HabariTech Profile picture
Jan 11 26 tweets 8 min read
🚀Thetan Arena MOBA

Leo tuzungumze kuhusiana na Game moja wapo unayoweza kulipwa kwa kuicheza. Game hii inaitwa Thetan Arena MOBA.

MOBA (Multiplayer Online Battle Arena). Hii ni gam ambayo unacheza kwa kupigana battles na watu wengine Online.

#HabariTech Image
🚀Kumekuwa na P2E games nyingi zilizoundwa hivi karibuni. Nyingi zikiwa na mfumo wa card based na nyingine trading based.

Thetan Arena inatumia mfumo wa battles (yaani kupiganisha characters ndani ya game).

Battles hizi zinapigwa mtandaoni kati ya character wako na wa adui yako Image
🚀Characters wa Thetan Arena tunawaita Heroes. Heroes hawa utawapiganisha katika teams.

Na kwa ushindi unaopata utazawadiwa tokens za game hii ambazo kwa sasa token moja ina thamani ya $4.
🚀Kwa sasa game inaweza chezwa katika mifumo ya Battle Royale, Superstar, Deathmatch, na Tower Seige.

Kila mfumo una namna yake ya kucheza. Mifumo karibu yote inahusisha wewe kupigana dhidi ya timu pinzani na timu yako itashinda kwa kuwa timu ya mwisho kuwa hai. Image
🚀Mfano Tower Siege unaicheza kwa kulinda tower ya timu yako na wakati huo huo kuipiga tower ya wapinzani wenu.

Mtakapo fanikiwa kuangusha tower ya wapinzani mnaibuka washindi na kujishindia Tokens ambazo unaweza uza na kupata pesa.
🚀Heroes wana classes (aina) ndani ya game. Classes hizi ziko aina 3, Assassin, Marksman na Tank.

Assassins ni wale hujificha na wanaweza kusababisha damage kubwa kwa maadui.

Marksman ni wale ambao wanaweza mdhuru adui yako kutoka mbali. ImageImage
🚀Tank hawa husababisha damage kubwa zaidi kuzidi wote na mara nyingi ndiyo huwa wanaongoza timu.

Nimechagua kuelezea Thetan Arena kwa sababu ni game unaweza anza kuicheza BURE. Yani wanakupa nafasi ya kufanya majaribio kabla hujaamua kuweka pesa yako ili upate nyingi zaidi.
🚀Utakapo jisajili kwenye game sasa hivi kwa mara ya kwanza utapewa kila hero mmoja BURE kwa kila class.

Huyu atakuwa mwenye uwezo mdogo na hatakushindia coins unazoweza uza na kupata pesa.

Kwa sababu huyu umepewa bure ili kufanyia mazoezi.
🚀Nilisema kwamba heroes wana classes 3. Kitu sikusema ni kwamba ndani ya class pia kuna level za hawa heroes.

Heroes hawa hata zawadi za ushindi pia wanatofautiana na gharama unayoweza mnunua pia wanatofautiana.
🚀Mfano tuchukulie class ya Assassin. Levels zake ni hizi

.Common Hero (level 1)
.Epic Hero (level 2)
.Legendary Hero (level 3)

Kadri level ya hero inavyokuwa kubwa ndivyo anavyokuwa bora na thamani yake inakuwa kubwa.
🚀Heroes wako wanakuwa na skills ambazo tayari utakuta ziko wazi kwa wewe kutumia.

Skills zaidi utaweza unaweza kuzipata kwa kushinda mechi na kupewa kama zawadi au kwa kununa kwenye duka la game.
🚀Skills hizi unaweza zichagua zipi utumie ndani ya game muda unacheza kulingana na hero husika.

Cha muhimu kuzingatia ni skills unazochagua. Je, zina uwezo wa kukupa ushindi unaotaka?

Ukikosea kuchagua skill utajikuta unapoteza mechi nyingi. Image
🚀Thetan Arena inatumia coin inaitwa THG. Coin hii ndiyo utapewa kama zawadi unaposhinda na ndiyo utakayotumia kununua vitu (skills) ndani ya game.

Sasa kabla ya yote kuna vitu tutahitaji ili kuweza cheza game hii. Kimoja cha muhimu ni simu ya Android au iOS au Windows PC. Image
🚀Vitu vingine vya muhimu ni hivi

1. Binance Account
Jiunge kupitia link hii utapata 10% kwenye transaction fees accounts.binance.com/en/register?re…

Account ya Binance tutaitumia kununua $BNB ambazo badae tutazihamisha kwenda kwenye Metamask Wallet.

Na hapa tunaenda kwenye kitu cha pili Image
2. Metamask Wallet
Hii ni wallet ambayo utaitumia kutunza $BNB ambazo utatumia kununua heroes wako utakao tumia kwenye game.

