My Authors
Read all threads
FAHAMU JUU YA UFUGAJI WA SAMAKI YAAN AQUACULTURE/ FISH FARMING

-THREAD AQUACULTURE-
Leo tushare ideas juu ya ufugaji wa samaki moja ya biashara inayowaingizia pesa sanaaa Bara la Asia huku 🇹🇿 ikisahaulika japo tukijitahidi
#NipeDili
#KilimoFursa

🔁Retweet ifike mbali
UFUGAJI WA SAMAKI

Tasnia ya ufugaji wa samaki inajumuisha ukuzaji wa viumbe vya kwenye maji (bahari na maji baridi) katika mazingira tofauti na yale ya asili. Lengo kuu ni kukuza kwa muda mfupi ili kujipatia lishe, kipato na kutunza mazingira ya bahari, mito, maziwa nk.
Ufugaji unagusa viumbe vya kwenye maji kuanzia mimea kama vile mwani, samaki wasio na mapezi (kaa-crabs, kambamiti-prawns, chaza-oyster, majongoo bahari nk) na samaki wenye mapezi (perege/sato, kambale, kibua, trout, chewa nk).
Aina ya ufugaji

Zifuatazo ni aina/level za ufugaji ambazo mkulima anaweza kufanya kulingana na malengo na uwezo wake:
1. Huria (Extensive farming)

Idadi ya samaki wanaopandikizwa: samaki 2-3 kwa mita ya mraba
Samaki hutegemea chakula cha asili (mimea ya majini-phytoplankton, wadudu/viumbe vidogo vya majini-zooplankton)
Hauitaji ubadilishaji wa maji
Hauihitaji huduma ya ziada ya hewa
2. Kati ya huria na nusu shadidi (Modified extensive);
Idadi ya samaki, 4-7 kwa mita ya mraba
Chakula cha asil na chakula cha ziada huitajika
Maji hubadilishwa sentimenta 10-20 kila baada ya 3-4weeks kulingana na hali ya samaki na maji yako.Huduma ya hewa ya ziada sio ya ulazima
3. Nusu shadidi (Semi-intensive)

Idadi ya samaki kwa mita ya mraba ni 10-25
Chakula cha asili na cha ziada
Huduma ya hewa ya ziada lazima
Maji hubadilishwa kila siku au kila baada ya siku kadhaa (15-25 cm)
4. Shadidi (Intensive)

Idadi ya samaki ni zaidi ya 25 kwa mita ya mraba
100% chakula cha kutengenezwa
Maji ni kuingia na kutoka
Hewa ya ziada masaa yote
Eneo linalotumika ni dogo ukilinganisha na mifumo mingine
Miundombinu ya ufugaji

Samaki wanaweza kufugwa katika miundombinu mbalimbali kama ifuatayo:

Bwawa
Kina 0.8-1.5m
Ukubwa 100 mita za mraba- 1ha
Matanki
Umbo-mstatili au mviringo nk
Kina 1-1.5m
Kipenyo kwa lile la mduara 3-10m
Ukubwa kwa la mstatili inategemea na uwezo lakini lisiwe kubwa ili kuhimili nguvu ya maji
Materials:Plastic,cement,chuma
NB: Simtank linafaa( Faida inapatikana kama utalitumia kwa intensive system)
Vizimba (Fish cages)
Huwekwa katika maji ya asili kama vile ziwani, baharini au katika bwawa. Vipo vinavyoundwa kwa local materials kama mianzi na vipo vya aluminium.
Eneo linalofaa kwa ufugaji
Baadhi ya maeneo yanayofaa ni yale mashamba ya mpunga, na maeneo yaliyo karibu na vyanzo vya maji. Zifuatazo ni sifa za maeneo yanayofaa:
1. Udongo: Mfinyanzi husaidia kupunguza gharama za ujenzi wa bwawa na maji kwakuwa linaweza kutuamisha maji na kuruhusu maji yasipotee. Likiwa la kichanga bwawa ni lazima lijengewe au kuwekwa nylon sheet ili kuzuia upotevu wa maji.
Unaweza ukahamisha udongo wa mfinyanzi kutoka sehemu moja hadi nyingine ili kuzuia upotevu wa maji (muone mtaalamu kwa ushauri zaidi juu ya mbinu ya kuhamisha udongo).
2. Chanzo cha maji ya uhakika
Eneo liwe na maji ya uhakika. Vyanzo vya maji ni kama vile mito, bahai, maziwa, chem chem., kisima, maji ya dawasco na mvua. Maji yasiwe na kemikali hatarishi kwa viumbe.
3. Miundombinu ya barabara: Inasaidia kwa ajili ya usafirishaji wa bidhaa na samaki wakati wa kuvuna.
4. Eneo lisiwe na historia ya mafuriko ili kuzuia athari za mafuriko kwa miundombinu yako. Utatumia gharama nyingi katika kuimarisha miundombinu yako.Jamii/aina ya samaki
5. Eneo lenye mwinuko wa wastani husaidia katika ujenzi wa bwawa.
6. Miundombinu ya umeme ni sifa ya ziada hususan kwa mkulima wa kati na wajuu kwa ajili ya kutumika katika kuendesha visambaza hewa.
7. Ulinzi muhimu
Note: Aina ya eneo lako ndilo linaweza kukufanya uchague muundombinu gani wa kufugia utumie

