BARUA KWA BINTI WA πŸ‡ΉπŸ‡Ώ #UZI
#PARTONE
Binti,
Salaam zikufikie pale ulipo kama upepo uvumavyo kutoka baharini kwenda nchi kavu. Natumaini hujambo. Mimi sijambo.
Kila siku nakuwaza sana. Nafikiria nifanyeje kugusa maisha yako.
Kabla ya yote nijitambulishe, mimi ni #DaktariMwandishi Image
Dhumuni la barua hii, ni kusema na wewe Binti. Natamani barua hii ningeiremba kwa maua, lakini naamini maneno nitakayoandika ni mbegu tosha.
Jana ilikuwa siku ya wapendanao, haijalishi ulipokea salamu au la, naomba pokea zangu; NAKUPENDA.
Enzi hizo nikiwa sekondari, ilikuwa siku
nzuri sana. Wale ma-admire/dada wa shule/vindende tuliandikiana kadi na kupeana zawadi. Ilipoangukia wikiendi kama hii, mambo yalikuwa moto zaidi, tulipokea kadi na barua kutoka kwa marafiki mbalimbali. Tukisubiria jumatatu tuibie kuingia facebook kuchungulia salam tulizotumiwa.
Natabasamu nikiandika hilo. Lakini kusudi langu sio kukupa stori yangu, ni kusema na wewe.
Natazama nyuma, nakumbuka vitu vingi nilivyosema, nilivyofanya, nilivyoandika na maamuzi mengi niliyofanya ambayo leo najiuliza "kwanini?"
Ni sehemu ya maisha.
Katika ukuaji wako, lazima
upitie haya. Katika safari yako, kuna vitu utavibakiza moyoni hutakaa useme kwasababu ni aibu. Kuna makosa utafanya. Si unajua? Unaanza kujiona umekua, unaweza fanya maamuzi yako, unatamani vitu kibao ukiona wenzio wanafanyiwa. Usiwe na tamaa. Niamini mimi, UTAVIKUTA. TENA VINGI.
JIPENDE. Upende mwili wako. Ipende afya yako ya akili. Katika ukuaji wako, kuna wakati unaweza kuuchukia mwili wako. Ngozi, umbo, sura, labda unatokwa na chunusi nyingi. Ni sehemu ya ukuaji, lakini usiruhusu ivunje kujiamini kwako. Nimepita huko. Nilipoumwa pumu ya ngozi,
niliharibika sana na kunenepa mno. Nilijichukia. Niliuchukia mwili wangu. Nilijiona sina mvuto. Imechukua miaka mingi kujifunza kujipenda tena. Nimetumia dawa nyingi kutoa makovu. Niamini, JIKUBALI. Wengi bado mna miili ya kitoto, usitake kuwa mtu mzima mapema. MUDA UTAFIKA.
Katika ukuaji wako, kitu kimoja hautaambiwa ni kuwa utavutiwa na wanaume. Tena wakati mwingine, watu wazima.
Si unajua, ukiwa Olevel wajanja wanatoka na wakaka wa Alevel, ukiwa Alevel, wajanja wanatoka na wakaka wa chuo. Ni ngumu kubadili hizi fikra ambazo zimeshajazwa kichwani
kwako, lakini niamini SIO UJANJA.
Ukiwa huko bweni, utamuona yule mwalimu kijana eeh, atakuvutia, utamchekeachekea labda, labda na yeye ataonyesha kukutaka pia. Vivyo hivyo utaenda jeshini, utamuona Afande, lile bakabaka, misuli utavutiwa. Nii kawaida, LAKINI kujenga mahusiano
SI SAWA. Wale ni watu wazima binti, si kila mtu mzima ana akili au aibu ya kukulinda wewe. Sikulaumu kama jamii inavyokulaumu kuwa "umejipeleka/umejitongozesha" lakini nakwambia JILINDE. CONTROL HISIA ZAKO.
Niamini mimi, ZINAPITA.
Kuna siku utatazama nyuma na kujicheka SANA kwa
kutamani hao.
Binti, bado jamii inatua gunia la misumari ya lawama kwa mwanamke. Tuna safari ndefu kuwajibisha wanaoharibu mabinti zetu. Wakati tunapigania hilo, naomba jilinde. Tumbo la mimba utabeba wewe mama. Magonjwa ya zinaa, majuto, aibu na masimango utapewa wewe.
KUWA MCHOYO. Kuwa mchoyo na kesho yako. Kuwa mchoyo na ndoto zako. Usiruhusu tamaa ya muda mfupi ibadilishe maisha yako.
Katika umri wako, bado hujaujua mwili wako, hujajua nini unapendwa kufanyiwa. Niamini mimi, muda UPO, utajua tu wakati ukiwadia. Utayafanya sana hadi upumzike.
Najua hili somo umeambiwa kwa maneno tofauti na wengi. Basi nasema hivi, ijue afya ya uzazi.
Ijue na uijue vema. Afya yako ya uzazi ni jukumu lako wewe peke yako.
Unapotimiza miaka 18, utakuwa na mipango mingi si kwasababu kisheria ndo umekuwa "mtu mzima" bwana? Naelewa. Amini.
Lakini kiukweli, hujawa mtu mzima. Nikukumbushe tu, hadi miaka michache iliyopita sheria ilikuruhusu uolewe ukiwa na miaka 14 kwa ruhusa ya mzazi. Sheria haimaanishi ni ukweli wa kiakili au kibaiolojia. Nini kinakufanya ufikiri kuwa ndani ya sekunde, siku, miezi ya kufikisha 18
ghafla umekuwa na utashi wa kiutu uzima. Wengi tumefanya makosa katika umri huo. Tumefanya maamuzi mabaya. Wengine hayakutudhuru, wengine yaliwadhuru. Jamii itakuaminisha "ushakuwa mtu mzima", lakini niamini, bado. Bado unahitaji kukua na kujifunza mengi.
Jifunze kwa makosa YETU.
Mengine utayarudia najua, lakini jitahidi mengi usiyarudie.
Dunia haijali binti, picha na video zinapovuja, lawama utabeba wewe na mama yako. Hata kama kuna mtu mzima mwenye makosa, jinsia yako itabeba lawama. Usirudie makosa YETU.
Tutasimama nawe katika safari yako, USITUANGUSHE