$BNB hizo ni zile utahamisha kutoka binance account uliyotengeneza hapo juu.

metamask.io Image
3. Thetan Arena Account

Account hii ndiyo utatumia kuchezea games na kuingia market place ya Thetan Arena ili kununua heroes.

Tumia link hii kuingia kwenye game ili uwepo kwenye team yangu thetanarena.page.link/FSMYy9UoPr4RM6…
🚀Baada ya kuwa umeshafanya hayo yote, sasa ni muda wa kununua heroe wako kwenye market place ya @ThetanArena

Sasa kabla ya yote muone @MaujanjaCrypto atakuuzia hizo $BNB kisha utahamisha kutoka Binance kwenda Metamask Wallet. Image
🚀Utaconnect metamask wallet yako na account yako ya Thetan arena kule kwenye market place.

Network unayotakiwa kutumia pale ni Binance Smart Chain. Kuna vitu vya kuzingatia wakati unanunua hero wako.
1. Class ya hero unataka.

2. Level ya hero wako. Kumbuka ukubwa wa level ndiyo ubora wa hero wako. Kwa maana ya kwamba hero mwenye level kubwa ana rewards & bonus kubwa zaidi. Pia anaweza cheza battles nyingi zaidi kwa siku.
3. Battles ambazo tayari amecheza.

Unaweza ona hero anauzwa bei ndogo sana ukaswawishika kumnunua. Lakini akawa amemaliza nusu ya battles anatakiwa kucheza

Frame 1: Hero anauzwa $94 lakini ameshacheza battles 100 kati ya 259 anazotakiwa kucheza. ImageImage
🚀Maana yake thamani yake itaisha mapema kwa kuwa kabakiza battles 139 tu.

Frame 2: Anauzwa $166 na ana battles 361, pia hajacheza battle yoyote bado.

Huyu ana nafasi ya kukupa faida kwa kuwa utamtumia muda mrefu zaidi.
🚀Najua utaogopa kuona $166 😂. Ukimtumia vizuri kwa hizo battle 361 na kushinda unaweza pata zaidi ya $1,000.

Pia hautapoteza hela yako yote, kwa sababu kwenye thetan arena hata ukipoteza mechi unapewa 1 THG kama zawaid ya kucheza game.
🚀Kwa maana hiyo una nafasi ya kurudisha pesa uliyoanzia au kupata zaidi, kulingana na thamani ya THG iko vipi muda huo.

Pia ukiona battles zinakushinda unaweza rudisha pesa yako kwa kumuuza hero wako.

Na hii ndiyo sababu nimechagua Thetan Arena kwa kuwa ni Win-Win game.
🚀Nimeandika uzi huu kwakuwa sikuweza elezea kwa undani ndani ya magazine ya @HabariTech 😁. Kule nimewapa mwanga wa uchumi mzima wa Play-To-Earn hapa sasa najazia nyama.

Uzuri wa hizi games sio lazima ucheze wewe mwenye. Wengine wanasema, "Mtu mzima hachezi games" 😂😂
🚀Sawa wewe huchezi basi mpe mwanao au mdogo wako anayependa games acheze.

Unajua nini?

Hautaita tena January Njaanuary 😉. Kwa kucheza hizi games mwanao anaweza kuanza jilipia ada yeye mwenyewe.

Haya naita Mafao ya Play-To-Earn. Chelewa Chelewa utakuta mwana si wako.
🚀Tunashukuru kwa sapoti yenu kusoma magazine ya @HabariTech mpaka sasa kwa magazine Toleo 3 tunawasomaji 260+.

Tunaomba kuongeza namba hii kwa kushare na wengi zaidi link hii habaritech.gumroad.com/l/habaritech3

Asante sana kwa muda wako.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with HabariTech

HabariTech Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @HabariTech

Jan 19
📡Camera Iliyofichwa

Kila siku inayoanza na kuisha kuna watu wanalala Hotelini, lodge, nyumba za wageni na wengine wanakuwa wageni majumbani mwa watu.

Watu wanaofatilia sana movies na conspiracies huwa na wasiwasi wa kuwa recorded na camera zilizofichwa.

#HabariTech Image
📡Mara nyingi camera zilizofichwa huwa na lengo zuri la kudaka wezi au matukio ambayo yanaweza hatarisha usalama.

Na wakati mwingine camera hizi hufungwa kwa lengo la kutumika kudaka matukio ya faragha ili kusambaza kwa lengo la kumtia mtu aibu au kufanya blackmail.
📡Itakuwa vyema leo nikikujuza kuwa unaweza tumia smartphone yako kujua kama kuna camera zimefichwa katika chumba ulichopo.