Aina ya samaki unaoweza kufuga Tanzania kwa sasa
Maji baridi

Sato/perege, Kambale, Kambamiti wa maji baridi na Trout (maeneo ya baridi kama vile Iringa, Kilimanjaro Arusha na Mbeya)
Maji bahari

Kambamiti wa maji bahari, mwatiko, chewa, kaa, chaza wa lulu

Upatikanaji wa Vifaranga vya samaki husika

Vyanzo vya vifaranga ni kutoka katika mito, bahari, maziwa na wale wa kuzalishwa katika vituo vya kuzalishia vifaranga.
Sato na Kambale

Vituo vya serikali Utapata sato wa kike na kiume mixed sex). Kingolwira Morogoro, LuhiraSongea, Mbegani-Bagamoyo . Kifaranga huuzwa Tsh. 50-100 kwa kifaranga.
Vituo binafsi kama vile Faith aquaculture-Kibamba (DSM) (utapata monosex sato), PeramihoSongea (mixed sex). Monosex huuzwa Tsh. 200 kwa kifaranga, na mixed ni 100 kwa kifaranga.

Trout

Mayai huagizwa toka Marekani, Israel
Kamba miti wa baharini Alphakrust Mafia.
Chakula cha samaki

Chakula cha asili

Hurutubishwa kwa mbolea ya wanyama kama vile kuku, ngombe, mbuzi nk. Kwa kiwango cha 1000kg/ha. Mbolea ya kuku ni kali hivyo unaweza punguza ikawa 250-500kg/ha.
Chakula cha kutengeneza

Samaki huitaji protein ili akuwe na kila samaki ana mahitaji yake hivyo ni species specific.Formula zipo kwa wale wanaotaka kutengeneza.Tanzania hakuna kiwanda kinachotengeneza. Ingredients zake ni kama vile dagaa, pumba,soya,unga wa ngano,unga wa muhongo
Uvunaji

Kwa kawaida ni miezi 4-6 amabapo unapata 250-400g kulingana na ulishaji wako. Kwa prawns ni miezi 3-6 wanafikia 30-50g ambayo ni ukubwa wa soko.
Tathmini ya uchumi

Perege/sato Mfano:
Ukubwa wa bwawa ni 20m by 30m= 600 mita za mraba
Idadi ya samaki (7 kwa mita ya mraba) kwa monosex tu= 600 x 7=4200 fish
Uzito hadi kuvuna (4-6months)- 250g= 4200 x 250g= 1050kg (Nimesha convert gram to kg) Bei kwa kilo ni 6000-8000 6m-8m.
Gharama unazoweza kutumia
Ujenzi wa bwawa
Kuchimba kwa vibarua ni 500,000-600,000
Kuchimba kwa machine ni 1,000,000-1,500,000 kulinganana mahali.Kama udongo ni kichanga itabidi ujengee (kujengea ni gharama na inaweza ikafika 3.5-4m kwa gharama zote kuanzia kuchimba hadi kujengea)
Chakula cha kutengeneza tani 1 inaweza kugharimu laki 7-9. Hapa ili uweze kuzalisha tani 1 ya samaki aina ya perege utahitaji tani 1-1.5 ya chakula.
Gharama ya vibarua 150,000-250,000 kwa mwezi.
Utakuwa na gharama ya chokaa kwa ajili ya kuua vidudu (laki 100,000-200,000),
mbolea kuzalisha chakula cha asili (gharama ni 50,000).

Jinsi ya kuhudumia bwawa, kuandaa chakula nitaandaa tips zingine.
Machache tumeshare pamoja imeletwa kwenu na Mbwmambo Alex Mwanafunzi wa udsm Kilimo biashara kwa maswali na ushauri usisite kuwauliza hawa pia @andy_mwakalobo @MwasomolaPaulo @KevnashEdson @Barrackah2 @Lwimiko6 @Daddieshoko @DeograciusTweet
@Roma_Mkatoliki @HusseinBashe @mkandamizaji nisaidieni kushare hii fursa
@p_tanzania retweet yako kwahiyo post 👆👆ifike mbalii
@JideJaydee naomba uretweet hii fursa iwafikie wengi
@DeucSnox @JohnieZeBest retweet zenu
@DeucSnox bro umesha pitia hapaaa
@chibelube umepitia huu uzi...kama bado rt yako bro
Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh.

Keep Current with Mbwambo

Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

Twitter may remove this content at anytime, convert it as a PDF, save and print for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video

1) Follow Thread Reader App on Twitter so you can easily mention us!

2) Go to a Twitter thread (series of Tweets by the same owner) and mention us with a keyword "unroll" @threadreaderapp unroll

You can practice here first or read more on our help page!

Follow Us on Twitter!

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!