β€’ β€’ β€’

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
γ€€

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Kuduishe Kisowile Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @Kudu_ze_Kudu

22 Sep 20
There is no need of that because girls are being taught that even before they attain menarche.
The question is, when are boys going to be taught how to actually be good husbands and their roles in marriage?
If you were a woman, you'd know that "ndoa" has been the backbone of
everything women are taught to do.
Literally, a girlchild is being groomed to be a wife from a young age, being shown their place and "responsibilities" as mothers and wives.
But I don't see that happening to a boychild. They are just let "to be boys" and suddenly they marry and
expected to transition to be men, fathers and husbands.
Nobody prepares them for that.
Nobody teaches them anything during puberty.
They are left to figure out everything themselves because "they are boys"
And then we wonder how comes the marriage institution is failing miserably
Read 16 tweets
20 Sep 20
Oooh Mama Afrika! Tunakusifu kwa kuijaza Afrika. Kwa kutupa matunda bora ya mbegu zilizopandwa kwako.
Tumeona kilio chako kutoka nyikani. Kilio chako kwa matunda yako yaliyopotea kabla hayajaiva.
Mama Afrika, kilio chako tumekisikia. Futa machozi.
Kwani #MaamuziYakoKeshoYako #UZI
Ni siku nyingine tulivu, baada ya purukushani za daladala kuwahi hospitali, nilimsalimu nesi wa zamu huku nikivaa koti langu tayari kuandaa meza kwa ajili ya kliniki ya kina mama wajawazito.
Mlipuko wa homa ya virusi vya Korona ulikuwa umeanza, na siku ile #MaamuziYakoKeshoYako
Tulikuwa na mengi ya kuongea na kina mama wajawazito.
Nesi alitupa kila mmoja jukumu la kuelezea kitu kimoja.
Kabla ya kliniki, kabla ya kugawa namba kwa ajili ya kumuona daktari, ni lazima tutoe MASOMO mbalimbali kwa faida ya kina mama wajawazito.
#MaamuziYakoKeshoYako
Read 20 tweets
18 Sep 20
NEW ARRIVALS πŸ”₯πŸ’™πŸ’šπŸ’›
SEHEMU YA PILI: 17,000TZS ImageImageImageImage
ImageImageImageImage
ImageImageImageImage
Read 5 tweets
18 Sep 20
NEW ARRIVALS πŸ’™πŸ”₯
#UZI SEHEMU YA KWANZA.
17,000TZS per pair. ImageImageImageImage
ImageImageImageImage
ImageImageImageImage
Read 4 tweets
15 Sep 20
Nilivyokuwa form 3, nilipendekezwa kuwa kiranja wa afya msaidizi, kiukweli nilikuwa sitaki, umoniter wa darasa ulikuwa unanitosha.
Tukaitwa ofisini kujinadi kwa staff, nikasema, "naitwa Kuduishe Kisowile, nimependekezwa kuwa kiranja msaidizi wa afya, na sitaki."
Nikasikia, (1/5)
mwalimu anasema, "unasema?"
Nikarudia, "sipo tayari, sitaki kuwa kiranja."
Wote wakacheka. Hakuna aliyetegemea lile jibu nadhani.
Wakaniruhusu nikaondoka.
Matokeo yalivyotoka nikachaguliwa.πŸ˜‚πŸ˜­
Nikaenda ofisini kwa mwalimu mkuu msaidizi nalia, sitaki kuwa kiranja. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜­ (2/5)
Nikamwambia, "kwanini mmenichagua wakati nilisema sitaki?"
Akasema, "ulidhani kusema vile kungefanya jina lako likatwe, lakini sisi tuliona kitu tofauti. Tuliona binti mwenye msimamo, anayejiamini ambaye haogopi kusema mawazo yake mbele ya viongozi wa shule, tukaona unafaa" (3/5)
Read 5 tweets
11 Sep 20
#UZI : NEW ARRIVALS πŸ”₯
Vile #ViwaloVyaKudu vimerudi tena! 😍πŸ”₯
-Ukipenda, screenshot tuma DM ulipie kama ipo.
-Nguo isiyolipiwa, haitotunzwa.
-Bei ni 17000Tshs, haipungui.
-Delivery J'PILI TU, Mikoani tunatuma, Unaweza kuja kuchukua KAIRUKI siku yoyote.
KARIBUπŸ’™
#DaktariMwandishi ImageImageImageImage
Karibuni πŸ’™πŸ”₯
Wale wa PAJAMA PARTY, SLEEP OVER, SLUMBER PARTY, πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹ ImageImageImageImage
Karibuni πŸ”₯πŸ’™
Wale mabibi harusi watarajiwa kwenye Bridal Photoshoot, Birthday photoshoot n.k πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯ ImageImageImageImage
Read 10 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!