UNATESEKA KUPATA MAUZO KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII?

Inawezekana una Bidhaa nzuri, una Huduma bora kabisa, una post kila siku kwenye account zako, lakini huoni ukipata faida yoyote kupitia mitandao ya kijamii unayotumia

Nina Habari njema sana kwako siku ya leo

Are you ready?🤔
Kabla haujafanya uamuzi wa kufuta post zako, au kufunga kabisa kurasa za biashara yako...

Nataka kukuonyesha Hatua 5 muhimu sana zinazoweza kukusaidia ili kupata matokeo mazuri.

Twende wote taratibu sasa...
1. Anza kwa kuweka Malengo Maalumu.

Inawezekana unafeli sehemu kubwa kwa sababu haujui ni nini unataka kutimiza kila siku, week au mwezi.

Anza kupanga Malengo maalumu kila siku. Haya yatakuwa kama...
Ngazi ya kukusukuma kwenda mbele.

Hakikisha malengo yako ni SMART.

Yaani

📍Specific - Maalumu
📍Measurable - Unaweza kutrack maendeleo yake
📍Attainable - Una uhakika unaweza kuyafikia.
📍Relevant - Yanaendana na uhalisia wako
📍Time - Bound - Unaweka Deadline yake.
Mfano: Usiseme "Nataka kupata followers wengi Twitter" kama @mafolebaraka
Au @NyandaAmosi

Badala yake, sema "Nataka kuongeza followers wangu twitter, kutoka 30 Mpaka 50 Ndani ya Mwezi huu."

Umeona tofauti hapo?

Hebu jaribu na wewe sasa katika angle nyingine...
2. Wasome wateja wako

Mtambue mteja wako ni nani kwa kufanya Research ndogo, sio kutumia mawazo yako.

Usiwe mvivu hapa!

Usipotambua nani anahitaji huduma au bidhaa yako, utaishia kujaribu kuuza kwa kila mtu.

Mwisho wa siku, hutauza kabisa!
Jihangaishe, ufahamu mteja wako ni mtu wa aina gani.

Anapenda maudhui ya aina gani, mahitaji na matamanio yake ni yapi?

Njia Rahisi ya kuanzia ni kuingia katika Magroup ya Facebook, Whatsapp, page za watu wanaofanya biashara au bidhaa kama yako nk.

Huko unaweza kupata...
Data za kuanzia ili kumsoma mteja wako kwa undani.

Wakati mwingine unaweza kutengeneza Survey ndogo na kuzituma kwa watu (Hasa watumiani wa huduma yako), ili kutambua mahitaji yao halisi na nini wanatamani kupata.
3. Usiwafumbie macho washindani wako.

Hakikisha unajua nani ni mshindani wako kibiashara.

Fuatilia anavyofanya. Angalia ubora na udhaifu wake.

Kwa namna yoyote tafuta Fursa kupitia yeye. Fanya zaidi ya ubora wake, na tumia udhaifu wake (Kibiashara tu) kama faida kwako.
4. Unahitaji maboresho katika Kurasa zako za kibiashara.

Katika Lugha ya kwetu, tunaita "Social Media Audit"

Chunguza effort zako, kisha jiulize

▶Ni wapi unafanya vizuri na wapi unahitaji kuongeza jubudi zaidi?
▶Ni watu gani wanatembelea sana ukurasa wako?
▶Mtandao upi unatumiwa sana na Wateja wako?
▶Unatumiaje Fursa ya kuwepo mtandaoni, ukilinganisha na washindani wako?

Hakikisha kila week unaangalia maendeleo yako, fursa ulizotumia na zile zilizokupita.

Mtandaoni hakuhitaji mtu MVIVU! Lazima ukubali kuchakarika kweri kweri😎
5. Hakikisha account yako inavutia na Kushawishi.

Kuandika jina tu na username yako, bado haitoshi.

Ukurasa wako unapaswa kuwaambia watu...

▶Wewe ni nani?
▶Unatoa huduma gani?
▶Wanawezaje kupata huduma yako?

Angalia mifano👇👇
Bado una mawazo ya kukata tamaa na kufunga ukurasa wako wa biashara?

Unaweza kuanza tena, and this time...It's going to be juust fine!

Kanuni yetu ya UPENDO bado ni ile ile...

RETWEET ili na wengine wapate Maarifa haya.

Your Friend
Ansey.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Anselmo

Anselmo Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @CoachAnsey

13 Oct
UNASHINDWA KUANDIKA CAPTION NZURI KATIKA POST ZAKO?

Kama una Brand au unaendesha biashara yako kupitia Mitandao ya kijamii...

... basi utakuwa unafahamu ni ngumu kiasi gani kuja na mawazo ya kuandika kila siku katika kila post unayoweka kwenye ukurasa wako.
Kutokana na jinsi unavyotaka watu wakutazame kupitia Brand/biashara yako...

...Unaweza kuchagua Tone ya sauti unayotaka watu wakutambue nayo.

Kupitia Caption zako, unaweza kuonekana Mcheshi, Mpole, au serious kiasi.

Sasa Social Media Entrepreneurs wengi ni WAVIVU mno...
katika uandishi wa Caption.

Unakuta mtu amepost Picha ya Viatu au Handbag, then kaandika tu

"Kiatu kama hiki ni Tsh 65,000/= Piga namba hii 0712 312XXX"

Come on! Hapo unaweza kusema umemshawishi mteja wako kununua?

Usichukulie poa, unazungumza na Mteja kupitia Caption yako!
Read 13 tweets
18 Aug
MBINU 5 ZITAKAZOKUSAIDIA KUKUZA BIASHARA YAKO KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII.

Inawezekana hapo ulipo umekwama, huoni maendeleo yoyote ya biashara yako, wakati huo huo unaona wapinzani wako wanaendelea kupiga hatua.

Upo katika hali hiyo?
Usiwe na wasiwasi, kila mfanyabiashara au mjasiriamali kama wewe, amewahi kupitia hali kama hiyo.

Kama umeshindwa leo, haina maana utaendelea kushindwa kila siku.

Au unasemaje Brother @mafolebaraka ?
Siku zote SILAHA kubwa katika biashara na MAARIFA!

Maarifa ndio silaha yako kubwa, ndio maana leo unapaswa kunisikiliza kwa makini kwa sababu ninaenda kukupa MAARIFA (Mbinu) takazokusaidia kufufua tena matumaini yako.
Read 21 tweets
16 Aug
JINSI YA KUTENGENEZA MAUDHUI (CONTENTS) YENYE KUONGEZA USHAWISHI KWA MTEJA.

Mara nyingi katika kutengeneza Maudhui, tunatumia mawazo, Ideas na ushawishi wetu binafsi...

..lakini, kuzingatia muonekano na aina ya Maudhui yanayoandikwa ni jambo muhimu mno.
Ni rahisi sana kutengeneza mawazo na topic mbalimbali kwa ajili ya wateja wako...

..Lakini, kama muuzaji, ni lazima uwe na uelewa mkubwa wa namna ya kuwasilisha mawazo hayo kwa mteja wako.
Ndio maana ni muhimu sana kufahamu namna mbalimbali ya kuandika maudhui yanayokidhi mahitaji ya mteja wako.

Kupitia mchanganyiko huu wa maudhui, itakusaidia kuongeza wafuasi wako zaidi, kufikia wateja wapya, na kutengeneza mazingira rafiki ya kuuza Bidhaa au huduma yako.
Read 13 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(