataka nifanyaje?"- Anonymous.
#WatuNiStory

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with WatuNiStory

WatuNiStory Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @watunistory

23 Sep
"Mwaka 2005 nilihitimu chuo cha ualimu Kabanga kilichopo mkoani Kigoma. Sikukaa muda mrefu mtaani, mwaka 2006 nilifanikiwa kupata ajira wilayani Moshi.

Nilifundisha pale miaka mitatu nikakutana na jamaa mmoja tukawa marafiki. Kumbe alikuwa mganga wa kienyeji.
Katika harakati zake, akanishawishi nikawa chawa wake. Siku zilivyoenda nikajikuta na mimi nimetamani kuwa mganga.
Sikuwa na majini ila kutokana na ukaribu wetu na nilivokua naona watu wengi wenye shida wanakuja kwake wanamuachia hela nyingi kiasi kwamba hela ambayo alikuwa anaipata ilikua inazidi mshahara wangu kama mwalimu.

Nikashawishika kuacha kazi ya ualimu na nikawa mganga.
Read 5 tweets
22 Sep
"Mwaka 2016 nilipoteza kazi niliyokuwa nimeajiriwa kwa makosa ambayo sikuhusika, lakini upepelezi ulipokuja kufanyika nilionekana ni kama na mimi nilihusika kwenye huo wizi ingawa ukweli sikuhusika.

Sikujua chochote na wala sikula hata sh 100.
Wanasema siku ya kusurubiwa kwako manabii wa uongo watakuja ili kukutolea ushahidi wa uongo lengo uangamie, ndio kilichonitokea mimi.
Baadae ya kupoteza kazi Mungu alinipa ujasiri sana maana sikuwahi kujutia kupoteza kazi bali nilianza kuwaza naishije kwa sasa na nafanya nini ili maisha yaende?.
Read 7 tweets
21 Sep
"Tulikuwa kwenye mahusiano miaka saba. Katika uhusiano wetu nilibahatika kupata mimba yake.

Aliikataa kabisa sio mimba yake. Niliumia sana. Ikabidi nilee mimba mwenyewe, hadi najifungua sikujua alipo na sikuwahi kumuona. Image
Mtoto alipokuwa na mwaka na nusu nilipost picha yake Facebook. Alimuona na akaanza kunifuatilia.

Badae alinitafuta akaja hadi nyumbani na kwa ndugu zangu, akaomba msamaha. Hatukuwa na hiyana nae, tulimsamehe.
Tukalea mtoto mpaka akanunua uwanja. Alianza kujenga na nyumba ilipoisha akanimbia nijiandae tufunge ndoa tumlee mtoto pamoja.

Gafla akaanza kubadilika na mwaka huu akaanza kuniambia kwao ndugu zake hawanitaki hivyo nitafute bwana na anioe na mtoto anamchukua.
Read 6 tweets
18 Aug
“Wakati naanza mwaka wa kwanza pale IFM nilimpa mimba mpenzi wangu. Nilikua naye toka mimi nikiwa Form 5. Bahati mbaya alifeli Form 4 akaishia hapo hapo.

Aliniambia mimba ni yangu na nilikubali nikaanza kuilea ile mimba. Japo tulisumbuana sana kwenye pesa za matumizi kwa sababu
sikua na pesa za kutosha kila kitu kwa wakati huo.

Chuki kwangu ikazidi balaa. Sikuiweka moyoni niliamini ni mimba inamsumbua.

Alienda kwao kujifungua mkoa mwingine. Na akajifungua mtoto wa kiume. Baada ya siku tatu akaniambia mtoto amefariki na baada ya hapo hakupokea simu
zangu tena wala za mama yangu. Mama yangu alilia sana.

Tayari tulishanunua vitu kibao vya kwake na vya mtoto. Kuna namna niliamini huu ni mchezo nimechezewa ila nilikaza maisha yakaendelea. Nikasonga na maisha mapya.

Baadae nikapata mwanamke mwingine na tulipendana sana japo
Read 7 tweets
16 Aug
“Nakumbuka nikiwa shule ya msingi maisha hayakua mazuri. Biashara ya mama yangu ya bagia ikawa ndio inaendesha maisha yetu. Mimi ndio mkubwa na ndiye mtoto wa kiume kwetu. Kwa kipindi hicho mdogo wangu wa kike alikua bado mdogo sana.

Ilinibidi nisaidiane na mama kuuza bagia. Image
Nikitoka shule nakuta zimeshatayarishwa nabeba sufuria natembeza mpaka vijiji vya jirani. Nahakikisha zimeisha ndipo narudi nyumbani.

Utaratibu ulikua ni huo huo tangu darasa la tatu hadi form three. Nakumbuka wenzangu walikua wananicheka. Nilikosa marafiki.
Kila mtu alikua ananitenga na kunidhihaki kwamba mtoto wa kiume nabebaje sufuria na kwenda kuuza bagia. Walisema ni kazi za kike.

Ilifika muda nikikuta wenzangubwanapiga stori nikifika tu wote wanatawanyika. Nabaki mnyonge.
Read 4 tweets
10 Aug
“Hii siri nitaitunza mpaka lini? Nibaki nayo au nijisalimishe?

Nilikuja Dar kutokea kijijini kupambania ugali. Mungu mwema mitikasi ilikubali. Kama unavyojua tena jiji la Dar wanawake warembo kila kona. Ni kama nilikua na ngekewa kila nilipotupa ndoano ilinasa. Nilijichanganya
nilitembea na kila aina ya mwanamke niliyemtamani.

Katika haya mahangaiko nilikutana na dada mmoja wa Songea. Huyu dada alikuja kunieleza amepata mjamzito. Ila akawa ameenda kwao Songea. Nilikua nikituma matumizi ila ilifika mahali mawasiliano yalikufa. Sikumpata tena. Ni miaka
mitano sasa sina mawasiliano yoyote sijui alipoteleaga wapi.

Maisha yaliendelea huku Dar nikakutana tena na mwanamke kutoka Kahama. Na yeye akapata ujauzito. Alirudi kwao Kahama pia ila mawasiliano yaliendelea kuwepo.

Ulifika muda nikaona hii njia sio sahihi. Nikabadilika
Read 5 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(