MUHIMU: Njia hizi hazihusiana na kutambua camera ya Smartphone iliyofichwa.
Read 16 tweets
Dec 28, 2021
✨Kwa sasa simu nyingine zinatumia sim card ile ya card ya kutoa na kuweka.

Ili mtu uwe na namba zaidi ya moja unalazimika kuwa na sim card zaidi ya moja.

eSim itakuja kuondoa hii tabu.

#HabariTech 🧵
✨eSim (Electronic Sim Card au Embedded Sim Card)

Hii ni sim card ambayo unaweza download ya mtandao wowote na kuitumia ndani ya simu yako. Nasema unaweza download kwa maana ya kwamba.

Ndani ya simu yako unakuwa na chip ambayo inafanya kazi kama hizi sim card za kawaida.
✨ili uweze kupata mtandao itakubidi uijaze na taarifa za mtandao husika unaotaka kutumia.

Kwa sasa ukiwa na namba moja ya Voda au Tigo kwenye sim card yako, huwezi ibadili hiyo namba bila kubadili sim card.
Read 7 tweets
Dec 27, 2021
Wengi sasa hivi mnatamani kuingia kwenye UX Designing. Inapendeza kuona watu kama @AbilMdone @mzabayuni na @iamKaga wanawapa motisha.

Ni rahisi kudrag & drop elements kufanya graphics designing ukidhani ni UX designing.
UX designing inahusiana na lengo la mtumiaji wa app au website yako. Haingii kwenye app au website kushangaza majo avutiwe na muonekano.

Anatumia website/app yako ili kufanyikisha jambo fulani.
Wengi tunakosea kudhani kwamba UI nzuri ni ile inayovutia tu machoni.

Ukweli ni kwamba UI nzuri ni ile mtuamiaji anaweza elewa na kutumia bila shida, ajiskie fahari kuitumia na imtongoze kuitumia.
Read 4 tweets
Nov 19, 2021
📡iOS ni Bora kuzidi Android mbali sana 👀

Hii vita tungewapa silaha nani atashinda? Tuachana na hayo tusifike huko.

Hii mada kila ikiwekwa mezani mashabaki wa hizo OS huongelea sana kwamba wanayotumia wao ni bora.

Je, Ni kweli?

#HabariTech
📡Najua kwamba kuna mtu tayari anajizuia sana mpaka amalize kusoma ndipo ajibu.

Kuwa mpole bro/sis maisha sio vita 😁.

Binafsi mimi ni shabiki mkubwa wa Android na huwezi nibadilisha kwa lolote, ila pale ambapo utaalamu utatumika ukweli lazima usemwe.
📡Kwa sababu hiyo kwa kujiamini kabisa naweza kusema kwamba iOS ni bora kuzidi Android kwa mtumiaji wa kawaida wa simu.

Swali tukiacha liwe na mjadala kwamba ipi bora kuna vitu lazima utasikia kutoka pande zote mbili.
Read 22 tweets
Nov 18, 2021
Sio expert sana upande wa engineering ila naweza jibu hivi.

Sidhani kama quantum computing itakuja kuuzwa kwa watumiaji wa kawaida kama mimi na wewe.

Labda sio kwa miaka 100 ijayo 😁 watumiaji wa kawaida kama mimi na wewe tunahitaji quantum computing ability kwa ajili ya nini?
Anyway tuseme itakuwa available kwa consumers nani yuko tayari kulipia gharama za kumiliki na kumaintain running costs za quantum computer?

Kila mtu anatamani kuwa na kifaa chenye super conducting ability, ila nikiwaza huo umeme wake 😂.
Alafu kuna ishu ya cooling. Kifaa cha quantum kinahitaji kuwa na cooling system iliyopo efficient sana na inaweza kuwa kubwa sio kawaida.

Kitu ambacho kufit kwenye PC ni meh! 🤔

Quantum computers zina advantage kunwa zikitumika kwenye sehemu kama data centers.
Read 5 tweets
Nov 8, 2021
📡Tabia zinazo haribu PC yako kwa haraka.

Sisi sote tunapenda kuona vifaa vyetu kama PC zikidumu kwa muda mrefu, lakini mara nyingi huwa zinaharibika mapema tofauti na mategemeo yetu.

#HabariTech Image
📡Huenda tabia zetu na namna tunatumia hivi vifaa ikawa ni sababu ya hizi mashine kuharibika haraka Image
📡Hakuna kitu kinachodumu milele na hasa vifaa vya elektroniki. Watengenezaji wa vifaa hutengeneza vifaa wakiwa na malengo kwamba kwa matumizi sahihi hicho kifaa kitadumu kwa miaka kadhaa.

Muda huo huwa sahihi ukitumia ipasavyo kwa usahihi.

Nini kinaua PC yako mapema?
Read 23 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(