Kuduishe Kisowile Profile picture
Sep 26, 2022 16 tweets 10 min read Read on X
Kuna safari hata ziwe fupi vipi, hazisahauliki. Hazisahauliki kwa mengi; watu uliosafiri nao, watu uliokutana nao, experience ya safari na mengine mengi.
Mimi safari hii pichani sitaisahau.
Nilipata wasaa wa kushare na @buguzi @NormanJonasMD @DrArabiFrank na @JuliethSebbaMD #UZI Image
Ilianza kama utani hivi, nikafahamishwa nimepata nafasi ya kufanya mafunzo Morogoro ambayo yaliandaliwa na @sikika1 na @tacaidsinfo
Na mimi mpenda safari na mpenda afya, naanzaje kukosa? Nikafungasha kibegi changu uelekeo mji kasoro bahari.
Moro bwana! Moro PAZURI NYIE! Basi tu. ImageImageImageImage
Katika mengi nilojifunza siku hizo mbili, kuna kitu kimoja kilichonivutia zaidi ya mandhari nzuri ya Morogoro, maana mara ya mwisho nilikuwa hapa ilikuwa ni trip ya Udzungwa na Mto Mawe.
Kitu hicho ni Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI Tanzania (ATF). Leo naomba niwashirikishe Image
Ulianzishwa Machi, 2015.
Lengo ni kuongeza mchango wa serikali na taasisi/sekta binafsi katika kutatua changamoto za raslimali zilizopo kwenye utekelezaji wa afua za VVU na UKIMWI hapa nchini.
Ifahamike kwamba, programu ya kitaifa ya VVU imekuwa ikitegemea sana fedha za wafadhili Image
Wafadhili wakuu ni pamoja na Serikali ya Marekani @PEPFAR , Mfuko wa Dunia @GlobalFund , ambao kwa pamoja wanachangia 93% ya fedha zote zinazopatikana kwa mapambano wa VVU nchini Tanzania.
Kutokana na mabadiliko ya kiuchumi na sera ya kujitegemea, kuna haja ya kuwa na vyanzo vya Image
ndani vya ziada ili kudhamini afua mbalimbali za VVU na UKIMWI nchini.
ATF imeanzishwa kwa lengo hilo. Kuziba pengo la ufadhili kwenye shughuli za utekelezaji wa afua za VVU na UKIMWI.
Fedha za mfuko hupatikana kutoka Serikali kuu pamoja na Harambee, michango ya simu n.k
Lengo
likiwa ni kuhakikisha mfuko wa ATF unaweza kuziba myanya katika utekelezaji wa afua za UKIMWI.
Fedha zilizokusanywa 2016-2020 zimetumika katika;
1. Bilioni 1.110 zilipelekwa @wizara_afyatz kwa ajili ya kununua dawa za magonjwa nyamelezi kwa Watu wanaoishi na VVU (WAVIU).
2. Shilingi Mil 250 zimetumika kujenga kituo cha kisasa cha kutolea huduma za VVU na UKIMWI kwa wachimbaji wa madini wa eneo la Mirerani, wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara, pamoja na wananchi wanaoishi maeneo ya jirani,
3. Shilingi Mil.182 zimetumika katika utekelezaji wa programu za kinga dhidi ya maambukizi ya VVU kwa vijana walio katika taasisi za elimu ya juu zilizopo jijini Dodoma

Hayo ni baadhi ya mafanikio ya mfuko huu pamoja na kuandika maandiko kupitia wataalamu elekezi na wataalamu wa
Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania. Yatako wasaidia Madereva wanaoendesha masafa marefu, Waendesha bodaboda/daladal na wavuvi maeneo mbalimbali nchini jinsi ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI.

Licha ya mafanikio hayo, mfuko bado una changamoto mbalimbali pamoja na: Image
1. Kutokuwepo kwa chanzo endelevu cha fedha kwa ajili ya kutunisha mfuko wa ATF
2. Mwitikio mdogo wa wadau katika kuchangia fedha kwenye mfuko wa ATF
3. Gharama kubwa za maandalizi ya shughuli za harambee

Vyanzo vinavyopendekezwa ni tozo mbalimbali kutumika kutunisha mfuko huu. Image
Katika kutekeleza uchangiaji wa mfuko huu, kutakuwa na ATF Marathon @atfmarathon trh 27 Nov, 2022 itakayofanyika viwanja vya Ilulu, LINDI.
Usajili ni TZS 35,000 TU utapata punguzo la TZS 5,000 ukijisajili mapema
Tembelea atfmarathon.co.tz au piga *150*50*1# ingiza 60491370 Image
Sote tuna jukumu la kuchangia maendeleo ya afua za VVU na UKIMWI, na kwa wale wapenzi wa marathon kina @TOTRunners, wapenda mazoezi wote mnakaribishwa kuhudhuria ATF Marathon
Mimi kwa kuwa sitaweza kuhudhuria, nitamlipia follower wangu MMOJA atakayekwenda. Huo ndio mchango wangu Image
Safari yetu iliisha salama hapo tulisimama kwenye restaurant fulani hivi niliiona ikanivutia somewhere Pwani, naomba boss @buguzi uendelee kuwa dereva wetu katika kuchangia maendeleo ya Afya. Image
Na safari nyingi zaidi ziendelee, zituzungushe viunga vyote vya nchi hii katika kutimiza maendeleo na kuchangia huduma za afya nchini.
Naomba @buguzi @DrArabiFrank @JuliethSebbaMD na @NormanJonasMD mseme AMINA kubwa sana.
Basi #NovembaTukutaneLindi @atfmarathon #DaktariMwandishi Image
@threadreaderapp please unroll

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Kuduishe Kisowile Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @Kudu_ze_Kudu

Jan 4
I woke up today with so much in my mind, and that Sylvia Plath quote pierced right through me and I felt every inch of it.
This made me think about the life cycle of a butterfly and how much it resonates with our lives. Female butterflies lay many eggs because not all will (1/?)
survive. Apparently, we are the eggs that survived long enough to become caterpillars. Oh the fun stage, probably the school years where we ate and ate and ate and ate again to grow and run around exploring everything. Then comes the pupa stage, the very uncomfortable (2/?)
one especially because hidden inside the coccoon is us knowing what we are cooking but outside it looks like we are stuck in a box for weeks, months and even years. This is a stage of patience and resilience. Depending on the species, the pupa may be suspended under a (3/?)
Read 9 tweets
Apr 23, 2023
A lot of people spend most of their lives away from their families and homes that they barely build a community around them. They become visitors of their own homes. Things that used to hold people who live around together don’t do that much anymore. Weddings, funerals conducted Image
far from home. Where one builds their house to call home is not where they live. So, you have this group of people who have spent most of their lives away from home for years and suddenly they have to build a home and make it work with those within it and around it.
Kids spend years in boarding schools away from home and holidays are for visiting relatives again away from home. For years & suddenly they get to university and have the new found freedom in their hostels and home becomes somewhere they visit when they can; again AWAY FROM HOME
Read 15 tweets
Mar 3, 2023
Mjadala uliofanyika leo katika mkutano mkuu wa MEWATA kuhusu afya ya akili baada ya kujifungua, umenikumbusha mbali.
Siku moja napita round wodi ya watoto wachanga nawahimiza kina mama kunyonyesha watoto, mama mmoja aliniita “dokta ukimaliza njoo” #UZI #MEWATA2023
Nilipoenda akamchukua mwanae akanikabidhi mkononi akasema, “shogaangu hebu niangalizie mwanangu, maana mie sijielewi”
Nikamuuliza, “unajiskiaje” nikidhani labda ana shida ya mwili ili tuwaite watu wa wodi ya kina mama waje kumhudumia. Akasema, “yani nikimbeba hivi mtoto kumpa
maziwa, kuna sauti zinaniambia kabisa nimnyonge. Yani nawaza nimzibe pumzi afe. Sasa mi sitaki kumdhuru mwanangu, naomba unilelee tu”

Unajua hivi vitu ukivisoma kwenye vitabu vinaonekanaga kama utani fulani hivi hadi siku unakutana navyo. Nikawasiliana na in charge tukatoa
Read 13 tweets
Oct 3, 2022
When I saw a stream of blood down my leg, I knew right there and then; it’s happening! My worst nightmare was coming true and I couldn’t believe it because it was already days after delivery. I have NEVER been that terrified ALL MY LIFE.
This is my story: SURVIVING PPH #Thread 🧵
I tried to be calm, but I could hear my heart pounding in my ears. It felt like someone ripped out my heart and put it in speaker right next to my ears. I felt dizzy, so I sat down. I can’t tell if I was dizzy because of blood loss or the fear of becoming a statistic.
As we prepared to go back to the hospital, I tried so hard to appear calm; a big smile on my face but in my heart I was terrified. I knew it very well, PostPartum Hemorrhage is no joke. In a matter of seconds EVERYTHING COULD GO WRONG.
I asked for ONE thing: my rozary ring.
Read 24 tweets
Jul 28, 2021
SEHEMU YA PILI #IjueChanjoNaDaktariMwandishi
Leo, saa 3 asubuhi, Rais SSH atazindua chanjo pale ikulu kwa kupata chanjo hiyo.
Wakati huo, tuendelee kujifunza kuhusu chanjo za COVID19 haswa aina ya Johnson&Johnson ambayo ndio imepokelewa. #UZI FUATILIA
#DaktariMwandishi
3. JE, NIKIPATA CHANJO YA COVID19 KUTANIFANYA NIWE NA SUMAKU (MAGENTIC)?

Hapana. Chanjo za COVID19 hazina uwezo wa kutengeneza "electromagnetic field" (uwezo wa wewe kuwa sumaku) na chanjo zote hazina metals.
Unaweza kuangalia nini kimo kwenye chanjo katika ukurasa wa CDC.
4. KWANINI BAADHI YA TAARIFA ZINASEMA TUMEPOKEA CHANJO YA JOHNSON&JOHNSON NA NYINGINE ZINASEMA "JANSSEN"?
Jina kamili la chanjo iliyopokelewa Tanzania kupitia mpango wa COVAX ni "Johnson&Johnson's Janssen(J&J/Janssen) COVID19 Vaccine" kwahiyo ni kitu kimoja wala si chanjo tofauti
Read 18 tweets
Jul 28, 2021
#IjueChanjoNaDaktariMwandishi
Bado naikumbuka siku ile ilipotangazwa chanjo ya kwanza ya COVID19, nilikuwa twitter, sikuwahi kufurahia matunda ya sayansi kama siku hiyo.
Wakati huo, tayari janga la COVID19 na upotoshwaji ulikuwa juu ...#UZI (SEHEMU YA KWANZA)
#DaktariMwandishi
kitu ambacho sikutegemea, ni upotoshwaji mkubwa zaidi uliokuja na chanjo.
Lakini, siwalaumu wenye maswali dhidi ya chanjo. Yapo maswali muhimu mno ambayo, hatuwezi kuyasukumia uvunguni kwa kigezo cha upotoshaji.
Ni lazima yajibiwe hata kidogo.
Nitajitahidi kutoa majibu machache.
Kabla sijajibu, naomba niseme kuwa ni sawa kuwa na maswali juu ya kile unachokipokea, lakini si sawa kusambaza taarifa za uongo na zisizo na ushahidi wowote.
Kufanya hivyo ni ugaidi. Ni uhalifu dhidi ya binadamu.
Kwanza niseme, mimi NAAMINI KATIKA CHANJO.
NAAMINI KATIKA SAYANSI.
Read 24 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us!

:(